Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 23.3
Bible en Swahili de l’est


Délivrance de Keïla par David

1 Kisha wakamwambia Daudi, kusema, Angalia, Wafilisti wanapigana vita juu ya Keila na kuiba nafaka sakafuni mwa kupuria.
Josué 15.44 Néhémie 3.17-3.18 Juges 6.11 Lévitique 26.16 Deutéronome 28.51
2 Basi Daudi akamwuliza Bwana, kusema, Je! Niende nikawapige hao Wafilisti? Naye Bwana akamwambia Daudi, Nenda ukawapige Wafilisti, na kuuokoa Keila.
2 Samuel 5.23 2 Samuel 5.19 1 Samuel 23.4 1 Samuel 30.8 1 Samuel 23.6
3 Ila watu wake Daudi wakamwambia, Tazama, sisi tunaogopa hapa katika Yuda; je! Si zaidi tukienda Keila juu ya majeshi ya Wafilisti?
1 Samuel 23.23 1 Samuel 23.26 Psaumes 11.1 Jérémie 12.5 1 Samuel 23.15
4 Basi Daudi akamwuliza Bwana tena, Naye Bwana akamjibu, akasema, Ondoka, ukashukie Keila; kwa kuwa nitawatia hao Wafilisti mikononi mwako.
Juges 7.7 Josué 8.7 1 Samuel 28.6 2 Samuel 5.19 Juges 6.39
5 Ndipo wakaenda Keila, Daudi na watu wake, wakapigana na hao Wafilisti, wakateka nyara ng’ombe zao, na kuwaua uuaji mkuu. Hivyo Daudi akawaokoa watu wa Keila.
6 Ikawa Abiathari, mwana wa Ahimeleki, alipomkimbilia Daudi huko Keila, alishuka na naivera mkononi mwake.
1 Samuel 22.20 Exode 28.30-28.31 1 Samuel 14.3 1 Samuel 14.18 1 Samuel 14.36-14.37
7 Kisha Sauli aliambiwa ya kwamba Daudi amefika Keila. Sauli akasema, Mungu amemtia mkononi mwangu; kwa maana amefungwa ndani, kwa vile alivyoingia katika mji wenye malango na makomeo.
1 Samuel 24.4-24.6 Job 20.5 Exode 14.3 Psaumes 71.10-71.11 Exode 15.9
8 Basi Sauli akawaita watu wote waende vitani, ili waishukie Keila, na kumhusuru Daudi na watu wake.
9 Naye Daudi alifahamu ya kuwa Sauli amemkusudia mabaya; akamwambia Abiathari, kuhani, Lete hapa hiyo naivera.
1 Samuel 30.7 1 Samuel 23.6 Nombres 27.21 Actes 23.16-23.18 Jérémie 11.18-11.19
10 Ndipo Daudi akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mimi mtumwa wako nimesikia hakika ya kuwa Sauli anataka kuja huku Keila, ili kuuharibu mji kwa ajili yangu.
Genèse 18.24 Proverbes 28.15 1 Samuel 22.19 1 Samuel 23.8 Romains 3.15-3.16
11 Je! Watu wa Keila watanitoa, nitiwe mkononi mwake? Je! Sauli atashuka, kama mtumwa wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, nakusihi, umwambie mtumwa wako. Naye Bwana akamjibu, Atashuka.
Psaumes 50.15 Jérémie 33.3 Matthieu 7.7-7.8
12 Ndipo Daudi akasema, Je! Watu wa Keila watanitia mimi na watu wangu mkononi mwake Sauli? Bwana akasema, Watakutia.
1 Samuel 23.20 Psaumes 118.8 Ecclésiaste 9.14-9.15 Esaïe 29.15 Psaumes 62.1

David dans les déserts de Ziph et de Maon

13 Basi Daudi na watu wake, ambao wapata kama mia sita, wakaondoka na kutoka Keila, wakaenda po pote walipoweza kwenda. Kisha Sauli akaambiwa ya kwamba Daudi amekimbia toka Keila; akaacha kutoka nje.
1 Samuel 25.13 1 Samuel 22.2 1 Samuel 30.9-30.10 2 Samuel 15.20
14 Basi Daudi alikuwa akikaa nyikani ngomeni, akakaa katika nchi ya milima milima kwenye nyika ya Zifu. Naye Sauli alikuwa akimtafuta kila siku, lakini Mungu hakumtia mikononi mwake.
Psaumes 54.3-54.4 Josué 15.55 Josué 15.24 Psaumes 32.7 1 Samuel 23.7
15 Daudi akaona ya kwamba Sauli ametoka nje ili kutafuta roho yake; naye Daudi akawako katika nyika ya Zifu, huko Horeshi.
16 Ndipo Yonathani, mwana wa Sauli, akainuka akamwendea Daudi huko Horeshi, akamtia nguvu mkono wake katika Mungu.
Esaïe 35.3-35.4 Hébreux 12.12-12.13 2 Timothée 2.1 Ephésiens 6.10 Luc 22.32
17 Akamwambia, Usiogope, kwa maana mkono wa Sauli, babangu, hautakupata; na wewe utakuwa mfalme juu ya Israeli; na mimi nitakuwa wa pili wako; ndivyo ajuavyo hata Sauli, babangu.
1 Samuel 20.31 1 Samuel 24.20 Hébreux 13.6 Esaïe 54.17 Esaïe 41.10
18 Na hao wawili wakafanya agano mbele za Bwana; Daudi naye akakaa huko Horeshi, na Yonathani akaenda nyumbani kwake.
1 Samuel 20.42 2 Samuel 21.7 1 Samuel 18.3 2 Samuel 9.1 1 Samuel 20.12-20.17
19 Ndipo wale Wazifi wakakwea kwa Sauli huko Gibea, wakasema, Je! Yule Daudi hakujificha kwetu ngomeni mwa Horeshi, kilimani pa Hakila upande wa kusini wa Yeshimoni?
1 Samuel 26.1 1 Samuel 26.3 Psaumes 54.1-54.7 Proverbes 29.12 1 Samuel 22.7-22.8
20 Basi sasa, Ee mfalme, ushuke, kama utakavyo nafsini mwako kushuka; na kazi yetu itakuwa kumtia mkononi mwa mfalme.
1 Samuel 23.12 Psaumes 112.10 Proverbes 11.23 2 Samuel 3.21 Psaumes 54.3
21 Naye Sauli akasema, Na mbarikiwe ninyi na Bwana; kwa sababu mmenihurumia.
1 Samuel 22.8 Esaïe 66.5 Michée 3.11 Psaumes 10.3 Juges 17.2
22 Nendeni, nawasihi, mkazidi kupata hakika, mkajue na kuona mahali pake anapojificha, tena ni nani aliyemwona huko; maana nimeambiwa ya kwamba atenda kwa hila nyingi.
Job 5.13
23 Chunguzeni basi, mkayajue maficho yake yote anapojificha; kisha njoni kwangu, tena msikose, nami nitakwenda pamoja nanyi; tena itakuwa, akiwapo katika nchi, mimi nitamtafuta-tafuta katika elfu zote za Yuda.
Marc 14.10-14.11 Proverbes 1.16 Jean 18.2-18.3 2 Samuel 17.11-17.13 Romains 3.15-3.16
24 Nao wakaondoka, wakaenda Zifu kumtangulia Sauli; lakini Daudi na watu wake walikuwapo nyikani pa Maoni, katika Araba upande wa kusini wa jangwa.
1 Samuel 25.2 Josué 15.55
25 Basi Sauli na watu wake wakaenda kumtafuta. Watu wakamwambia Daudi; basi kwa hiyo akashuka mpaka mwambani, akakaa nyikani pa Maoni. Naye Sauli alipopata habari, alimwinda Daudi nyikani pa Maoni.
1 Samuel 23.28 Juges 15.8
26 Sauli akaenda upande huu wa mlima, na Daudi na watu wake wakaenda upande huu wa mlima; naye Daudi akafanya haraka sana kwenda zake kwa hofu ya Sauli; kwa sababu Sauli na watu wake wakamzunguka Daudi na watu wake ili kuwakamata.
Psaumes 17.9 2 Samuel 17.21-17.22 2 Chroniques 20.12 Psaumes 118.11-118.13 Psaumes 31.22
27 Lakini akaja mjumbe kwa Sauli, kusema, Njoo upesi, kwa kuwa Wafilisti wameishambulia nchi.
2 Rois 19.9 Deutéronome 32.36 Psaumes 116.3 Apocalypse 12.16 Genèse 22.14
28 Basi Sauli akarudi kutoka kumwinda Daudi, akaenda kinyume cha Wafilisti; kwa hiyo wakapaita mahali pale, Selahamalekothi.
29 Naye Daudi akakwea kutoka huko, akakaa katika ngome ya Engedi.
2 Chroniques 20.2 Josué 15.62 Cantique 1.14 Ezéchiel 47.10 Genèse 14.7

Cette Bible est dans le domaine public.