Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 36.6
Bible en Swahili de l’est


Le sort des justes et des coupables

1 Tena Elihu akaendelea na kusema,
2 Ningojee kidogo nami nitakueleza; Kwa kuwa nikali na maneno kwa ajili ya Mungu.
2 Corinthiens 5.20 Job 21.3 Jérémie 15.19 Job 33.31-33.33 Hébreux 13.22
3 Nitayaleta maarifa yangu kutoka mbali, Nami nitampa haki Muumba wangu.
Apocalypse 15.3 Jacques 1.17 Jacques 3.17 Jacques 1.5 Psaumes 11.7
4 Kwani yakini maneno yangu si ya uongo; Aliyekamilika katika maarifa yu pamoja nawe.
Job 37.16 2 Timothée 3.16-3.17 1 Corinthiens 14.20 Job 13.7 2 Corinthiens 2.17
5 Tazama, Mungu ni hodari, wala hamdharau mtu ye yote; Ana uweza katika nguvu za fahamu.
Psaumes 22.24 Psaumes 138.6 Job 37.23 Psaumes 147.5 Jérémie 10.12
6 Hauhifadhi uhai wa waovu; Lakini huwapa wateswao haki yao.
Psaumes 72.12-72.14 Proverbes 22.22-22.23 Psaumes 140.12 2 Pierre 2.9 Jérémie 12.1-12.2
7 Yeye hawaondolei macho yake wenye haki; Lakini pamoja na wafalme huwaweka Katika viti vya enzi milele, nao hutukuzwa.
Psaumes 33.18 Psaumes 34.15 Psaumes 113.7-113.8 Sophonie 3.17 2 Thessaloniciens 3.3
8 Nao wakifungwa kwa pingu, Wakitwaliwa kwa kamba za mateso;
Psaumes 107.10 Proverbes 5.22 Psaumes 18.5 Job 33.18-33.19 Lamentations 3.9
9 Ndipo huwaonyesha matendo yao, Na makosa yao, ya kuwa wametenda kwa kujivuna.
1 Corinthiens 11.32 1 Timothée 1.15 Job 15.25 Psaumes 119.67 Psaumes 94.12
10 Yeye huyafunua masikio yao, wasikie maonyo, Na kuwaagiza warudi kuuacha uovu.
Proverbes 8.4-8.5 Job 33.16-33.23 Job 36.15 Esaïe 50.5 Matthieu 3.8
11 Kama wakisikia na kumtumikia, Watapisha siku zao katika kufanikiwa, Na miaka yao katika furaha.
Jérémie 7.23 Deutéronome 4.30 Jérémie 26.13 Jacques 5.5 Job 22.23
12 Lakini wasiposikia, wataangamia kwa upanga, Nao watakufa pasipo maarifa.
Job 4.21 Esaïe 3.11 Deutéronome 18.15-18.22 Deutéronome 29.15-29.20 Esaïe 1.20
13 Lakini hao wasiomcha Mungu mioyoni hujiwekea hasira Hawalilii msaada hapo awafungapo.
Romains 2.5 Job 36.8 Job 35.9-35.10 Job 27.8-27.10 Nombres 32.14
14 Wao hufa wakali vijana, Na uhai wao huangamia katikati ya wachafu.
Deutéronome 23.17 Job 15.32 Job 22.16 Psaumes 55.23 Job 21.23-21.25
15 Yeye humponya aliyetaabika kwa njia ya taabu yake, Na kuyafunua masikio yao kwa maonevu.
Job 36.10 2 Chroniques 12.8
16 Naam, yeye angekuongoza utoke katika msiba Hata mahali penye nafasi, ambapo hapana msonge; Na kilichowekwa mezani pako kingejaa mafuta.
Psaumes 23.5 Psaumes 18.19 Psaumes 118.5 Psaumes 31.8 Psaumes 36.8
17 Lakini umejaa hukumu ya waovu; Hukumu na haki hukushika.
Job 16.5 Romains 1.32 Job 34.8 Job 22.11 Apocalypse 18.4
18 Basi ujitunze, isije hasira ikakuvuta hata ukafanya mzaha; Wala usikubali ukuu wa ukombozi ukugeuze.
Job 33.24 Romains 1.18 Ephésiens 5.6 Psaumes 2.5 Psaumes 110.5
19 Je! Mali yako yatatosha, hata usiwe katika taabu, Au uwezo wote wa nguvu zako?
Proverbes 11.4 Proverbes 11.21 Esaïe 2.20 Esaïe 37.36 Psaumes 33.16-33.17
20 Usiutamani usiku, Wakati watu wakatwapo katika mahali pao.
Job 34.25 Job 34.20 Actes 1.25 Job 6.9 Proverbes 14.32
21 Jitunze, usiutazame uovu; Kwani umeuchagua huo zaidi ya taabu.
Psaumes 66.18 Hébreux 11.25 1 Pierre 3.17 Actes 5.40-5.41 Daniel 3.16-3.18
22 Tazama, Mungu hutenda makuu kwa uweza wake; Ni nani afundishaye kama yeye?
Romains 13.1 Luc 1.52 1 Samuel 2.7-2.8 Job 35.11 Jérémie 31.38
23 Ni nani aliyemwagiza njia yake? Au ni nani awezaye kusema, Wewe umetenda yasiyo haki?
1 Corinthiens 2.16 Job 8.3 Esaïe 40.13-40.14 Romains 11.34 Romains 2.5
24 Kumbuka kuitukuza kazi yake, Watu waliyoiimbia.
Luc 1.46 Psaumes 34.3 Apocalypse 15.3 Psaumes 72.18 Psaumes 138.5
25 Wanadamu wote wameitazama; Watu huiangalia kwa mbali
26 Tazama, Mungu ni mkuu, nasi hatumjui; Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
Psaumes 90.2 Job 37.23 Psaumes 145.3 Hébreux 1.12 Job 37.5
27 Kwani yeye huvuta juu matone ya maji, Yamwagikayo katika mvua kutoka kungeni mwake;
Psaumes 147.8 Job 38.25-38.28 Job 36.33 Psaumes 148.8 Job 5.9
28 Ambayo mawingu yainyesha Na kudondoza juu ya wanadamu kwa wingi.
Proverbes 3.20 Genèse 7.11-7.12 Job 37.11-37.13
29 Naam, mtu aweza kuelewa na matandazo ya mawingu, Ngurumo za makao yake?
Job 37.16 Job 37.2-37.5 Job 38.9 Psaumes 104.3 Job 38.37
30 Tazama, yeye huutandaza mwanga wake, umzunguke; Naye hufunika vilindi vya bahari.
Job 38.25 Psaumes 104.5-104.9 Exode 15.4-15.5 Job 38.34-38.35 Psaumes 18.11-18.16
31 Kwani huwahukumu kabila za watu kwa njia hizi; Hutoa chakula kwa ukarimu.
Actes 14.17 Psaumes 136.25 Job 37.13 Psaumes 104.27-104.28 Psaumes 104.13-104.15
32 Yeye huifunika mikono yake kwa umeme; Na kuuagiza shabaha utakayopiga.
Psaumes 148.8 Psaumes 147.8-147.9 Job 37.12 Exode 10.21-10.23 Psaumes 18.11
33 Mshindo wake hutoa habari zake, Anayewaka hasira juu ya uovu.
Job 37.2 Joël 1.18 Job 36.29 Joël 2.22 1 Rois 18.41-18.45

Cette Bible est dans le domaine public.