Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 34.9
Bible en Swahili de l’est


Jugement des bergers infidèles

1 Neno la Bwana likanijia, kusema,
2 Mwanadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli, toa unabii, uwaambie, naam, hao wachungaji, Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao wachungaji wa Israeli, wanaojilisha wenyewe; je! Haiwapasi wachungaji kuwalisha kondoo?
Jérémie 23.1 Jérémie 3.15 Esaïe 40.11 Jean 21.15-21.17 Luc 20.46-20.47
3 Mnawala walionona, mnajivika manyoya, mnawachinja walionona; lakini hamwalishi kondoo.
Zacharie 11.16 Zacharie 11.5 Jérémie 2.30 1 Rois 21.13-21.16 Ezéchiel 19.3
4 Wagonjwa hamkuwatia nguvu, wala hamkuwaponya wenye maradhi, wala hamkuwafunga waliovunjika, wala hamkuwarudisha waliofukuzwa, wala hamkuwatafuta waliopotea; bali kwa nguvu na kwa ukali mmewatawala.
Ezéchiel 34.16 Matthieu 9.36 Matthieu 18.12-18.13 Exode 1.13-1.14 Zacharie 11.15-11.16
5 Nao wakatawanyika, kwa sababu hapakuwa na mchungaji; wakawa chakula cha wanyama- mwitu, wakatawanyika.
Matthieu 9.36 Jérémie 50.17 Esaïe 56.9 1 Rois 22.17 Jérémie 23.2
6 Kondoo zangu walitanga-tanga katika milima yote, na juu ya kila kilima kirefu; naam, kondoo zangu walitawanyika juu ya uso wote wa dunia; wala hapakuwa na mtu aliyewaulizia, wala kuwatafuta.
1 Pierre 2.25 Psaumes 142.4 Jérémie 40.11-40.12 Ezéchiel 7.16 Jean 10.16
7 Basi, enyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana;
Jérémie 13.13 Malachie 2.1 Ezéchiel 34.9 Luc 11.39-11.54 Jérémie 22.2-22.3
8 Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, kwa sababu kondoo zangu walikuwa mateka, kondoo zangu wakawa chakula cha wanyama-mwitu wote, kwa sababu hapakuwa na mchungaji, wala wachungaji wangu hawakutafuta kondoo zangu, bali wachungaji walijilisha wenyewe wala hawakuwalisha kondoo zangu;
Ezéchiel 34.31 Ezéchiel 34.18 Ezéchiel 34.2-34.3 Ezéchiel 34.5-34.6 Ezéchiel 34.10
9 kwa sababu hiyo, enyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana;
10 Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu ya wachungaji; nami nitawataka kondoo zangu mikononi mwao, nami nitawaachisha hiyo kazi ya kuwalisha kondoo; nao wachungaji hawatajilisha wenyewe tena; nami nitawaokoa kondoo zangu vinywani mwao, wasiwe tena chakula chao.
Ezéchiel 34.2 Zacharie 10.3 Jérémie 21.13 Ezéchiel 13.8 Ezéchiel 3.18

Le vrai berger d’Israël

11 Maana, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi mwenyewe, naam, mimi, nitawatafuta kondoo zangu, na kuwaulizia.
Luc 19.10 Psaumes 80.1 Jérémie 31.8 Deutéronome 32.39 Esaïe 40.10-40.11
12 Kama vile mchungaji atafutavyo kondoo zake, siku ile anapokuwa kati ya kondoo zake waliotawanyika; ndivyo nitakavyowatafuta kondoo zangu; nami nitawaokoa katika mahali pote walipotawanyika, katika siku ya mawingu na giza.
Jean 10.11-10.12 Ezéchiel 30.3 Luc 15.4-15.6 Luc 19.10 Esaïe 40.11
13 Nami nitawatoa katika watu wa mataifa, na kuwakusanya katika nchi zote, nami nitawarudisha katika nchi yao wenyewe; nami nitawalisha juu ya milima ya Israeli, kando ya mifereji ya maji; na katika mahali pote pa nchi panapokaliwa na watu.
Ezéchiel 28.25-28.26 Ezéchiel 11.17 Esaïe 11.11-11.16 Esaïe 65.9-65.10 Psaumes 106.47
14 Nami nitawalisha malisho mema, pa juu ya milima ya mahali palipoinuka pa Israeli litakuwa zizi lao; huko watalala katika zizi jema; nao watakula malisho mema, juu ya milima ya Israeli.
Jean 10.9 Jérémie 31.12-31.14 Jérémie 31.25 Esaïe 30.23-30.24 Apocalypse 7.16
15 Mimi mwenyewe nitawalisha kondoo zangu, nami nitawalaza, asema Bwana MUNGU.
Jérémie 3.15 Osée 2.18 Jean 21.15 Ezéchiel 34.23 Esaïe 27.10
16 Nami nitawatafuta waliopotea, nitawarudisha waliofukuzwa, nitawafunga waliovunjika, nitawatia nguvu wagonjwa; nao wanono na wenye nguvu nitawaharibu; nitawalisha hukumu.
Esaïe 49.26 Esaïe 10.16 Esaïe 5.17 Luc 19.10 Ezéchiel 34.4
17 Na kwa habari zenu, Enyi kundi langu, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nahukumu kati ya mnyama na mnyama, kondoo waume na mbuzi waume pia.
Matthieu 25.32-25.33 Ezéchiel 34.20-34.22 Zacharie 10.3 Ezéchiel 20.37-20.38
18 Je! Mwaona ya kuwa ni neno dogo ninyi kulishwa malisho mema, hata mkawa hamna budi hukanyaga kwa miguu yenu yaliyosalia? Na kuwa mmekunywa maji yaliyo safi, nanyi hamna budi kuyatibua kwa miguu yaliyobaki?
Matthieu 23.13 Nombres 16.13 Esaïe 7.13 Luc 11.52 Ezéchiel 32.2
19 Na kwa habari za kondoo zangu, wao wanakula hayo mliyoyakanyaga kwa miguu yenu, nao wanakunywa maji mliyoyatibua kwa miguu yenu.
20 Kwa sababu hiyo, Bwana MUNGU awaambia hivi; Tazama, mimi, naam, mimi, nitahukumu kati ya wanyama walionona na wanyama waliokonda.
Ezéchiel 34.10 Psaumes 22.12-22.16 Ezéchiel 34.17 Matthieu 25.31-25.46
21 Kwa kuwa mmesukuma kwa ubavu, na kwa mabega, na kuwapiga wenye maradhi kwa pembe zenu, hata mkawatawanyia mbali;
Zacharie 11.5 Luc 13.14-13.16 Deutéronome 33.17 Daniel 8.3-8.10 Zacharie 11.16-11.17
22 basi mimi nitaliokoa kundi langu, wala hawatakuwa mateka tena; nami nitahukumu kati ya mnyama na mnyama.
Psaumes 72.12-72.14 Jérémie 23.2-23.3 Ezéchiel 34.10 Zacharie 11.7-11.9
23 Nami nitaweka mchungaji mmoja juu yao, naye atawalisha, naam, mtumishi wangu, Daudi; yeye atawalisha, naye atakuwa mchungaji wao.
Jean 10.11 Esaïe 40.11 Jérémie 30.9 Ezéchiel 37.24-37.25 Apocalypse 22.16
24 Na mimi, Bwana, nitakuwa Mungu wao, na mtumishi wangu, Daudi, atakuwa mkuu kati yao; mimi, Bwana, nimesema haya.
Ezéchiel 37.27 Ezéchiel 36.28 Josué 5.13-5.15 Michée 5.2 Matthieu 28.18
25 Nami nitafanya agano la amani nao, nami nitawakomesha wanyama wakali kati yao; nao watakaa salama jangwani, na kulala misituni.
Esaïe 11.6-11.9 Lévitique 26.6 Ezéchiel 37.26 Esaïe 35.9 Ezéchiel 34.28
26 Nami nitawafanya wao, na mahali palipo pande zote za mlima wangu, kuwa baraka, nami nitaleta manyunyu kwa wakati wake; yatakuwako manyunyu ya baraka.
Deutéronome 28.12 Lévitique 26.4 Malachie 3.10 Genèse 12.2 Esaïe 44.3
27 Na mti wa kondeni utazaa matunda yake, nayo ardhi itatoa mazao yake, nao watakuwa salama katika nchi yao; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapovunja vifungo vya kongwa lao, na kuwaokoa katika mikono ya watu wale waliowatumikisha.
Jérémie 30.8 Lévitique 26.13 Esaïe 52.2-52.3 Lévitique 26.4 Ezéchiel 39.28
28 Hawatakuwa mateka ya makafiri tena, wala mnyama wa nchi hatawala; bali watakaa salama salimini, wala hapana mtu atakayewatia hofu.
Jérémie 30.10 Ezéchiel 34.25 Ezéchiel 39.26 Ezéchiel 36.15 Jérémie 46.27
29 Nami nitawainulia miche iwe sifa njema, wala hawataangamizwa kwa njaa katika nchi yao tena, wala hawatachukua tena aibu ya makafiri.
Ezéchiel 36.29 Esaïe 4.2 Ezéchiel 34.26-34.27 Ezéchiel 36.15 Esaïe 49.9-49.10
30 Nao watajua ya kuwa mimi, Bwana, Mungu wao, ni pamoja nao, na ya kuwa wao, nyumba ya Israeli, ni watu wangu, asema Bwana MUNGU.
Psaumes 46.7 Ezéchiel 37.27 Ezéchiel 34.24 Psaumes 46.11 Esaïe 8.9-8.10
31 Na ninyi, kondoo zangu, kondoo za malisho yangu, ni wanadamu, na mimi ni Mungu wenu, asema Bwana MUNGU.
Psaumes 100.3 Psaumes 80.1 Ezéchiel 36.38 Psaumes 78.52 Jean 10.16

Cette Bible est dans le domaine public.