Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 18.13
Bible en Swahili de l’est


Jusqu’à la chute du royaume de Juda

Règne d’Ézéchias sur Juda

1 Ikawa katika mwaka wa tatu wa Hoshea, mwana wa Ela, mfalme wa Israeli, Hezekia, mwana wa Ahazi, mfalme wa Yuda, alianza kutawala.
2 Rois 16.2 Matthieu 1.9-1.10 2 Rois 15.30 1 Chroniques 3.13 2 Rois 18.9
2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na kenda katika Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Abiya, binti Zekaria.
2 Chroniques 29.1-29.2
3 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, mfano wa yote aliyoyafanya Daudi, baba yake.
2 Rois 20.3 1 Rois 11.38 Exode 15.26 1 Rois 3.14 1 Rois 11.4
4 Alipaondoa mahali pa juu, akazibomoa nguzo, akaikata hiyo Ashera; akaivunja vipande vipande ile nyoka ya shaba aliyoifanya Musa; maana hata siku zile wana wa Israeli walikuwa wakiifukizia uvumba; naye akaiita jina lake Nehushtani
2 Chroniques 31.1 Nombres 21.8-21.9 2 Rois 18.22 Juges 6.28 1 Rois 15.12-15.14
5 Alimtumaini Bwana, Mungu wa Israeli; hata baada yake hapakuwa na mfano wake katika wafalme wote wa Yuda, wala katika hao waliomtangulia.
2 Rois 19.10 2 Rois 23.25 Psaumes 46.1-46.2 Psaumes 84.12 Psaumes 27.1-27.2
6 Maana alishikamana na Bwana, hakuacha kumfuata, bali alizishika amri zake Bwana alizomwamuru Musa.
Josué 23.8 Deutéronome 10.20 Jean 14.15 Jean 15.10 Jérémie 11.4
7 Naye Bwana akawa pamoja naye, kila alikokwenda alifanikiwa; tena alimwasi mfalme wa Ashuru, wala hakumtumikia.
1 Samuel 18.14 2 Rois 16.7 Genèse 39.2-39.3 Psaumes 60.12 2 Chroniques 15.2
8 Akawapiga Wafilisti mpaka Gaza na mipaka yake, tangu mnara wa walinzi hata mji wenye boma.
Esaïe 14.29 2 Rois 17.9 2 Chroniques 28.18 1 Chroniques 4.41 Esaïe 5.2
9 Hata katika mwaka wa nne wa Hezekia, ndio mwaka wa saba wa Hoshea, mwana wa Ela, mfalme wa Israeli, Shalmanesa, mfalme wa Ashuru, akakwea ili kupigana na Samaria, akauhusuru.
Osée 10.14 2 Rois 18.1 2 Rois 17.3-17.23
10 Wakautwaa baada ya miaka mitatu; yaani, katika mwaka wa sita wa Hezekia, ndio mwaka wa kenda wa Hoshea, mfalme wa Israeli, ndipo Samaria ulipotwaliwa.
Osée 13.16 Michée 6.16 Amos 6.7 Amos 3.11-4.3 Michée 7.13
11 Mfalme wa Ashuru akawahamisha Israeli mpaka Ashuru, akawaweka katika Hala, na katika Habori, karibu na mto wa Gozani, na katika miji ya Wamedi;
1 Chroniques 5.26 Esaïe 37.12 2 Rois 17.6 Esaïe 8.4 Esaïe 10.5
12 kwa sababu hawakuitii sauti ya Bwana, Mungu wao, bali waliyahalifu maagano yake, mambo yote ambayo Musa mtumishi wa Bwana aliwaamuru, wasikubali kuyasikiliza, wala kuyatenda.
1 Pierre 2.8 Néhémie 9.26-9.27 Daniel 9.6-9.11 Deutéronome 31.17 Jérémie 3.8

Tentative d’invasion assyrienne

13 Ikawa katika mwaka wa kumi na nne wa kumiliki kwake mfalme Hezekia, Senakeribu, mfalme wa Ashuru, akapanda ili kupigana na miji yote ya Yuda yenye boma, akaitwaa.
Esaïe 36.1-36.22 Esaïe 10.5 Esaïe 7.17-7.25 2 Chroniques 32.1-32.23 Osée 12.1-12.2
14 Basi Hezekia, mfalme wa Yuda, akapeleka wajumbe waende Lakishi kwa mfalme wa Ashuru, kusema, Nimekosa; uniache ukarudi kwako; cho chote utakachoweka juu yangu, nitakichukua. Mfalme wa Ashuru akamtoza Hezekia, mfalme wa Yuda, talanta za fedha mia tatu, na talanta za dhahabu thelathini.
2 Rois 18.7 1 Rois 20.4 Proverbes 29.25 Luc 14.32
15 Hezekia akampa fedha yote iliyoonekana katika nyumba ya Bwana, na katika hazina za nyumba ya mfalme.
2 Rois 16.8 1 Rois 15.18-15.19 2 Rois 12.18 2 Chroniques 16.2 1 Rois 15.15
16 Wakati huo Hezekia aliiondoa dhahabu iliyokuwa juu ya milango ya hekalu la Bwana, na juu ya nguzo, ambazo Hezekia, mfalme wa Yuda, alikuwa amezitia dhahabu, akampa mfalme wa Ashuru.
2 Chroniques 29.3 1 Rois 6.31-6.35
17 Mfalme wa Ashuru akawatuma jemadari wake, na mkuu wa matowashi, na amiri wake toka Lakishi ,kwa mfalme Hezekia huko Yerusalemu, pamoja na jeshi kubwa. Nao wakakwea wakafika Yerusalemu. Na walipokwisha kufika , wakaja wakasimama karibu na mfereji wa birika la juu, lililo katika njia kuu ya kuuendea uwanda wa dobi.
Esaïe 7.3 2 Rois 20.20 Esaïe 20.1 Esaïe 36.2 2 Chroniques 32.9
18 Na walipokwisha kumwita mfalme, wakatokewa na Eliakimu, mwana wa Hilkia, aliyekuwa msimamizi wa nyumba ya mfalme, na Shebna, mwandishi, na Yoa, mwana wa Asafu, mwenye kuandika tarehe.
2 Rois 19.2 1 Rois 4.3 Esaïe 37.2 Esaïe 22.15-22.24 Esaïe 36.3
19 Yule amiri akawaambia ,haya mwambieni Hezekia,kusema ,Mfalme mkuu,mfalme wa Ashuru, asema hivi, Ni tumaini gani hili unalolitumainia?
Esaïe 36.4 Psaumes 4.2 Esaïe 37.10 2 Rois 19.10 2 Rois 18.29-18.30
20 Wewe wasema, lakini ni maneno yasiyo na maana, kwamba, Lipo shauri na zipo nguvu kwa vita hivi. Basi, unamtumaini nani hata ukaniasi mimi?
Proverbes 21.30-21.31
21 Sasa tazama, unaitumainia fimbo ya mwanzi huu uliopondeka, yaani, Misri, ambayo mtu akiitegemea, humwingia mkononi na kumchoma; ndivyo alivyo Farao, mfalme wa Misri, kwa wote wamtumainio.
Esaïe 30.7 Ezéchiel 29.6-29.7 Esaïe 30.2-30.3 2 Rois 17.4 Jérémie 46.17
22 Lakini mkiniambia, Tunamtumaini Bwana, Mungu wetu; je! Si yeye ambaye Hezekia ameondoa mahali pake pa juu, na madhabahu zake, akawaambia watu wa Yuda na Yerusalemu, Sujuduni mbele ya madhabahu hii hapa Yerusalemu?
2 Chroniques 31.1 2 Rois 18.4-18.5 Matthieu 27.43 1 Corinthiens 2.15 Daniel 3.15
23 Basi sasa, tafadhali mpe bwana wangu, mfalme wa Ashuru, dhamana, nami nitakupa farasi elfu mbili, ikiwa wewe kwa upande wako waweza kupandisha watu juu yao.
1 Rois 20.18 Psaumes 123.3-123.4 1 Samuel 17.42 1 Samuel 17.44 Néhémie 4.2-4.5
24 Wawezaje, basi, kurudisha nyuma uso wa akida mmoja wa watumishi walio wadogo wa bwana wangu, na kuitumainia Misri upewe magari na farasi?
Esaïe 10.8 Esaïe 31.3 Psaumes 20.7-20.8 Esaïe 36.9 Jérémie 37.7
25 Je! Nimepanda mimi, ili kupigana na mahali hapa na kupaangamiza, bila shauri la Bwana? Bwana ndiye aliyeniambia, Panda upigane na nchi hii na kuiangamiza.
2 Rois 19.6 Amos 3.6 2 Rois 19.22-19.37 2 Chroniques 35.21 Jean 19.10-19.11
26 Ndipo Eliakimu, mwana wa Hilkia, na Shebna, na Yoa, wakamwambia yule amiri, Tafadhali, sema na watumishi wako kwa lugha ya Kiashuri; maana tunaifahamu; wala usiseme nasi kwa lugha ya Kiyahudi, masikioni mwa hao watu walio ukutani.
Esdras 4.7 Daniel 2.4 Esaïe 36.11-36.12 2 Rois 18.18
27 Lakini yule amiri akawaambia, Je! Bwana wangu amenituma kwa bwana wako, na kwako wewe, niseme maneno haya? Je! Hakunituma kwa watu hawa walio ukutani, ili wale mavi yao wenyewe na kunywa mkojo wao pamoja nanyi?
Ezéchiel 4.13 Ezéchiel 4.15 Psaumes 73.8 Lamentations 4.5 Deutéronome 28.53-28.57
28 Kisha yule amiri akasimama akalia kwa sauti kuu kwa lugha ya Kiyahudi, akasema, Lisikieni neno la mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru.
Esdras 7.12 Esaïe 36.13-36.18 Apocalypse 19.6 Ezéchiel 31.3-31.10 Ezéchiel 29.3
29 Mfalme asema hivi, Hezekia asiwadanganye; kwa maana, hataweza kuwaokoa katika mkono wake.
2 Chroniques 32.15 Psaumes 73.8-73.9 Daniel 6.16 Jean 19.10-19.11 Daniel 3.15-3.17
30 Wala Hezekia asiwatumainishe katika Bwana, akisema, Hakika Bwana atatuokoa, wala mji huu hautatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.
Psaumes 11.1 Matthieu 27.43 Psaumes 71.11 Psaumes 71.9 Psaumes 22.7-22.8
31 Msimsikilize Hezekia; kwa sababu mfalme wa Ashuru asema hivi, Fanyeni suluhu na mimi, mkatoke mnijie; mkale kila mtu matunda ya mzabibu wake na matunda ya mtini wake, mkanywe kila mmoja maji ya birika lake mwenyewe;
1 Rois 4.25 1 Rois 4.20 Proverbes 18.16 Genèse 33.11 Genèse 32.20
32 hata nije nikawachukue mpaka nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai, nchi ya chakula na mashamba ya mizabibu, nchi ya mafuta ya mzeituni na asali, ili mpate kuishi, msife; wala msimsikilize Hezekia, awadanganyapo, akisema, Bwana atatuokoa.
Deutéronome 8.7-8.9 Exode 3.8 Deutéronome 11.12 2 Rois 24.14-24.16 2 Rois 17.23
33 Je! Yuko mungu mmoja wa mataifa aliyewaokoa watu wake wakati wo wote na mkono wa mfalme wa Ashuru?
Esaïe 10.10-10.11 2 Chroniques 32.14-32.17 2 Rois 19.12-19.13 2 Chroniques 32.19 2 Rois 19.17-19.18
34 Iko wapi miungu ya Hamathi, na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu, na ya Hena, na ya Iva? Je! Imeuokoa Samaria na mkono wangu?
Esaïe 10.9 2 Rois 17.23-17.33 2 Samuel 8.9 Nombres 13.21 Esaïe 37.18-37.19
35 Katika miungu ya nchi hizi zote, ni miungu gani iliyookoa nchi yao na mkono wangu, hata Bwana auokoe Yerusalemu na mkono wangu?
Daniel 3.15 2 Rois 19.17 Exode 5.2 Job 15.25-15.26 Esaïe 10.15
36 Lakini hao watu wakanyamaza kimya; wala hawakumjibu hata neno moja; maana amri ya mfalme ilikuwa kwamba, Msimjibu neno.
Psaumes 38.13-38.14 Matthieu 7.6 Amos 5.13 Psaumes 39.1 Proverbes 9.7
37 Ndipo Eliakimu, mwana wa Hilkia, aliyekuwa msimamizi wa nyumba ya mfalme, na Shebna, mwandishi, na Yoa, mwana wa Asafu, mwenye kuandika tarehe, wakaenda kwa Hezekia, na nguo zao zimeraruliwa, wakamwambia maneno ya yule amiri.
2 Rois 22.19 2 Rois 6.30 2 Rois 22.11 2 Rois 5.7 Esaïe 36.21-36.22

Cette Bible est dans le domaine public.