Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 15.20
Bible en Swahili de l’est


Transport de l’arche à Jérusalem

1 Basi Daudi akajifanyia nyumba katika mji wa Daudi; akapaweka tayari mahali kwa ajili ya sanduku la Mungu, akalipigia hema.
1 Chroniques 16.1 1 Chroniques 17.1-17.5 1 Chroniques 15.3 Psaumes 132.5 2 Samuel 5.9
2 Ndipo Daudi akasema, Haimpasi mtu awaye yote kulichukua sanduku la Mungu, isipokuwa Walawi peke yao; kwa kuwa hao ndio aliowachagua Bwana, ili walichukue sanduku la Mungu, na kumtumikia daima.
Deutéronome 10.8 Deutéronome 31.9 Josué 6.6 Nombres 4.19-4.20 Nombres 8.24-8.26
3 Basi Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu, ili kulipandisha sanduku la Bwana, mpaka mahali pake alipoliwekea tayari.
1 Rois 8.1 1 Chroniques 13.5 1 Chroniques 15.1 2 Samuel 6.12 2 Samuel 6.17
4 Daudi akawakutanisha wana wa Haruni, na Walawi;
1 Chroniques 6.49-6.50 Exode 6.16-6.22 Nombres 3.4 1 Chroniques 6.16-6.30 1 Chroniques 12.26-12.28
5 wa wana wa Kohathi; Urieli mkuu wao, na nduguze mia na ishirini;
1 Chroniques 6.22-6.24
6 wa wana wa Merari; Asaya mkuu wao, na nduguze mia mbili na ishirini;
1 Chroniques 6.29-6.30
7 wa wana wa Gershoni; Yoeli mkuu wao, na nduguze mia na thelathini;
1 Chroniques 23.8 1 Chroniques 15.11
8 wa wana wa Elsafani; Shemaya mkuu wao, na nduguze mia mbili;
Exode 6.22
9 wa wana wa Hebroni; Elieli mkuu wao, na nduguze themanini;
Exode 6.18 1 Chroniques 23.19 1 Chroniques 23.12 1 Chroniques 26.23 1 Chroniques 26.30-26.31
10 wa wana wa Uzieli; Aminadabu mkuu wao, na nduguze mia na kumi na wawili.
1 Chroniques 23.12 Exode 6.22 1 Chroniques 6.18 1 Chroniques 6.22 Exode 6.18
11 Tena, Daudi akawaita Sadoki na Abiathari makuhani, na hao Walawi, Urieli, Asaya, Yoeli, Shemaya, Elieli, na Aminadabu,
1 Chroniques 12.28 1 Rois 2.35 1 Samuel 22.20-22.23 1 Rois 2.26 2 Samuel 20.25
12 akawaambia, Ninyi ni vichwa vya mbari za baba za Walawi; jitakaseni, ninyi na ndugu zenu, ili mlipandishe sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli, mpaka mahali pale nilipoliwekea tayari.
2 Chroniques 35.6 Exode 19.14-19.15 2 Chroniques 30.15 1 Chroniques 15.1 Ezéchiel 48.11
13 Kwani kwa sababu ninyi hamkulichukua safari ya kwanza, Bwana, Mungu wetu, alitufurikia, kwa maana hatukumtafuta sawasawa na sheria.
2 Samuel 6.3 2 Chroniques 30.17-30.20 Nombres 4.15 Proverbes 28.13 Deutéronome 31.9
14 Basi makuhani na Walawi wakajitakasa, ili wapate kulipandisha sanduku la Bwana, Mungu wa Israeli.
Lévitique 10.3 Joël 2.16-2.17 2 Chroniques 29.15 2 Chroniques 29.34
15 Na wana wa Walawi wakalichukua sanduku la Mungu mabegani mwao kwa miti yake, kama vile Musa alivyoamuru, sawasawa na neno la Bwana.
Nombres 4.15 Nombres 7.9 Exode 37.3-37.5 Nombres 4.5-4.6 Exode 40.20
16 Kisha Daudi akamwambia mkuu wa Walawi, kwamba awaagize ndugu zao waimbaji, pamoja na vyombo vyao vya kupigia ngoma, vinanda, na vinubi, na matoazi, wavipige na kupaza sauti kwa furaha.
1 Chroniques 13.8 1 Chroniques 16.42 1 Chroniques 23.5 2 Chroniques 5.13 Néhémie 12.36
17 Basi Walawi wakamwagiza Hemani mwana wa Yoeli; na wa nduguze, Asafu mwana wa Berekia; na wa wana wa Merari ndugu zao, Ethani mwana wa Kishi;
1 Chroniques 6.44 1 Chroniques 6.39 1 Chroniques 6.33 Psaumes 83.1 Psaumes 73.1
18 na pamoja nao ndugu zao kwa cheo cha pili, Zekaria, na Yaasieli, na Shemiramothi, na Yehieli, na Uni, na Eliabu; na Benaya, na Maaseya, na Matithia, na Elifelehu, na Mikneya, na Obed-edomu, na Yeieli, mabawabu.
1 Chroniques 26.4 1 Chroniques 16.5-16.6 1 Chroniques 25.9-25.31 1 Chroniques 13.14 1 Chroniques 26.8
19 Hivyo hao waimbaji, Hemani, Asafu, na Ethani, wakaagizwa kupiga matoazi yao ya shaba kwa sauti kuu;
1 Chroniques 25.6 1 Chroniques 16.5 Psaumes 150.5 1 Chroniques 25.1 1 Chroniques 13.8
20 na Zekaria, na Yaasieli na Shemiramothi, na Yehieli, na Uni, na Eliabu, na Maaseya, na Benaya, wenye vinanda vya sauti ya Alamothi;
Psaumes 46.1-46.11
21 na Matithiya, na Elifelehu, na Mikneya, na Obed-edomu, na Yeieli, na Azazia, wenye vinubi vya sauti ya Sheminithi,
1 Samuel 10.5 Psaumes 6.1-6.10 Psaumes 92.3 Psaumes 33.2 Psaumes 150.3
22 waongoze. Na Kenania, mkuu wa Walawi, alikuwa juu ya uchukuzi; yeye aliusimamia uchukuzi, kwa sababu alikuwa mstadi.
1 Chroniques 15.16 1 Chroniques 25.7-25.8 1 Chroniques 15.27
23 Na Berekia na Elkana walikuwa mabawabu kwa ajili ya sanduku.
Psaumes 84.10 2 Rois 25.18 1 Chroniques 9.21-9.23 2 Rois 22.4
24 Na Shebania, na Yoshafati, na Nethaneli, na Amasai, na Zekaria, na Benaya, na Eliezeri, makuhani, wakapiga baragumu mbele ya sanduku la Mungu; na Obed-edomu na Yehia walikuwa mabawabu kwa ajili ya sanduku.
1 Chroniques 16.6 1 Chroniques 15.28 Nombres 10.8 1 Chroniques 15.23 Joël 2.1
25 Basi Daudi, na wazee wa Israeli, na maakida wa maelfu, wakaenda, ili kulipandisha sanduku la agano la Bwana kutoka nyumbani mwa Obed-edomu kwa furaha kuu;
2 Samuel 6.12-6.23 Psaumes 95.1-95.2 Deutéronome 16.11 Philippiens 3.3 Deutéronome 12.7
26 hata ikawa, Mungu alipowajalia Walawi waliolichukua sanduku la agano la Bwana, wakachinja ng’ombe saba, na kondoo waume saba.
Nombres 23.29 Job 42.8 Psaumes 66.13-66.15 1 Samuel 7.12 Ezéchiel 45.23
27 Naye Daudi alikuwa amevaa joho ya kitani safi, na Walawi wote waliolichukua sanduku, na waimbaji, na Kenania msimamizi wa uchukuzi, na waimbaji; naye Daudi alikuwa amevaa naivera ya kitani.
2 Samuel 6.14 1 Samuel 2.18
28 Ndivyo Israeli wote walivyolipandisha sanduku la agano la Bwana kwa shangwe na kwa sauti ya tarumbeta, na kwa baragumu, na kwa matoazi, wakipiga sauti kuu kwa vinanda na vinubi.
1 Chroniques 13.8 1 Chroniques 15.16 Psaumes 150.3-150.5 Psaumes 47.1-47.5 Psaumes 98.4-98.6
29 Hata ikawa, sanduku la agano la Bwana lilipofika mjini kwa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani, akamwona mfalme Daudi, akicheza na kushangilia; akamdharau moyoni mwake.
2 Samuel 6.16 Psaumes 150.4 Jérémie 30.19 1 Samuel 19.11-19.17 Deutéronome 31.26

Cette Bible est dans le domaine public.