Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 13
Bible en Swahili de l’est


1 Na wakati uo huo walikuwapo watu waliompasha habari ya Wagalilaya wale ambao Pilato alichanganya damu yao na dhabihu zao.
Lamentations 2.20 Matthieu 27.2 1 Pierre 4.17-4.18 Actes 5.37 Ezéchiel 9.5-9.7
2 Akawajibu akawaambia, Je! Mwadhani ya kwamba Wagalilaya hao walikuwa wenye dhambi kuliko Wagalilaya wote, hata wakapatwa na mambo hayo?
Jean 9.2 Actes 28.4 Job 22.5-22.16 Luc 13.4
3 Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.
Matthieu 12.45 Matthieu 3.2 Luc 13.5 Actes 3.19 Matthieu 24.21-24.29
4 Au wale kumi na wanane, walioangukiwa na mnara huko Siloamu, ukawaua, mwadhani ya kwamba wao walikuwa wakosaji kuliko watu wote waliokaa Yerusalemu?
Jean 9.11 Jean 9.7 Matthieu 6.12 Luc 11.4 Néhémie 3.15
5 Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.
Luc 13.3 Ezéchiel 18.30 Esaïe 28.10-28.13
6 Akanena mfano huu; Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu; akaenda akitafuta matunda juu yake, asipate.
Jérémie 2.21 Galates 5.22 Matthieu 21.19-21.20 Esaïe 5.1-5.4 Psaumes 80.8-80.13
7 Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu; uukate, mbona hata nchi unaiharibu?
Matthieu 7.19 Luc 3.9 Exode 32.10 Romains 2.4-2.5 Daniel 4.14
8 Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi;
Romains 10.1 Jérémie 15.1 Joël 2.17 2 Pierre 3.9 Exode 34.9
9 nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa, ndipo uukate.
Apocalypse 16.5-16.7 Daniel 9.5-9.8 Esdras 9.14-9.15 Jean 15.2 1 Thessaloniciens 2.15

Guérison de la femme courbée

10 Siku ya sabato alikuwa akifundisha katika sinagogi mojawapo.
Matthieu 4.23 Luc 4.44 Luc 4.15-4.16
11 Na tazama, palikuwa na mwanamke aliyekuwa na pepo wa udhaifu muda wa miaka kumi na minane, naye amepindana, hawezi kujinyosha kabisa.
Luc 13.16 Luc 8.2 Luc 8.43 Psaumes 6.2 Actes 14.8-14.10
12 Yesu alipomwona alimwita, akamwambia, Mama, umefunguliwa katika udhaifu wako.
Luc 6.8-6.10 Psaumes 107.20 Matthieu 8.16 Joël 3.10 Esaïe 65.1
13 Akaweka mikono yake juu yake, naye akanyoka mara hiyo, akamtukuza Mungu.
Marc 5.23 Psaumes 103.1-103.5 Luc 18.43 Psaumes 107.20-107.22 Marc 16.18
14 Basi mkuu wa sinagogi alikasirika kwa sababu Yesu amemponya mtu siku ya sabato, akajibu, akawaambia mkutano, Kuna siku sita zifaazo kufanya kazi, basi njoni mponywe katika siku hizo, wala si katika siku ya sabato.
Exode 20.9 Luc 8.41 Matthieu 12.2 Actes 18.8 Actes 13.15
15 Lakini Bwana akajibu akasema, Enyi wanafiki, kila mmoja wenu, je! Hamfungui ng’ombe wake au punda wake siku ya sabato katika zizi, aende naye kumnywesha?
Luc 14.5 Actes 13.9-13.10 Matthieu 15.7 Luc 6.42 Matthieu 23.28
16 Na huyu mwanamke, aliye wa uzao wa Ibrahimu, ambaye Shetani amemfunga miaka kumi na minane hii, haikupasa afunguliwe kifungo hiki siku ya sabato?
Luc 19.9 Luc 3.8 Jean 8.44 Actes 13.26 Matthieu 4.10
17 Aliposema haya wakatahayari wote walioshindana naye; mkutano wote wakafurahi kwa sababu ya mambo matukufu yaliyotendwa na yeye.
Psaumes 132.18 1 Pierre 3.16 Luc 18.43 Exode 15.11 Esaïe 4.2

La graine de moutarde et le levain

18 Kisha alisema, Ufalme wa Mungu umefanana na nini? Nami niufananishe na nini?
Luc 13.20 Matthieu 13.31-13.32 Matthieu 13.24 Marc 4.30-4.34 Luc 7.31
19 Umefanana na punje ya haradali aliyotwaa mtu akaitupa katika shamba lake; ikamea, ikawa mti; ndege wa angani wakakaa katika matawi yake.
Matthieu 17.20 Actes 15.14-15.18 Actes 4.4 Luc 17.6 Cantique 4.12
20 Akasema mara ya pili, Niufananishe na nini ufalme wa Mungu?
21 Umefanana na chachu aliyotwaa mwanamke akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga, hata ukachacha wote pia.
Matthieu 13.33 1 Corinthiens 5.6 Jean 15.2 Psaumes 92.13-92.14 Job 17.9

L’entrée dans le royaume

22 Naye alikuwa akipita katika miji na vijiji, akifundisha, katika safari yake kwenda Yerusalemu.
Luc 9.51 Marc 6.6 Matthieu 9.35 Luc 4.43-4.44 Actes 10.38
23 Mtu mmoja akamwuliza, Je! Bwana, watu wanaookolewa ni wachache? Akawaambia,
Matthieu 7.14 Actes 1.7-1.8 Marc 13.4-13.5 Matthieu 19.25 Luc 21.7-21.8
24 Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.
2 Pierre 1.10 Proverbes 21.25 Jean 7.34 Genèse 32.25-32.26 Romains 9.31-9.33
25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;
Matthieu 25.10-25.12 Luc 13.27 Luc 6.46 Matthieu 7.21-7.23 Hébreux 12.17
26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.
Tite 1.16 Esaïe 58.2 2 Timothée 3.5
27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.
Matthieu 25.41 Luc 13.25 Psaumes 6.8 1 Corinthiens 8.3 Psaumes 119.115
28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje.
Matthieu 25.30 Matthieu 8.11-8.12 Matthieu 22.13 2 Thessaloniciens 1.5 2 Pierre 1.11
29 Nao watakuja watu toka mashariki na magharibi, na toka kaskazini na kusini, nao wataketi chakulani katika ufalme wa Mungu.
Actes 28.28 Malachie 1.11 Ephésiens 3.6-3.8 Colossiens 1.6 Marc 13.27
30 Na tazama, wako walio wa mwisho watakaokuwa wa kwanza, na wa kwanza watakaokuwa wa mwisho.
Matthieu 19.30 Marc 10.31 Matthieu 20.16 Matthieu 8.11-8.12 Matthieu 3.9-3.10
31 Saa ile ile Mafarisayo kadha wa kadha walimwendea, wakamwambia, Toka hapa, uende mahali pengine, kwa sababu Herode anataka kukuua.
Néhémie 6.9-6.11 Psaumes 11.1-11.2 Amos 7.12-7.13 Matthieu 14.1 Luc 3.1
32 Akawaambia, Nendeni, mkamwambie yule mbweha, Tazama, leo na kesho natoa pepo na kuponya wagonjwa, siku ya tatu nakamilika.
Hébreux 2.10 Hébreux 5.9 Marc 6.26-6.28 Luc 9.7-9.9 Jean 19.30
33 Pamoja na hayo imenipasa kushika njia yangu leo na kesho na kesho kutwa; kwa kuwa haimkini nabii aangamie nje ya Yerusalemu.
Matthieu 21.11 Jean 9.4 Luc 9.53 Jean 12.35 Jean 4.34
34 Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii na kuwapiga kwa mawe waliotumwa kwako, mara ngapi nimetaka kuwakusanya watoto wako kama vile kuku avikusanyavyo vifaranga vyake chini ya mbawa zake, wala hamkutaka.
Deutéronome 32.11-32.12 Actes 7.52 Matthieu 23.37-23.39 Luc 19.44 Luc 19.41-19.42
35 Angalieni, mmeachiwa nyumba yenu! Nami nawaambia, Hamtaniona tena kamwe, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana.
Psaumes 118.26 Matthieu 21.9 Zacharie 11.1-11.2 Romains 10.9-10.15 Luc 21.24

Cette Bible est dans le domaine public.