1 Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;
Colossiens 3.18  1 Corinthiens 7.16  Genèse 3.16  1 Corinthiens 11.3  Ephésiens 5.33  
 2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.
1 Pierre 2.12  Philippiens 1.27  1 Timothée 4.12  Ephésiens 6.5  1 Pierre 3.15-3.16  
 3 Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;
1 Timothée 2.9-2.10  Esaïe 3.18-3.24  Tite 2.3-2.15  Ezéchiel 16.7-16.13  Genèse 24.53  
 4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.
Romains 2.29  Romains 7.22  1 Samuel 16.7  Tite 3.2  Colossiens 3.12  
 5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.
1 Timothée 5.5  Tite 2.3-2.4  1 Timothée 2.10  1 Samuel 2.1  1 Timothée 2.15  
 6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote.
Genèse 18.12  Daniel 3.16-3.18  Actes 4.8-4.13  1 Pierre 3.14-3.15  Genèse 18.15  
 7 Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.
Colossiens 3.19  Ephésiens 5.33  Malachie 2.14-2.16  Ephésiens 5.25-5.28  1 Thessaloniciens 4.4  
 8 Neno la mwisho ni hili; mwe na nia moja, wenye kuhurumiana, wenye kupendana kama ndugu, wasikitikivu, wanyenyekevu;
Ephésiens 4.31-5.2  Romains 12.10  1 Pierre 1.22  Ephésiens 4.2  Colossiens 3.12  
 9 watu wasiolipa baya kwa baya, au laumu kwa laumu; bali wenye kubariki; kwa sababu hayo ndiyo mliyoitiwa ili mrithi baraka.
Romains 12.17  Romains 12.14  Proverbes 20.22  1 Thessaloniciens 5.15  Matthieu 5.39  
 10 Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.
Psaumes 34.12-34.16  Jacques 1.26  1 Pierre 2.22  Jean 12.25  Jean 1.47  
 11 Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana.
Matthieu 5.9  Psaumes 34.14  Hébreux 12.14  Romains 12.18  1 Timothée 6.18  
 12 Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake husikiliza maombi yao; Bali uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya.
Jean 9.31  Proverbes 15.29  Psaumes 34.15-34.16  Proverbes 15.3  Proverbes 15.8  
 13 Naye ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema?
Proverbes 16.7  Romains 8.28  Psaumes 38.20  Proverbes 15.9  3 Jean 1.11  
 14 Lakini mjapoteswa kwa sababu ya haki mna heri. Msiogope kutisha kwao, wala msifadhaike; bali mtakaseni Kristo Bwana mioyoni mwenu.
1 Pierre 2.19-2.20  Esaïe 8.12-8.13  Luc 6.22-6.23  Matthieu 10.28  Marc 10.29  
 15 Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu.
Colossiens 4.6  2 Timothée 2.25-2.26  Luc 21.14-21.15  1 Pierre 3.2  Hébreux 6.1  
 16 Nanyi mwe na dhamiri njema, ili katika neno lile mnalosingiziwa, watahayarishwe wale wautukanao mwenendo wenu mwema katika Kristo.
1 Pierre 2.12  Hébreux 13.18  1 Pierre 2.15  Matthieu 5.11  1 Pierre 2.19  
 17 Maana ni afadhali kuteswa kwa kutenda mema, ikiwa ndiyo mapenzi ya Mungu, kuliko kwa kutenda mabaya.
1 Pierre 2.15  1 Pierre 2.20  1 Pierre 3.14  1 Pierre 4.19  Actes 21.14  
 18 Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa,
1 Pierre 4.1  Hébreux 9.28  Hébreux 9.26  Tite 2.14  1 Pierre 4.6  
 19 ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri;
1 Pierre 4.6  Esaïe 61.1  Esaïe 42.7  Esaïe 49.9  Apocalypse 20.7  
 20 watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji.
Genèse 6.3  Hébreux 11.7  Genèse 6.5  2 Pierre 2.5  Genèse 8.18  
 21 Mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unaowaokoa ninyi pia siku hizi; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo.
Marc 16.16  Galates 3.27  1 Pierre 1.3  Actes 2.38  1 Corinthiens 12.13  
 22 Naye yupo mkono wa kuume wa Mungu, amekwenda zake mbinguni, malaika na enzi na nguvu zikiisha kutiishwa chini yake.Marc 16.19  Hébreux 8.1  Ephésiens 1.20-1.21  Romains 8.38  1 Corinthiens 15.24