Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esdras 4.22
Bible en Swahili de l’est


Interruption des travaux

1 Basi adui za Yuda na Benyamini, waliposikia ya kuwa wana wa uhamisho wanamjengea Bwana, Mungu wa Israeli, hekalu,
Esdras 1.11 Esdras 6.19-6.20 1 Rois 5.4-5.5 Daniel 5.13 Esdras 10.7
2 wakamkaribia Zerubabeli, na wakuu wa mbari za mababa, wakawaambia, Na tujenge sisi nasi pamoja nanyi; kwa maana tunamtafuta Mungu wenu kama ninyi, nasi twamtolea dhabihu tangu zamani za Esar-hadoni, mfalme wa Ashuru, aliyetupandisha mpaka hapa.
2 Rois 19.37 2 Rois 17.24 2 Rois 17.41 2 Rois 17.27-17.33 Esdras 3.12
3 Lakini Zerubabeli, na Yoshua, na wakuu wengine wa mbari za mababa katika Israeli, wakawaambia, Ninyi haiwahusu kushirikiana nasi katika kumjengea Mungu wetu nyumba; bali sisi wenyewe peke yetu tutamjengea Bwana, Mungu wa Israeli, nyumba, kama mfalme Koreshi, mfalme wa Uajemi, alivyotuamuru.
Néhémie 2.20 Actes 8.21 Esdras 6.3-6.5 Jean 4.22-4.23 2 Chroniques 36.22-1.3
4 Ndipo watu wa nchi wakaidhoofisha mikono ya watu wa Yuda, wakawasumbua, walipokuwa wakijenga.
Esdras 3.3 Néhémie 4.11 Néhémie 6.9 Jérémie 38.4 Néhémie 4.7-4.8
5 Wakawaajiri washauri juu yao, ili kuwapinga kusudi lao, siku zote za Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata wakati wa kutawala kwake Dario, mfalme wa Uajemi.
Psaumes 2.1-2.2 Nahum 1.11 Esdras 5.5-6.18 Actes 24.1-24.27 Esdras 4.24
6 Tena, wakati wa kutawala kwake Ahasuero, mwanzo wa kutawala kwake, watu wakaandika mashitaka juu ya wenyeji wa Yuda na Yerusalemu.
Daniel 9.1 Esther 1.1 Actes 24.5-24.9 Actes 25.7 Actes 24.13
7 Na tena, katika siku za Artashasta, Mithredathi, na Tabeeli na mabaki ya wenziwe, wakimwandikia Artashasta, mfalme wa Uajemi, salamu za heri; na mwandiko wa waraka huo, ukaandikwa kwa herufi za Kiaramu, na kunenwa kwa lugha ya Kiaramu.
2 Rois 18.26 Daniel 2.4 Esaïe 36.11 Esdras 5.6 Esdras 4.9
8 Nao Rehumu, Bwana shauri, na Shimshai, mwandishi, wakaandika waraka juu ya Yerusalemu kwa Artashasta, mfalme, kama hivi;
2 Samuel 20.25 Esdras 4.9 2 Samuel 8.17 2 Rois 18.18
9 Rehumu, Bwana shauri, na Shimshai, mwandishi, na mabaki ya wenzao, makadhi wa Kiajemi na madiwani wa Kiajemi; na Waarkewi, Wababeli, Washushani, yaani, Waelami;
Esdras 6.6 Esdras 5.6 2 Rois 17.24 2 Rois 17.30-17.31 Esther 1.2
10 na mabaki ya mataifa, ambao Asur-bani-pali mkuu, mwenye heshima, aliwavusha, na kuwakalisha katika mji wa Samaria, na mahali penginepo, ng’ambo ya Mto; wakadhalika.
Esdras 4.17 Esdras 7.12 Esdras 4.11 2 Rois 17.24-17.41 Esdras 4.1
11 Hii ndiyo nakili ya waraka waliyompelekea mfalme Artashasta;watumishi wako,watu walio ng`ambo ya mto wakadhalika.
12 Ijulikane kwa mfalme ya kuwa Wayahudi, waliokwea kutoka kwako, wamefika kwetu Yerusalemu; nao wanaujenga ule mji mwasi, mbaya; wamemaliza kuta zake, na kuitengeneza misingi yake.
Esdras 5.3 2 Chroniques 36.13 Esdras 5.9 Esaïe 1.21-1.23 2 Rois 18.20
13 Basi, ijulikane kwa mfalme, ya kuwa mji huu ukijengwa, na kuta zake zikimalizika, hawatatoa kodi, wala ada, wala ushuru, na mwisho wake wafalme watapata hasara.
Esdras 7.24 Néhémie 5.4 Matthieu 9.9 Psaumes 52.2 Psaumes 119.69
14 Na sisi, kwa kuwa tunakula chumvi ya nyumba ya mfalme, wala si wajibu wetu kumwona mfalme akivunjiwa heshima, basi tumetuma watu na kumwarifu mfalme.
Jean 12.5-12.6 Jean 19.12-19.15 Ezéchiel 33.31
15 Ili habari zitafutwe katika kitabu cha tarehe za baba zako; ndivyo utakavyopata kujua kwa kitabu cha tarehe ya kuwa mji huo ni mji mwasi, wenye kuwadhuru wafalme, na maliwali, na ya kuwa wenyeji wake wamefanya fitina katika mji huo zamani; ndiyo sababu mji huo ukaangamizwa.
Néhémie 6.6 Esther 3.5-3.8 Jérémie 52.3-52.34 2 Rois 25.4 Néhémie 2.19
16 Twamwarifu mfalme ya kuwa mji huo ukijengwa, na kuta zake zikimalizika, hutakuwa na sehemu ya nchi ng’ambo ya Mto.
2 Samuel 8.3 1 Rois 4.24 Esdras 4.20
17 Ndipo mfalme akapeleka majibu;Kwa Rehumu,Bwana shauri, na Shimshai,mwandishi na wenzao wengine waliokaa katika Samaria,na penginepo ng`ambo ya mto, Salamu; wakadharika.
Esdras 5.7 Actes 23.26 Esdras 4.9-4.11 Esdras 7.12 Esdras 4.7
18 Ule waraka mlionipelekea umesomwa mbele yangu, nami nikaelewa na maana yake.
Néhémie 8.8
19 Nikatoa amri, na watu wametafuta habari; ikaonekana ya kuwa mji huu zamani umefanya fitina juu ya wafalme, na ya kuwa uasi na fitina zimefanyika ndani yake.
2 Rois 18.7 2 Rois 24.20 Esdras 5.17-6.2 Esdras 4.15 Deutéronome 13.14
20 Tena walikuwako wafalme wakuu juu ya Yerusalemu, waliotawala nchi yote iliyo ng’ambo ya Mto; wakapewa kodi, na ada, na ushuru.
1 Rois 4.21 Genèse 15.18 Psaumes 72.8 1 Chroniques 18.3 Esdras 4.16
21 Sasa toeni amri kuwakomesha watu hawa kazi yao, mji huu usijengwe, hata mimi nitakapotoa amri.
22 Tena jihadharini, msilegee katika jambo hili; kwa nini madhara yazidi, na wafalme wapate hasara?
Esther 7.3-7.4 Esther 3.8-3.9 Esdras 4.13
23 Hata nakala ya waraka huo wa mfalme Artashasta uliposomwa mbele ya Rehumu, Bwana shauri, na Shimshai, mwandishi, na wenzao, wakaenda Yerusalemu upesi, kwa Wayahudi, wakawakomesha kwa nguvu na kwa kuwashurutisha.
Romains 3.15 Proverbes 4.16 Esdras 4.8-4.9 Esdras 4.17 Michée 2.1
24 Hivyo kazi ya nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu ikakoma; nayo ikakoma hata mwaka wa pili wa kutawala kwake Dario, mfalme wa Uajemi.
Aggée 1.15 Job 20.5 Néhémie 6.3 Néhémie 6.9 Esdras 5.5

Cette Bible est dans le domaine public.