Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 25.5
Bible en Swahili de l’est


Recherche du pardon de Dieu

1 Ee Bwana, nakuinulia nafsi yangu,
Psaumes 143.8 Psaumes 86.4 Lamentations 3.41 Psaumes 24.4 1 Samuel 1.15
2 Ee Mungu wangu, Nimekutumaini Wewe, nisiaibike, Adui zangu wasifurahi kwa kunishinda.
Psaumes 31.1 Psaumes 41.11 Esaïe 49.23 Psaumes 71.1 Esaïe 26.3
3 Naam, wakungojao hawataaibika hata mmoja; Wataaibika watendao uhaini bila sababu.
Lamentations 3.25 Esaïe 49.23 Psaumes 62.5 Esaïe 40.31 Michée 7.7
4 Ee Bwana, unijulishe njia zako, Unifundishe mapito yako,
Exode 33.13 Psaumes 27.11 Psaumes 5.8 Psaumes 86.11 Psaumes 143.8
5 Uniongoze katika kweli yako, Na kunifundisha. Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu, Nakungoja Wewe mchana kutwa.
Psaumes 88.1 Psaumes 79.9 Apocalypse 7.17 Jérémie 31.9 Proverbes 8.34
6 Ee Bwana, kumbuka rehema zako na fadhili zako, Maana zimekuwako tokea zamani.
Psaumes 103.17 Psaumes 69.16 Esaïe 63.15 Psaumes 98.3 Psaumes 106.1
7 Usiyakumbuke makosa ya ujana wangu, Wala maasi yangu. Unikumbuke kwa kadiri ya fadhili zako, Ee Bwana kwa ajili ya wema wako.
Psaumes 51.1 Job 13.26 Job 20.11 Jérémie 3.25 Esaïe 38.17
8 Bwana yu mwema, mwenye adili, Kwa hiyo atawafundisha wenye dhambi njia.
Psaumes 92.15 Psaumes 32.8 Jacques 1.5 Matthieu 9.13 Luc 11.13
9 Wenye upole atawaongoza katika hukumu, Wenye upole atawafundisha njia yake.
Jean 14.6 Jacques 1.21 Psaumes 27.11 1 Pierre 3.15 Matthieu 5.5
10 Njia zote za Bwana ni fadhili na kweli, Kwao walishikao agano lake na shuhuda zake.
Jean 1.17 Hébreux 12.14 Hébreux 8.8-8.12 Genèse 48.15-48.16 Psaumes 103.17-103.18
11 Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, Unisamehe uovu wangu, maana ni mwingi.
Psaumes 79.9 Psaumes 31.3 Esaïe 43.25 Psaumes 109.21 1 Jean 2.12
12 Ni nani amchaye Bwana? Atamfundisha katika njia anayoichagua.
Psaumes 37.23 2 Thessaloniciens 2.10-2.12 Psaumes 32.8 Psaumes 111.10 Proverbes 1.7
13 Nafsi yake itakaa hali ya kufanikiwa; Wazao wake watairithi nchi.
Proverbes 1.33 Proverbes 19.23 Psaumes 37.11 Matthieu 5.5 Psaumes 69.36
14 Siri ya Bwana iko kwao wamchao, Naye atawajulisha agano lake.
Jean 7.17 Proverbes 3.32 Jean 15.15 1 Corinthiens 2.14 Matthieu 13.11-13.12
15 Macho yangu humwelekea Bwana daima, Naye atanitoa miguu yangu katika wavu.
Psaumes 141.8 Psaumes 31.4 Psaumes 123.2 2 Timothée 2.25-2.26 Psaumes 121.1-121.2
16 Uniangalie na kunifadhili, Maana mimi ni mkiwa na mteswa.
Psaumes 143.4 Psaumes 86.16 Daniel 9.17 Michée 7.19 Psaumes 60.1
17 Katika shida za moyo wangu unifanyie nafasi, Na kunitoa katika dhiki zangu.
1 Corinthiens 4.11-4.13 Psaumes 107.6 Habakuk 3.17-3.19 Psaumes 77.2-77.4 2 Corinthiens 4.8-4.9
18 Utazame teso langu na taabu yangu; Unisamehe dhambi zangu zote.
2 Samuel 16.12 1 Samuel 1.11 Matthieu 9.2 Psaumes 32.1-32.5 Psaumes 119.153
19 Uwatazame adui zangu, maana ni wengi, Wananichukia kwa machukio ya ukali.
Psaumes 57.4 2 Samuel 16.11 Psaumes 3.1-3.2 2 Samuel 17.2-17.4 Luc 23.21-23.23
20 Unilinde nafsi yangu na kuniponya, Nisiaibike, maana nakukimbilia Wewe.
Joël 2.26-2.27 Psaumes 17.8 Psaumes 86.2 Actes 7.59 Psaumes 121.7
21 Ukamilifu na unyofu zinihifadhi, Maana nakungoja Wewe.
Psaumes 41.12 Proverbes 20.7 Daniel 6.22 1 Samuel 24.11-24.13 Proverbes 11.3
22 Ee Mungu, umkomboe Israeli, Katika taabu zake zote.
Psaumes 130.8 Psaumes 122.6 Psaumes 14.7 Psaumes 51.18-51.19

Cette Bible est dans le domaine public.