Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 19.3
Bible en Swahili de l’est


Délivrance de Jérusalem

1 Ikawa mfalme Hezekia aliposikia hayo, alizirarua nguo zake, akajivika nguo za magunia, akaingia katika nyumba ya Bwana.
2 Rois 18.37 1 Rois 21.27 Genèse 37.34 Esaïe 37.1-37.7 2 Chroniques 32.20-32.22
2 Akamtuma Eliakimu aliyekuwa msimamizi wa nyumba yake na Shebna, mwandishi, na wazee wa makuhani, wamevikwa nguo za magunia, waende kwa Isaya nabii, mwana wa Amozi.
Esaïe 1.1 Esaïe 2.1 2 Rois 18.18 Matthieu 4.14 Esaïe 37.2-37.5
3 Wakamwambia, Hezekia asema hivi, Siku hii ni siku ya dhiki, na aibu, na matukano; maana watoto wa tayari kuzaliwa, wala hapana nguvu za kuwazaa.
Jérémie 30.5-30.7 Esaïe 66.9 Esaïe 26.17-26.18 Psaumes 95.8 Psaumes 39.11
4 Yamkini Bwana, Mungu wako, atayasikia maneno yote ya amiri huyu, ambaye mfalme wa Ashuru ,bwana wake,amemtuma ili amtukane Mungu aliye hai,naye atayakemea hayo maneno aliyoyasikia BWANA ,Mungu wako;kwa sababu hii inua dua yako kwa ajili ya mabaki yaliyobakia.
2 Samuel 16.12 Josué 14.12 2 Rois 17.5-17.6 Deutéronome 32.36 2 Rois 18.13
5 Basi watumishi wa mfalme Hezekia wakamwendea Isaya.
6 Isaya akawaambia, Mwambieni bwana wenu maneno haya; Bwana asema hivi, Usiyaogope maneno hayo uliyoyasikia, ambayo watumishi wa mfalme wa Ashuru wamenitukana.
2 Rois 18.35 2 Rois 18.17 2 Rois 18.22-18.25 Psaumes 74.23 Deutéronome 20.3-20.4
7 Tazama, nitatia roho ya hofu ndani yake, naye atasikia kivumi, na kuirudia nchi yake mwenyewe; nami nitamwangusha kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.
2 Rois 7.6 Job 15.21 Jérémie 51.46 Esaïe 11.4 Jérémie 49.14
8 Basi yule amiri akarudi, akamkuta mfalme wa Ashuru, anapigana na Libna; maana alikuwa amesikia ya kwamba ameondoka, akaacha Lakishi.
2 Rois 18.14 Josué 10.29 2 Rois 8.22 Esaïe 37.8-37.9 Josué 12.15
9 Na aliposikia habari ya Tirhaka mfalme wa Kushi, ya kwamba, Tazama, ametoka ili kupigana nawe; alituma wajumbe kwa Hezekia mara ya pili, kusema,
1 Samuel 23.27 Esaïe 37.9 2 Rois 18.17
10 Mwambieni Hezekia, mfalme wa Yuda, maneno haya, mkisema, Asikudanganye Mungu wako unayemtumaini, akisema, Yerusalemu hautatiwa katika mikono ya mfalme wa Ashuru.
2 Rois 18.5 2 Rois 18.29-18.30 2 Chroniques 32.15-32.19 Esaïe 37.10-37.14
11 Tazama, umesikia ni mambo gani wafalme wa Ashuru waliyozitenda nchi zote, kwa kuziangamiza kabisa; je! Utaokoka wewe?
2 Rois 19.17-19.18 2 Rois 17.5-17.11 Esaïe 10.8-10.11 2 Chroniques 32.13-32.14
12 Je! Miungu ya mataifa wale, ambao baba zangu waliwaangamiza, imewaokoa? Yaani, Gozani, na Harani, na Resefu, na wana wa Adini waliokuwa katika Telasari?
2 Rois 17.6 Genèse 11.31 Ezéchiel 27.23 Esaïe 37.12 2 Rois 18.33-18.34
13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi, na mfalme wa Arpadi, na mfalme wa mji wa Sefarvaimu, na wa Hena, na wa Iva?
2 Rois 18.34 Zacharie 9.2 2 Rois 17.24 Nombres 13.21 Jérémie 49.23
14 Basi Hezekia akaupokea waraka katika mikono ya wale wajumbe, akausoma; kisha Hezekia akapanda, akaingia katika nyumba ya Bwana, akaukunjua mbele za Bwana.
Esaïe 37.14 Psaumes 91.1-91.2 Esdras 9.5 Psaumes 123.1-123.4 1 Rois 8.28-8.30
15 Naye Hezekia akaomba mbele za Bwana, akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, ukaaye juu ya makerubi, wewe, naam, wewe peke yako, ndiwe Mungu wa falme zote za dunia; wewe ndiwe uliyeziumba mbingu na nchi.
Exode 25.22 Esaïe 44.6 1 Rois 18.39 2 Rois 5.15 1 Samuel 4.4
16 Tega sikio lako, Ee Bwana, usikie; fumbua macho yako, Ee Bwana, uone; uyasikie maneno ya Senakeribu, ambayo amemtuma mtu aje nayo ili kumtukana Mungu aliye hai.
2 Chroniques 6.40 Psaumes 31.2 Esaïe 37.17 2 Rois 19.4 Daniel 9.18
17 Ni kweli, Bwana, wafalme wa Ashuru wamewaharibu mataifa na nchi zao,
Luc 22.59 1 Chroniques 5.26 Esaïe 5.9 2 Rois 17.6 Actes 4.27
18 na kuitupa miungu yao motoni; kwa maana haikuwa miungu, bali ni kazi ya mikono ya wanadamu; ilikuwa miti na mawe tu, ndiyo sababu wakaiharibu.
Actes 17.29 Jérémie 10.3-10.9 Esaïe 44.9-44.20 Jérémie 10.14-10.16 Esaïe 46.1-46.2
19 Basi sasa, Ee Bwana, Mungu wetu, utuokoe na mkono wake, nakusihi, ili kwamba falme zote za dunia zipate kujua ya kuwa wewe ndiwe Bwana Mungu, wewe peke yako.
Psaumes 83.18 1 Rois 8.43 1 Rois 20.28 Psaumes 67.1-67.2 2 Rois 19.15
20 Ndipo Isaya, mwana wa Amozi, akapeleka ujumbe kwa Hezekia, akisema, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kwa kuwa umeniomba juu ya Senakeribu, mfalme wa Ashuru, mimi nimekusikia.
2 Rois 20.5 Actes 10.31 Job 22.27 Jérémie 33.3 2 Chroniques 32.20-32.21
21 Tamko alilolitamka Bwana katika habari zake ndilo hili, Bikira, binti Sayuni, amekudharau, na kukudhihaki sana; binti Yerusalemu ametikisa kichwa chake juu yako.
Lamentations 2.13 Job 16.4 Jérémie 14.17 Matthieu 27.39 Psaumes 22.7-22.8
22 Ni nani uliyemshutumu na kumtukana? Umeinua sauti yako juu ya nani, na kuinua macho yako juu? Juu ya Mtakatifu wa Israeli.
Esaïe 5.24 Psaumes 71.22 Esaïe 30.11-30.12 Esaïe 30.15 Jérémie 51.5
23 Kwa vinywa vya wajumbe wako umemshutumu Bwana, ukasema, Kwa wingi wa magari yangu nimepanda juu ya vilele vya milima, mpaka mahali pa ndani pa Lebanoni. Nami nitaikata mierezi yake mirefu, na misunobari yake mizuri; nami nitaingia ndani ya makazi yake yaliyo mbali sana, na msitu wa shamba lake lizaalo sana.
Psaumes 20.7 2 Rois 18.17 Esaïe 10.18 Esaïe 10.7-10.11 Esaïe 37.24-37.25
24 Nimechimba na kunywa maji mageni, na kwa nyayo za miguu yangu nitaikausha mito yote ya Misri.
Daniel 4.30 Esaïe 19.6 1 Rois 20.10 Exode 15.9 2 Samuel 17.13
25 Je! Hukusikia wewe ya kuwa mimi ndimi niliyeyatenda hayo tokea zamani, na kuyafanya tokea siku za kale? Sasa mimi nimelitimiza jambo hili, iwe kazi yako kuangamiza miji yenye boma, hata ikawe chungu na magofu.
Esaïe 45.7 Esaïe 37.26-37.27 Esaïe 46.10-46.11 Psaumes 33.11 Esaïe 10.5-10.6
26 Ndiyo sababu wenyeji wao walikuwa na nguvu chache, wakafadhaika, na kuhangaika; wakawa kama majani ya mashamba, kama miche mibichi, kama majani juu ya dari, na kama ngano iliyokaushwa kabla haijaiva.
Jérémie 51.30 Jérémie 50.36-50.37 Psaumes 102.11 Nombres 11.23 Psaumes 129.6-129.8
27 Lakini nakujua, kuketi kwako, na kutoka kwako, na kuingia kwako; na ghadhabu yako unayonighadhibikia.
Psaumes 139.1-139.11 Esaïe 37.28-37.29 Deutéronome 28.19 Jérémie 23.23-23.24 Deutéronome 28.6
28 Kwa sababu ya kunighadhibikia kwako, na kwa sababu kutakabari kwako kumefika masikioni mwangu; kwa sababu hiyo nitatia kulabu yangu puani mwako, na hatamu yangu midomoni mwako, nami nitakurudisha nyuma kwa njia ile ile uliyoijia.
Ezéchiel 29.4 2 Rois 19.33 Amos 4.2 Ezéchiel 38.4 Job 41.2
29 Na kwako wewe hii ndiyo dalili; mwaka huu mtakula vitu viotavyo vyenyewe; na mwaka wa pili mtakula mazao ya vitu hivyo; na mwaka wa tatu pandeni mbegu, kavuneni; mkapande mashamba ya mizabibu, mkale matunda yake.
2 Rois 20.8-20.9 Luc 2.12 1 Samuel 2.34 Esaïe 37.30 Exode 3.12
30 Na mabaki yaliyookoka ya nyumba ya Yuda yatatia mizizi chini, na kuzaa matunda juu.
2 Chroniques 32.22-32.23 2 Rois 19.4 Esaïe 10.20-10.22 Esaïe 37.31-37.32 Esaïe 1.9
31 Maana mabaki yatatoka katika Yerusalemu, na wao watakaookoka katika mlima wa Sayuni wivu wa Bwana utatimiza jambo hilo.
Esaïe 9.7 Romains 9.27 Zacharie 1.14 Jérémie 44.14 Romains 11.5
32 Basi Bwana asema hivi katika habari za mfalme wa Ashuru, Yeye hatauingia mji huu, wala hatapiga mshale hapa, wala hatakuja mbele yake kwa ngao, wala hatajenga boma juu yake.
2 Samuel 20.15 Esaïe 8.7-8.10 Esaïe 10.24-10.25 Luc 19.43-19.44 Esaïe 10.28-10.32
33 Njia ile ile aliyojia, kwa njia iyo hiyo atarudi zake, wala hataingia ndani ya mji huu, asema Bwana.
2 Rois 19.28 2 Rois 19.36
34 Maana nitaulinda mji huu, niuokoe, kwa ajili yangu mwenyewe, na kwa ajili ya Daudi, mtumishi wangu.
2 Rois 20.6 1 Rois 11.12-11.13 Esaïe 31.5 Esaïe 38.6 1 Rois 15.4
35 Ikawa usiku uo huo malaika wa Bwana alitoka, akakiingia kituo cha Waashuri, akawapiga watu mia na themanini na tano elfu. Na watu walipoondoka asubuhi na mapema, kumbe! Hao walikuwa maiti wote pia.
Exode 12.29-12.30 2 Samuel 24.16 2 Chroniques 32.21-32.22 Daniel 5.30 Esaïe 10.16-10.19
36 Basi Senakeribu mfalme wa Ashuru akaondoka, akaenda zake, akarudi akakaa Ninawi.
Jonas 1.2 2 Rois 19.28 2 Rois 19.7 2 Rois 19.33 Nahum 2.8
37 Ikawa, alipokuwa akiabudu nyumbani mwa Nisroki, mungu wake, Adrameleki na Shareza wakampiga kwa upanga; wakaikimbilia nchi ya Ararati. Na Esar-hadoni mwanawe akatawala mahali pake.
Esdras 4.2 Genèse 8.4 2 Rois 19.7 Jérémie 51.27 Esaïe 37.37-37.38

Cette Bible est dans le domaine public.