Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 22.29
Bible en Swahili de l’est


Oracles contre les derniers rois de Juda

1 Bwana akasema hivi, Shuka nyumbani kwa mfalme wa Yuda, ukaseme neno hili huko,
2 Chroniques 19.2-19.3 Amos 7.13 2 Samuel 24.11-24.12 Jérémie 21.11 Marc 6.18
2 ya kwamba, Sikia neno la Bwana, Ee mfalme wa Yuda; wewe uketiye katika kiti cha enzi cha Daudi, wewe, na watumishi wako, na watu wako wote waingiao kwa malango haya;
Luc 1.32 Esaïe 9.7 Jérémie 22.4 Ezéchiel 34.7 Amos 7.16
3 Bwana asema hivi, Fanyeni hukumu na haki, mkamtoe yeye aliyetekwa katika mikono ya mdhalimu; wala msiwatende mabaya mgeni, wala yatima, wala mjane, wala kuwadhulumu, wala msimwage damu ya mtu asiye na hatia katika mahali hapa.
Jérémie 21.12 Jérémie 22.17 Ezéchiel 22.7 Michée 6.8 Joël 3.19
4 Kwa maana mkifanya haya kweli kweli, ndipo watakapoingia kwa malango ya nyumba hii wafalme wenye kuketi katika kiti cha enzi cha Daudi, wanakwenda kwa magari, na wamepanda farasi yeye, na watumishi wake, na watu wake.
Jérémie 17.25
5 Lakini kama hamtaki kusikia maneno haya, mimi naapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, ya kuwa nyumba hii itakuwa ukiwa.
Hébreux 6.13 Amos 6.8 Genèse 22.16 Jérémie 17.27 Deutéronome 32.40-32.42
6 Kwa maana Bwana asema hivi, katika habari ya nyumba ya mfalme wa Yuda; Wewe u Gileadi kwangu, na kichwa cha Lebanoni; Ila hakika nitakufanya kuwa jangwa, na miji isiyokaliwa na watu.
Esaïe 6.11 Psaumes 107.34 Michée 3.12 Esaïe 27.10 Genèse 37.25
7 Nami nitakufanyia tayari watu wenye kuharibu, kila mtu na silaha zake; Nao watakata mierezi miteule yako, na kuitupa motoni.
Esaïe 10.33-10.34 Esaïe 37.24 Jérémie 4.6-4.7 Ezéchiel 9.1-9.7 Jérémie 21.14
8 Na mataifa mengi watapita karibu na mji huu, nao watasema kila mtu na jirani yake, Nini maana yake Bwana kuutenda hivi mji huu mkubwa?
1 Rois 9.8-9.9 2 Chroniques 7.20-7.22 Lamentations 2.15-2.17 Deutéronome 29.23-29.26 Daniel 9.7
9 Ndipo watakapojibu, Ni kwa sababu waliliacha agano la Bwana, Mungu wao, wakaabudu miungu mingine, na kuitumikia.
2 Rois 22.17 2 Chroniques 34.25 Jérémie 40.2-40.3 Deutéronome 29.25-29.28 Jérémie 50.7
10 Msimlilie aliyekufa, wala msimwombolezee, Bali mlilieni huyo aendaye zake mbali; Kwa maana yeye hatarudi tena, Wala hataiona nchi aliyozaliwa.
Ecclésiaste 4.2 Esaïe 57.1 Lamentations 4.9 Jérémie 22.11 2 Rois 23.30-23.34
11 Maana Bwana asema hivi, katika habari za Shalumu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda; aliyemiliki badala ya Yosia, baba yake, yeye aliyetoka mahali hapa; Hatarudi huku tena;
1 Chroniques 3.15 2 Chroniques 36.1-36.4 2 Rois 23.34 2 Rois 23.31 2 Chroniques 28.12
12 bali katika mahali pale walipomchukua mateka ndipo atakapokufa, wala hataiona nchi hii tena kamwe.
2 Rois 23.34 Jérémie 22.18
13 Ole wake aijengaye nyumba yake kwa uovu! Na vyumba vyake kwa udhalimu! Atumiaye utumishi wa mwenzake bila ujira, Wala hampi mshahara wake;
Michée 3.10 Lévitique 19.13 Jacques 5.4 Deutéronome 24.14-24.15 Habakuk 2.9-2.11
14 Asemaye, Nitajijengea nyumba pana na vyumba vipana; Naye hujikatia madirisha; Na kuta zake zimefunikwa kwa mierezi, Na kupakwa rangi nyekundu.
2 Samuel 7.2 Aggée 1.4 Esaïe 5.8-5.9 Cantique 1.17 Proverbes 17.19
15 Je! Utatawala kwa sababu unashindana na watu kwa mierezi? Baba yako, je! Hakula na kunywa, na kufanya hukumu na haki? Hapo ndipo alipofanikiwa.
2 Rois 23.25 Esaïe 3.10 Proverbes 29.4 Proverbes 25.5 Ecclésiaste 10.17
16 Alihukumu maneno ya maskini na mhitaji; hapo ndipo alipofanikiwa. Je! Huku siko kunijua, asema Bwana?
Jérémie 9.24 Psaumes 72.12-72.13 Psaumes 72.1-72.4 Esaïe 1.17 Tite 1.16
17 Bali macho yako na moyo wako hauna utakalo ila kutamani, na kumwaga damu isiyo na hatia, na kudhulumu, na kutenda jeuri.
2 Rois 24.4 2 Pierre 2.14 Ezéchiel 19.6 Jérémie 22.3 Psaumes 10.3
18 Basi, Bwana asema hivi, katika habari ya Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda; Hawatamwombolezea, wakisema, Aa! Ndugu yangu; au, Aa! Dada yangu; wala hawatamlilia, wakisema, Aa! Bwana wangu; au, Aa! Utukufu wake.
Jérémie 16.6 1 Rois 13.30 Jérémie 22.10 Jérémie 16.4 2 Chroniques 35.25
19 Atazikwa maziko ya punda, akibururwa, na kutupwa nje ya malango ya Yerusalemu.
Jérémie 36.30 1 Rois 21.23-21.24 1 Rois 14.10 Jérémie 36.6 Jérémie 15.3
20 Haya panda Lebanoni, ukalie Upalize sauti yako katika Bashani; Ukalie kutoka Abarimu; Maana wapenzi wako wote wameangamia.
Nombres 27.12 Ezéchiel 23.22 Lamentations 1.2 Lamentations 1.19 Esaïe 31.1-31.3
21 Mimi nalisema nawe wakati wa kufanikiwa kwako; lakini ulisema, Sitaki kusikia. Hii ndiyo iliyokuwa desturi yako tangu ujana wako, kutokuitii sauti yangu.
Jérémie 3.25 Jérémie 32.30 Proverbes 30.9 Esaïe 48.8 Jérémie 7.22-7.28
22 Upepo utawalisha wachungaji wako wote, na wapenzi wako watakwenda kufungwa; hakika wakati huo utatahayarika, na kufadhaika kwa sababu ya uovu wako wote.
Jérémie 10.21 Jérémie 12.10 Osée 13.15 Jérémie 23.1-23.2 Zacharie 11.17
23 Wewe ukaaye Lebanoni, Ufanyaye kioto chako katika mierezi, Utakuwa na hali ya kuhurumiwa sana, Upatapo utungu kama wa mwanamke azaaye.
Jérémie 6.24 Jérémie 4.30-4.31 Jérémie 22.6 Amos 9.2 Habakuk 2.9
24 Kama niishivyo mimi, asema Bwana, hata Konia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, angekuwa pete yenye muhuri katika mkono wangu wa kuume, ningekung’oa wewe hapo;
Jérémie 37.1 Aggée 2.23 Cantique 8.6 1 Chroniques 3.16 2 Rois 24.6-24.8
25 nami nitakutia katika mikono ya watu wale wakutafutao roho yako, na katika mikono yao unaowaogopa, naam, katika mikono ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, na katika mikono ya Wakaldayo.
Jérémie 34.20-34.21 Jérémie 21.7 2 Rois 24.15-24.16 Proverbes 10.24 Jérémie 22.28
26 Nami nitakutupa nje, wewe na mama yako aliyekuzaa, mwende nchi nyingine ambayo hamkuzaliwa huko, nanyi mtakufa huko.
2 Rois 24.15 2 Rois 24.8 Esaïe 22.17 Jérémie 15.2-15.4 Ezéchiel 19.9-19.14
27 Lakini nchi ile ambayo wanatamani kuirudia, hawatairudia kamwe.
Jérémie 44.14 Jérémie 52.31-52.34 Jérémie 22.11 Psaumes 86.4 2 Rois 25.27-25.30
28 Je! Mtu huyu, Konia, ni chombo kilichodharauliwa, na kuvunjika? Ni chombo kisichopendeza? Mbona wametupwa, yeye na wazao wake, na kutupwa katika nchi wasiyoijua?
Osée 8.8 Psaumes 31.12 Jérémie 48.38 Romains 9.21-9.23 Matthieu 1.12-1.16
29 Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la Bwana.
Michée 1.2 Deutéronome 32.1 Jérémie 6.19 Deutéronome 4.26 Michée 6.1-6.2
30 Bwana asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda.
Jérémie 36.30 Psaumes 94.20 Luc 1.32-1.33 Jérémie 10.21 Matthieu 1.11-1.16

Cette Bible est dans le domaine public.