Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 36.13
Bible en Swahili de l’est


Les prophéties de Jérémie brûlées

1 Ikawa katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, neno hili likamjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, kusema,
Jérémie 25.1 2 Chroniques 36.5 2 Rois 24.1-24.2 Jérémie 45.1 Jérémie 35.1
2 Twaa gombo la chuo, ukaandike ndani yake maneno yote niliyokuambia juu ya Israeli, na juu ya Yuda, na juu ya mataifa yote, tangu siku ile niliponena nawe, tangu siku za Yosia, hata siku hii ya leo.
Jérémie 30.2 Exode 17.14 Jérémie 25.3 Jérémie 1.10 Esaïe 8.1
3 Huenda nyumba ya Yuda watasikia mabaya yote niliyokusudia kuwatenda; wapate kurudi, kila mtu akaiache njia yake mbaya; nami nikawasamehe uovu wao na dhambi yao.
Jérémie 18.8 Jérémie 26.3 Ezéchiel 12.3 Jérémie 36.7 Deutéronome 30.2
4 Kisha Yeremia akamwita Baruku, mwana wa Neria; naye Baruku akaandika katika gombo la chuo maneno yote ya Bwana, yaliyotoka kinywani mwa Yeremia, ambayo Bwana amemwambia.
Jérémie 32.12 Ezéchiel 2.9 Jérémie 36.32 Jérémie 43.3 Jérémie 45.1-45.2
5 Yeremia akamwagiza Baruku, ya kwamba, Mimi nimefungwa, siwezi kuingia katika nyumba ya Bwana.
Jérémie 32.2 Jérémie 33.1 2 Corinthiens 11.23 Jérémie 38.6 Ephésiens 3.1
6 Basi, enenda wewe, ukasome katika gombo la chuo, ambacho umeandika ndani yake, maneno ya Bwana yaliyotoka kinywani mwangu, ukiyasoma katika masikio ya watu, ndani ya nyumba ya Bwana, siku ya kufunga; pia utayasoma masikioni mwa watu wote wa Yuda, watokao katika miji yao.
Jérémie 36.8-36.9 Jérémie 26.2 Jérémie 19.14 Ezéchiel 2.3-2.7 Lévitique 23.27-23.32
7 Labda wataomba dua zao mbele za Bwana, na kurudi, kila mtu akiiacha njia yake mbaya; kwa maana hasira na ghadhabu ni kuu sana, alizotamka Bwana juu ya watu hawa.
Jérémie 36.3 Jérémie 21.5 Jérémie 4.4 2 Rois 22.17 2 Rois 22.13
8 Basi, Baruku, mwana wa Neria, akafanya sawasawa na hayo yote, ambayo Yeremia, nabii, amemwagiza, akisoma katika chuo hicho, maneno ya Bwana, ndani ya nyumba ya Bwana.
Jérémie 1.17 Philippiens 2.19-2.22 Luc 4.16-4.30 Néhémie 8.3 1 Corinthiens 16.10
9 Basi, ikawa katika mwaka wa tano wa Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, katika mwezi wa kenda, watu wote waliokuwa katika Yerusalemu, na watu wote waliokuja Yerusalemu kutoka miji yote ya Yuda, wakapiga mbiu ya kufunga mbele za Bwana.
2 Chroniques 20.3 Jonas 3.5 Jérémie 36.22 Esther 4.16 Jérémie 36.1
10 Basi, wakati huo Baruku akayasoma maneno ya Yeremia katika nyumba ya Bwana, katika chumba cha Gemaria, mwana wa Shafani, mwandishi, katika ua wa juu, mahali pa kuingilia kwa lango jipya la nyumba ya Bwana, akiyasoma katika masikio ya watu wote.
Jérémie 36.11 Jérémie 26.10 Jérémie 52.25 Jérémie 35.4 2 Samuel 8.17
11 Basi, Mikaya, mwana wa Gemaria, mwana wa Shafani, aliposikia maneno yote ya Bwana yaliyokuwa katika chuo hicho,
2 Rois 25.22 Jérémie 36.10 2 Chroniques 34.20 2 Rois 22.12-22.14
12 akashuka, akaingia katika nyumba ya mfalme, katika chumba cha mwandishi, na, tazama, wakuu wote wameketi humo, nao ni hawa, Elishama, mwandishi, na Delaya, mwana wa Shemaya, na Elnathani, mwana wa Akbori, na Gemaria, mwana wa Shafani, na Sedekia, mwana wa Hanania, na wakuu wote.
Jérémie 26.22 Jérémie 36.25 2 Rois 22.12 Jérémie 41.1 Jérémie 36.10-36.11
13 Naye Mikaya akawaeleza maneno yote aliyoyasikia, hapo Baruku alipokuwa akikisoma kitabu masikioni mwa watu.
2 Rois 22.10 2 Chroniques 34.24 2 Rois 22.19 2 Chroniques 34.16-34.18 Jonas 3.6
14 Basi, wakuu wote wakamtuma Yehudi, mwana wa Nethania, mwana wa Shelemia, mwana wa Kushi, aende kwa Baruku, kumwambia, Litwae mkononi mwako gombo lile ulilolisoma masikioni mwa watu, uje huku. Basi, Baruku, mwana wa Neria, akalitwaa gombo lile mkononi mwake, akaenda kwao.
Jérémie 36.2 Jérémie 36.21 Jérémie 41.18 Jérémie 41.16 Matthieu 10.16
15 Nao wakamwambia, Keti sasa, ukalisome masikioni mwetu. Basi, Baruku akalisoma masikioni mwao.
16 Ikawa, walipoyasikia maneno hayo yote, wakatazamana kwa hofu, wakamwambia Baruku, Hatuna budi kumwambia mfalme maneno haya yote.
Jérémie 36.24 Amos 7.10-7.11 Jérémie 13.18 Actes 24.25-24.26 Jérémie 38.1-38.4
17 Wakamwuliza Baruku, wakisema, Tuambie sasa; ulipataje kuyaandika maneno haya yote kinywani mwake?
Jean 9.15 Jean 9.26-9.27 Jean 9.10-9.11
18 Baruku akawajibu, Alinitamkia maneno haya yote kwa kinywa chake, nami nikayaandika kwa wino kitabuni.
Jérémie 36.4 Jérémie 36.2 Proverbes 26.4-26.5 Jérémie 43.2-43.3
19 Ndipo hao wakuu wakamwambia Baruku, Enenda ukajifiche, wewe na Yeremia, wala mtu asipajue mlipo.
1 Rois 17.3 1 Rois 18.4 1 Rois 18.10 Jérémie 36.26 Jérémie 26.20-26.24
20 Wakaenda kwa mfalme uwandani; lakini walikuwa wameliweka lile gombo katika chumba cha Elishama, mwandishi wakayanena maneno hayo yote masikioni mwa mfalme.
Jérémie 36.12 Jérémie 36.21
21 Basi, mfalme akamtuma Yehudi aende akalilete lile gombo; naye akalitoa katika chumba cha Elishama, mwandishi. Yehudi akalisoma masikioni mwa mfalme, na masikioni mwa wakuu waliosimama mbele ya mfalme.
2 Rois 22.10 Ezéchiel 2.4-2.5 2 Chroniques 34.18 Jérémie 23.28 Jérémie 36.15
22 Basi mfalme alikuwa ameketi katika nyumba iliyotumika wakati wa baridi, mwezi wa kenda; na pale palikuwa na moto wa makaa mbele yake.
Amos 3.15 Jérémie 36.9 Jérémie 3.20 Jérémie 22.14-22.16
23 Hata ikawa, Yehudi alipokuwa amekwisha kusoma kurasa tatu nne, mfalme akalikata kwa kijembe, akalitupa katika moto wa makaa, hata gombo lote likawa limekwisha kuteketea katika huo moto wa makaa.
1 Rois 22.8 Proverbes 13.13 Proverbes 1.30 Proverbes 21.30 Esaïe 28.14-28.15
24 Lakini hawakuogopa, wala hawakurarua mavazi yao, wala mfalme, wala watumishi wake hata mmoja waliosikia maneno hayo yote.
Jérémie 36.16 Psaumes 36.1 Esaïe 36.22-37.1 2 Rois 19.1-19.2 Jonas 3.6
25 Hata hivyo Elnathani, na Delaya, na Gemaria, walikuwa wamemsihi mfalme asiliteketeze gombo lile, lakini hakukubali kuwasikia.
Actes 5.34-5.39 Genèse 37.22 Jérémie 36.12 Genèse 37.26-37.28 Matthieu 27.4
26 Mfalme akamwamuru Yerameeli, mwana wa mfalme, na Seraya, mwana wa Azrieli, na Shelemia, mwana wa Abdeeli, wamkamate Baruku, mwandishi, na Yeremia, nabii; lakini Bwana aliwaficha.
1 Rois 19.10 Psaumes 91.1 1 Rois 19.1-19.3 1 Rois 19.14 1 Rois 17.3
27 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia, hapo mfalme alipokuwa amekwisha kuliteketeza gombo lile, na maneno yale aliyoyaandika Baruku, yaliyotoka katika kinywa cha Yeremia, kusema,
Jérémie 36.4
28 Haya! Twaa wewe gombo lingine, ukaandike ndani yake maneno yote ya kwanza, yaliyokuwa katika gombo la kwanza, ambalo Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, ameliteketeza.
Zacharie 1.5-1.6 Jérémie 28.13-28.14 Jérémie 44.28 Job 23.13 Matthieu 24.35
29 Na katika habari za Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, utasema, Bwana asema hivi, Umeliteketeza gombo hili, ukisema, Mbona umeandika ndani yake, ukisema, Bila shaka mfalme wa Babeli atakuja, na kuiharibu nchi hii, na kukomesha mwanadamu na mnyama pia ndani yake?
Jérémie 26.9 Esaïe 30.10 Job 15.24 Esaïe 45.9 Jérémie 32.3
30 Basi, Bwana aseme hivi, katika habari za Yehoyakimu, mfalme wa Yuda; Hatakuwa na mtu wa kukaa katika kiti cha enzi cha Daudi; na mzoga wake utatupwa nje wakati wa mchana upigwe kwa hari, na wakati wa usiku upigwe kwa baridi.
Jérémie 22.30 2 Rois 24.12-24.15 Genèse 31.40 Jérémie 22.18-22.19
31 Nami nitamwadhibu yeye, na wazao wake, na watumishi wake, kwa sababu ya uovu wao, nami nitaleta juu yao, na juu ya wenyeji wa Yerusalemu, na juu ya watu wa Yuda, mabaya yote niliyoyatamka juu yao, lakini hawakukubali kusikiliza.
Proverbes 29.1 Jérémie 23.34 Jérémie 35.17 Jérémie 19.15 Jérémie 11.8
32 Ndipo Yeremia akatwaa gombo lingine, akampa Baruku, mwandishi, mwana wa Neria, naye akayaandika maneno yote yaliyotoka katika kinywa cha Yeremia, ya kitabu kile alichokiteketeza Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, katika moto; tena maneno mengi zaidi kama yale yakatiwa ndani yake.
Jérémie 36.4 Jérémie 36.18 Exode 4.15-4.16 Jérémie 36.23 Lévitique 26.28

Cette Bible est dans le domaine public.