Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 23.11
Bible en Swahili de l’est


1 Kisha Yesu akawaambia makutano na wanafunzi wake, akasema,
Luc 12.1 Matthieu 15.10-15.20 Marc 7.14 Luc 20.45-20.46 Luc 12.57
2 Waandishi na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa;
Luc 20.46 Marc 12.38 Esdras 7.25 Esdras 7.6 Malachie 2.7
3 basi, yo yote watakayowaambia, myashike na kuyatenda; lakini kwa mfano wa matendo yao, msitende; maana wao hunena lakini hawatendi.
2 Timothée 3.5 Tite 1.16 2 Chroniques 30.12 Exode 18.23 Deutéronome 17.9-17.12
4 Wao hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole chao.
Actes 15.10 Luc 11.46 Galates 6.13 Matthieu 11.28-11.30 Actes 15.28
5 Tena matendo yao yote huyatenda ili kutazamwa na watu; kwa kuwa hupanua hirizi zao, huongeza matamvua yao;
Matthieu 6.1-6.16 Deutéronome 6.8 Jean 5.44 Matthieu 9.20 Exode 13.9
6 hupenda viti vya mbele katika karamu, na kuketi mbele katika masinagogi,
Jacques 2.1-2.4 Luc 20.46-20.47 Marc 12.38-12.39 Luc 11.43-11.54 3 Jean 1.9
7 na kusalimiwa masokoni, na kuitwa na watu, Rabi.
Jean 1.38 Jean 1.49 Jean 3.2 Jean 3.26 Jean 6.25
8 Bali ninyi msiitwe Rabi, maana mwalimu wenu ni mmoja, nanyi nyote ni ndugu.
Jacques 3.1 Luc 22.32 Matthieu 23.10 Matthieu 26.49 2 Corinthiens 1.24
9 Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni.
Malachie 1.6 Romains 8.14-8.17 Hébreux 12.9 Job 32.21-32.22 1 Jean 3.1
10 Wala msiitwe viongozi; maana kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo.
11 Naye aliye mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu.
Galates 5.13 2 Corinthiens 4.5 Luc 22.26-22.27 Marc 10.43-10.44 Jean 13.14-13.15
12 Na ye yote atakayejikweza, atadhiliwa; na ye yote atakayejidhili, atakwezwa.
1 Pierre 5.5 Jacques 4.6 Luc 14.11 Luc 18.14 Proverbes 29.23
13 Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnawafungia watu ufalme wa mbinguni; ninyi wenyewe hamwingii, wala wanaoingia hamwaachi waingie.
Luc 11.52 Matthieu 23.27 Matthieu 23.29 Actes 8.1 Zacharie 11.17
14 [Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnakula nyumba za wajane, na kwa unafiki mnasali sala ndefu; kwa hiyo mtapata hukumu iliyo kubwa zaidi.]
15 Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnazunguka katika bahari na nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja kuwa mwongofu; na akiisha kufanyika, mnamfanya kuwa mwana wa jehanum mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe.
Actes 13.43 Actes 2.10 Actes 6.5 Matthieu 5.22 Actes 17.5-17.6
16 Ole wenu viongozi vipofu, ninyi msemao, Mtu atakayeapa kwa hekalu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa dhahabu ya hekalu, amejifunga.
Matthieu 15.14 Matthieu 23.24 Matthieu 5.33-5.35 Matthieu 23.17 Matthieu 23.19
17 Wapumbavu ninyi na vipofu; maana ni ipi iliyo kubwa, ile dhahabu, au lile hekalu liitakasalo dhahabu?
Matthieu 23.19 Nombres 16.38-16.39 Psaumes 94.8 Exode 30.26-30.29
18 Tena, Mtu atakayeapa kwa madhabahu, si kitu; bali mtu atakayeapa kwa sadaka iliyo juu yake, amejifunga.
19 Vipofu ninyi; maana ni ipi iliyo kubwa, ile sadaka, au ile madhabahu iitakasayo sadaka?
Exode 29.37 Exode 30.29
20 Basi yeye aapaye kwa madhabahu, huapa kwa hiyo, na kwa vitu vyote vilivyo juu yake.
21 Naye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo, na kwa yeye akaaye ndani yake.
1 Rois 8.13 Psaumes 26.8 2 Chroniques 6.2 2 Chroniques 7.2 Colossiens 2.9
22 Naye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa yeye aketiye juu yake.
Matthieu 5.34 Psaumes 11.4 Esaïe 66.1 Apocalypse 4.2-4.3 Actes 7.49
23 Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, na rehema, na imani; hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache.
Luc 11.42 Michée 6.8 Osée 6.6 1 Samuel 15.22 Lévitique 27.30
24 Viongozi vipofu, wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia.
Matthieu 19.24 Luc 6.7-6.10 Matthieu 15.2-15.6 Matthieu 27.6-27.8 Matthieu 23.16
25 Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya kikombe na chano, na ndani yake vimejaa unyang’anyi na kutokuwa na kiasi.
Luc 11.39-11.40 Matthieu 15.19-15.20 Esaïe 28.7-28.8 Marc 7.4-7.13
26 Ewe Farisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikombe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi.
Jacques 4.8 Luc 6.45 Jérémie 13.27 Matthieu 12.33 Ezéchiel 18.31
27 Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa mifupa ya wafu, na uchafu wote.
Actes 23.3 Luc 11.44 Nombres 19.16 Esaïe 58.1-58.2
28 Vivyo hivyo ninyi nanyi, kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, bali ndani mmejaa unafiki na maasi.
Matthieu 23.5 Luc 16.15 Marc 7.21-7.23 Matthieu 15.19-15.20 1 Samuel 16.7
29 Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnayajenga makaburi ya manabii, na kuyapamba maziara ya wenye haki,
Luc 11.47-11.48 Actes 2.29
30 na kusema, Kama sisi tungalikuwako zamani za baba zetu, hatungalishirikiana nao katika damu ya manabii.
Matthieu 21.35-21.36 2 Chroniques 36.15 Jérémie 2.30 Matthieu 23.34-23.35
31 Hivi mwajishuhudia wenyewe, ya kwamba ninyi ni wana wao waliowaua manabii.
Actes 7.51-7.52 1 Thessaloniciens 2.15-2.16 Josué 24.22 Psaumes 64.8 Job 15.5-15.6
32 Kijazeni basi kipimo cha baba zenu.
Genèse 15.16 Nombres 32.14 1 Thessaloniciens 2.16 Zacharie 5.6-5.11
33 Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum?
Matthieu 12.34 Matthieu 3.7 Luc 3.7 Jean 8.44 Matthieu 5.22
34 Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji;
Matthieu 10.16-10.17 Matthieu 10.23 Matthieu 13.52 Actes 13.1 Actes 5.40
35 hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu.
Zacharie 1.1 Genèse 4.8 Hébreux 11.4 2 Chroniques 24.20-24.22 Apocalypse 18.24
36 Amin, nawaambieni, Mambo hayo yote yatakuja juu ya kizazi hiki.
Matthieu 24.34 Matthieu 10.23 Luc 21.32-21.33 Ezéchiel 12.21-12.28 Marc 13.30-13.31
37 Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka!
Deutéronome 32.11-32.12 Ruth 2.12 Matthieu 5.12 Luc 13.34-13.35 Jérémie 6.16-6.17
38 Angalieni, nyumba yenu mmeachiwa hali ya ukiwa.
Jérémie 22.5 Luc 21.24 Marc 13.14 Zacharie 11.1-11.2 Psaumes 69.24
39 Kwa maana nawaambia, Hamtaniona kamwe tangu sasa, hata mtakaposema, Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana.
Psaumes 118.26 Matthieu 21.9 Romains 11.25 Jean 8.56 Luc 17.22

Cette Bible est dans le domaine public.