Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 31.39
Bible en Swahili de l’est


1 Basi Yakobo akasikia maneno ya wana wa Labani, wakisema, Yakobo amechukua mali yote ya baba yetu; na kwa mali ya baba yetu amepata fahari hii yote.
Ecclésiaste 4.4 Proverbes 27.4 Jérémie 9.23 Esther 5.11 Matthieu 4.8
2 Yakobo akaona uso wa Labani, ya kuwa hakumtazama vema kama jana na juzi.
Genèse 4.5 Exode 4.10 Daniel 3.19 Deutéronome 28.54 Deutéronome 19.4
3 Bwana akamwambia Yakobo, Urudi mpaka nchi ya baba zako na kwa jamaa zako, nami nitakuwa pamoja nawe.
Genèse 28.15 Genèse 32.9 Genèse 31.13 Genèse 21.22 Genèse 35.1
4 Yakobo akatuma watu, akawaita Raheli na Lea waje nyikani kwenye wanyama wake. Akawaambia,
5 Naona uso wa baba yenu, kwamba hanitazami vema kama jana na juzi. Lakini Mungu wa baba yangu amekuwa pamoja nami.
Genèse 31.2-31.3 Genèse 31.53 Genèse 31.42 Genèse 31.13 Genèse 48.15
6 Nanyi mmejua ya kwamba kwa nguvu zangu zote nimemtumikia baba yenu.
Genèse 30.29 Tite 2.9-2.10 Genèse 31.38-31.42 Ephésiens 6.5-6.8 1 Pierre 2.18
7 Na baba yenu amenidanganya, akabadili mshahara wangu mara kumi; lakini Mungu hakumwacha kunidhuru.
Néhémie 4.12 Zacharie 8.23 Psaumes 37.28 Genèse 31.29 Genèse 31.41
8 Aliposema, Walio na madoadoa watakuwa mshahara wako, wanyama wote wakazaa madoadoa. Aliposema, Walio na milia watakuwa mshahara wako, ndipo wanyama wote wakazaa wenye milia.
Genèse 30.32
9 Hivi Mungu akamnyang’anya mali yake baba yenu, na kunipa mimi.
Genèse 31.1 Genèse 31.16 Proverbes 13.22 Psaumes 50.10 Matthieu 20.15
10 Ikawa, wakati wale wanyama walipochukua mimba, naliinua macho yangu nikaona katika ndoto, na tazama, mabeberu waliowapanda hao wanyama walikuwa na milia, na madoadoa, na marakaraka.
Deutéronome 13.1 Genèse 28.12 1 Rois 3.5 Nombres 12.6 Genèse 30.39
11 Na malaika wa Mungu akaniambia katika ndoto, Yakobo! Nikasema, Mimi hapa.
Esaïe 58.9 Genèse 31.13 1 Samuel 3.16 Genèse 18.1 1 Samuel 3.8
12 Akasema, Inua, basi, macho yako, ukaone; mabeberu wote wanaopanda wanyama wana milia, na madoadoa, na marakaraka; maana nimeona yote aliyokutendea Labani.
Exode 3.7 Psaumes 12.5 Deutéronome 24.15 Exode 3.9 Psaumes 139.3
13 Mimi ni Mungu wa Betheli, huko ulikotia mafuta nguzo, na kuniwekea nadhiri. Sasa ondoka, toka katika nchi hii, urudi mpaka nchi ile uliyozaliwa.
Genèse 31.3 Genèse 32.9 Genèse 28.12-28.22 Genèse 35.7
14 Raheli na Lea wakajibu, wakamwambia, Je! Imetubakia sehemu au urithi katika nyumba ya baba yetu?
Genèse 29.29 Ruth 4.11 Genèse 29.24 Genèse 2.24
15 Hakutufanya kama wageni, maana ametuuza, naye amekula fedha zetu kabisa?
Genèse 30.26 Genèse 29.15-29.20 Exode 21.7-21.11 Genèse 29.27-29.30 Genèse 31.41
16 Maana mali yote ambayo Mungu amemnyang’anya baba yetu, mali hiyo ndiyo yetu na ya wana wetu. Basi yo yote Mungu aliyokuambia, uyafanye.
Genèse 31.9 Genèse 30.35-31.1 Psaumes 45.10
17 Ndipo Yakobo akaondoka, akapandisha wanawe na wakeze juu ya ngamia.
1 Samuel 30.17 Genèse 24.61 Genèse 24.10
18 Akachukua wanyama wake wote, na mali yake yote aliyokuwa ameyapata, na wanyama aliowapata katika Padan-aramu, ili afike kwa Isaka babaye katika nchi ya Kanaani.
Genèse 27.1-27.2 Genèse 28.21 Genèse 35.27-35.29 Genèse 27.41
19 Basi Labani alikuwa amekwenda kuwakata manyoya kondoo zake, na Raheli akaviiba vinyago vya babaye.
Genèse 31.30 Osée 3.4 1 Samuel 19.13 Genèse 35.2 Genèse 31.34
20 Yakobo akamhadaa Labani, Mshami, kwa kuwa hakumwambia ya kwamba anakimbia.
21 Basi akakimbia yeye na yote aliyokuwa nayo; akaondoka akauvuka mto, akaelekeza uso wake kwenda mlima wa Gileadi.
2 Rois 12.17 Genèse 15.18 Nombres 32.1 Josué 24.2-24.3 Genèse 31.23

Jacob poursuivi par Laban

22 Hata siku ya tatu Labani akaambiwa ya kwamba Yakobo amekimbia,
Job 5.12-5.13 Genèse 30.36 Exode 14.5-14.31
23 akatwaa ndugu zake pamoja naye, akamfuata mwendo wa siku saba. Akampata katika mlima wa Gileadi.
Exode 2.13 Exode 2.11 Genèse 13.8 Genèse 24.27
24 Mungu akamjia Labani, Mshami, katika ndoto ya usiku, akamwambia, Ujihadhari, usimwambie Yakobo neno la heri wala la shari.
Genèse 20.3 Genèse 24.50 Genèse 31.29 Genèse 31.42 Nombres 24.13
25 Labani akamfikia Yakobo, na Yakobo alikuwa amepiga hema zake katika mlima, na Labani na ndugu zake wakapiga hema zao katika mlima wa Gileadi.
Genèse 33.18 Genèse 12.8 Hébreux 11.9
26 Labani akamwambia Yakobo, Umefanya nini? Umenihadaa, ukawachukua binti zangu kama mateka waliotwaliwa kwa upanga.
1 Samuel 30.2 Genèse 2.24 Genèse 31.16 Genèse 4.10 1 Samuel 14.43
27 Mbona umekimbia kwa siri ukanihadaa, wala hukuniambia, nipate kuagana nawe uende zako kwa furaha, na nyimbo, na ngoma, na kinubi?
Exode 15.20 Proverbes 26.23-26.26 Juges 6.27 Genèse 31.20-31.21 Job 21.11-21.14
28 Wala hukuniacha niwabusu wanangu, na binti zangu; basi umetenda upumbavu.
Genèse 31.55 Ruth 1.14 Ruth 1.9 Actes 20.37 1 Rois 19.20
29 Ninao uwezo mkononi mwangu wa kukufanyia madhara; lakini Mungu wa baba yako usiku huu ameniambia, akisema, Ujihadhari, usimwambie Yakobo neno la heri wala la shari.
Genèse 31.53 Genèse 31.42 Genèse 28.13 Genèse 31.24 Actes 5.38-5.39
30 Basi sasa, umetoka kwa sababu umetamani sana nyumba ya baba yako. Mbona basi umeiiba miungu yangu?
Genèse 31.19 Juges 18.24 Esaïe 46.1-46.2 Exode 12.12 Jérémie 43.12
31 Yakobo akajibu, akamwambia Labani, Kwa sababu naliogopa, nikasema, Usije ukaninyang’anya binti zako kwa nguvu.
Proverbes 29.25 Genèse 20.11 Genèse 31.26-31.27
32 Awaye yote utakayemwona kuwa nayo miungu yako, yeye asiishi. Mbele ya ndugu zetu ukitambue kilicho chako kwangu, ukakichukue. Maana Yakobo hakujua ya kwamba Raheli ameiiba.
Genèse 30.33 Genèse 31.23 Genèse 31.19 Genèse 31.30 1 Samuel 12.3-12.5
33 Labani akaingia katika hema ya Yakobo, na hema ya Lea, na hema ya vijakazi wawili, wala hakuiona. Akatoka katika hema ya Lea, akaingia katika hema ya Raheli.
Genèse 24.28 Genèse 24.67
34 Basi Raheli alikuwa amevitwaa vile vinyago ameviweka katika matandiko ya ngamia, na kuvikalia. Labani akapapasa hema yote wala hakuviona.
Genèse 31.17 Genèse 31.19
35 Naye Raheli akamwambia babaye, Bwana wangu asikasirike kwa sababu siwezi kuinuka mbele yako, maana nimeshikwa na mambo ya kike. Akatafuta, wala hakuviona vile vinyago.
Lévitique 19.32 Exode 20.12 Lévitique 19.3 Genèse 18.11-18.12 1 Pierre 3.6
36 Yakobo akakasirika, akagombana na Labani. Yakobo akajibu, akamwambia Labani, N’nini hatia yangu? Nayo ni nini dhambi yangu, hata ukanifuatia namna hii?
2 Rois 13.19 Genèse 30.2 Marc 3.5 Nombres 16.15 Ephésiens 4.26
37 Umepapasa-papasa vyombo vyangu vyote; ni kitu gani ulichokiona cha nyumbani mwako? Kiweke hapa mbele ya ndugu zangu, na ndugu zako, wakaamue kati yetu.
1 Thessaloniciens 2.10 1 Pierre 3.16 Josué 7.23 Hébreux 13.18 1 Pierre 2.12
38 Miaka hii ishirini nimekaa kwako; kondoo zako wala mbuzi zako wake hawakuharibu mimba wala waume katika wanyama wako sikuwala.
Genèse 30.30 Deutéronome 28.4 Genèse 30.27 Ezéchiel 34.2-34.4 Exode 23.26
39 Kilichoraruliwa na hayawani sikukuletea, mimi mwenyewe nimetwaa hasara yake, wewe umekidai katika mkono wangu, ikiwa kilichukuliwa mchana, au ikiwa kilichukuliwa usiku.
Exode 22.31 Exode 22.10-22.13 Lévitique 22.8 1 Samuel 17.34-17.35 Luc 2.8
40 Hii ilikuwa hali yangu; mchana jua likanipata, na baridi usiku, usingizi ukanitoka machoni mwangu.
Luc 2.8 Osée 12.12 Exode 2.19-2.22 Psaumes 78.70-78.71 1 Pierre 5.2-5.4
41 Miaka hii ishirini nimekaa nyumbani mwako; nilikutumikia miaka kumi na minne kwa binti zako wawili, na miaka sita kwa wanyama wako, nawe umebadili mshahara wangu mara kumi.
Genèse 31.7 2 Corinthiens 11.26 Genèse 31.38 1 Corinthiens 15.10 Genèse 30.33-30.40
42 Kama Mungu wa baba yangu, Mungu wa Ibrahimu na Hofu ya Isaka, hangalikuwa pamoja nami, hakika sasa ungalinifukuza mikono mitupu. Mateso yangu na kazi za mikono yangu Mungu ameziona, akakukemea usiku huu.
Genèse 31.53 Genèse 31.29 Genèse 29.32 Esaïe 8.13 Psaumes 124.1-124.3
43 Labani akajibu, akamwambia Yakobo, Hao binti ni binti zangu, na wana ni wanangu, na wanyama ni wanyama wangu, na yote uyaonayo ni yangu; nami naweza kuwatendea nini leo binti zangu na wana wao waliowalea?
44 Haya! Na tufanye agano, mimi na wewe, liwe kwa ushahidi kati ya mimi na wewe.
Genèse 31.52 Josué 24.25-24.27 Genèse 15.18 Genèse 26.28-26.31 Deutéronome 31.21
45 Yakobo akatwaa jiwe akalisimamisha kama nguzo.
Genèse 28.18-28.22
46 Yakobo akawaambia ndugu zake, Kusanyeni mawe. Wakatwaa mawe, wakafanya chungu, nao wakala huko karibu na ile chungu.
Genèse 31.37 Genèse 31.32 Josué 4.5-4.9 2 Samuel 18.17 Genèse 31.54
47 Labani aliiita Yegarsahadutha, lakini Yakobo aliiita Galedi.
Hébreux 12.1
48 Labani akasema, Chungu hii ni shahidi kati ya mimi na wewe hivi leo. Kwa hiyo likaitwa jina lake Galedi,
Josué 24.27 Deutéronome 3.16 Deutéronome 2.36 Josué 13.8-13.9 Genèse 31.23
49 na Mispa, maana alisema, Mungu avizie kati ya mimi na wewe, wakati tusipoonana.
Juges 11.29 1 Rois 15.22 1 Samuel 7.5-7.6 Juges 10.17 Osée 5.1
50 Ukiwatesa binti zangu, na ukitwaa wake zaidi ya binti zangu, wala hapana mtu pamoja nasi, tazama, Mungu ni shahidi kati ya mimi na wewe.
Jérémie 42.5 Jérémie 29.23 1 Samuel 12.5 Juges 11.10 Michée 1.2
51 Labani akamwambia Yakobo, Tazama chungu hii utazame na nguzo niliyoitia kati ya mimi na wewe.
52 Chungu hii na iwe shahidi, na nguzo hii na iwe shahidi, ya kuwa mimi sitapita chungu hii kuja kwako, wala wewe hutapita chungu hii na nguzo hii uje kwangu, kwa madhara.
Genèse 31.48 Genèse 31.44-31.45
53 Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Nahori, Mungu wa baba yao, ahukumu kati yetu.
Genèse 31.42 Genèse 16.5 Josué 24.2 Exode 3.6 Genèse 11.24-11.29
54 Yakobo akachinja sadaka katika mlima, akawaita ndugu zake waje wale chakula, nao wakala chakula, wakakaa usiku kucha mlimani.
Exode 18.12 2 Samuel 3.20-3.21 Genèse 37.25 Genèse 21.8 Genèse 26.30
55 Labani akaondoka asubuhi na mapema, akawabusu wanawe na binti zake, akawabariki; kisha Labani akaenda zake, akarudi kwao.
Genèse 31.28 Genèse 30.25 Genèse 18.33 Ruth 1.14 Proverbes 16.7

Cette Bible est dans le domaine public.