Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 3.28
Bible en Swahili de l’est


1 Basi Myahudi ana ziada gani? Na kutahiriwa kwafaa nini?
Malachie 3.14 Hébreux 13.9 Romains 2.25-2.29 Genèse 25.32 1 Corinthiens 15.32
2 Kwafaa sana kwa kila njia. Kwanza kwa kuwa wamekabidhiwa mausia ya Mungu.
Actes 7.38 Romains 11.15-11.23 1 Pierre 4.11 Hébreux 5.12 Néhémie 9.13-9.14
3 Ni nini, basi, ikiwa baadhi yao hawakuamini? Je! Kutokuamini kwao kutaubatili uaminifu wa Mungu?
Hébreux 4.2 2 Timothée 2.13 Romains 11.1-11.7 Romains 10.16 Nombres 23.19
4 Hasha! Mungu aonekane kuwa amini na kila mtu mwongo; kama ilivyoandikwa, Ili ujulike kuwa una haki katika maneno yako, Ukashinde uingiapo katika hukumu.
Psaumes 51.4 Psaumes 116.11 Galates 2.17 Romains 3.31 Luc 20.16
5 Lakini, ikiwa udhalimu wetu waithibitisha haki ya Mungu, tuseme nini? Je! Mungu ni dhalimu aletaye ghadhabu? (Nasema kwa jinsi ya kibinadamu.)
Galates 3.15 Romains 6.19 1 Corinthiens 9.8 Romains 7.7 Romains 4.1
6 Hasha! Kwa maana hapo Mungu atawezaje kuuhukumu ulimwengu?
Genèse 18.25 Job 8.3 Psaumes 50.6 Psaumes 9.8 Psaumes 98.9
7 Lakini, ikiwa kweli ya Mungu imezidi kudhihirisha utukufu wake kwa sababu ya uongo wangu, mbona mimi ningali nahukumiwa kuwa ni mwenye dhambi?
Romains 3.4 Romains 9.19-9.20 Actes 2.23 Matthieu 26.34 Matthieu 26.69-26.75
8 Kwa nini tusiseme (kama tulivyosingiziwa, na kama wengine wanavyokaza kusema ya kwamba twasema hivyo), Na tufanye mabaya, ili yaje mema? Ambao kuhukumiwa kwao kuna haki.
Romains 6.1 Romains 6.15 Romains 7.7 1 Pierre 3.16-3.17 Romains 5.20
9 Ni nini basi? Tu bora kuliko wengine? La! Hata kidogo. Kwa maana tumekwisha kuwashitaki Wayahudi na Wayunani ya kwamba pia wamekuwa chini ya dhambi;
Galates 3.22 Romains 3.19 Romains 6.15 Luc 18.9-18.14 Romains 1.18-2.29
10 kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Hakuna mwenye haki hata mmoja.
Psaumes 53.1-53.3 Psaumes 14.1-14.3 Romains 3.23 Marc 7.21-7.22 Job 15.14
11 Hakuna afahamuye; Hakuna amtafutaye Mungu.
Psaumes 14.2-14.4 Psaumes 53.2 Tite 3.3 Matthieu 13.19 Matthieu 13.13-13.14
12 Wote wamepotoka, wameoza wote pia; Hakuna mtenda mema, la! Hata mmoja.
Psaumes 14.3 Ecclésiaste 7.20 Jacques 1.16-1.17 Ephésiens 2.3 Esaïe 53.6
13 Koo lao ni kaburi wazi, Kwa ndimi zao wametumia hila. Sumu ya fira i chini ya midomo yao.
Psaumes 5.9 Psaumes 140.3 Jacques 3.5-3.8 Matthieu 23.27-23.28 Psaumes 12.3-12.4
14 Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu.
Psaumes 10.7 Psaumes 59.12 Psaumes 109.17-109.18 Jacques 3.10
15 Miguu yao ina mbio kumwaga damu.
Esaïe 59.7-59.8 Proverbes 1.16 Proverbes 6.18
16 Uharibifu na mashaka yamo njiani mwao.
17 Wala njia ya amani hawakuijua.
Esaïe 59.8 Luc 1.79 Romains 5.1 Matthieu 7.14 Esaïe 57.21
18 Kumcha Mungu hakupo machoni pao.
Psaumes 36.1 Apocalypse 19.5 Proverbes 16.6 Proverbes 8.13 Proverbes 23.17
19 Basi twajua ya kuwa mambo yote inenayo torati huyanena kwa hao walio chini ya torati, ili kila kinywa kifumbwe, na ulimwengu wote uwe chini ya hukumu ya Mungu;
Job 9.2-9.3 Psaumes 107.42 Job 5.16 Romains 2.12-2.18 Ezéchiel 16.63
20 kwa sababu hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele zake kwa matendo ya sheria; kwa maana kutambua dhambi huja kwa njia ya sheria.
Galates 2.16 Actes 13.39 Romains 3.28 Romains 4.15 Romains 9.32

Déclarés justes par la foi en Christ

21 Lakini sasa, haki ya Mungu imedhihirika pasipo sheria; inashuhudiwa na torati na manabii;
Actes 10.43 Jérémie 33.16 Romains 1.2 Romains 1.17 Daniel 9.24
22 ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti;
Romains 10.12 Galates 3.28 Colossiens 3.11 Galates 2.16 Romains 5.1-5.11
23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;
Ecclésiaste 7.20 1 Jean 1.8-1.10 Romains 3.9 Galates 3.22 Romains 3.19
24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu;
Colossiens 1.14 Romains 4.16 Romains 5.9 Tite 3.5-3.7 Ephésiens 1.6-1.7
25 ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake,ili aonyeshe haki yake ,kwa sababu ya kuziachilia katika ustahimili wa MUNGU dhambi zote zilzotangulia kufanywa.
1 Jean 4.10 1 Jean 2.2 Lévitique 16.15 Actes 17.30 Exode 25.17-25.22
26 apate kuonyesha haki yake wakati huu, ili awe mwenye haki na mwenye kumhesabu haki yeye amwaminiye Yesu.
Actes 13.38-13.39 Deutéronome 32.4 Esaïe 45.21 Romains 8.33 Apocalypse 15.3
27 Ku wapi, basi, kujisifu? Kumefungiwa nje. Kwa sheria ya namna gani? Kwa sheria ya matendo? La! Bali kwa sheria ya imani.
Romains 2.23 Romains 4.2 1 Corinthiens 1.29-1.31 Romains 2.17 Romains 7.25
28 Basi, twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria.
Jacques 2.24 1 Corinthiens 6.11 Philippiens 3.9 Jean 6.40 Romains 3.26
29 Au je! Mungu ni Mungu wa Wayahudi tu? Siye Mungu wa Mataifa pia? Naam, ni Mungu wa Mataifa pia;
Zacharie 2.11 Osée 1.10 Romains 15.9-15.13 Malachie 1.11 Genèse 17.18
30 kama kwa kweli Mungu ni mmoja, atakayewahesabia haki wale waliotahiriwa katika imani, nao wale wasiotahiriwa atawahesabia haki kwa njia ya imani iyo hiyo.
Galates 3.8 Galates 3.20 Galates 2.14-2.16 Galates 3.28 Romains 10.12-10.13
31 Basi, je! Twaibatilisha sheria kwa imani hiyo? Hasha! Kinyume cha hayo twaithibitisha sheria.
Matthieu 5.17 Romains 8.4 Galates 2.21 Romains 7.7-7.14 Matthieu 3.15

Cette Bible est dans le domaine public.