Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 3.14
Bible en Swahili de l’est


Guérison d’un boiteux

1 Basi Petro na Yohana walikuwa wakikwea pamoja kwenda hekaluni, saa ya kusali, saa tisa.
Psaumes 55.17 Actes 4.13 Actes 2.46 Luc 1.10 Luc 22.8
2 Na mtu mmoja aliyekuwa kiwete toka tumboni mwa mamaye alichukuliwa na watu, ambaye walimweka kila siku katika mlango wa hekalu uitwao Mzuri, ili aombe sadaka kwa watu waingiao ndani ya hekalu.
Luc 16.20 Jean 9.8 Actes 14.8 Luc 18.35 Actes 10.4
3 Mtu huyu akiwaona Petro na Yohana wakiingia hekaluni aliomba apewe sadaka.
4 Na Petro, akimkazia macho, pamoja na Yohana, akasema, Tutazame sisi.
Jean 5.6 Luc 4.20 Actes 14.9-14.10 Actes 3.12 Jean 11.40
5 Akawaangalia, akitaraji kupata kitu kwao.
6 Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende.
Actes 3.16 Actes 4.10 Actes 9.34 Actes 10.38 Actes 2.22
7 Akamshika mkono wa kuume, akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikatiwa nguvu.
Marc 5.41 Actes 9.41 Marc 1.31 Luc 13.13 Marc 9.27
8 Akaondoka upesi akasimama, akaanza kwenda; akaingia ndani ya hekalu pamoja nao, akienda, akiruka-ruka, na kumsifu Mungu.
Actes 14.10 Esaïe 35.6 Luc 6.23 Luc 17.15-17.18 Psaumes 103.1-103.2
9 Watu wote wakamwona akienda, akimsifu Mungu.
Actes 4.21 Actes 4.16 Luc 13.17 Actes 14.11 Marc 2.11-2.12
10 Wakamtambua, ya kuwa yeye ndiye aliyekuwa akiketi na kuomba sadaka penye mlango Mzuri wa hekalu; wakajaa ushangao wakastaajabia mambo yale yaliyompata.
Actes 3.2 Jean 9.3 Luc 9.43 Actes 4.21-4.22 Actes 4.14-4.16
11 Basi alipokuwa akiwashika Petro na Yohana, watu wote wakawakusanyikia mbio katika tao lile lililoitwa tao la Sulemani, wakishangaa sana.
Actes 5.12 Jean 10.23 Luc 8.38 Actes 2.6 Luc 22.8
12 Hata Petro alipoyaona haya akawajibu wale watu, Enyi Waisraeli, mbona mnastaajabia haya, au mbona mnatukazia macho sisi, kana kwamba tumemfanya huyu aende kwa nguvu zetu sisi, au kwa utauwa wetu sisi?
2 Corinthiens 3.5 Jean 3.27-3.28 Actes 14.11-14.15 Genèse 41.16 Romains 11.1
13 Mungu wa Ibrahimu na wa Isaka na wa Yakobo, Mungu wa baba zetu, amemtukuza mtumishi wake Yesu, ambaye ninyi mlimsaliti na kumkana mbele ya Pilato, alipokuwa ametoa hukumu yake afunguliwe.
Jean 19.15 Matthieu 27.2 Actes 7.32 Matthieu 22.32 Jean 17.1-17.5
14 Bali ninyi mlimkana yule Mtakatifu, yule Mwenye haki, mkataka mpewe mwuaji;
Marc 1.24 Actes 4.27 1 Pierre 3.18 Actes 7.52 Jacques 5.6
15 mkamwua yule Mkuu wa uzima, ambaye Mungu amemfufua katika wafu; na sisi tu mashahidi wake.
Actes 2.24 Actes 2.32 Jean 5.26 1 Jean 5.11-5.12 Actes 10.40-10.41
16 Na kwa imani katika jina lake, jina lake limemtia nguvu mtu huyu mnayemwona na kumjua; na imani ile iliyo kwake yeye imempatia huyu uzima huu mkamilifu mbele yenu ninyi nyote.
Actes 3.6 Matthieu 21.21-21.22 Actes 14.9 Marc 16.17-16.18 Actes 16.18
17 Basi sasa, ndugu, najua ya kuwa mliyatenda haya kwa kutokujua kwenu, kama na wakuu wenu walivyotenda.
Luc 23.34 Actes 13.27 1 Corinthiens 2.8 1 Timothée 1.13 Jean 16.3
18 Lakini mambo yale aliyohubiri Mungu tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake wote, ya kwamba Kristo wake atateswa, ameyatimiza hivyo.
Actes 26.22-26.23 Actes 2.23 Luc 24.26-24.27 Actes 17.2-17.3 Zacharie 12.10
19 Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana;
Actes 2.38 Esaïe 44.22 Esaïe 43.25 Psaumes 51.9 Matthieu 13.15
20 apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa tangu zamani;
Marc 13.26 2 Thessaloniciens 2.2 Luc 21.27 Matthieu 24.3 Hébreux 9.28
21 ambaye ilimpasa kupokewa mbinguni hata zije zamani za kufanywa upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu tokea mwanzo wa ulimwengu.
Actes 1.11 Luc 1.70 Malachie 4.5-4.6 Romains 8.21 Marc 9.11-9.13
22 Kwa maana Musa kweli alisema ya kwamba, Bwana Mungu wenu atawainulieni nabii, katika ndugu zenu, kama mimi; msikieni yeye katika mambo yote atakayonena nanyi.
Actes 7.37 Deutéronome 18.15-18.19 Marc 9.4-9.7 Luc 9.30-9.35 Esaïe 55.3-55.4
23 Na itakuwa ya kwamba kila mtu asiyemsikiliza nabii huyo ataangamizwa na kutengwa na watu wake.
Deutéronome 18.19 2 Thessaloniciens 1.7-1.9 Apocalypse 13.8 Jean 8.24 Hébreux 10.28-10.30
24 Naam, na manabii wote tangu Samweli na wale waliokuja baada yake, wote walionena, walihubiri habari za siku hizi.
Actes 3.21 1 Samuel 3.20 Psaumes 99.6 Actes 13.20 1 Samuel 3.1
25 Ninyi mmekuwa watoto wa manabii na wa maagano yale, ambayo Mungu aliagana na baba zenu, akimwambia Ibrahimu, Katika uzao wako kabila zote za ulimwengu zitabarikiwa.
Genèse 22.18 Actes 2.39 Genèse 12.3 Romains 9.4-9.5 Psaumes 22.27
26 Mungu, akiisha kumfufua mtumishi wake Yesu, alimtuma kwenu ninyi kwanza, ili kuwabarikia kwa kumwepusha kila mmoja wenu na maovu yake.
Actes 3.22 Jude 1.24 Actes 3.25 Romains 1.16 Matthieu 1.21

Cette Bible est dans le domaine public.