Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 22.12
Bible en Swahili de l’est


David dans la grotte d’Adullam

1 Basi Daudi akaondoka huko, akakimbilia pango la Adulamu; na ndugu zake na watu wote wa mbari ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
Psaumes 57.1-57.11 Josué 15.35 Psaumes 142.1-142.7 Josué 12.15 1 Chroniques 11.15
2 Na kila mtu aliyekuwa katika hali ya dhiki, na kila mtu aliyekuwa na deni, na watu wote wenye uchungu mioyoni mwao, wakakusanyika kwake; naye akawa jemadari wao; nao waliokuwa pamoja naye walipata kama watu mia nne.
1 Samuel 30.6 Psaumes 72.12-72.14 1 Samuel 30.22-30.24 1 Samuel 25.13 1 Samuel 9.16
3 Kutoka huko Daudi akaenda Mispa ya Moabu; akamwambia mfalme wa Moabu, Tafadhali ukubali baba yangu na mama yangu watoke huko waliko, wakakae kwenu, hata nitakapojua Mungu atakalotenda kwa ajili yangu.
Juges 11.29 1 Samuel 3.18 Ruth 4.17 Genèse 47.11 2 Samuel 15.25-15.26
4 Akawaleta mbele ya mfalme wa Moabu, nao wakakaa pamoja naye wakati wote Daudi alipokuwa ngomeni.
2 Samuel 23.13-23.14 1 Samuel 23.1-23.6 1 Chroniques 12.16 1 Chroniques 21.9 Néhémie 6.11
5 Kisha nabii Gadi akamwambia Daudi, Usikae hapa ngomeni; ondoka, ukaende mpaka nchi ya Yuda. Ndipo Daudi akaondoka, akaenda zake, akakaa katika msitu wa Herethi.
1 Chroniques 21.9 2 Chroniques 29.25 1 Chroniques 29.29 2 Samuel 24.11

Massacre des prêtres de Nob

6 Kisha Sauli akasikia ya kwamba Daudi ameonekana, na wale watu waliokuwa pamoja naye. Basi Sauli alikuwa akikaa Gibea, chini ya mkwaju katika mahali palipoinuka, naye alikuwa na mkuki wake mkononi, na watumishi wake wote wakimzunguka.
1 Samuel 20.33 1 Samuel 19.9 Juges 4.5 1 Samuel 18.10 Genèse 21.33
7 Naye Sauli akawaambia watumishi wake waliomzunguka, Sikieni sasa, enyi Wabenyamini; je! Huyu mwana wa Yese atawapa ninyi kila mmoja mashamba, na mashamba ya mizabibu, atawafanya kuwa maakida wa watu elfu, na maakida wa watu mia;
1 Rois 12.16 Esaïe 11.10 1 Samuel 22.13 1 Samuel 20.27 2 Samuel 20.1
8 hata ninyi nyote mkafanya fitina juu yangu, wala hapana mtu anifunuliaye habari hii mwanangu afanyapo agano na mwana wa Yese, wala hapana mmoja wenu anayenisikitikia, wala kunifunulia ya kuwa mwanangu amemwondokesha mtumishi wangu juu yangu, anivizie kama hivi leo?
1 Samuel 18.3 1 Samuel 23.21 1 Samuel 20.2 1 Samuel 23.16-23.18 1 Samuel 20.30-20.34
9 Ndipo akajibu Doegi, Mwedomi, aliyesimama karibu na watumishi wa Sauli, akasema, Mimi nalimwona mwana wa Yese akienda Nobu, kwa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu.
Psaumes 52.1-52.9 Proverbes 19.5 Ezéchiel 22.9 Matthieu 26.59-26.61 1 Samuel 14.3
10 Naye akamwuliza Bwana kwa ajili yake, akampa vyakula, akampa na ule upanga wa Goliathi, Mfilisti.
Nombres 27.21 1 Samuel 23.4 1 Samuel 23.2 1 Samuel 30.8 1 Samuel 10.22
11 Ndipo mfalme akatuma watu waende kumwita Ahimeleki, kuhani, mwana wa Ahitubu, na jamaa yote ya baba yake, hao makuhani, waliokuwako huko Nobu; nao wakaenda kwa mfalme wote pia.
Romains 3.15
12 Sauli akasema, Sikia sasa, Ewe mwana wa Ahitubu. Naye akaitika, Mimi hapa, bwana wangu.
1 Samuel 22.13 Esaïe 65.1 1 Samuel 22.7 2 Samuel 9.6
13 Sauli akamwuliza, Mbona mmefanya fitina juu yangu, wewe na mwana wa Yese? Kwa maana umempa mikate, na upanga, nawe umemwuliza Mungu kwa ajili yake, ili aniondokee na kunivizia kama hivi leo?
1 Samuel 22.8 Amos 7.10 Psaumes 119.69 Luc 23.2-23.5
14 Basi Ahimeleki akamjibu mfalme, akasema, Katika watumishi wako wote ni nani aliye mwaminifu kama Daudi, aliye mkwewe mfalme, tena msiri wako, mwenye heshima nyumbani mwako?
1 Samuel 19.4-19.5 1 Samuel 20.32 1 Samuel 26.23 1 Samuel 24.11 1 Samuel 22.13
15 Je! Mimi nimeanza leo tu kumwuliza Mungu kwa ajili yake? Hasha! Mfalme asinidhanie mimi, mtumishi wake neno hili, Wala jamaa yote ya baba yangu, kwa maana mimi, mtumishi wako siyajui hayo yote, yaliyopungua au yaliyozidi.
1 Samuel 25.36 1 Pierre 3.16-3.17 2 Samuel 15.11 Genèse 20.5-20.6 2 Corinthiens 1.12
16 Naye mfalme akasema, Kufa utakufa, Ahimeleki, wewe na jamaa yote ya baba yako.
Proverbes 28.15 1 Rois 19.2 1 Rois 18.4 1 Samuel 14.44 Matthieu 2.16
17 Kisha mfalme akawaambia askari walinzi waliosimama karibu naye Geukeni, mkawaue hao makuhani wa Bwana, kwa sababu mkono wao u pamoja na Daudi, na kwa sababu walijua ya kuwa amekimbia, wasiniarifu. Lakini watumishi wa mfalme walikataa kunyosha mkono na kuwaangukia makuhani wa Bwana.
Exode 1.17 Actes 4.19 1 Samuel 20.33 2 Rois 1.13-1.14 1 Rois 1.5
18 Basi mfalme akamwambia Doegi, Geuka wewe, ukawaangukia hao makuhani. Basi Doegi, Mwedomi, akageuka, akawaangukia makuhani, akaua siku ile watu themanini na watano wenye kuvaa naivera ya kitani.
Sophonie 3.3 1 Samuel 3.12-3.14 1 Samuel 2.18 1 Samuel 2.30-2.33 Exode 28.40
19 Kisha akaupiga Nobu, mji wa makuhani, kwa makali ya upanga, wanaume na wanawake, watoto na wanyonyao, na ng’ombe, na punda, na kondoo.
1 Samuel 15.3 Osée 10.14 Josué 6.21 Josué 6.17 Jacques 2.13
20 Na katika wana wa Ahimeleki, mwana wa Ahitubu, akaokoka mtu mmoja tu, aliyeitwa jina lake Abiathari, akamkimbilia Daudi.
1 Samuel 23.6 1 Rois 2.26-2.27 1 Samuel 30.7 1 Samuel 23.9 2 Samuel 20.25
21 Naye Abiathari akamweleza Daudi ya kwamba Sauli amewaua makuhani wa Bwana.
22 Daudi akamwambia Abiathari, Siku ile alipokuwako Doegi, Mwedomi, nalijua yakini ya kuwa atamwambia Sauli; mimi nimewapatia watu wote wa jamaa ya baba yako kifo.
1 Samuel 21.1-21.9 Psaumes 44.22
23 Kaa wewe pamoja nami, usiogope; kwa maana yeye atafutaye roho yangu, ndiye atafutaye na roho yako; nawe utakaa kwangu salama.
1 Rois 2.26 Jean 10.28-10.30 Jean 15.20 Hébreux 12.1-12.3 Jean 18.9

Cette Bible est dans le domaine public.