Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ephésiens 5.5
Bible en Swahili de l’est


1 Hivyo mfuateni Mungu, kama watoto wanaopendwa;
Matthieu 5.48 1 Pierre 1.15-1.16 Colossiens 3.12 Ephésiens 4.32 1 Jean 4.11
2 mkaenende katika upendo, kama Kristo naye alivyowapenda ninyi tena akajitoa kwa ajili yetu, sadaka na dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukato.
Jean 13.34 Colossiens 3.14 Galates 2.20 Jean 15.12-15.13 Matthieu 20.28
3 Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu;
Colossiens 3.5 Ephésiens 5.5 Galates 5.19-5.21 1 Corinthiens 6.18 1 Corinthiens 6.13
4 wala aibu wala maneno ya upuzi wala ubishi; hayo hayapendezi; bali afadhali kushukuru.
Colossiens 3.8 Ephésiens 4.29 Jacques 3.4-3.8 Psaumes 107.21-107.22 2 Corinthiens 9.15
5 Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu.
Galates 5.21 Colossiens 3.5 1 Corinthiens 6.9-6.10 Ephésiens 5.3 Apocalypse 21.8
6 Mtu asiwadanganye kwa maneno yasiyo na maana; kwa kuwa kwa sababu ya hayo hasira ya Mungu huwajia wana wa uasi.
Romains 1.18 Colossiens 2.8 Colossiens 3.6 Matthieu 24.4 Galates 6.7-6.8
7 Basi msishirikiane nao.
Nombres 16.26 Proverbes 9.6 Psaumes 50.18 Proverbes 1.10-1.17 Ephésiens 3.6
8 Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika Bwana; enendeni kama watoto wa nuru,
Jean 8.12 Actes 26.18 1 Pierre 2.9-2.11 1 Jean 1.7 Luc 16.8
9 kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli;
Romains 15.14 Ephésiens 6.14 Ephésiens 4.25 Hébreux 1.8 1 Pierre 2.24-2.25
10 mkihakiki ni nini impendezayo Bwana.
Romains 12.1-12.2 Hébreux 12.28 1 Thessaloniciens 5.21 1 Timothée 5.4 Philippiens 4.18
11 Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee;
1 Timothée 5.20 Romains 13.12 2 Thessaloniciens 3.6 Romains 6.21 Romains 16.17
12 kwa kuwa yanayotendeka kwao kwa siri, ni aibu hata kuyanena.
1 Pierre 4.3 Romains 2.16 Ephésiens 5.3 Romains 1.24-1.27 Luc 12.1-12.2
13 Lakini yote yaliyokemewa hudhihirishwa na nuru maana kila kilichodhihirika ni nuru.
Jean 3.20-3.21 Osée 2.10 Lamentations 2.14 Osée 7.1 Hébreux 1.13
14 Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza.
Esaïe 60.1 Esaïe 26.19 1 Thessaloniciens 5.6 Romains 13.11-13.12 Esaïe 52.1
15 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;
Colossiens 4.5 Philippiens 1.27 1 Timothée 6.9 Apocalypse 19.10 1 Pierre 1.22
16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.
Colossiens 4.5 Amos 5.13 Ecclésiaste 12.1 Ephésiens 6.13 Galates 6.10
17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.
Romains 12.2 Colossiens 1.9 1 Thessaloniciens 4.1-4.3 Jérémie 4.22 1 Thessaloniciens 5.18

Les relations mutuelles

18 Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;
Proverbes 20.1 1 Corinthiens 5.11 Esaïe 5.22 Romains 13.13 Luc 1.15
19 mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;
Colossiens 3.16 1 Corinthiens 14.26 Actes 16.25 Jacques 5.13 Jean 4.23-4.24
20 na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;
Colossiens 3.17 1 Thessaloniciens 5.18 2 Thessaloniciens 1.3 Ephésiens 5.4 Hébreux 13.15
21 hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo.
Philippiens 2.3 Ephésiens 5.22 1 Pierre 5.5 Ephésiens 5.24 Hébreux 13.17
22 Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu.
Colossiens 3.18-4.1 1 Pierre 3.1-3.6 Genèse 3.16 Tite 2.5 Ephésiens 5.22-6.9
23 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili.
1 Corinthiens 11.3-11.10 Colossiens 1.18 Ephésiens 1.22-1.23 Ephésiens 4.15 Apocalypse 5.9
24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.
Ephésiens 5.33 Tite 2.9 Exode 23.13 Colossiens 3.22 Tite 2.7
25 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;
1 Pierre 3.7 Colossiens 3.19 Ephésiens 5.28 Genèse 2.24 Ephésiens 5.2
26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;
Jean 15.3 Jean 3.5 1 Corinthiens 6.11 Tite 2.14 Ezéchiel 36.25
27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa.
2 Corinthiens 11.2 Colossiens 1.22 Ephésiens 1.4 Colossiens 1.28 Jude 1.24
28 Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.
Ephésiens 5.25 Ephésiens 5.33 Genèse 2.21-2.24 Ephésiens 5.31 Matthieu 19.5
29 Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa.
Proverbes 11.17 Ecclésiaste 4.5 Ezéchiel 34.14-34.15 Matthieu 23.37 Esaïe 40.11
30 Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake.
1 Corinthiens 6.15 Ephésiens 1.23 1 Corinthiens 12.12-12.27 Genèse 2.23 Colossiens 2.19
31 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja.
Genèse 2.24 Matthieu 19.5 Marc 10.7-10.8 1 Corinthiens 6.16
32 Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa.
2 Corinthiens 11.2 Esaïe 54.5 Apocalypse 21.2 Colossiens 2.2 Esaïe 62.4-62.5
33 Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.
Ephésiens 5.25 Colossiens 3.19 1 Pierre 3.2-3.7 Esther 1.20 Hébreux 12.9

Cette Bible est dans le domaine public.