Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 22.60
Bible en Swahili de l’est


1 Ikakaribia sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu, iitwayo Sikukuu ya Pasaka.Exode 12.6-12.23 Marc 14.1-14.2 Lévitique 23.5-23.6 Marc 14.12 Jean 11.55-11.57
2 Na wakuu wa makuhani na waandishi walikuwa wakitafuta njia ya kumwua; maana walikuwa wakiwaogopa watu.Jean 11.47-11.53 Jean 11.57 Luc 20.19 Matthieu 26.3-26.5 Matthieu 21.45-21.46
3 Shetani akamwingia Yuda, aitwaye Iskariote, naye ni mmoja wa wale Thenashara.Marc 14.10-14.11 Jean 13.2 Actes 5.3 Luc 6.16 Jean 13.26-13.27
4 Akaondoka, akaenda akasema na wakuu wa makuhani na majemadari, jinsi atakavyoweza kumtia mikononi mwao.Actes 4.1 Actes 5.24 Matthieu 26.14 Actes 5.26 Luc 22.52
5 Wakafurahi, wakapatana naye kumpa fedha.Matthieu 27.3-27.5 2 Pierre 2.3 2 Pierre 2.15 Actes 1.18 1 Timothée 6.9-6.10
6 Akakubali, akatafuta nafasi ya kumsaliti kwao pasipokuwapo mkutano.Matthieu 26.5 Marc 14.2
7 Ikafika siku ya mikate isiyotiwa chachu, ambayo ilipasa kuchinja pasaka.Exode 12.18 Luc 22.1 Exode 12.6 Marc 14.12-14.16 1 Corinthiens 5.7
8 Akawatuma Petro na Yohana, akisema, Nendeni, mkatuandalie pasaka tupate kuila.Marc 14.13-14.16 Actes 4.13 Galates 4.4-4.5 Matthieu 3.15 Actes 8.14
9 Wakamwambia, Wataka tuandae wapi? 10 Akawaambia, Tazama, mtakapoingia mjini mtakutana na mwanamume akichukua mtungi wa maji; mfuateni mkaingie katika nyumba atakayoingia yeye.Actes 8.26-8.29 Matthieu 26.18-26.19 Luc 19.29-19.40 1 Samuel 10.2-10.7 Jean 16.4
11 Na mtamwambia mwenye nyumba, Mwalimu akuambia, Ki wapi chumba cha wageni, nipate kula pasaka humo pamoja na wanafunzi wangu?Jean 11.28 Luc 19.34 Matthieu 21.3 Luc 19.5 Luc 19.31
12 Naye atawaonyesha chumba kikubwa orofani, kimekwisha andikwa; andaeni humo.Actes 1.13 Actes 20.8 Jean 2.25 Jean 21.17 Actes 16.14-16.15
13 Wakaenda, wakaona kama alivyowaambia, wakaiandaa pasaka.Jean 2.5 Hébreux 11.8 Luc 19.32 Luc 21.33 Jean 11.40
14 Hata saa ilipofika aliketi chakulani, yeye na wale mitume pamoja naye.Matthieu 26.20 Marc 14.17 Deutéronome 16.6-16.7 Marc 6.30
15 Akawaambia, Nimetamani sana kuila pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu;Luc 12.50 Jean 17.1 Jean 13.1 Jean 4.34
16 kwa maana nawaambia ya kwamba siili tena hata itakapotimizwa katika ufalme wa Mungu.Luc 14.15 Apocalypse 19.9 Luc 22.30 Jean 6.50-6.58 1 Corinthiens 5.7-5.8
17 Akapokea kikombe, akashukuru, akasema, Twaeni hiki, mgawanye ninyi kwa ninyi;Psaumes 116.13 Luc 22.19 Romains 14.6 Deutéronome 8.10 1 Samuel 9.13
18 Maana nawaambia ya kwamba tangu sasa sinywi mazao ya mzabibu hata ufalme wa Mungu utakapokuja.Matthieu 26.29 Luc 22.16 Marc 14.25 Daniel 2.44 Marc 15.23
19 Akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa, akisema, [Huu ndio mwili wangu unaotolewa kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.1 Corinthiens 11.23-11.29 Luc 22.20 1 Corinthiens 10.16 Jean 6.51 Matthieu 26.26-26.28
20 Kikombe nacho vivyo hivyo baada ya kula; akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu, inayomwagika kwa ajili yenu.]1 Corinthiens 11.25 Zacharie 9.11 2 Corinthiens 3.6 Matthieu 26.28 Exode 24.8
21 Walakini, tazama, mkono wake yeye anayenisaliti upo hapa pamoja nami mezani,Psaumes 41.9 Jean 13.26 Matthieu 26.21-26.24 Michée 7.5-7.6 Jean 13.18-13.19
22 Kwa kuwa Mwana wa Adamu aenda zake kama ilivyokusudiwa; lakini, ole wake mtu yule amsalitiye!Actes 2.23 Psaumes 22.1-22.31 Marc 14.21 1 Corinthiens 15.3-15.4 Psaumes 109.6-109.15
23 Wakaanza kuulizana wao kwa wao, ni yupi miongoni mwao atakayelitenda jambo hilo.Matthieu 26.22 Jean 13.22-13.25 Marc 14.19
24 Yakatokea mashindano kati yao, kwamba ni nani anayehesabiwa kuwa mkubwa.Luc 9.46 Marc 9.34 1 Pierre 5.5-5.6 Jacques 4.5-4.6 Marc 10.37-10.41
25 Akawaambia, Wafalme wa Mataifa huwatawala, na wenye mamlaka juu yao huitwa Wenye fadhili;Matthieu 20.25-20.28 Marc 10.41-10.45
26 lakini kwenu ninyi sivyo; bali aliye mkubwa kwenu na awe kama aliye mdogo; na mwenye kuongoza kama yule atumikaye.Luc 9.48 1 Pierre 5.3 Matthieu 18.3-18.5 Romains 12.2 1 Pierre 5.5
27 Maana aliye mkubwa ni yupi? Yeye aketiye chakulani, au yule atumikaye? Siye yule aketiye chakulani? Lakini mimi kati yenu ni kama atumikaye.Matthieu 20.28 Luc 12.37 2 Corinthiens 8.9 Philippiens 2.7-2.8 Luc 17.7-17.9
28 Nanyi ndinyi mliodumu pamoja nami katika majaribu yangu.Hébreux 2.18 Hébreux 4.15 Jean 8.31 Matthieu 24.13 Actes 1.25
29 Nami nawawekea ninyi ufalme, kama vile Baba yangu alivyoniwekea mimi;2 Timothée 2.12 Matthieu 25.34 Matthieu 28.18 1 Pierre 5.4 Apocalypse 21.14
30 mpate kula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu; na kuketi katika viti vya enzi, huku mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.Matthieu 19.28 Luc 14.15 Matthieu 8.11 Apocalypse 2.26-2.27 1 Corinthiens 6.2-6.3
31 Akasema, Simoni, Simoni, tazama, Shetani amewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano;1 Pierre 5.8 Amos 9.9 Zacharie 3.1 Job 1.6-1.12 Job 2.1-2.6
32 lakini nimekuombea wewe ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako.Jean 21.15-21.17 Romains 8.34 Matthieu 18.3 Hébreux 12.12-12.13 Romains 5.9-5.10
33 Akamwambia, Bwana, niwapo pamoja nawe, mimi ni tayari kwenda gerezani au hata kifoni.Marc 14.29 Matthieu 26.33-26.35 Marc 14.31 Matthieu 26.40-26.41 Marc 14.37-14.38
34 Akasema, Nakuambia, Petro, jogoo hatawika leo, kabla wewe hujanikana mara tatu ya kuwa hunijui.Jean 13.38 Matthieu 26.34 Marc 14.30 Marc 14.71-14.72 Jean 18.27
35 Akawauliza, Je! Hapo nilipowatuma hamna mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu? Wakasema, La!Luc 10.4 Luc 9.3 Matthieu 10.9-10.10 Marc 6.8-6.9 Matthieu 6.31-6.33
36 Akawaambia, Lakini sasa mwenye mfuko na auchukue, na mkoba vivyo hivyo; naye asiye na upanga, na auze joho yake akanunue. 37 Kwa kuwa nawaambia, hayo yaliyoandikwa hayana budi kutimizwa kwangu; ya kuwa, Alihesabiwa pamoja na wahalifu. Kwa sababu yanipasayo yanao mwisho wake.Esaïe 53.12 Galates 3.13 Jean 10.35 2 Corinthiens 5.21 Jean 17.4
38 Wakasema, Bwana, tazama, hapa pana panga mbili. Akawaambia, Basi.2 Corinthiens 10.3-10.4 1 Thessaloniciens 5.8 Ephésiens 6.10-6.18 Luc 22.49 1 Pierre 5.9
39 Akatoka akaenda mpaka mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa desturi yake; wanafunzi wake nao wakafuatana naye.Luc 21.37 Jean 18.1-18.2 Matthieu 21.1 Matthieu 26.36-26.38 Marc 14.26
40 Alipofika mahali pale aliwaambia, Ombeni kwamba msiingie majaribuni.Matthieu 6.13 Luc 22.46 Ephésiens 6.18-6.19 1 Pierre 4.7 Marc 14.32-14.42
41 Mwenyewe akajitenga nao kama kiasi cha kutupa jiwe, akapiga magoti akaomba,Matthieu 26.39 Marc 14.35 Luc 18.11
42 akisema, Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke.Matthieu 20.22 Jean 12.27-12.28 Marc 14.36 Matthieu 26.42 Jean 6.38
43 Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.Matthieu 4.11 Hébreux 1.14 Psaumes 91.11-91.12 Hébreux 1.6 Matthieu 26.53
44 Naye kwa vile alivyokuwa katika dhiki, akazidi sana kuomba; hari yake ikawa kama matone ya damu yakidondoka nchini.]Lamentations 1.12 Hébreux 5.7 Psaumes 22.12-22.21 Jean 12.27 Psaumes 143.6-143.7
45 Alipoondoka katika kuomba kwake, akawajia wanafunzi wake, akawakuta wamelala usingizi kwa huzuni.Marc 14.40-14.41 Matthieu 26.40 Matthieu 26.43 Marc 14.37
46 Akawaambia, Mbona mmelala usingizi? Ondokeni, mkaombe, msije mkaingia majaribuni.Luc 22.40 Luc 21.34-21.36 Jonas 1.6 Proverbes 6.4-6.11
47 Basi alipokuwa katika kusema, tazama, mkutano wa watu, na yule aitwaye Yuda, ambaye ni mmoja wa wale Thenashara, amewatangulia. Akamkaribia Yesu ili kumbusu.Luc 22.3-22.6 Matthieu 26.45-26.56 Matthieu 26.14-26.16 Marc 14.41-14.50 Jean 18.2-18.11
48 Yesu akamwambia, Yuda, wamsaliti Mwana wa Adamu kwa kumbusu?Proverbes 27.6 Psaumes 55.21 2 Samuel 20.9-20.10 Matthieu 26.48-26.50 Marc 14.44-14.46
49 Na wale waliokuwa karibu naye walipoona yatakayotukia, walisema, Bwana, tuwapige kwa upanga?Luc 22.38
50 Mmoja wao akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio la kuume.Jean 18.10-18.11 Marc 14.47 Matthieu 26.51-26.54 2 Corinthiens 10.4 Romains 12.19
51 Yesu akajibu akasema, Mwe radhi kwa hili. Akamgusa sikio, akamponya.Romains 12.21 2 Corinthiens 10.1 Jean 17.12 1 Pierre 2.21-2.23 Jean 18.8-18.9
52 Yesu akawaambia wakuu wa makuhani, na maakida wa hekalu, na wazee, waliokuja juu yake, Je! Mmekuja wenye panga na marungu kama kukamata mnyang’anyi?Luc 22.4 Matthieu 26.55 Marc 14.48-14.49 Actes 5.26 Jean 17.12
53 Kila siku nilipokuwa pamoja nanyi hekaluni hamkuninyoshea mikono, lakini hii ndiyo saa yenu, na mamlaka ya giza.Jean 12.27 Ephésiens 6.12 Actes 26.18 Jean 16.20-16.22 Jean 7.25-7.26
54 Wakamkamata, wakamchukua, wakaenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Na Petro alimfuata kwa mbali.Matthieu 26.57-26.58 Marc 14.53-14.54 Jean 18.12-18.17 Jean 18.24 2 Chroniques 32.31
55 Na walipokwisha washa moto katikati ya kiwanja, waliketi pamoja, naye Petro akaketi kati yao.Psaumes 26.4-26.5 Matthieu 26.3 Proverbes 13.20 Psaumes 1.1 Psaumes 28.3
56 Ndipo mjakazi mmoja akamwona ameketi mwangani, akamkazia macho akasema, Na huyu alikuwa pamoja naye.Marc 14.66-14.68 Matthieu 26.69 Marc 14.17 Marc 14.6 Jean 18.17
57 Akakana, akisema, Ee mwanamke, simjui.1 Jean 1.9 Jean 18.27 Luc 12.9 Matthieu 26.70 Matthieu 10.33
58 Baadaye kitambo mtu mwingine alimwona akasema, Wewe nawe u mmoja wao. Petro akasema, Ee mtu, si mimi.Jean 18.25 Matthieu 26.71-26.72 Marc 14.69-14.70
59 Halafu, yapata saa moja, mtu mwingine alikaza kusema, Hakika na huyu alikuwa pamoja naye, kwa kuwa yeye pia ni Mgalilaya.Jean 18.26-18.27 Marc 14.69-14.70 Matthieu 26.73-26.74
60 Petro akasema, Ee mtu, sijui usemalo. Na papo hapo alipokuwa katika kusema, jogoo aliwika.Marc 14.71-14.72 Luc 22.34 Jean 18.27 Matthieu 26.74-26.75
61 Bwana akageuka akamtazama Petro. Petro akalikumbuka lile neno la Bwana jinsi alivyomwambia, Leo kabla hajawika jogoo utanikana mara tatu.Luc 22.34 Matthieu 26.75 Job 33.27 Marc 5.30 Luc 10.41
62 Akatoka nje akalia kwa majonzi.Matthieu 26.75 Matthieu 5.4 Psaumes 130.1-130.4 Psaumes 126.5-126.6 1 Corinthiens 10.12
63 Na wale watu waliokuwa wakimshika Yesu walimfanyia dhihaka, wakampiga.Jean 18.22 Psaumes 69.7-69.12 Psaumes 22.13 Michée 5.1 Matthieu 27.28-27.31
64 Wakamfunika macho, kisha wakamwuliza-uliza wakisema, Tabiri, ni nani aliyekupiga?Juges 16.21 Juges 16.25
65 Wakamtolea na maneno mengine mengi ya kumtukana.Matthieu 27.39 Actes 26.11 1 Timothée 1.13-1.14 Matthieu 12.31-12.32 Luc 12.10
66 Hata kulipokucha, walikutanika jamii ya wazee, na wakuu wa makuhani, na waandishi, wakamleta katika baraza yao, wakisema,Matthieu 27.1 Marc 15.1 Actes 22.5 Actes 4.25-4.28 Matthieu 5.22
67 Kama wewe ndiwe Kristo, tuambie. Akawaambia, Nijapowaambia, hamtasadiki kabisa.Matthieu 11.3-11.5 Jean 5.39-5.47 Jean 9.27-9.28 Jean 12.37-12.43 Jean 8.43-8.45
68 Tena, nikiwauliza, hamtajibu.Luc 20.41-20.44 Luc 20.3-20.7
69 Lakini tangu sasa Mwana wa Adamu atakuwa ameketi upande wa kuume wa Mungu Mwenyezi.Marc 16.19 Psaumes 110.1 Hébreux 1.3 Ephésiens 1.20-1.23 Matthieu 22.44
70 Wakasema wote, Basi, wewe ndiwe Mwana wa Mungu? Akawaambia, Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.Luc 23.3 Matthieu 27.11 Marc 15.2 Matthieu 26.64 Matthieu 4.3
71 Wakasema, Basi, tuna haja gani tena ya ushuhuda? Maana, sisi wenyewe tumesikia maneno ya kinywa chake.Marc 14.63-14.64 Matthieu 26.65-26.66

Cette Bible est dans le domaine public.