Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 10.9
Bible en Swahili de l’est


Exemple d’Israël dans le désert

1 Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari;
Exode 14.29 Néhémie 9.11-9.12 Psaumes 105.39 Psaumes 66.6 Psaumes 78.13-78.14
2 wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari;
Jean 9.28-9.29 Exode 14.31 Galates 3.27 1 Corinthiens 1.13-1.16 Romains 6.3
3 wote wakala chakula kile kile cha roho;
Deutéronome 8.3 Néhémie 9.20 Exode 16.35 Néhémie 9.15 Psaumes 105.40
4 wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo.
Exode 17.6 Nombres 20.11 Psaumes 78.15 Jean 4.10 Psaumes 105.41
5 Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani.
Hébreux 3.17 Jude 1.5 Nombres 14.28-14.35 Nombres 26.64-26.65 Psaumes 106.26
6 Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani.
Nombres 11.4 1 Corinthiens 10.11 Hébreux 9.24 1 Pierre 3.21 Sophonie 3.6-3.7
7 Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze.
Exode 32.6-32.8 Exode 32.19 Deutéronome 9.12 Psaumes 106.19-106.20 Exode 32.17
8 Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu.
Nombres 25.1-25.9 Psaumes 106.29 1 Corinthiens 6.18 1 Corinthiens 6.9 Apocalypse 2.14
9 Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.
Nombres 21.5-21.6 Exode 17.7 Exode 17.2 Psaumes 78.18 Psaumes 106.14
10 Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu.
Exode 12.23 2 Samuel 24.16 1 Chroniques 21.15 Nombres 16.41 Hébreux 11.28
11 Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.
Romains 15.4 1 Corinthiens 9.10 Romains 13.11 Philippiens 4.5 1 Jean 2.18
12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.
Romains 11.20 Matthieu 26.40-26.41 Matthieu 26.33-26.34 Apocalypse 3.17-3.18 Proverbes 16.18

Conclusion : agir pour la gloire de Dieu

13 Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.
2 Pierre 2.9 2 Timothée 4.18 1 Pierre 5.8-5.9 Luc 22.46 Daniel 3.17
14 Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu.
1 Corinthiens 10.7 1 Jean 5.21 1 Pierre 2.11 2 Corinthiens 7.1 2 Corinthiens 12.15
15 Nasema kama na watu wenye akili; lifikirini ninyi ninenalo.
1 Corinthiens 8.1 1 Thessaloniciens 5.21 Job 34.2-34.3 1 Corinthiens 11.13 1 Corinthiens 4.10
16 Kikombe kile cha baraka tukibarikicho, je! Si ushirika wa damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo?
Actes 2.42 Matthieu 26.26-26.28 1 Jean 1.7 Actes 20.7 Luc 22.19-22.20
17 Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja; kwa maana sisi sote twapokea sehemu ya ule mkate mmoja.
Romains 12.5 1 Corinthiens 12.12 Colossiens 3.15 1 Corinthiens 12.27 Ephésiens 1.22-1.23
18 Waangalieni hao Waisraeli walivyokuwa kwa jinsi ya mwili; wale wazilao dhabihu, je! Hawana shirika na madhabahu?
Romains 4.1 Romains 4.12 Philippiens 3.3-3.5 1 Samuel 9.12-9.13 Lévitique 7.6
19 Basi niseme nini? Ya kwamba kile kilichotolewa sadaka kwa sanamu ni kitu? Au ya kwamba sanamu ni kitu?
1 Corinthiens 8.4 Esaïe 41.29 Esaïe 40.17 1 Corinthiens 3.7 2 Corinthiens 12.11
20 Sivyo, lakini vitu vile wavitoavyo sadaka wavitoa kwa mashetani, wala si kwa Mungu; nami sipendi ninyi kushirikiana na mashetani. Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani.
Apocalypse 9.20 Psaumes 106.37-106.39 2 Chroniques 11.15 Deutéronome 32.16-32.17 2 Corinthiens 4.4
21 Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani.
Matthieu 6.24 Esaïe 65.11 1 Rois 18.21 Deutéronome 32.37-32.38 2 Corinthiens 6.15-6.17
22 Au twamtia Bwana wivu? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye?
Deutéronome 32.21 Ezéchiel 22.14 Deutéronome 32.16 Ecclésiaste 6.10 Esaïe 45.9
23 Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo.
1 Corinthiens 6.12 1 Corinthiens 8.9 Ephésiens 4.29 2 Corinthiens 12.19 1 Corinthiens 8.1
24 Mtu asitafute faida yake mwenyewe, bali ya mwenzake.
1 Corinthiens 13.5 Philippiens 2.21 1 Corinthiens 10.33 Philippiens 2.4-2.5 Romains 15.1-15.2
25 Kila kitu kiuzwacho sokoni kuleni, bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri;
1 Corinthiens 8.7 Actes 10.15 Romains 14.14 Tite 1.15 Romains 13.5
26 maana, Dunia ni mali ya Bwana na vyote viijazavyo.
Psaumes 24.1 Psaumes 50.12 Job 41.11 Deutéronome 10.14 Exode 19.5
27 Na mtu asiyeamini akiwaalika, nanyi mnataka kwenda, kuleni kila kitu kiwekwacho mbele yenu bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri.
2 Corinthiens 1.13 1 Corinthiens 10.25 1 Corinthiens 5.9-5.11 2 Corinthiens 5.11 2 Corinthiens 4.2
28 Lakini mtu akiwaambia, Kitu hiki kimetolewa kiwe sadaka, msile, kwa ajili yake yeye aliyeonyesha, na kwa ajili ya dhamiri.
Psaumes 115.16 1 Corinthiens 8.10-8.13 Exode 9.29 Psaumes 24.1 Jérémie 27.5-27.6
29 Nasema, dhamiri, lakini si yako, bali ya yule mwingine. Maana kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?
1 Corinthiens 9.19 1 Corinthiens 10.32 Romains 14.15-14.21 2 Corinthiens 8.21 1 Corinthiens 8.9-8.13
30 Ikiwa mimi natumia sehemu yangu kwa shukrani, kwa nini nitukanwe, kwa ajili ya kitu nikishukuriacho?
Romains 14.6 1 Timothée 4.3-4.4
31 Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.
Colossiens 3.17 Colossiens 3.23 1 Pierre 4.11 Luc 11.41 Deutéronome 12.18
32 Msiwakoseshe Wayahudi wala Wayunani wala kanisa la Mungu,
Actes 20.28 1 Corinthiens 8.13 Romains 14.13 1 Timothée 3.5 2 Corinthiens 6.3
33 vile vile kama mimi niwapendezavyo watu wote katika mambo yote, nisitake faida yangu mwenyewe, ila faida yao walio wengi, wapate kuokolewa.
1 Corinthiens 10.24 1 Corinthiens 9.19-9.23 2 Corinthiens 11.28-11.29 Romains 11.14 Romains 15.2-15.3

Cette Bible est dans le domaine public.