Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Pierre 3.5
Bible en Swahili de l’est


1 Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;
Colossiens 3.18 1 Corinthiens 7.16 1 Corinthiens 11.3 Genèse 3.16 1 Corinthiens 9.19-9.22
2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.
Philippiens 1.27 1 Pierre 2.12 Colossiens 3.22 1 Pierre 3.5-3.6 Ephésiens 5.33
3 Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;
Esaïe 3.18-3.24 1 Timothée 2.9-2.10 Tite 2.3-2.15 Esaïe 52.1 Esther 5.1
4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.
Romains 2.29 Romains 7.22 1 Samuel 16.7 Colossiens 3.12 2 Corinthiens 4.16
5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.
1 Timothée 5.5 Tite 2.3-2.4 Jérémie 49.11 Luc 2.37 Actes 1.14
6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote.
Genèse 18.12 Esaïe 57.11 Romains 9.7-9.9 Galates 4.22-4.26 Matthieu 26.69-26.75
7 Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.
Colossiens 3.19 Ephésiens 5.33 Malachie 2.14-2.16 Ephésiens 5.25-5.28 1 Thessaloniciens 4.4
8 Neno la mwisho ni hili; mwe na nia moja, wenye kuhurumiana, wenye kupendana kama ndugu, wasikitikivu, wanyenyekevu;
Ephésiens 4.31-5.2 Romains 12.10 1 Pierre 1.22 Ephésiens 4.2 Colossiens 3.12
9 watu wasiolipa baya kwa baya, au laumu kwa laumu; bali wenye kubariki; kwa sababu hayo ndiyo mliyoitiwa ili mrithi baraka.
Romains 12.17 Romains 12.14 Proverbes 20.22 Matthieu 5.39 Romains 12.19-12.21
10 Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.
Psaumes 34.12-34.16 Jacques 1.26 1 Pierre 2.1 Apocalypse 14.5 Proverbes 8.35
11 Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana.
Matthieu 5.9 Psaumes 34.14 Hébreux 12.14 Romains 12.18 Jacques 4.17
12 Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake husikiliza maombi yao; Bali uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya.
Jean 9.31 Proverbes 15.29 Psaumes 34.15-34.16 Proverbes 15.3 Proverbes 15.8
13 Naye ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema?
Proverbes 16.7 Romains 8.28 Psaumes 38.20 3 Jean 1.11 1 Timothée 5.10
14 Lakini mjapoteswa kwa sababu ya haki mna heri. Msiogope kutisha kwao, wala msifadhaike; bali mtakaseni Kristo Bwana mioyoni mwenu.
1 Pierre 2.19-2.20 Esaïe 8.12-8.13 Matthieu 10.28 Marc 10.29 Jean 14.27
15 Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu.
Colossiens 4.6 2 Timothée 2.25-2.26 Luc 21.14-21.15 1 Pierre 3.2 Hébreux 6.1
16 Nanyi mwe na dhamiri njema, ili katika neno lile mnalosingiziwa, watahayarishwe wale wautukanao mwenendo wenu mwema katika Kristo.
1 Pierre 2.12 Hébreux 13.18 Matthieu 5.11 1 Pierre 2.19 1 Pierre 2.15
17 Maana ni afadhali kuteswa kwa kutenda mema, ikiwa ndiyo mapenzi ya Mungu, kuliko kwa kutenda mabaya.
1 Pierre 3.14 1 Pierre 4.19 1 Pierre 2.15 1 Pierre 2.20 Matthieu 26.39

Christ, un exemple dans la souffrance

18 Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa,
1 Pierre 4.1 Hébreux 9.28 Hébreux 9.26 1 Pierre 4.6 1 Jean 1.9
19 ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri;
1 Pierre 4.6 Esaïe 61.1 Esaïe 42.7 Esaïe 49.9 1 Pierre 1.11-1.12
20 watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji.
Hébreux 11.7 Genèse 6.3 Genèse 6.5 2 Pierre 2.5 Genèse 8.18
21 Mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unaowaokoa ninyi pia siku hizi; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo.
Marc 16.16 Galates 3.27 1 Pierre 1.3 Actes 2.38 Colossiens 2.12
22 Naye yupo mkono wa kuume wa Mungu, amekwenda zake mbinguni, malaika na enzi na nguvu zikiisha kutiishwa chini yake.
Marc 16.19 Hébreux 8.1 Ephésiens 1.20-1.21 Romains 8.38 Colossiens 3.1

Cette Bible est dans le domaine public.