Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 16.14
Bible en Swahili de l’est


1 Wakamjia Mafarisayo na Masadukayo, wakamjaribu, wakamwomba awaonyeshe ishara itokayo mbinguni.
Luc 11.16 Matthieu 16.6 Actes 4.1 1 Corinthiens 1.22 Jean 8.6
2 Akajibu, akawaambia, [Kukiwa jioni, mwasema, Kutakuwa na kianga; kwa maana mbingu ni nyekundu.
Luc 12.54-12.56
3 Na asubuhi, mwasema, Leo kutakuwa na dhoruba; kwa maana mbingu ni nyekundu, tena kumetanda. Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa mbingu; lakini, je! Ishara za zamani hizi hamwezi kuzitambua?]
Luc 12.56 1 Chroniques 12.32 Matthieu 11.5 Matthieu 23.13 Luc 11.44
4 Kizazi kibaya na cha zinaa chataka ishara; wala hakitapewa ishara, isipokuwa ishara ya Yona. Akawaacha, akaenda zake.
Matthieu 12.39-12.40 Luc 11.29-11.30 Osée 4.17 Actes 18.6 Genèse 6.3
5 Nao wanafunzi wakaenda hata ng’ambo, wakasahau kuchukua mikate.
Marc 8.13-8.14 Matthieu 15.39
6 Yesu akawaambia, Angalieni, jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.
Luc 12.1 Marc 8.15 Galates 5.9 1 Corinthiens 5.6-5.8 2 Timothée 2.16-2.17
7 Wakabishana wao kwa wao, wakisema, Ni kwa sababu hatukuchukua mikate.
Marc 9.10 Luc 9.46 Actes 10.14 Marc 8.16-8.18 Matthieu 15.16-15.18
8 Naye Yesu akafahamu, akawaambia, Mbona mnabishana ninyi kwa ninyi, enyi wa imani chache, kwa sababu hamna mikate?
Matthieu 6.30 Matthieu 14.31 Matthieu 8.26 Marc 16.14 Jean 16.30
9 Hamjafahamu bado, wala hamkumbuki ile mikate mitano kwa wale elfu tano, na vikapu vingapi mlivyoviokota?
Matthieu 14.17-14.21 Matthieu 15.16-15.17 Jean 6.9-6.13 Luc 24.25-24.27 Marc 6.38-6.44
10 Wala ile mikate saba kwa watu elfu nne, na makanda mangapi mliyoyaokota?
Matthieu 15.34-15.38 Marc 8.17-8.21 Marc 8.5-8.9
11 Imekuwaje hamkufahamu ya kuwa si kwa sababu ya mkate naliwaambia? Ila jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.
Matthieu 16.6 Luc 12.56 Marc 8.21 Jean 8.43 Marc 4.40
12 Ndipo walipofahamu ya kuwa hakuwaambia kujilinda na chachu ya mkate, bali na mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.
Matthieu 23.13-23.28 Matthieu 5.20 Matthieu 15.4-15.9 Actes 23.8

Pierre reconnaît Jésus comme le Messie

13 Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?
Luc 9.18-9.20 Daniel 7.13 Matthieu 8.20 Matthieu 12.32 Matthieu 12.8
14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.
Marc 6.15 Matthieu 14.2 Malachie 4.5 Luc 9.8 Jean 7.12
15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?
Luc 9.20 Matthieu 13.11 Marc 8.29
16 Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.
Jean 11.27 1 Timothée 4.10 Matthieu 27.54 Matthieu 14.33 Matthieu 26.63
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.
Galates 1.16 Jean 6.45 Galates 1.11-1.12 Ephésiens 1.17-1.18 Matthieu 13.16-13.17
18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.
Ephésiens 2.19-2.22 Colossiens 1.18 1 Corinthiens 3.9-3.11 Jean 1.42 1 Timothée 3.15
19 Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.
Matthieu 18.18 Apocalypse 1.18 Esaïe 22.22 Jean 20.23 Apocalypse 3.7
20 Ndipo alipowakataza sana wanafunzi wake wasimwambie mtu ye yote ya kwamba yeye ndiye Kristo.
Marc 8.30 Luc 9.21 Matthieu 17.9 Matthieu 8.4 Jean 1.41
21 Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaonya wanafunzi wake ya kwamba imempasa kwenda Yerusalemu, na kupata mateso mengi kwa wazee na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu kufufuka.
Matthieu 27.63 Matthieu 17.12 Matthieu 17.22-17.23 Matthieu 20.28 Luc 24.6-24.7
22 Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata.
Marc 8.32 Actes 21.11-21.13 Matthieu 16.16-16.17 Matthieu 26.51-26.53 Jean 13.6-13.8
23 Akageuka, akamwambia Petro, Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.
Colossiens 3.2 Philippiens 3.19 Marc 8.33 Matthieu 4.10 Romains 8.5-8.8
24 Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.
Matthieu 10.38 Luc 14.27 1 Pierre 4.1-4.2 Marc 10.21 2 Timothée 3.12
25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.
Matthieu 10.39 Apocalypse 12.11 Actes 20.23-20.24 Marc 8.35 Luc 17.33
26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
Job 27.8 Luc 12.20 Marc 8.36-8.37 Luc 9.25 Psaumes 49.7-49.8
27 Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
Romains 2.6 2 Corinthiens 5.10 Apocalypse 22.12-22.15 Zacharie 14.5 Proverbes 24.12
28 Amin, nawaambieni, Pana watu katika hawa wasimamao hapa, ambao hawataonja mauti kabisa, hata watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika ufalme wake.
Luc 9.27 Jean 8.52 Hébreux 2.9 Marc 9.1 Matthieu 10.23

Cette Bible est dans le domaine public.