Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 21.11
Bible en Swahili de l’est


1 Basi Daudi akaenda Nobu kwa Ahimeleki, kuhani. Ahimeleki akaenda kumlaki Daudi, akitetemeka, akamwambia, Kwani wewe kuwa peke yako, wala hapana mtu pamoja nawe?
Néhémie 11.32 Esaïe 10.32 1 Samuel 16.4 1 Samuel 14.3 Marc 2.26

Fuite de David à Nob et à Gath

2 Daudi akamwambia Ahimeleki, kuhani, Mfalme ameniagiza shughuli, akaniambia, Asijue mtu awaye yote habari ya shughuli hii ninayokutuma, wala ya neno hili ninalokuamuru; nami nimewaagiza vijana waende mahali fulani.
Psaumes 119.29 1 Rois 13.18 Genèse 27.24 1 Samuel 19.17 Colossiens 3.9
3 Kuna nini basi, chini ya mkono wako? Nipe mkononi mwangu mikate mitano, au cho chote ulicho nacho hapa.
1 Samuel 21.4 Esaïe 3.6 Juges 9.29
4 Yule kuhani akamjibu Daudi, akasema, Hapana mikate ya sikuzote chini ya mkono wangu, ila mikate mitakatifu; ikiwa wale vijana wamejitenga na wanawake.
Exode 25.30 Exode 19.15 Matthieu 12.3-12.4 Lévitique 24.5-24.9 Zacharie 7.3
5 Naye Daudi akamjibu kuhani, akamwambia, Hakika tumejitenga na wanawake siku hizi tatu; napo nilipotoka, vyombo vya vijana hawa vilikuwa vitakatifu, ingawa ilikuwa safari ya sikuzote; basi leo je! Vyombo vyetu havitakuwa vitakatifu zaidi?
2 Timothée 2.20-2.21 1 Thessaloniciens 4.3-4.4 Actes 9.15 1 Pierre 3.17 Lévitique 8.26
6 Ndipo kuhani akampa ile mikate mitakatifu; kwa maana hapakuwa na mikate ila ile ya Wonyesho, nayo imekwisha kuondolewa mbele za Bwana, ili itiwe mikate ya moto siku ile ilipoondolewa.
Matthieu 12.3-12.4 Luc 6.3-6.4 Marc 2.25-2.27 Lévitique 24.5-24.9
7 Basi siku ile palikuwapo na mtu mmoja wa watumishi wa Sauli, amezuiwa hapo mbele za Bwana jina lake akiitwa Doegi, Mwedomi, mkubwa wa wachungaji wa Sauli.
1 Samuel 22.9 Psaumes 52.1-52.9 1 Chroniques 27.29 Jérémie 7.9-7.11 Genèse 13.7-13.8
8 Tena Daudi akamwambia Ahimeleki, Na hapa chini ya mkono wako, je! Hapana mkuki, au upanga? Kwa maana sikuleta upanga, wala silaha zangu, kwa sababu ile shughuli ya mfalme ilitaka haraka.
9 Yule kuhani akasema, upanga wa Goliathi, yule Mfilisti, uliyemwua katika bonde la Ela, tazama, upo hapa, umefungwa ndani ya nguo nyuma ya naivera; ukipenda kuuchukua, haya! Uchukue, maana hapa hapana mwingine ila huo tu. Daudi akasema, Hapana mwingine kama ule; haya! Nipe.
1 Samuel 17.2 Exode 28.6-28.14 1 Samuel 31.10 1 Samuel 17.50-17.54
10 Basi Daudi akaondoka, akakimbia siku ile, kwa hofu ya Sauli, akamwendea Akishi, mfalme wa Gathi.
Psaumes 34.1-34.22 1 Rois 19.3 Jérémie 26.21 1 Samuel 27.1-27.2
11 Nao watumishi wa Akishi wakamwambia, Je! Huyu siye yule Daudi, mfalme wa nchi? Je! Hawakuimbiana habari zake katika ngoma zao, kusema,Sauli amewaua elfu zake,Na Daudi makumi elfu yake.
1 Samuel 29.5 1 Samuel 16.1 Psaumes 56.1-56.13 1 Samuel 18.7-18.8
12 Naye Daudi akayatia maneno hayo moyoni mwake, akamwogopa sana Akishi, mfalme wa Gathi.
Luc 2.19 Psaumes 119.11 Genèse 12.11-12.13 Psaumes 56.3 Luc 2.51
13 Akaubadilisha mwenendo wake mbele yao, akajifanya mwenye wazimu mikononi mwao, akakuna-kuna katika mbao za mlango, na kuyaacha mate yake kuanguka juu ya ndevu zake.
Proverbes 29.25 Ecclésiaste 7.7 Psaumes 34.1-34.22
14 Ndipo huyo Akishi akawaambia watumishi wake, Angalieni, mwaona ya kuwa mtu huyu ana wazimu; basi, maana yake nini kumleta kwangu?
Ecclésiaste 7.7
15 Je! Mimi nina haja ya watu wenye wazimu, hata mmemleta kiumbe hiki ili aonyeshe wazimu wake machoni pangu? Je! Huyu ataingia nyumbani mwangu?

Cette Bible est dans le domaine public.