Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Galates 4.26
Bible en Swahili de l’est


1 Lakini nasema ya kuwa mrithi, wakati wote awapo mtoto, hana tofauti na mtumwa, angawa ni bwana wa yote;
Galates 4.29 Galates 4.23 2 Rois 10.1-10.2 2 Rois 11.12 Genèse 24.2-24.3
2 bali yu chini ya mawakili na watunzaji, hata wakati uliokwisha kuamriwa na baba.
3 Kadhalika na sisi, tulipokuwa watoto, tulikuwa tukitumikishwa na kawaida za kwanza za dunia.
Galates 4.9 Galates 2.4 Colossiens 2.8 Colossiens 2.20 Galates 4.31-5.1
4 Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria,
Marc 1.15 Jean 1.14 Ephésiens 1.10 Luc 1.35 Luc 2.7
5 kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana.
Ephésiens 1.5 Romains 8.23 Galates 3.26 Jean 1.12 Hébreux 1.3
6 Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba.
Romains 8.15-8.17 Romains 5.5 Romains 8.9 Ephésiens 4.30 Philippiens 1.19
7 Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu.
Galates 3.29-4.2 Romains 8.16-8.17 Galates 4.5-4.6 Galates 4.31-5.1 Lamentations 3.24

L’inquiétude de Paul pour les Galates

8 Lakini wakati ule, kwa kuwa hamkumjua Mungu, mliwatumikia wao ambao kwa asili si miungu.
1 Thessaloniciens 4.5 1 Corinthiens 1.21 2 Thessaloniciens 1.8 1 Corinthiens 8.4 1 Thessaloniciens 1.9
9 Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini kuyarejea tena mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena?
1 Corinthiens 8.3 Hébreux 7.18 Galates 3.3 Romains 8.3 1 Corinthiens 13.12
10 Mnashika siku, na miezi, na nyakati, na miaka.
Romains 14.5 Colossiens 2.16-2.17 Lévitique 23.1-23.44 Lévitique 25.13 Nombres 28.1-28.29
11 Nawachelea, isiwe labda nimejitaabisha bure kwa ajili yenu.
1 Thessaloniciens 3.5 Galates 2.2 2 Jean 1.8 Galates 5.2-5.4 Esaïe 49.4
12 Ndugu zangu, nawasihi, iweni kama mimi, maana mimi ni kama ninyi. Hamkunidhulumu kwa lo lote.
Genèse 34.15 1 Rois 22.4 2 Corinthiens 2.5 Actes 21.21 Philippiens 3.7-3.8
13 Lakini mwajua ya kuwa naliwahubiri Injili mara ya kwanza kwa sababu ya udhaifu wa mwili;
1 Corinthiens 2.3 2 Corinthiens 12.7-12.10 2 Corinthiens 11.30 2 Corinthiens 11.6 Galates 1.6
14 na jaribu lililowapata katika mwili wangu hamkulidharau wala kulikataa, bali mlinipokea kama malaika wa Mungu, kama Kristo Yesu.
Matthieu 10.40 1 Thessaloniciens 2.13 2 Corinthiens 5.20 Malachie 2.7 Psaumes 119.141
15 Ku wapi, basi, kule kujiita heri? Maana nawashuhudu kwamba, kama ingaliwezekana, mngaling’oa macho yenu, mkanipa mimi.
Romains 5.2 Romains 10.2 Romains 15.13 Galates 4.19 1 Thessaloniciens 2.8
16 Je! Nimekuwa adui wenu kwa sababu nawaambia yaliyo kweli?
Amos 5.10 Jean 7.7 Proverbes 9.8 Psaumes 141.5 Galates 2.5
17 Hao wana shauku nanyi, lakini si kwa njia nzuri, bali wanataka kuwafungia nje, ili kwamba ninyi mwaonee wao shauku.
Romains 16.18 2 Pierre 2.3 2 Corinthiens 11.13-11.15 Matthieu 23.15 Philippiens 2.21
18 Navyo ni vizuri kuonewa shauku katika neno jema sikuzote, wala si wakati nikiwapo mimi pamoja nanyi tu.
Apocalypse 3.19 Philippiens 1.27 Galates 4.13 Philippiens 2.12 Tite 2.14
19 Vitoto vyangu, ambao kwamba nawaonea utungu tena mpaka Kristo aumbike ndani yenu;
Ephésiens 4.13 Romains 8.29 1 Corinthiens 4.14-4.15 Romains 13.14 Ephésiens 4.24
20 laiti ningekuwapo pamoja nanyi sasa, na kuigeuza sauti yangu! Maana naona shaka kwa ajili yenu.
1 Thessaloniciens 2.17-2.18 1 Corinthiens 4.19-4.21 1 Thessaloniciens 3.9

Les deux descendances d’Abraham

21 Niambieni, ninyi mnaotaka kuwa chini ya sheria, je! Hamwisikii sheria?
Romains 7.5-7.6 Matthieu 22.29-22.32 Romains 10.3-10.10 Jean 10.34 Galates 3.10
22 Kwa maana imeandikwa ya kuwa, Ibrahimu alikuwa na wana wawili mmoja kwa mjakazi, na mmoja kwa mwungwana.
Genèse 16.15 Genèse 21.1-21.2 Genèse 21.10 Genèse 16.2-16.4
23 Lakini yule wa mjakazi alizaliwa kwa mwili, yule wa mwungwana kwa ahadi.
Hébreux 11.11 Genèse 21.1-21.2 Genèse 18.10-18.14 Romains 9.7-9.8 Genèse 17.15-17.19
24 Mambo haya husemwa kwa mfano; kwa maana hawa ndio kama maagano mawili, moja kutoka mlima Sinai, lizaalo kwa utumwa, ambalo ni Hajiri.
1 Corinthiens 10.11 Genèse 21.9-21.13 Osée 11.10 Galates 5.1 Hébreux 9.15-9.24
25 Maana Hajiri ni kama mlima Sinai ulioko Arabuni, umelingana na Yerusalemu wa sasa; kwa kuwa anatumika pamoja na watoto.
Juges 5.5 Galates 1.17 Luc 19.44 Actes 1.11 Psaumes 68.8
26 Bali Yerusalemu wa juu ni mwungwana, naye ndiye mama yetu sisi.
Hébreux 12.22 Apocalypse 3.12 Philippiens 3.20 Apocalypse 21.2 Michée 4.1-4.2
27 Kwa maana imeandikwa, Furahi, wewe uliye tasa, usiyezaa; Paza sauti, ulie, wewe usiye na utungu; Maana watoto wake aliyeachwa pekee ni wengi Kuliko wa huyo aliye na mume.
Esaïe 49.21 2 Samuel 13.20 Psaumes 113.9 Esaïe 54.1-54.5 Ruth 4.14-4.16
28 Basi, ndugu zangu, kama Isaka sisi tu watoto wa ahadi.
Galates 3.29 Galates 4.23 Romains 9.8-9.9 Romains 4.13-4.18 Actes 3.25
29 Lakini kama vile siku zile yule aliyezaliwa kwa mwili alivyomwudhi yule aliyezaliwa kwa Roho, ndivyo ilivyo na sasa.
Genèse 21.9 Galates 5.11 Matthieu 23.34-23.37 Jean 15.9 Romains 8.1
30 Lakini lasemaje andiko? Mfukuze mjakazi na mwanawe, kwa maana mwana wa mjakazi hatarithi kabisa pamoja na mwana wa mwungwana.
Jean 8.35 Romains 8.15-8.17 Galates 3.8 Romains 11.7-11.11 Jacques 4.5
31 Ndiposa, ndugu zangu, sisi si watoto wa mjakazi, bali tu watoto wa huyo aliye mwungwana.
Galates 5.1 Jean 8.36 Jean 1.12-1.13 1 Jean 3.1-3.2 Hébreux 2.14-2.15

Cette Bible est dans le domaine public.