Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Apocalypse 1
Bible en Swahili de l’est


Message à sept Églises d’Asie

Titre et salutation

1 Ufunuo wa Yesu Kristo, aliopewa na Mungu awaonyeshe watumwa wake mambo ambayo kwamba hayana budi kuwako upesi; naye akatuma kwa mkono wa malaika akamwonyesha mtumwa wake Yohana;
Apocalypse 22.6 Apocalypse 22.16 Apocalypse 1.19 Daniel 2.28-2.29 Apocalypse 1.9
2 aliyelishuhudia Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu Kristo, yaani, mambo yote aliyoyaona.
Apocalypse 12.17 Jean 19.35 1 Corinthiens 1.6 Apocalypse 1.19 Apocalypse 1.9
3 Heri asomaye na wao wayasikiao maneno ya unabii huu, na kuyashika yaliyoandikwa humo; kwa maana wakati u karibu.
Romains 13.11 Luc 11.28 Apocalypse 22.10 Proverbes 8.34 1 Pierre 4.7
4 Yohana, kwa yale makanisa saba yaliyoko Asia; Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwake yeye aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja; na zitokazo kwa roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi;
Apocalypse 3.1 Apocalypse 4.5 Esaïe 11.2 Apocalypse 5.6 Zacharie 4.10
5 tena zitokazo kwa Yesu Kristo, shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake,
Psaumes 89.27 Colossiens 1.18 Apocalypse 3.14 Apocalypse 17.14 Apocalypse 19.16
6 na kutufanya kuwa ufalme, na makuhani kwa Mungu, naye ni Baba yake; utukufu na ukuu una Yeye hata milele na milele. Amina.
Apocalypse 5.10 Apocalypse 20.6 1 Pierre 4.11 1 Pierre 2.5-2.9 Jude 1.25
7 Tazama, yuaja na mawingu; na kila jicho litamwona, na hao waliomchoma; na kabila zote za dunia wataomboleza kwa ajili yake. Naam. Amina.
Zacharie 12.10 Daniel 7.13 Jean 19.37 Matthieu 24.30 Luc 21.27
8 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema Bwana Mungu, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.
Esaïe 44.6 Apocalypse 21.6 Esaïe 43.10 Apocalypse 22.13 Esaïe 48.12

Vision du Fils de l’homme

9 Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na subira ya Yesu Kristo, nalikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya Neno la Mungu, na ushuhuda wa Yesu.
Actes 14.22 Jean 16.33 Apocalypse 1.2 Philippiens 4.14 Apocalypse 3.10
10 Nalikuwa katika Roho, siku ya Bwana; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, kama sauti ya baragumu,
Apocalypse 17.3 Apocalypse 4.1-4.2 Apocalypse 21.10 Matthieu 22.43 Actes 20.7
11 ikisema, Haya uyaonayo uyaandike katika chuo, ukayapeleke kwa hayo makanisa saba: Efeso, na Smirna, na Pergamo, na Thiatira, na Sardi, na Filadelfia, na Laodikia.
Apocalypse 1.4 Apocalypse 3.1 Apocalypse 3.7 Habakuk 2.2 Apocalypse 2.8
12 Nikageuka niione ile sauti iliyosema nami. Na nilipogeuka, niliona vinara vya taa saba vya dhahabu;
Zacharie 4.2 Exode 25.37 Apocalypse 1.20-2.1 Apocalypse 1.13 Ezéchiel 43.5-43.6
13 na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa Mwanadamu, amevaa vazi lililofika miguuni, na kufungwa mshipi wa dhahabu matitini.
Daniel 7.13 Apocalypse 15.6 Daniel 10.16 Apocalypse 14.14 Exode 28.6-28.8
14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji; na macho yake kama mwali wa moto;
Daniel 7.9 Daniel 10.6 Apocalypse 19.12 Apocalypse 2.18 Matthieu 28.3
15 na miguu yake kama shaba iliyosuguliwa sana, kana kwamba imesafishwa katika tanuru; na sauti yake kama sauti ya maji mengi.
Ezéchiel 43.2 Apocalypse 14.2 Daniel 10.6 Apocalypse 19.6 Apocalypse 2.18
16 Naye alikuwa na nyota saba katika mkono wake wa kuume; na upanga mkali, wenye makali kuwili, ukitoka katika kinywa chake; na uso wake kama jua liking’aa kwa nguvu zake.
Hébreux 4.12 Apocalypse 2.12 Esaïe 49.2 Apocalypse 2.16 Apocalypse 19.15
17 Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,
Esaïe 44.6 Apocalypse 22.13 Daniel 8.17-8.18 Esaïe 48.12 Esaïe 41.4
18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.
Romains 6.9 Hébreux 7.25 Romains 14.8-14.9 Apocalypse 4.9 Hébreux 7.16
19 Basi, uyaandike mambo hayo uliyoyaona, nayo yaliyopo, na yale yatakayokuwa baada ya hayo.
Apocalypse 4.1-4.11 Apocalypse 1.11-2.3
20 Siri ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume, na ya vile vinara saba vya dhahabu. Zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba; na vile vinara saba ni makanisa saba.
Apocalypse 2.1 Zacharie 4.2 Apocalypse 3.1 Apocalypse 1.16 Matthieu 5.14-5.16

Cette Bible est dans le domaine public.