Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Pierre 3.10
Bible en Swahili de l’est


1 Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;Colossiens 3.18 1 Corinthiens 7.16 1 Corinthiens 11.3 Genèse 3.16 1 Corinthiens 9.19-9.22
2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.Philippiens 1.27 1 Pierre 2.12 Ephésiens 5.33 1 Pierre 1.15 Philippiens 3.20
3 Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;Esaïe 3.18-3.24 1 Timothée 2.9-2.10 Tite 2.3-2.15 Genèse 24.22 Exode 32.2
4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.Romains 2.29 Romains 7.22 1 Samuel 16.7 Esaïe 61.1 Matthieu 23.26
5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.1 Timothée 5.5 Tite 2.3-2.4 Actes 1.14 Actes 9.36 Luc 8.2-8.3
6 Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote.Genèse 18.12 Galates 4.22-4.26 Matthieu 26.69-26.75 Actes 4.19 Daniel 3.16-3.18
7 Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.Colossiens 3.19 Ephésiens 5.33 Malachie 2.14-2.16 Ephésiens 5.25-5.28 1 Thessaloniciens 4.4
8 Neno la mwisho ni hili; mwe na nia moja, wenye kuhurumiana, wenye kupendana kama ndugu, wasikitikivu, wanyenyekevu;Ephésiens 4.31-5.2 Romains 12.10 1 Pierre 1.22 Colossiens 3.12 Ephésiens 4.2
9 watu wasiolipa baya kwa baya, au laumu kwa laumu; bali wenye kubariki; kwa sababu hayo ndiyo mliyoitiwa ili mrithi baraka.Romains 12.17 Romains 12.14 Proverbes 20.22 Romains 12.19-12.21 1 Thessaloniciens 5.15
10 Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.Psaumes 34.12-34.16 Jacques 1.26 Apocalypse 14.5 Proverbes 8.35 Jacques 3.1-3.10
11 Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana.Matthieu 5.9 Psaumes 34.14 Hébreux 12.14 Romains 12.18 Galates 5.22
12 Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake husikiliza maombi yao; Bali uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya.Jean 9.31 Proverbes 15.29 Psaumes 34.15-34.16 Proverbes 15.8 Proverbes 15.3
13 Naye ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema?Proverbes 16.7 Romains 8.28 Psaumes 38.20 1 Thessaloniciens 5.15 1 Corinthiens 14.1
14 Lakini mjapoteswa kwa sababu ya haki mna heri. Msiogope kutisha kwao, wala msifadhaike; bali mtakaseni Kristo Bwana mioyoni mwenu.1 Pierre 2.19-2.20 Esaïe 8.12-8.13 Marc 10.29 Jean 14.27 Esaïe 41.10-41.14
15 Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu.Colossiens 4.6 2 Timothée 2.25-2.26 Luc 21.14-21.15 1 Pierre 3.2 Hébreux 6.1
16 Nanyi mwe na dhamiri njema, ili katika neno lile mnalosingiziwa, watahayarishwe wale wautukanao mwenendo wenu mwema katika Kristo.1 Pierre 2.12 Hébreux 13.18 Matthieu 5.11 1 Pierre 2.19 1 Pierre 2.15
17 Maana ni afadhali kuteswa kwa kutenda mema, ikiwa ndiyo mapenzi ya Mungu, kuliko kwa kutenda mabaya.1 Pierre 4.19 1 Pierre 2.15 1 Pierre 2.20 1 Pierre 3.14 1 Pierre 4.15
18 Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa,1 Pierre 4.1 Hébreux 9.28 Hébreux 9.26 1 Pierre 4.6 1 Jean 1.9
19 ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri;1 Pierre 4.6 Esaïe 61.1 Esaïe 42.7 Esaïe 49.9 Apocalypse 20.7
20 watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji.Hébreux 11.7 Genèse 6.3 Genèse 6.5 2 Pierre 2.5 Genèse 8.18
21 Mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unaowaokoa ninyi pia siku hizi; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo.Marc 16.16 Galates 3.27 1 Pierre 1.3 Actes 2.38 Actes 22.16
22 Naye yupo mkono wa kuume wa Mungu, amekwenda zake mbinguni, malaika na enzi na nguvu zikiisha kutiishwa chini yake.Hébreux 8.1 Ephésiens 1.20-1.21 Romains 8.38 Marc 16.19 Hébreux 1.3

Cette Bible est dans le domaine public.