Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 3.2
Bible en Swahili de l’est


Assassinat d’Abner

1 Basi kulikuwa na vita siku nyingi kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi; Daudi akaendelea akasitawi, lakini nyumba ya Sauli ikaendelea kudhoofika.
1 Rois 14.30 2 Samuel 2.17 Galates 5.17 Psaumes 45.3-45.5 Genèse 3.15
2 Naye Daudi akazaliwa wana huko Hebroni; mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Amnoni, wa Ahinoamu wa Yezreeli;
1 Chroniques 3.1-3.4 1 Samuel 25.42-25.43 2 Samuel 13.1-13.29 Genèse 49.3-49.4
3 na wa pili wake Danieli, wa Abigaili mkewe Nabali wa Karmeli; na wa tatu Absalomu, mwana wa Maaka binti Talmai, mfalme wa Geshuri,
1 Samuel 27.8 2 Samuel 13.37-13.38 1 Samuel 25.42 2 Samuel 17.1-17.14 Deutéronome 3.14
4 na wa nne Adoniya, mwana wa Hagithi; na wa tano Shefatia, mwana wa Abitali;
1 Rois 1.5-1.18 1 Rois 2.13-2.25
5 na wa sita Ithreamu, wa Egla, mkewe Daudi. Hawa walizaliwa kwa Daudi huko Hebroni.
6 Ikawa, wakati vilipokuwapo vita kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi, Abneri akajipatia nguvu nyumbani kwa Sauli.
2 Samuel 2.8-2.9 Esaïe 8.9-8.10 2 Chroniques 25.8 Matthieu 12.30 Joël 3.9-3.13
7 Basi Sauli alikuwa na suria, jina lake akiitwa Rispa, binti Aya; Ishboshethi akamwuliza Abneri, Kwa nini umeingia kwa suria ya babangu?
2 Samuel 21.8-21.11 2 Samuel 16.21-16.22 1 Rois 2.17 1 Rois 2.21-2.22 2 Samuel 12.8
8 Basi Abneri akakasirika kwa maneno ya Ishboshethi, akasema, Je! Mimi ni kichwa cha mbwa, aliye wa Yuda? Hata leo hivi nawafanyia fadhili nyumba ya Sauli babako, na ndugu zake, na rafiki zake, nisikutie wewe mkononi mwa Daudi; nawe hata hivyo wanitia hatiani leo kwa mwanamke huyu.
2 Samuel 9.8 2 Samuel 16.9 1 Samuel 24.14-24.15 1 Samuel 15.28 2 Samuel 5.2
9 Mungu amfanyie Abneri vivyo, na kuzidi, nisipomtendea Daudi kama vile Bwana alivyomwapia;
1 Samuel 15.28 1 Rois 19.2 2 Samuel 3.35 1 Chroniques 12.23 Ruth 1.17
10 kuupitisha ufalme toka nyumba ya Sauli, na kukisimamisha kiti cha Daudi juu ya Israeli, na juu ya Yuda, toka Dani mpaka Beer-sheba.
Juges 20.1 1 Rois 4.25 2 Samuel 24.2 1 Samuel 3.20 2 Samuel 17.11
11 Wala hakuweza kumjibu Abneri tena, kwa sababu alimwogopa.
12 Basi Abneri akatuma wajumbe kwa Daudi mahali alipokuwapo, akisema, Nchi hii ni ya nani? Fanya agano nami, na tazama, mkono wangu utakuwa pamoja nawe, ili kuwaleta Israeli wote kwako.
1 Chroniques 12.38-12.40 Matthieu 21.8-21.10 1 Chroniques 11.1-11.3 2 Samuel 3.21 2 Samuel 3.27
13 Daudi akasema, Vema, nitafanya agano nawe, lakini nina sharti moja nitakalo kwako, nalo ni hili; Hutaniona uso wangu, isipokuwa uniletee Mikali, binti Sauli, hapo ujapo kuniona uso wangu.
Genèse 43.3 Genèse 44.26 Genèse 44.23 2 Samuel 3.20-3.23 1 Samuel 19.11-19.17
14 Basi Daudi akatuma wajumbe kwa Ishboshethi, mwana wa Sauli, kusema, Nipe mke wangu Mikali, niliyemposa kwa govi mia za Wafilisti.
1 Samuel 18.27 1 Samuel 18.25 2 Samuel 2.10
15 Basi Ishboshethi akatuma watu, akamnyang’anya Paltieli, mwana wa Laishi, mumewe, mwanamke huyo.
1 Samuel 25.44
16 Huyo mumewe akafuatana naye, akiendelea na kulia, akamfuata mpaka Bahurimu. Ndipo Abneri akamwambia, Haya, rudi. Naye akarudi.
2 Samuel 16.5 2 Samuel 19.16 2 Samuel 17.18 1 Rois 2.8 Proverbes 9.17-9.18
17 Basi Abneri akafanya mashauri na wazee wa Israeli, akasema, Zamani mlitaka Daudi awamiliki;
18 basi, sasa, fanyeni hayo; kwa maana Bwana amemtaja Daudi, akisema, kwa mkono wa mtumishi wangu, Daudi, nitawaokoa watu wangu Israeli katika mikono ya Wafilisti, na katika mikono ya adui zao wote.
1 Samuel 15.28 2 Samuel 3.9 Psaumes 132.17-132.18 1 Samuel 16.1 1 Samuel 9.16
19 Tena Abneri alinena masikioni mwa Benyamini; kisha Abneri akaenda ili kunena masikioni mwa Daudi huko Hebroni maneno yote yaliyoonekana kuwa mema machoni pa Israeli, na machoni pa nyumba yote ya Benyamini.
1 Chroniques 12.29 1 Samuel 10.20-10.21 Psaumes 68.27
20 Basi Abneri akamwendea Daudi huko Hebroni, na watu ishirini pamoja naye. Daudi akamfanyia karamu Abneri, na watu wote waliokuwa pamoja naye.
Genèse 26.30 Genèse 31.54 Esther 1.3
21 Kisha Abneri akamwambia Daudi, Nitaondoka, niende zangu; nami nitamkusanyia bwana wangu mfalme Israeli wote, ili wafanye agano nawe, ukamiliki juu ya wote inaowatamani roho yako. Basi Daudi akamruhusu Abneri; naye akaenda zake kwa amani.
2 Samuel 3.12 1 Rois 11.37 2 Samuel 3.10 2 Samuel 2.9 Philippiens 2.21
22 Na tazama, watumishi wa Daudi pamoja na Yoabu walitoka jeshini, wakaleta mateka mengi pamoja nao; lakini Abneri hakuwako Hebroni kwa Daudi; maana alikuwa amemruhusu, naye amekwisha kwenda zake kwa amani.
23 Hata Yoabu, na jeshi lote waliokuwa pamoja naye, walipofika, watu wakamwambia Yoabu, wakisema, Abneri, mwana wa Neri, alikuja kwa mfalme, naye amemruhusu, naye amekwenda zake kwa amani.
24 Basi Yoabu akamwendea mfalme, akasema, Umefanyaje? Tazama, Abneri amekuja kwako; mbona umemruhusu, naye amekwisha kwenda zake?
Jean 18.35 Nombres 23.11 2 Samuel 3.8 2 Samuel 3.39 2 Samuel 19.5-19.7
25 Wewe wamjua Abneri, mwana wa Neri, ya kuwa alikuja ili kukudanganya, apate kujua kutoka kwako, na kuingia kwako, akajue yote uyatendayo.
Deutéronome 28.6 Esaïe 37.28 Jean 7.12 Psaumes 121.8 Genèse 42.12
26 Naye Yoabu alipotoka kwa Daudi, akapeleka wajumbe kumfuata Abneri, wakamrudisha kutoka kisima cha Sira; lakini Daudi alikuwa hana habari.
Proverbes 26.23-26.26 Proverbes 27.4-27.6
27 Basi Abneri alipokuwa amerudi Hebroni, Yoabu akamchukua kando hata katikati ya lango, ili aseme naye kwa faragha; akampiga mkuki wa tumbo huko, hata akafa; kwa ajili ya damu ya Asaheli, ndugu yake.
1 Rois 2.5 2 Samuel 20.9-20.10 1 Rois 2.32 Jérémie 41.2 2 Samuel 2.19-2.23
28 Hata baadaye Daudi aliposikia, akasema, Mimi na ufalme wangu hatuna hatia milele mbele za Bwana, kwa sababu ya damu ya Abneri, mwana wa Neri;
Genèse 4.10 Genèse 9.6 Deutéronome 21.1-21.9 Matthieu 27.24 Exode 21.12
29 na imwangukie Yoabu kichwani pake, na nyumba yote ya babaye, tena hiyo nyumba ya Yoabu isikose kuwa na mtu mwenye kutoka damu, au aliye na ukoma, au mwenye kutegemea fimbo, au mwenye kuanguka kwa upanga au mwenye kuhitaji chakula.
2 Samuel 1.16 1 Rois 2.31-2.34 2 Rois 5.1 1 Samuel 2.32-2.36 Lévitique 13.44-13.46
30 Basi Yoabu, na Abishai nduguye, walimwua Abneri, kwa sababu yeye alimwua ndugu yao Asaheli katika vita huko Gibeoni.
Proverbes 28.17 Actes 28.4 2 Samuel 2.19-2.23
31 Kisha Daudi alimwambia Yoabu, na watu wote waliokuwa pamoja naye, Rarueni nguo zenu, mkajivike nguo za magunia, mkamlilie Abneri. Naye mfalme Daudi akaifuata jeneza.
Genèse 37.34 2 Samuel 1.2 2 Samuel 1.11 Josué 7.6 Juges 11.35
32 Wakamzika Abneri katika Hebroni; naye mfalme akapaza sauti yake, akalia kaburini kwa Abneri, nao watu wote wakalia.
Proverbes 24.17 Job 31.28 2 Samuel 1.12 2 Samuel 18.33 1 Samuel 30.4
33 Ndipo mfalme akamwomboleza Abneri, akasema, Ilimpasaje Abneri kufa afavyo mpumbavu?
2 Samuel 1.17 2 Samuel 13.12-13.13 Proverbes 18.7 Ecclésiaste 2.15-2.16 Jérémie 17.11
34 Mikono yako haikufungwa, Wala miguu yako haikutiwa pingu; Aangukavyo mtu mbele ya wana wa uovu, ndivyo ulivyoanguka. Na watu wote wakaongeza kumlilia.
Job 24.14 2 Samuel 1.12 Psaumes 107.10-107.11 Osée 6.9 Juges 16.21
35 Wakaja na watu wote wamshurutishe Daudi kula chakula, ukalipo bado mchana; lakini Daudi akaapa, akasema Mungu anitendee vivyo, na kuzidi, nikionja mkate, au kingine cho chote kabla lichwapo jua.
2 Samuel 12.17 2 Samuel 1.12 Ruth 1.17 Jérémie 16.7 Juges 20.26
36 Wakaangalia watu wote, yakawa mema machoni pao; kama yalivyokuwa mema machoni pao yote aliyoyatenda mfalme.
Marc 7.37 Psaumes 62.9 2 Samuel 15.6 Marc 15.11-15.13 2 Samuel 15.13
37 Wakajua watu wote, na Israeli wote, siku ile, ya kuwa si nia ya mfalme kwamba auawe Abneri, mwana wa Neri.
38 Kisha mfalme akawaambia watumishi wake, Hamjui ya kuwa mkuu mmoja, naye ni mtu mkubwa ameanguka leo katika Israeli?
2 Samuel 2.8 2 Samuel 3.12 Job 32.9 1 Samuel 14.50-14.51
39 Nami leo nimedhoofika, hata nijapotiwa mafuta niwe mfalme; na watu hao, wana wa Seruya, ni wagumu kwangu mimi; Bwana amlipie mwovu sawasawa na uovu wake.
1 Rois 2.33-2.34 Psaumes 28.4 1 Rois 2.5-2.6 2 Timothée 4.14 Psaumes 101.8

Cette Bible est dans le domaine public.