Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 42.33
Bible en Swahili de l’est


Les frères de Joseph en Égypte

1 Basi Yakobo akaona ya kuwa kuna nafaka katika Misri, Yakobo akawaambia wanawe, Kwa nini mnatazamana?
Actes 7.12 Genèse 41.54 2 Rois 8.3-8.4 Galates 2.7 Esdras 10.4
2 Akasema, Angalia, nimesikia ya kuwa kuna nafaka Misri; shukeni huko mkatununulie chakula, tupate kuishi wala tusife.
Genèse 43.8 Matthieu 4.4 Esaïe 38.1 Psaumes 118.17 Genèse 45.9
3 Basi ndugu kumi wa Yusufu wakashuka Misri ili wanunue nafaka.
Genèse 42.5 Genèse 42.13
4 Walakini Benyamini, ndugu wa Yusufu, Yakobo hakumpeleka pamoja na ndugu zake, maana alisema, Mabaya yasimpate.
Genèse 42.38 Genèse 44.27-44.34 Genèse 35.16-35.19 Genèse 44.20-44.22 Genèse 43.14
5 Wana wa Israeli wakaja wanunue chakula miongoni mwao waliokuja, kwa kuwa kulikuwa na njaa katika nchi ya Kanaani.
Actes 7.11 Genèse 41.57 Genèse 12.10 Genèse 26.1 Actes 11.28
6 Naye Yusufu alikuwa ni liwali juu ya nchi, ndiye aliyewauzia watu wote wa nchi. Nao ndugu zake Yusufu wakaja, wakainama kifudifudi mbele yake.
Apocalypse 3.9 Genèse 19.1 Genèse 45.8 Genèse 37.7-37.10 Genèse 45.26
7 Yusufu akawaona nduguze, akawatambua, lakini alijifanya kama mgeni kwao. Akasema nao kwa maneno makali, akawaambia, Mmetoka wapi ninyi? Wakasema. Tumetoka nchi ya Kanaani, ili tununue chakula.
Genèse 42.30 Genèse 42.19-42.20 Genèse 42.14-42.17 Genèse 42.9-42.12 Matthieu 15.23-15.26
8 Yusufu akawatambua nduguze, bali wao hawakumtambua yeye.
Jean 21.4 Luc 24.16 Jean 20.14 Genèse 37.2
9 Yusufu akazikumbuka zile ndoto alizowaotea. Akawaambia, Wapelelezi ninyi, mmekuja ili mwuone utupu wa nchi.
Genèse 37.5-37.9 Exode 32.35 Genèse 42.16 Josué 2.1 Nombres 13.16-13.20
10 Wakamwambia, Hasha, bwana, watumwa wako tumekuja ili tununue chakula.
Genèse 37.8 1 Samuel 26.17 1 Rois 18.7 Genèse 27.29 Genèse 27.37
11 Sisi sote ni wana wa mtu mmoja tu watu wa kweli sisi; watumwa wako si wapelelezi.
Genèse 42.19 Genèse 42.33-42.34 Jean 7.18 2 Corinthiens 6.4
12 Akawaambia, Sivyo, mmekuja ili mwuone utupu wa nchi.
13 Wakamwambia, Sisi watumwa wako tu ndugu kumi na wawili, wana wa mtu mmoja katika nchi ya Kanaani; na mdogo wetu yuko pamoja na baba yetu leo, na mmoja hayuko.
Genèse 37.30 Genèse 42.32 Genèse 44.20 Genèse 43.7 Nombres 1.1-1.54
14 Yusufu akawaambia, Ndivyo nilivyowaambia, nikisema, Wapelelezi ninyi.
Job 19.11 Matthieu 15.21-15.28 Genèse 42.9-42.11 Job 13.24
15 Mtabainika kwa njia hii; aishivyo Farao, hamtoki hapa, asipokuja huku huyo ndugu yenu mdogo.
1 Samuel 17.55 Genèse 43.3 Genèse 42.16 1 Samuel 1.26 Genèse 42.7
16 Mpelekeni mmoja wenu, aende akamlete ndugu yenu, na ninyi mtafungwa, hata maneno yenu yahakikishwe, kama mna kweli ninyi; ikiwa sivyo, aishivyo Farao, ninyi ni wapelelezi.
Genèse 42.11
17 Akawatia wote gerezani siku tatu.
Genèse 40.4 Genèse 40.7 Genèse 41.10 Esaïe 24.22 Actes 4.3
18 Yusufu akawaambia siku ya tatu, Fanyeni hivi, mkaishi, maana mimi namcha Mungu.
Lévitique 25.43 Néhémie 5.15 Genèse 20.11 Luc 18.2 Luc 18.4
19 Kama ni wa kweli ninyi ndugu yenu mmoja na afungwe gerezani, nanyi nendeni mkachukue nafaka kwa njaa ya nyumba zenu,
Genèse 42.26 Jérémie 37.15 Genèse 42.1-42.2 Genèse 43.1-43.2 Esaïe 42.7
20 mkamlete ndugu yenu mdogo kwangu; hivyo maneno yenu yatahakikishwa, wala hamtakufa. Ndivyo walivyofanya.
Genèse 43.5 Genèse 42.34 Genèse 44.23 Genèse 42.15 Genèse 6.22
21 Wakaambiana, Kweli sisi tulimkosa ndugu yetu, kwa kuwa tuliona shida ya roho yake, alipotusihi, wala hatukusikia kwa hiyo shida hii imetupata.
Osée 5.15 Genèse 37.23-37.28 Job 36.8-36.9 Proverbes 21.13 Proverbes 1.27-1.28
22 Reubeni akajibu, akawaambia, Sikuwaambia, nikisema, msimkose kijana? Wala hamkusikia; kwa hiyo damu yake inatakwa tena.
2 Chroniques 24.22 1 Rois 2.32 Psaumes 9.12 Genèse 37.21-37.22 Genèse 9.5-9.6
23 Wala hawakujua ya kwamba Yusufu anawasikia, kwa sababu alikuwapo mkalimani kati yao.
2 Corinthiens 5.20 Jean 16.13-16.14
24 Akajitenga nao akalia. Kisha akawarudia, na kusema nao, akamtwaa Simeoni miongoni mwao, akamfunga mbele ya macho yao.
Genèse 43.30 Genèse 34.25 1 Corinthiens 12.26 Luc 19.41 Hébreux 4.15
25 Yusufu akaamuru kuvijaza vyombo vyao nafaka, na kumrudishia kila mtu fedha yake katika gunia lake, na kuwapa chakula cha njiani.
1 Pierre 3.9 Genèse 45.21 Romains 12.17-12.21 Esaïe 55.1 Genèse 44.1-44.2
26 Navyo ndivyo walivyofanyiwa. Wakaweka nafaka yao juu ya punda zao, wakatoka huko.
27 Mmoja wao alipofungua gunia lake ili ampe punda wake chakula katika nyumba ya wageni, aliiona fedha yake; kumbe! Iko kinywani mwa gunia lake.
Exode 4.24 Luc 2.7 Genèse 44.11 Genèse 43.21-43.22 Luc 10.34
28 Akawaambia nduguze, Fedha yangu imerudishwa, angalia, imo humo guniani mwangu. Mioyo yao ikazimia, wakageukiana wakitetemeka, wakasema, N’nini hii Mungu aliyotutendea?
Psaumes 61.2 Lamentations 3.37 Genèse 27.33 Genèse 42.36 Luc 21.26
29 Wakaja kwa Yakobo, baba yao, katika nchi ya Kanaani, wakampasha habari za yote yaliyowapata, wakisema,
30 Mtu yule aliye bwana wa nchi alisema nasi kwa maneno makali, akatufanya tu wapelelezi wa nchi.
Genèse 42.7
31 Tukamwambia, Tu watu wa kweli sisi, wala si wapelelezi.
Genèse 42.11
32 Sisi tu ndugu kumi na wawili, wana wa baba yetu. Mmoja hayuko, na mdogo wetu yuko pamoja na baba yetu leo katika nchi ya Kanaani.
33 Yule mtu, bwana wa nchi, akatuambia, Kwa njia hii nitawajua kama ninyi ni watu wa kweli; ndugu yenu mmoja mwacheni huku kwangu, kachukueni nafaka kwa njaa ya nyumba zenu, mwende zenu.
Genèse 42.19-42.20 Genèse 42.15
34 Mkaniletee ndugu yenu mdogo; ndipo nitakapojua kama ninyi si wapelelezi, bali ni watu wa kweli; basi nitawarudishia ndugu yenu, nanyi mtafanya biashara katika nchi hii.
Genèse 34.10 Genèse 34.21 1 Rois 10.15 Ezéchiel 17.4
35 Ikawa walipomimina magunia yao, kumbe! Bahasha ya fedha ya kila mtu imo katika gunia lake. Nao walipoziona bahasha za fedha zao, wao na baba yao waliogopa.
Genèse 43.21 Genèse 43.12 Genèse 43.15 Genèse 42.27-42.28
36 Yakobo baba yao akawaambia, Mmeniondolea watoto wangu; Yusufu hayuko, wala Simeoni hayuko, na Benyamini mnataka kumchukua naye; mambo hayo yote yamenipata mimi.
Genèse 43.14 Ecclésiaste 7.8 Job 7.7 Esaïe 41.13-41.14 Genèse 45.28
37 Reubeni akamwambia babaye, akasema, Uwaue wanangu wawili nisipomrudisha kwako; mtie katika mikono yangu, nami nitamrudisha kwako.
Genèse 46.9 Genèse 44.32-44.34 Genèse 43.9 Michée 6.7
38 Akasema, Mwanangu hatashuka pamoja nanyi, maana nduguye amekufa, naye amesalia peke yake; mabaya yakimpata katika njia mtakayoiendea ndipo mtakaposhusha mvi zangu kwa sikitiko mpaka kaburini.
Genèse 37.35 Genèse 37.33 Genèse 42.4 Genèse 42.13 Genèse 35.16-35.18

Cette Bible est dans le domaine public.