Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 8.66
Bible en Swahili de l’est


Inauguration du temple

1 Ndipo Sulemani alipowakusanya wazee wa Israeli, na wakuu wote wa kabila, wakuu wa mbari za mababa wa wana wa Israeli, wamwendee mfalme Sulemani huko Yerusalemu, ili walipandishe sanduku la agano la Bwana kutoka mji wa Daudi, yaani, Sayuni.
2 Chroniques 5.2-5.10 1 Chroniques 15.25 2 Samuel 6.12-6.17 1 Pierre 2.6 1 Chroniques 28.1
2 Wakakutana mbele ya mfalme Sulemani watu wote wa Israeli wakati wa sikukuu, katika mwezi wa Ethanimu, ndio mwezi wa saba.
Lévitique 23.34 2 Chroniques 7.8-7.10 Esdras 3.4 Deutéronome 16.13 Zacharie 14.16-14.19
3 Wazee wote wa Israeli wakaja, nao makuhani wakajitwika sanduku.
Deutéronome 31.9 Josué 3.6 Josué 3.3 Nombres 4.15 Josué 6.6
4 Wakalipandisha sanduku la Bwana, na ile hema ya kukutania, na vyombo vitakatifu vyote vilivyokuwa katika ile Hema; vitu hivyo makuhani na Walawi wakavipandisha.
2 Chroniques 1.3 1 Rois 3.4 Exode 40.2-40.33
5 Mfalme Sulemani, na mkutano wote wa Israeli waliokutanika kwake, walikuwako pamoja naye mbele ya sanduku, wakichinja sadaka kondoo na ng’ombe, wasioweza kuhesabiwa wala kufahamiwa idadi yao kwa kuwa wengi.
2 Samuel 6.13 1 Rois 8.62-8.63 1 Chroniques 16.1
6 Makuhani wakalileta sanduku la agano la Bwana hata mahali pake, katika chumba cha ndani cha ile nyumba, patakatifu pa patakatifu, naam, chini ya mbawa za makerubi.
1 Rois 6.19 2 Samuel 6.17 1 Rois 6.27 Exode 26.33-26.34 2 Samuel 6.2
7 Kwa maana makerubi yalinyosha mbawa zao, juu ya mahali pa sanduku, makerubi yakalifunika lile sanduku na miti yake kwa juu.
8 Na ile miti kwa kuwa mirefu, ncha za miti zilionekana katika mahali patakatifu, mbele ya chumba cha ndani; lakini hazikuonekana nje; nayo iko kuko huko hata leo.
Exode 25.13-25.15 Exode 37.4-37.5 Josué 4.9 Matthieu 28.15 Exode 40.20
9 Hamkuwa na kitu ndani ya sanduku, ila zile mbao mbili za mawe ambazo Musa aliziweka ndani huko Horebu, Bwana alipofanya agano na wana wa Israeli, hapo walipotoka katika nchi ya Misri.
Exode 25.21 Hébreux 9.4 Exode 40.20 Deutéronome 4.13 Exode 34.27-34.28
10 Ikawa, makuhani walipotoka katika patakatifu, nyumba ya Bwana ikajaa wingu;
Exode 40.34-40.35 2 Chroniques 7.1-7.2
11 hata makuhani hawakuweza kusimama ili kufanya huduma yao, kwa sababu ya wingu lile; kwa kuwa nyumba ya Bwana ilikuwa imejaa utukufu wa Bwana.
Actes 7.55 Lévitique 9.23 2 Corinthiens 4.6 Ezéchiel 43.4-43.5 Apocalypse 21.11
12 Ndipo Sulemani akanena, Bwana alisema ya kwamba atakaa katika giza nene.
Psaumes 97.2 Lévitique 16.2 Esaïe 45.15 2 Chroniques 6.1-6.11 Deutéronome 5.22
13 Hakika nimekujengea nyumba ya kukaa, iwe mahali pa makao yako milele.
2 Samuel 7.13 Psaumes 132.13-132.14 Exode 15.17 1 Chroniques 22.10-22.11 1 Chroniques 17.12
14 Mfalme akageuza uso wake, akawabariki mkutano wote wa Israeli; na mkutano wote wa Israeli wakasimama.
2 Samuel 6.18 Néhémie 9.2 Néhémie 8.7 2 Chroniques 6.3 1 Rois 8.55-8.56
15 Akasema, Bwana, Mungu wa Israeli, ahimidiwe, aliyenena na Daudi baba yangu kwa kinywa chake akalitimiza kwa mkono wake, akasema,
Luc 1.68 1 Chroniques 29.20 Néhémie 9.5 1 Chroniques 29.10 Psaumes 138.2
16 Tokea siku ile nilipowatoa watu wangu Israeli katika Misri, sikuchagua mji wo wote katika kabila zote za Israeli ili kujenga nyumba, jina langu liwe hapo; lakini nalimchagua Daudi awe juu ya watu wangu Israeli.
1 Samuel 16.1 Deutéronome 12.11 2 Samuel 7.4-7.8 1 Chroniques 28.4 1 Chroniques 17.5-17.6
17 Basi ilikuwa moyoni mwake Daudi, baba yangu, kujenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
2 Samuel 7.2-7.3 1 Chroniques 17.1-17.15 1 Chroniques 28.2 1 Chroniques 22.7
18 Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, Kwa kuwa ilikuwa moyoni mwako kujenga nyumba kwa jina langu, ulifanya vema kuwaza hivi moyoni mwako.
2 Chroniques 6.7-6.9 2 Corinthiens 8.12
19 Lakini wewe hutanijengea nyumba hiyo; ila mwanao atakayetoka katika viuno vyako, yeye ndiye atakayeijenga nyumba kwa jina langu.
2 Samuel 7.5 2 Samuel 7.12-7.13 1 Chroniques 17.11-17.12 1 Chroniques 22.8-22.10 1 Chroniques 17.4
20 Basi Bwana amelitimiza neno lile alilolinena; nami nimesimama mahali pa Daudi baba yangu, na kuketi katika kiti cha enzi cha Israeli, kama Bwana alivyoahidi, nami nimeijenga nyumba kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
1 Chroniques 28.5-28.6 Esaïe 9.7 Néhémie 9.8 Ezéchiel 37.14 Ezéchiel 12.25
21 Na humo sanduku hili nimelifanyizia mahali, ambalo ndani yake mna maagano ya Bwana, aliyoyafanya na baba zetu, hapo alipowatoa katika nchi ya Misri.
Deutéronome 31.26 1 Rois 8.9 Deutéronome 9.11 Exode 34.28 Deutéronome 9.9
22 Sulemani akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana, machoni pa mkutano wote wa Israeli, akaikunjua mikono yake mbinguni.
Esdras 9.5 Exode 9.33 1 Rois 8.54 Exode 9.29 Esaïe 1.15
23 Akasema Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe, mbinguni juu wala duniani chini; ushikaye maagano na rehema kwa watumishi wako, waendao mbele zako kwa mioyo yao yote.
Deutéronome 7.9 2 Samuel 7.22 Néhémie 1.5 Daniel 9.4 1 Samuel 2.2
24 Umemtimizia mtumishi wako, Daudi, baba yangu, ahadi uliyomwahidia; naam, ulinena kwa kinywa chako, ukayatimiza kwa mkono wako, kama ilivyo leo.
1 Rois 8.15 2 Chroniques 6.14-6.15 2 Samuel 7.16 2 Samuel 7.12
25 Na sasa, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, umfikilizie mtumishi wako, Daudi, baba yangu, ahadi uliyomwahidia, ukisema, Hutakosa kuwa na mtu wa kuketi katika kiti cha enzi cha Israeli machoni pangu, kama watoto wako wakiangalia njia zao, ili kuenenda mbele zangu kama wewe ulivyoenenda.
1 Rois 2.4 2 Chroniques 6.16-6.17 1 Chroniques 28.9 1 Rois 9.4-9.6 Jérémie 33.17-33.26
26 Sasa, Ee Mungu wa Israeli, nakusihi, ulithibitishe neno lako, ulilomwambia mtumishi wako, Daudi, baba yangu.
Esaïe 45.3 Esaïe 41.17 Ezéchiel 36.36-36.37 Exode 24.10 2 Chroniques 1.9
27 Lakini Mungu je? Atakaa kweli kweli juu ya nchi? Tazama, mbingu hazikutoshi, wala mbingu za mbingu; sembuse nyumba hii niliyoijenga!
Esaïe 66.1 Jérémie 23.24 2 Chroniques 2.6 Psaumes 139.7-139.16 Actes 7.48-7.49
28 Walakini uyaelekee maombi ya mtumwa wako, na dua yake, Ee Bwana, Mungu wangu, uisikilize sauti na maombi ya mtumwa wako, aombayo mbele zako leo.
Psaumes 5.1 Psaumes 141.2 Psaumes 88.1-88.2 Luc 18.7 Daniel 9.17-9.19
29 Macho yako yafumbuke na kuielekea nyumba hii usiku na mchana, mahali hapa ulipopataja, ukasema, Hapa ndipo litakapokuwapo jina langu; ili uyasikie maombi ya mtumwa wako aombapo akikabili mahali hapa.
Néhémie 1.6 Deutéronome 12.11 2 Chroniques 6.20 Daniel 6.10 1 Rois 8.52
30 Uisikie dua ya mtumwa wako, na ya watu wako Israeli, watakapoomba wakikabili mahali hapa; naam, sikia huko mbinguni, makao yako; nawe usikiapo, samehe.
1 Rois 8.39 1 Rois 8.36 1 Rois 8.34 Psaumes 130.3-130.4 Ecclésiaste 5.2
31 Ikiwa mtu amemkosa mwenzake, na kupewa sharti ya kiapo aapishwe, naye akija na kuapa hapa mbele ya madhabahu yako, katika nyumba hii;
Exode 22.8-22.11 Proverbes 30.9 2 Chroniques 6.22-6.23 Nombres 5.16-5.22 Lévitique 5.1
32 basi, usikie huko mbinguni, ukatende, ukawahukumu watumwa wako; ukimpatiliza mtu mbaya, kwa kuleta njia yake juu ya kichwa chake; na kumpa mwenye haki haki yake, ukimjalia kwa kadiri ya haki yake.
Deutéronome 25.1 Romains 2.13 Esaïe 3.10-3.11 Romains 7.9 Romains 2.6-2.10
33 Ikiwa watu wako Israeli wamepigwa mbele ya adui zao, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakirejea tena kwako, na kulikiri jina lako wakikuomba na kukusihi katika nyumba hii;
Lévitique 26.17 Deutéronome 28.25 Lévitique 26.39-26.42 Deutéronome 28.48 Lévitique 26.25
34 basi, usikie huko mbinguni, ukawaachilie watu wako Israeli dhambi yao, ukawarejeze tena katika nchi uliyowapa baba zao.
Amos 7.2 Daniel 9.12 1 Rois 8.30 Genèse 13.15 Jérémie 31.4-31.9
35 Ikiwa mbingu zimefungwa, hata hakuna mvua, kwa sababu wamekukosa wewe; kama wakiomba wakikabili mahali hapa, na kulikiri jina lako, na kuiacha dhambi yao, wakati ule utakapowatesa;
Deutéronome 11.17 1 Rois 8.33 Lévitique 26.19 Apocalypse 11.6 Luc 4.25
36 basi, usikie huko mbinguni, ukaisamehe dhambi ya watumwa wako, na ya watu wako Israeli; unapowafundisha njia iliyo njema, iwapasayo kuiendea; ukanyeshe mvua juu ya nchi yako, uliyowapa watu wako iwe urithi wao.
Psaumes 27.11 1 Samuel 12.23 Jérémie 6.16 1 Rois 18.1 Psaumes 25.4-25.5
37 Ikiwa nchi imeingia njaa, au tauni, au ukosefu wa mvua, au ukungu, au nzige, au panzi; ikiwa adui wamewahusuru katika nchi ya miji yao; au ukiwapo msiba wo wote, au uele wo wote;
Deutéronome 28.21-28.22 Lévitique 26.16 2 Chroniques 20.9 Deutéronome 28.38-28.42 2 Rois 6.25-6.29
38 maombi yo yote au dua yo yote ikifanywa na mtu awaye yote, au na watu wako Israeli wote pamoja, watakaojua kila mtu maradhi ya moyo wake, na kuikunjua mikono yake kuielekea nyumba hii;
Romains 7.24 Esaïe 1.15 1 Rois 8.22 Psaumes 42.6 Proverbes 14.10
39 basi, usikie huko mbinguni, makao yako, ukasamehe, ukatende, ukampe kila mtu kwa kadiri ya njia zake; wewe ujuaye moyo wake; (maana wewe peke yako ndiwe uijuaye mioyo ya wanadamu wote);
1 Chroniques 28.9 1 Samuel 16.7 Actes 1.24 Jérémie 17.10 1 Rois 8.36
40 ili wakuche wewe siku zote watakazoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
Psaumes 130.4 Hébreux 12.28 Apocalypse 15.4 Actes 10.2 Deutéronome 6.13
41 Hata na mgeni naye, asiyekuwa mmoja wa watu wako Israeli, atakapokuja kutoka nchi iliyo mbali sana kwa ajili ya jina lako;
1 Rois 10.1-10.2 Jean 12.20 2 Chroniques 6.32 Matthieu 8.10-8.11 Actes 8.27-8.40
42 (maana watasikia habari za jina lako kuu, na za mkono wako ulio hodari, na za mkono wako ulionyoshwa); atakapokuja na kuomba kuielekea nyumba hii;
Deutéronome 3.24 Daniel 4.37 Daniel 3.28 Exode 13.14 Exode 3.13-3.16
43 basi, usikie huko mbinguni, makao yako, ukatende kwa kadiri ya yote atakayokuomba mgeni huyo; ili watu wote wa dunia wapate kulijua jina lako, na kukucha wewe kama watu wako Israeli, nao wajue ya kuwa nyumba hii, niliyoijenga, imeitwa kwa jina lako.
Psaumes 102.15 1 Samuel 17.46 Psaumes 67.2 2 Rois 19.19 2 Chroniques 6.33
44 Ikiwa watu wako watoka kwenda kupigana na adui zao, kwa njia yo yote utakayowapeleka, wakikuomba, Bwana, kuuelekea mji huu uliouchagua, na nyumba hii niliyoijenga kwa jina lako;
Josué 6.2-6.5 2 Chroniques 18.31 Juges 6.14 Nombres 31.1-31.12 Deutéronome 20.1-20.4
45 basi, uyasikie huko mbinguni maombi yao na dua yao, ukaitetee haki yao.
Genèse 18.25 Psaumes 9.4 Jérémie 5.28
46 Ikiwa wamekutenda dhambi, (maana hakuna mtu asiyetenda dhambi), hata ukawaghadhibikia, ukawatia katika mikono ya adui zao, wawachukue mateka mpaka nchi ya adui zao, iliyo mbali au iliyo karibu;
Ecclésiaste 7.20 Proverbes 20.9 1 Jean 1.8-1.10 Lévitique 26.34-26.39 2 Rois 17.6
47 basi, wakijirudia nafsi zao katika nchi ile watakayochukuliwa mateka, wakitubu, na kukusihi katika nchi ya hao waliowachukua mateka, wakisema, Tumekosa, tumefanya ukaidi, tumetenda maovu;
Psaumes 106.6 Esdras 9.6-9.7 Ezéchiel 18.28 Luc 15.17-15.18 2 Chroniques 33.12-33.13
48 watakaporejea kwako kwa mioyo yao yote, na kwa nia zao zote, katika nchi ya adui zao, waliowachukua mateka, wakikuomba, kwa kuikabili nchi yao, uliyowapa baba zao, na mji huu uliouchagua, na nyumba hii niliyoijenga kwa jina lako;
Daniel 6.10 Deutéronome 4.29 Jérémie 29.12-29.14 1 Samuel 7.3-7.4 Jonas 2.4
49 basi, uyasikie maombi yao na dua yao, huko mbinguni, makao yako, ukaitetee haki yao;
2 Rois 19.19 Zacharie 1.15-1.16 1 Rois 8.45
50 ukawasamehe watu wako waliokutenda dhambi, na makosa yao yote waliyokukosa; ukawape kuonewa huruma mbele yao waliowachukua mateka, ili wapate kuwahurumia.
Psaumes 106.46 2 Chroniques 30.9 Actes 7.10 Daniel 1.9-1.10 Proverbes 16.7
51 Kwa kuwa ni watu wako, na urithi wako, uliowatoa katika Misri, toka katikati ya tanuu ya chuma.
Deutéronome 4.20 Jérémie 11.4 Néhémie 1.10 Exode 32.11-32.12 Jérémie 51.19
52 Macho yako na yafumbuke, na kuielekea dua ya mtumwa wako, na dua za watu wako Israeli, ukawasikilize kila wakati watakapokulilia.
1 Rois 8.29 Psaumes 145.18 Psaumes 86.5 2 Chroniques 6.40
53 Kwa maana uliwatenga na watu wote wa dunia, wawe urithi wako, kama ulivyonena kwa mdomo wa Musa, mtumishi wako, hapo ulipowatoa baba zetu katika Misri, Ee Bwana MUNGU.
Exode 19.5-19.6 Deutéronome 32.9 Deutéronome 14.2 Exode 33.16 Tite 2.14
54 Hata ikawa, Sulemani alipokwisha kumwomba Bwana maombi hayo, na dua hiyo yote, akasimama na kuondoka hapo mbele ya madhabahu ya Bwana, hapo alipokuwa amepiga magoti, na kuikunjua mikono yake kuelekea mbinguni.
Luc 22.45 Actes 20.36 Actes 21.5 Psaumes 95.6 1 Rois 8.22
55 Akasimama, na kuwabariki mkutano wote wa Israeli kwa sauti kuu, akasema,
1 Rois 8.14 2 Samuel 6.18 Nombres 6.23-6.26 1 Chroniques 16.2
56 Na ahimidiwe Bwana, aliyewapa watu wake Israeli kustarehe, vile vile kama yote aliyoyaahidi. Halikukosa kupatikana neno lo lote katika ahadi yake njema, aliyoahidi kwa mkono wa Musa, mtumishi wake.
Josué 23.14-23.15 Josué 21.44-21.45 Deutéronome 12.10 Luc 1.72-1.73 1 Samuel 3.19
57 Bwana, Mungu wetu, na akae nasi, kama alivyokaa na baba zetu; asituache, wala asitutupe;
Deutéronome 31.6 Josué 1.5 Hébreux 13.5 Esaïe 8.10 1 Samuel 12.22
58 aielekeze mioyo yetu kwake, ili tuende katika njia zake zote, na kuzishika amri zake, na sheria zake, na hukumu zake, alizowaamuru baba zetu.
Psaumes 119.36 Jérémie 31.33 Ezéchiel 36.26-36.27 Cantique 1.4 Deutéronome 4.45
59 Na maneno yangu haya, niliyoyaomba mbele za Bwana, na yawe karibu na Bwana, Mungu wetu, mchana na usiku, ili aitetee haki ya mtumishi wake, na haki ya watu wake Israeli, kwa kadiri ya haja zao za kila siku.
Jean 17.9 1 Jean 2.2 Psaumes 102.1-102.2 Jean 17.20-17.24 Psaumes 141.2
60 Watu wote wa ulimwengu wajue ya kuwa Bwana ndiye Mungu; hakuna mwingine.
Deutéronome 4.35 1 Rois 18.39 Jérémie 10.10-10.12 Josué 4.24 2 Rois 19.19
61 Mioyo yenu na iwe kamili kwa Bwana, Mungu wetu, kuenenda katika sheria zake, na kuzishika amri zake, kama ilivyo leo.
2 Rois 20.3 1 Rois 11.4 1 Rois 15.3 1 Rois 15.14 Deutéronome 18.13
62 Ndipo mfalme, na Israeli wote pamoja naye, wakatoa sadaka mbele za Bwana.
2 Samuel 6.17-6.19 2 Chroniques 7.4-7.10 Esdras 6.16-6.17
63 Sulemani akatoa sadaka za amani, alizomtolea Bwana, ng’ombe ishirini na mbili elfu, na kondoo mia na ishirini elfu. Ndivyo mfalme na wana wa Israeli wote walivyoifanya wakfu nyumba ya Bwana.
Esdras 6.16-6.17 Néhémie 12.27 Michée 6.7 1 Chroniques 29.21 2 Chroniques 2.4
64 Siku ile ile mfalme akaitakasa behewa ya katikati iliyokuwa mbele ya nyumba ya Bwana; kwa kuwa hapo ndipo alipotoa sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya unga, na mafuta ya sadaka za amani; kwa sababu ile madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele za Bwana ilikuwa ndogo, haikutosha kuzipokea sadaka za kuteketezwa, na sadaka za unga, na mafuta ya sadaka za amani.
2 Chroniques 4.1 2 Chroniques 7.7
65 Basi, wakati ule Sulemani akafanya sikukuu, na Israeli wote pamoja naye, kusanyiko kubwa sana, kutoka maingilio ya Hamathi mpaka kijito cha Misri, mbele za Bwana, Mungu wetu, siku saba na siku saba, yaani siku kumi na nne.
Nombres 34.5 1 Rois 8.2 Nombres 34.8 Genèse 15.18 Juges 3.3
66 Hata siku ya nane akaagana na watu, nao wakambarikia mfalme, wakaenda hemani kwao, wakifurahi na kuchangamka moyoni kwa wema wote Bwana aliomfanyia Daudi mtumishi wake, na Israeli watu wake.
1 Rois 8.1 Psaumes 95.1-95.2 2 Chroniques 7.10 Deutéronome 16.11 Zacharie 9.9

Cette Bible est dans le domaine public.