Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 11.44
Bible en Swahili de l’est


Sacre de David sur Israël

1 Ndipo Israeli wote wakamkusanyikia Daudi huko Hebroni, wakisema, Tazama, sisi tu mfupa wako na nyama yako.
1 Chroniques 12.23-12.40 Nombres 13.22 Deutéronome 17.15 Genèse 29.14 Ephésiens 5.30
2 Katika zamani za kale, hata hapo Sauli alipokuwa mfalme, wewe ndiwe uliyewatoa na kuwaingiza Israeli. Naye Bwana, Mungu wako, akakuambia, Ndiwe, utakayewalisha watu wangu Israeli, ndiwe utakayekuwa mkuu juu ya watu wangu Israeli.
2 Samuel 5.2 Psaumes 78.71 2 Samuel 7.7 Matthieu 2.6 1 Samuel 16.13
3 Basi wazee wote wa Israeli wakamjia mfalme huko Hebroni; naye Daudi akafanya agano nao huko Hebroni mbele za Bwana; nao wakamtia Daudi mafuta, awe mfalme wa Israeli, sawasawa na neno la Bwana kwa mkono wa Samweli.
1 Samuel 16.12-16.13 1 Samuel 16.1 2 Samuel 5.3 1 Samuel 16.3 2 Samuel 2.4
4 Kisha Daudi na Israeli wote wakaenda Yerusalemu, (ndio Yebusi;) nao Wayebusi, wenyeji wa nchi, walikuwamo.
Juges 1.21 Genèse 15.21 Josué 15.8 Genèse 10.16 Josué 15.63
5 Na hao wenyeji wa Yebusi wakamwambia Daudi, Hutaingia humu. Walakini Daudi akaitwaa ngome ya Sayuni; huu ndio mji wa Daudi.
Psaumes 2.6 Psaumes 48.12-48.13 1 Rois 8.1 1 Samuel 17.36 2 Samuel 5.9
6 Naye Daudi akasema, Mtu ye yote atakayekuwa wa kwanza wa kuwapiga Wayebusi, yeye atakuwa mkuu na jemadari. Naye wa kwanza aliyepanda ni Yoabu mwana wa Seruya, naye akawa mkuu.
2 Samuel 8.16 2 Samuel 3.27 2 Samuel 20.23 Josué 15.16-15.17 1 Samuel 17.25
7 Basi Daudi akakaa ngomeni; kwa hiyo huuita mji wa Daudi.
1 Chroniques 11.5 2 Samuel 5.7 Psaumes 2.6
8 Akaujenga huo mji pande zote, toka Milo na kuuzunguka; naye Yoabu akautengeneza mji uliosalia.
1 Rois 9.15 Néhémie 4.2 Juges 9.6 1 Rois 11.27 2 Rois 12.20
9 Naye Daudi akaendelea, akazidi kuwa mkuu; kwa maana Bwana wa majeshi alikuwa pamoja naye.
2 Samuel 3.1 Esaïe 9.7 Psaumes 46.11 1 Chroniques 9.20 Esaïe 41.14

Les vaillants hommes de David

10 Basi hawa ndio wakuu wa mashujaa aliokuwa nao Daudi, waliojitia nguvu pamoja naye katika ufalme wake, pamoja na Israeli wote, ili kumfanya awe mfalme, sawasawa na neno la Bwana alilonena juu ya Israeli.
1 Chroniques 11.3 2 Samuel 3.21 2 Samuel 23.8-23.39 2 Samuel 3.17-3.18 1 Samuel 16.1
11 Na hii ndiyo hesabu ya hao mashujaa aliokuwa nao Daudi; Yashobeamu, Mhakmoni, mkuu wa maakida; huyo aliuinua mkuki wake juu ya watu mia tatu, akawaua pamoja.
2 Samuel 23.8 1 Chroniques 12.18 1 Chroniques 27.2
12 Na baada yake kulikuwa na Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu.
1 Chroniques 27.4 2 Samuel 23.17-23.19 1 Chroniques 11.19 1 Chroniques 11.21 1 Chroniques 8.4
13 Huyo alikuwa pamoja na Daudi huko Pasdamimu; ndiko Wafilisti walikokusanyika vitani, palipokuwa na konde limejaa shayiri ;na hao watu wakakimbia mbele ya wafilisti.
1 Samuel 17.1 2 Samuel 23.11-23.12
14 Ndipo hao wakasimama katikati ya konde lile, wakalipigania, wakawaua Wafilisti; naye Bwana akafanya wokovu mkuu.
Psaumes 18.50 Psaumes 144.10 1 Samuel 14.23 1 Samuel 19.5 Proverbes 21.31
15 Tena, watatu miongoni mwa wale thelathini waliokuwa wakuu wakashuka mwambani, wakamwendea Daudi, hata pango la Adulamu; na jeshi la Wafilisti walikuwa wamefanya kambi bondeni mwa Warefai.
1 Chroniques 14.9 Esaïe 17.5 Josué 15.8 2 Samuel 5.22 2 Samuel 23.13-23.39
16 Na Daudi wakati ule alikuwako ngomeni, na walinzi wa Wafilisti wakati ule walikuwa huko Bethlehemu.
1 Samuel 10.5 1 Samuel 13.4 1 Samuel 13.23 1 Samuel 23.25 1 Samuel 22.1
17 Naye Daudi akatamani, akasema, Laiti mtu angeninywesha maji ya kisima cha Bethlehemu, kilicho karibu na lango!
2 Samuel 23.15-23.16 Jean 4.14 Nombres 11.4-11.5 Psaumes 42.1-42.2 Psaumes 143.6
18 Basi hao watatu wakapenya jeshi la Wafilisti, wakateka maji kutoka kile kisima cha Bethlehemu, kilicho karibu na lango, wakayachukua, wakamletea Daudi; walakini Daudi hakukubali kuyanywa, akayamimina mbele za Bwana;
Actes 21.13 1 Samuel 7.6 1 Samuel 19.5 Cantique 8.6 2 Corinthiens 5.14-5.15
19 akasema, Mungu wangu apishe mbali, nisifanye hivi; je! Ninywe damu ya watu hao waliohatirisha nafsi zao? Maana kwa hatari ya nafsi zao wameyaleta. Kwa hiyo hakukubali kuyanywa. Hayo ndiyo waliyoyafanya wale mashujaa watatu.
1 Rois 21.3 2 Samuel 23.17 Juges 9.17 Job 31.31 Romains 6.1-6.2
20 Tena Abishai, nduguye Yoabu, alikuwa mkuu wa wale watatu; kwa kuwa aliuinua mkuki wake juu ya watu mia tatu, akawaua; akawa na jina kati ya wale watatu.
1 Samuel 26.6 2 Samuel 3.30 2 Samuel 2.18 2 Samuel 23.18-23.39 1 Chroniques 2.16
21 Katika wale watatu yeye alikuwa mwenye heshima kuliko hao wawili, akawa akida wao; ila hakudiriki kuwamo katika wale watatu.
Matthieu 13.8 1 Corinthiens 15.41
22 Tena, Benaya, mwana wa Yehoyada, mtu hodari, wa Kabseeli, aliyekuwa amefanya mambo makuu, ndiye aliyewaua simba wakali wawili wa Moabu; pia akashuka ,akamwua simba katikati ya shimo wakati wa theruji.
2 Samuel 8.18 Josué 15.21 1 Chroniques 27.5-27.6 1 Rois 2.30 1 Rois 1.38
23 Huyo akamwua Mmisri, mtu mrefu sana, aliyekuwa wa dhiraa tano urefu wake; na yule Mmisri alikuwa na mkuki kama mti wa mfumaji mkononi; lakini yeye akamshukia na gongo, akamnyakulia Mmisri mkuki mkononi, akamwua kwa mkuki wake mwenyewe.
1 Samuel 17.7 Deutéronome 3.11 1 Samuel 17.4 1 Chroniques 20.5 1 Samuel 17.51
24 Mambo hayo ndiyo aliyoyafanya Benaya, mwana wa Yehoyada, akawa na jina kati ya wale mashujaa watatu.
25 Tazama, alikuwa mwenye heshima kuliko wale thelathini, ila hakudiriki kuwamo katika wale watatu; naye Daudi akamweka juu ya walinzi wake.
2 Samuel 20.23
26 Tena hawa ndio mashujaa wa majeshi ya askari; Asaheli nduguye Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo wa Bethlehemu;
1 Chroniques 27.7 2 Samuel 23.24 2 Samuel 2.18-2.23 2 Samuel 21.19 2 Samuel 3.30
27 Shama Mharodi, Helesi Mpeloni;
2 Samuel 23.25-23.26
28 Ira mwana wa Ikeshi Mtekoi, Abiezeri Mwanathothi;
1 Chroniques 27.12 1 Chroniques 27.9 2 Samuel 23.27
29 Sibekai Mhushathi, Salmoni Mwahohi;
1 Chroniques 27.11 2 Samuel 23.27-23.28
30 Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana Mnetofathi;
1 Chroniques 27.15 1 Chroniques 27.13 2 Samuel 23.29
31 Itai mwana wa Ribai wa Gibea wa wana wa Benyamini, Benaya Mpirathoni;
2 Samuel 23.29
32 Hurai wa vijito vya Gaashi, Abieli Mwaibathi;
2 Samuel 23.30-23.31
33 Azmawethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni;
34 wana wa Yasheni Mgiloni, Yonathani mwana wa Shama Mharari;
2 Samuel 23.32-23.33
35 Ahiamu mwana wa Sharari Mharari, Elifeleti mwana wa Ahasbai; Heferi
2 Samuel 23.33-23.34
36 Mmaakathi, Ahia Mpeloni;
37 Hezro Mkarmeli, Paarai mwana wa Ezbai Mwarki;
2 Samuel 23.35
38 Yoeli nduguye Nathani, Mibhari mwana wa Hagri;
2 Samuel 23.36
39 Seleki Mwamoni, Naharai Mbeorothi, mchukua silaha wa Yoabu, mwana wa Seruya;
40 Ira Mwithri, Garebu Mwithri;
2 Samuel 20.26
41 Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Alai;
2 Samuel 11.6-11.27 2 Samuel 23.39 1 Chroniques 2.36
42 Adina mwana wa Shiza Mreubeni, mkuu wa Wareubeni, na thelathini pamoja naye;
43 Hanani mwana wa Maaka, na Yoshafati Mmithni;
44 Uzia Mwashterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Mwaroeri;
45 Yediaeli mwana wa Shimri, na Yoha nduguye, Muzi;
46 Elieli Mmahawi, na Yeribai, na Yoshavia, wana wa Elnaamu, na Ithma Mmoabi;
47 Elieli, na Obedi, na Yaasieli Mmesobai.

Cette Bible est dans le domaine public.