Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 39.14
Bible en Swahili de l’est


Joseph chez Potiphar

1 Basi Yusufu akaletwa mpaka Misri naye Potifa, akida wa Farao, mkuu wa askari, mtu wa Misri, akamnunua mkononi mwa hao Waishmaeli waliomleta huko.
Genèse 37.25 Genèse 37.36 Genèse 37.28 Psaumes 105.17 Genèse 45.4
2 Bwana akawa pamoja na Yusufu, naye akasitawi; naye alikuwa katika nyumba ya bwana wake, yule Mmisri.
1 Samuel 18.14 Genèse 21.22 Genèse 26.28 Genèse 26.24 Jérémie 15.20
3 Bwana wake akaona ya kwamba Bwana yu pamoja naye, na ya kuwa Bwana anafanikisha mambo yote mkononi mwake.
Psaumes 1.3 Genèse 26.28 Genèse 21.22 Genèse 30.27 2 Chroniques 26.5
4 Yusufu akaona neema machoni pake, akamtumikia. Naye akamweka awe msimamizi juu ya nyumba yake, na yote yaliyomo akayaweka mkononi mwake.
Genèse 19.19 Genèse 18.3 Genèse 33.10 Genèse 24.2 Genèse 39.8
5 Ikawa tokea wakati alipomweka awe msimamizi juu ya nyumba yake, na vyote vilivyomo, Bwana akabariki nyumba ya yule Mmisri kwa ajili ya Yusufu. Mbaraka wa Bwana ukawa juu ya vyote alivyokuwa navyo katika nyumba, na katika shamba.
Genèse 30.27 Psaumes 21.6 Genèse 19.29 Genèse 12.2 Psaumes 72.17
6 Akayaacha yote aliyokuwa nayo mkononi mwa Yusufu; wala hakujua habari za kitu cho chote chake, ila hicho chakula alichokula tu.
1 Samuel 16.12 Genèse 29.17 1 Samuel 17.42 Actes 7.20 Genèse 39.8
7 Ikawa baada ya mambo hayo, mke wa bwana wake akamtamani Yusufu, akamwambia, Lala nami.
2 Samuel 13.11 Ezéchiel 23.12-23.16 Ezéchiel 23.5-23.6 Proverbes 5.9 Genèse 6.2
8 Lakini akakataa, akamwambia mke wa bwana wake, Tazama, bwana wangu hajui kitu kilichowekwa kwangu nyumbani, na vyote alivyo navyo amevitia mkononi mwangu.
Proverbes 2.16-2.19 Proverbes 7.5 Proverbes 6.20-6.25 Proverbes 7.25-7.27 Proverbes 5.3-5.8
9 Hakuna mkuu katika nyumba hii kuliko mimi, wala hakunizuilia kitu cho chote ila wewe, kwa kuwa wewe u mkewe. Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu?
Genèse 42.18 2 Samuel 12.13 Genèse 20.6 Psaumes 51.4 Jérémie 50.7
10 Akawa akizidi kusema na Yusufu siku baada ya siku, lakini hakumsikia alale naye, wala aongee naye.
1 Corinthiens 6.18 Proverbes 6.25-6.26 1 Thessaloniciens 5.22 1 Corinthiens 15.33 Proverbes 5.3
11 Ikawa, siku moja, akaingia nyumbani atende kazi yake, wala hapakuwa na mtu katika watu wa nyumbani humo ndani;
Ephésiens 5.12 Ephésiens 5.3 Jérémie 23.24 Proverbes 9.17 Job 24.15
12 huyo mwanamke akamshika nguo zake, akisema, Lala nami. Yusufu akaiacha nguo yake mkononi mwake, akakimbia, akatoka nje.
Ecclésiaste 7.26 Proverbes 5.8 Proverbes 7.13-7.27 2 Timothée 2.22 Proverbes 6.5
13 Ikawa alipoona ya kwamba amemwachilia nguo yake mkononi mwake, naye amekimbia nje,
14 akawaita watu wa nyumbani mwake, akasema nao, akinena, Angalieni, ametuletea mtu Mwebrania atufanyie dhihaka. Ameingia kwangu, ili alale nami, nikalia kwa sauti kuu.
Esaïe 51.7 Genèse 10.21 Matthieu 26.59 Genèse 40.15 Esaïe 54.17
15 Ikawa, aliposikia ya kuwa nimepaza sauti yangu na kulia, aliiacha nguo yake kwangu, akakimbia, akatoka nje.
16 Basi akaiweka ile nguo kwake hata bwana wake aje nyumbani.
Psaumes 37.12 Tite 3.3 Jérémie 4.22 Psaumes 37.32 Jérémie 9.3-9.5
17 Naye akamwambia kama maneno hayo, akisema, Yule mtumwa Mwebrania uliyemleta kwetu, aliingia kwangu anidhihaki.
Exode 23.1 Exode 20.16 Psaumes 55.3 Genèse 39.14 1 Rois 21.9-21.13
18 Ikawa nilipopaza sauti yangu, nikalia, akaacha nguo yake kwangu akakimbia nje.
19 Ikawa bwana wake aliposikia maneno ya mkewe aliyomwambia, akisema, Mtumwa wako amenitendea mambo kama haya, hasira yake ikawaka.
2 Thessaloniciens 2.11 Proverbes 29.12 Job 29.16 Proverbes 18.17 Proverbes 6.34-6.35
20 Bwana wake akamtwaa Yusufu, akamtia gerezani, mahali walipofungwa wafungwa wa mfalme, naye akawamo humo gerezani.
Genèse 40.15 Psaumes 105.18-105.19 2 Timothée 2.9 Esaïe 53.8 Genèse 41.9-41.14

Joseph en prison

21 Lakini Bwana akawa pamoja na Yusufu, akamfadhili, akampa kibali machoni pa mkuu wa gereza.
Exode 3.21 Genèse 39.2 Exode 11.3 Actes 7.9-7.10 Psaumes 105.19
22 Mkuu wa gereza akawatia mkononi mwa Yusufu watu wote waliofungwa, waliomo gerezani; na yote yaliyofanyika humo ndiye aliyeyafanya.
Genèse 39.4 Genèse 40.3-40.4 Psaumes 37.11 Psaumes 37.3 Genèse 39.9
23 Wala mkuu wa gereza hakuangalia neno lililoko mkononi mwa Yusufu; kwa kuwa Bwana alikuwa pamoja naye. Bwana akayafanikisha yote aliyoyafanya.
Genèse 39.2-39.3 Psaumes 1.3 Esaïe 43.2 1 Samuel 2.30 Daniel 6.22

Cette Bible est dans le domaine public.