Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Apocalypse 9.21
Bible en Swahili de l’est


1 Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu.
Apocalypse 8.10 Luc 8.31 Apocalypse 9.2 Apocalypse 1.18 Romains 10.7
2 Akalifungua shimo la kuzimu; moshi ukapanda kutoka mle shimoni kama moshi wa tanuru kubwa; jua na anga vikatiwa giza kwa sababu ya ule moshi wa shimoni.
Genèse 19.28 Joël 2.2 Joël 2.10 Apocalypse 14.11 Esaïe 14.31
3 Nzige wakatoka katika ule moshi, wakaenda juu ya nchi, wakapewa nguvu kama nguvu waliyo nayo nge wa nchi.
Apocalypse 9.5 Ezéchiel 2.6 Deutéronome 8.15 Joël 2.25 Exode 10.4-10.15
4 Wakaambiwa wasiyadhuru majani ya nchi, wala kitu cho chote kilicho kibichi, wala mti wo wote, ila wale watu wasio na muhuri ya Mungu katika vipaji vya nyuso zao.
Apocalypse 6.6 Apocalypse 8.7 Ezéchiel 9.4 Apocalypse 7.2-7.4 Exode 12.23
5 Wakapewa amri kwamba wasiwaue, bali wateswe miezi mitano. Na maumivu yao yalikuwa kama kuumwa na nge, aumapo mwanadamu.
Apocalypse 9.10 Apocalypse 9.3 Job 2.6 Apocalypse 13.7 Apocalypse 11.7
6 Na siku zile wanadamu watatafuta mauti, wala hawataiona kamwe. Nao watatamani kufa, nayo mauti itawakimbia.
Jérémie 8.3 Apocalypse 6.16 Job 7.15-7.16 Job 3.20-3.22 Luc 23.30
7 Na maumbo ya hao nzige yalikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita, na juu ya vichwa vyao kama taji, mfano wa dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama nyuso za wanadamu.
Daniel 7.8 Nahum 3.17 Joël 2.4-2.5 Daniel 7.4
8 Nao walikuwa na nywele kama nywele za wanawake. Na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.
Joël 1.6 1 Pierre 3.3 1 Timothée 2.9 Esaïe 3.24 1 Corinthiens 11.14-11.15
9 Nao walikuwa na dirii kifuani kama dirii za chuma. Na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari, ya farasi wengi waendao kasi vitani.
Job 39.25 Joël 2.5-2.8 Esaïe 9.5 Apocalypse 9.17 Job 41.23-41.30
10 Nao wana mikia kama ya nge, na miiba; na nguvu yao ya kuwadhuru wanadamu miezi mitano ilikuwa katika mikia yao.
Apocalypse 9.5 Apocalypse 9.3 Apocalypse 9.19
11 Na juu yao wanaye mfalme, naye ni malaika wa kuzimu, jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kiyunani analo jina lake Apolioni.
Ephésiens 2.2 2 Corinthiens 4.4 Jean 14.30 Job 26.6 1 Jean 4.4
12 Ole wa kwanza umekwisha pita. Tazama, bado ziko ole mbili, zinakuja baadaye.
Apocalypse 11.14 Apocalypse 8.13-9.2 Apocalypse 9.13-9.21
13 Malaika wa sita akapiga baragumu, nikasikia sauti moja iliyotoka katika zile pembe za madhabahu ya dhahabu iliyo mbele za Mungu,
Apocalypse 8.3-8.5 Hébreux 10.21 Apocalypse 9.1 Exode 30.2-30.3 Hébreux 9.24
14 ikimwambia yule malaika wa sita aliyekuwa na baragumu, Wafungue nao malaika wanne waliofungwa kwenye mto mkubwa Frati.
Apocalypse 16.12 Apocalypse 9.15 Apocalypse 8.6 Jérémie 51.63 Genèse 2.14
15 Wale malaika wanne wakafunguliwa, waliokuwa wamewekwa tayari kwa ile saa na siku na mwezi na mwaka, ili kwamba waue theluthi ya wanadamu.
Apocalypse 8.7 Apocalypse 9.18 Apocalypse 8.11-8.12 Apocalypse 8.9 Apocalypse 9.5
16 Na hesabu ya majeshi ya wapanda farasi ilikuwa elfu ishirini mara elfu kumi; nilisikia hesabu yao.
Apocalypse 7.4 Ezéchiel 38.4 Daniel 7.10 Psaumes 68.17 Apocalypse 5.11
17 Hiyo ndivyo nilivyowaona hao farasi katika maono yangu, nao waliokaa juu yao, wana dirii kifuani, kama za moto, na za samawi, na za kiberiti; na vichwa vya farasi hao ni kama vichwa vya simba, na katika vinywa vyao hutoka moto na moshi na kiberiti.
Apocalypse 14.10 Apocalypse 9.18 Apocalypse 21.8 Esaïe 5.28-5.29 1 Chroniques 12.8
18 Theluthi ya wanadamu wakauawa kwa mapigo matatu hayo, kwa moto huo na moshi huo na kiberiti hicho, yaliyotoka katika vinywa vyao.
Apocalypse 9.15 Apocalypse 9.17
19 Kwa maana nguvu za hao farasi ni katika vinywa vyao, na katika mikia yao; maana mikia yao ni mfano wa nyoka, ina vichwa, nao wanadhuru kwa hivyo.
Esaïe 9.15 Ephésiens 4.14 Apocalypse 9.10
20 Na wanadamu waliosalia, wasiouawa kwa mapigo hayo, hawakuzitubia zile kazi za mikono yao, hata wasiwasujudie mashetani, na sanamu za dhahabu na za fedha na za shaba na za mawe na za miti, zisizoweza kuona wala kusikia wala kuenenda.
Daniel 5.23 Deutéronome 31.29 Actes 7.41 Apocalypse 16.8 Jérémie 10.3-10.5
21 Wala hawakuutubia uuaji wao, wala uchawi wao, wala uasherati wao, wala wivi wao.
Apocalypse 21.8 Apocalypse 17.2 Apocalypse 17.5 Esaïe 47.12 Apocalypse 22.15

Cette Bible est dans le domaine public.