Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Rois 17.6
Bible en Swahili de l’est


Règne d’Osée sur Israël

1 Katika mwaka wa kumi na mbili wa Ahazi mfalme wa Yuda Hoshea mwana wa Ela alianza kutawala juu ya Israeli katika Samaria; akatawala miaka kenda.
2 Rois 15.30
2 Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, ila si kama wafalme wa Israeli waliomtangulia.
2 Rois 15.9 2 Rois 13.11 2 Rois 10.31 2 Rois 15.24 2 Chroniques 30.5-30.11
3 Naye Shalmanesa mfalme wa Ashuru akakwea juu yake, Hoshea akawa mtumishi wake, akampa kodi.
Osée 10.14 2 Rois 18.9-18.16 Esaïe 7.7-7.8 Esaïe 10.5-10.6 2 Rois 19.36-19.37
4 Mfalme wa Ashuru akaona fitina katika huyo Hoshea; kwa maana alikuwa ametuma wajumbe kwa So, mfalme wa Misri, wala hakumletea kodi mfalme wa Ashuru, kama alivyofanya mwaka kwa mwaka; kwa hiyo mfalme wa Ashuru akamfunga, akamtia kifungoni.
2 Rois 18.21 Psaumes 149.7-149.8 2 Rois 24.1 Esaïe 31.1-31.3 2 Rois 25.7
5 Ndipo mfalme wa Ashuru akakwea katikati ya nchi yote, akaenda Samaria, akauhusuru miaka mitatu.
Osée 13.16 2 Rois 25.1-25.3 2 Rois 18.9 Jérémie 52.4-52.5
6 Katika mwaka wa kenda wa Hoshea, huyo mfalme wa Ashuru akautwaa Samaria, akawahamisha Israeli mpaka Ashuru, akawaweka katika Hala na Habori, karibu na mto wa Gozani, na katika miji ya Wamedi.
Deutéronome 28.64 Osée 13.16 1 Chroniques 5.26 Lévitique 26.32-26.33 Deutéronome 29.27-29.28

Les raisons de l’exil d’Israël

7 Yalitukia hayo kwa sababu wana wa Israeli walikuwa wametenda dhambi juu ya Bwana, Mungu wao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri watoke chini ya mkono wa Farao mfalme wa Misri, wakawaacha miungu mingine.
Josué 23.16 Néhémie 9.26 Exode 20.2 Exode 14.15-14.30 Deutéronome 31.29
8 Wakaziendea sheria za mataifa, ambao Bwana aliwafukuza mbele ya wana wa Israeli, na sheria za wafalme wa Israeli walizozifanya.
Lévitique 18.3 Deutéronome 18.9 2 Rois 16.3 Lévitique 18.27-18.30 2 Rois 21.2
9 Tena, wana wa Israeli wakafanya kwa siri mambo yasiyokuwa mema juu ya Bwana, Mungu wao, wakajijengea mahali pa juu katika miji yao yote, kutoka mnara wa walinzi hata katika miji yenye boma.
2 Rois 18.8 Osée 12.11 Ezéchiel 8.12 Deutéronome 27.15 Deutéronome 13.6
10 Wakajisimamishia nguzo na maashera juu ya kila mlima mrefu, na chini ya kila mti wenye majani mabichi;
1 Rois 14.23 Exode 34.13 Michée 5.14 2 Rois 16.4 Deutéronome 16.21
11 wakafukiza uvumba huko katika kila mahali pa juu, kama mataifa walivyofanya, ambao Bwana aliwafukuza mbele yao; wakaunda mambo mabaya, ili wamkasirishe Bwana;
1 Rois 13.1 Psaumes 78.56-78.58 2 Chroniques 28.25 Jérémie 44.17 2 Rois 21.6
12 wakatumikia sanamu, ambazo Bwana aliwakataza, akasema, Msitende jambo hili.
Exode 20.3-20.5 Deutéronome 4.23-4.25 Lévitique 26.1 Deutéronome 4.15-4.19 Deutéronome 12.4
13 Pamoja na hayo Bwana aliwashuhudia Israeli, na Yuda, kwa kinywa cha kila nabii, na cha kila mwonaji, akisema, Geukeni, na kuziacha njia zenu mbaya, mkazishike amri zangu na hukumu zangu, sawasawa na ile sheria yote niliyowaamuru baba zenu, nikawapelekea kwa kinywa cha manabii watumishi wangu.
1 Samuel 9.9 Jérémie 18.11 Jérémie 35.15 Jérémie 7.3-7.7 Néhémie 9.29-9.30
14 Walakini hawakutaka kusikia, bali walifanya shingo zao kuwa ngumu, kama shingo za baba zao, wasiomwamini Bwana, Mungu wao.
Deutéronome 31.27 Actes 7.51 Hébreux 3.12 Psaumes 78.32 Romains 2.4-2.5
15 Wakazikataa sheria zake, na agano lake, alilolifanya na baba zao; na shuhuda zake alizowashuhudia; wakafuata ubatili, wakawa ubatili, nao wakaandamana na mataifa waliowazunguka, ambao Bwana alikuwa amewaagiza, wasitende kwa mfano wao.
Deutéronome 12.30-12.31 Deutéronome 32.21 Jérémie 2.5 Romains 1.21-1.23 1 Rois 16.13
16 Wakaziacha amri zote za Bwana, Mungu wao, wakajifanyizia sanamu za kusubu, yaani, ndama mbili, wakafanya na Ashera, wakaliabudu jeshi lote la mbinguni, wakamtumikia Baali.
1 Rois 12.28 1 Rois 14.23 1 Rois 16.31 1 Rois 14.15 Deutéronome 4.19
17 Wakawapitisha watoto wao, waume na wake, motoni, wakapiga ramli, wakafanya uchawi, wakajiuza nafsi zao wapate kufanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, hata kumkasirisha.
2 Rois 21.6 1 Rois 21.20 2 Rois 16.3 Deutéronome 18.10-18.12 Ezéchiel 23.37
18 Kwa hiyo Bwana akawaghadhibikia Israeli sana, akawahamisha mbali na uso wake; wala hapana aliyesalia ila kabila ya Yuda peke yake.
1 Rois 11.32 1 Rois 11.13 1 Rois 12.20 Osée 11.12 1 Rois 11.36
19 Hata na watu wa Yuda hawakuyashika maagizo ya Bwana, Mungu wao, lakini walikwenda katika amri za Israeli walizokuwa wamezifanya wenyewe.
2 Rois 16.3 1 Rois 14.22-14.23 2 Chroniques 21.11 2 Chroniques 21.13 Jérémie 3.8-3.11
20 Basi Bwana akakikataa kizazi chote cha Israeli, akawatesa, na kuwatia katika mikono ya watu wenye kuwateka nyara, hata alipokwisha kuwatupa, watoke machoni pake.
2 Rois 15.29 Jérémie 6.30 2 Rois 13.3 Néhémie 9.2 2 Rois 13.7
21 Maana aliwatenga mbali Israeli na nyumba ya Daudi; nao wakamfanya Yeroboamu mwana wa Nebati kuwa mfalme; Yeroboamu akawavuta Israeli wasimfuate Bwana, akawakosesha kosa kubwa.
1 Rois 11.11 1 Rois 11.31 1 Rois 14.16 1 Rois 12.28-12.30 1 Samuel 2.24
22 Nao wana wa Israeli wakaendelea katika dhambi zote za Yeroboamu alizozifanya; hawakujiepusha nazo;
2 Rois 13.2 2 Rois 15.9 2 Rois 3.3 2 Rois 10.29 2 Rois 13.6
23 hata Bwana akawaondoa Waisraeli wasiwe mbele zake, kama vile alivyosema kwa kinywa cha watumishi wake wote, manabii. Basi Waisraeli walichukuliwa mateka kutoka nchi yao wenyewe, waende nchi ya Ashuru, hata leo.
2 Rois 17.6 2 Rois 17.13 2 Rois 17.20 Amos 5.27 1 Rois 14.16

Repeuplement de la Samarie

24 Naye mfalme wa Ashuru akaleta watu kutoka Babeli, na Kutha, na Ava, na Hamathi, na Sefarvaimu, akawaweka katika miji ya Samaria badala ya wana wa Israeli; wakaumiliki Samaria, wakakaa katika miji yake.
2 Rois 18.34 2 Rois 19.13 2 Rois 17.30-17.31 1 Rois 8.65 Esdras 4.2-4.10
25 Basi ikawa, wakati ule walipoanza kukaa huko, hawakumcha Bwana; kwa hiyo Bwana akapeleka simba kati yao, nao wakawaua baadhi yao.
2 Rois 17.32 2 Rois 17.41 2 Rois 17.34 Jérémie 15.3 Daniel 6.26
26 Kwa hiyo wakamwambia mfalme wa Ashuru, wakasema, Wale wa mataifa uliowahamisha, na kuwaweka katika miji ya Samaria, hawaijui kawaida ya Mungu wa nchi; kwa hiyo amepeleka simba kati yao, na tazama, wanawaua, kwa sababu hawaijui kawaida ya Mungu wa nchi.
1 Samuel 10.25 Amos 8.14 1 Samuel 8.9 2 Rois 17.27
27 Ndipo mfalme wa Ashuru akatoa amri, akasema, Mpelekeni mmojawapo wa makuhani, mliowachukua kutoka huko; aende akakae huko, akawafundishe kawaida ya Mungu wa nchi.
Juges 17.13 1 Rois 12.31 1 Rois 13.2 2 Chroniques 11.15
28 Basi mmoja wa makuhani waliochukuliwa kutoka Samaria akaenda akakaa katika Betheli, akawafundisha jinsi ilivyowapasa kumcha Bwana.
1 Rois 12.29-12.32 Esaïe 29.13 Matthieu 15.14
29 Lakini pamoja na hayo watu wa kila taifa wakajifanyia miungu yao wenyewe, wakaiweka katika nyumba za mahali pa juu, walipopafanya Wasamaria, kila taifa katika miji yao walimokaa.
Michée 4.5 1 Rois 12.31 Esaïe 44.9-44.20 Psaumes 115.4-115.8 Jérémie 10.3-10.5
30 Watu wa Babeli wakafanya Sukoth-benothi kuwa mungu wao, watu wa Kutha wakafanya Nergali, watu wa Hamathi wakafanya Ashima,
2 Rois 17.24
31 Waavi wakafanya Nibhazi na Tartaki; nao Wasefarvi wakawaunguza wana wao katika moto kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.
2 Rois 17.24 2 Rois 17.17 2 Rois 19.37 Esdras 4.9 Deutéronome 12.31
32 Basi hivyo wakamcha Bwana, nao wakijifanyia wengine wao kuwa makuhani wa mahali pa juu, ambao waliwafanyia dhabihu katika nyumba za mahali pa juu.
1 Rois 12.31 2 Rois 17.29 1 Rois 13.31 2 Rois 23.19 Sophonie 1.5
33 Wakamcha Bwana, na kuitumikia miungu yao wenyewe, sawasawa na kawaida za mataifa ambao wao walihamishwa kutoka kwao.
Luc 16.13 Matthieu 6.24 1 Rois 18.21 2 Rois 17.41 Osée 10.2
34 Hata siku hii ya leo hufanya sawasawa na kawaida za kwanza; wala hawamwogopi Bwana, wala hawazifuati sheria zao, wala hukumu zao, wala ile torati, wala ile amri Bwana aliyowaamuru wana wa Yakobo, ambaye alimpa jina la Israeli;
Genèse 32.28 Genèse 35.10 1 Rois 11.31 2 Rois 17.25 Genèse 33.20
35 hao ambao Bwana alifanya agano nao, akawaamuru, akasema, Msiche miungu mingine, wala kuisujudia, wala kuitumikia, wala kuitolea sadaka;
Juges 6.10 Josué 23.16 Deutéronome 4.23-4.27 Exode 20.4-20.5 Exode 34.12-34.17
36 ila yeye Bwana, aliyewaleta kutoka nchi ya Misri kwa nguvu nyingi, na kwa mkono ulionyoshwa, yeye ndiye mtakayemcha, yeye ndiye mtakayemsujudia, yeye ndiye mtakayemtolea sadaka;
Exode 6.6 Deutéronome 6.13 Exode 9.15 Lévitique 19.32 Actes 4.30
37 na sheria, na hukumu, na torati, na amri, alizowaandikia, hizo ndizo mtakazozishika na kuzifanya hata milele; wala msiche miungu mingine.
Deutéronome 4.44-4.45 Psaumes 105.44-105.45 Deutéronome 5.31-6.2 Néhémie 9.13-9.14 Lévitique 19.37
38 Na hilo agano nililofanya nanyi, msilisahau; wala msiche miungu mingine;
Deutéronome 4.23 Deutéronome 6.12 Deutéronome 8.14-8.18
39 lakini Bwana, Mungu wenu, ndiye mtakayemcha; naye atawaokoa mikononi mwa adui zenu wote.
2 Rois 17.36 Esaïe 8.12-8.14 Néhémie 9.27 1 Samuel 12.24 Jérémie 10.7
40 Walakini hawakusikia, bali wakafanya sawasawa na kawaida zao za kwanza.
2 Rois 17.8 2 Rois 17.12 Deutéronome 4.28 Jérémie 13.23 2 Rois 17.34
41 Basi mataifa hawa wakamcha Bwana, tena wakaziabudu sanamu zao za kuchongwa; na wana wao vile vile, na wana wa wana wao; kama walivyofanya baba zao, wao nao hufanya vivyo hivyo hata leo.
Sophonie 1.5 Matthieu 6.24 1 Rois 18.21 2 Rois 17.32-17.33 Josué 24.14-24.20

Cette Bible est dans le domaine public.