Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Josué 15.34
Bible en Swahili de l’est


Territoire accordé à Juda

1 Kura ya kabila ya wana wa Yuda kwa kuandama jamaa zao ilikuwa kufikilia hata mpaka wa Edomu, hata bara ya Sini upande wa kusini, huko mwisho upande wa kusini.
Ezéchiel 47.19 Nombres 26.55-26.56 Nombres 34.3-34.5 Nombres 33.36-33.37 Josué 14.2
2 Mpaka wao wa kusini ulikuwa kutoka mwisho wa Bahari ya Chumvi, kutoka ile hori ielekeayo kusini;
Josué 3.16 Nombres 34.3 Ezéchiel 47.18 Esaïe 11.15 Genèse 14.3
3 nao ukaendelea upande wa kusini wa kukwea kwenda Akrabimu, kisha ukaendelea hata Sini, kisha ukaenda upande wa kusini wa Kadesh-barnea, kisha ukaendelea karibu na Hesroni, kisha ukafikilia Adari, na kuzunguka kwendea Karka;
Nombres 34.4 Juges 1.36 Genèse 14.7 Nombres 32.8 Nombres 20.1
4 kisha ukaendelea hata Azmoni, na kutokea hapo penye kijito cha Misri; na matokeo ya huo mpaka yalikuwa baharini; huu ndio mpaka wenu wa upande wa kusini.
Nombres 34.5 Josué 13.3 Genèse 15.18 Exode 23.31
5 Na mpaka wa upande wa mashariki ulikuwa Bahari ya Chumvi, hata mwisho wa mto wa Yordani. Na mpaka wa upande wa kaskazini ulikuwa kutoka pale penye hori ya baharini mwisho wa mto wa Yordani;
Nombres 34.12 Josué 18.15-18.19 Nombres 34.10
6 na huo mpaka ukaendelea hata Beth-hogla, kisha ukaendelea upande wa kaskazini wa Beth-araba; kisha mpaka ukaendelea hata jiwe la Bohani mwana wa Reubeni;
Josué 18.17 Josué 18.19-18.21
7 kisha mpaka ukaendelea hata Debiri kutoka bonde la Akori, vivyo ukaendelea upande wa kaskazini, kwa kuelekea Gilgali, iliyo mkabala wa kukwelea kwenda Adumimu, ulio upande wa kusini wa mto; kisha huo mpaka ukaendelea hata ukafikilia maji ya Enshemeshi, na matokeo yake yalikuwa hapo Enrogeli;
1 Rois 1.9 2 Samuel 17.17 Josué 7.26 Osée 2.5 Esaïe 65.10
8 kisha mpaka ukaendelea karibu na bonde la mwana wa Hinomu, na kufikilia ubavuni mwa huyu Myebusi upande wa kusini (ndio Yerusalemu); kisha mpaka ukaendelea hata kilele cha mlima ulio pale mkabala wa bonde la Hinomu upande wa magharibi, lililo pale mwisho wa bonde la Warefai upande wa kaskazini;
Josué 18.16 Josué 15.63 Josué 18.28 Juges 19.10 Juges 1.21
9 kisha mpaka ulipigwa kutoka juu ya mlima huo hata kufikilia chemchemi ya maji ya Neftoa kisha ukatokea hata miji ya kilima cha Efroni; kisha mpaka ulipigwa hata kufikilia Baala (ndio Kiriath-yearimu);
1 Chroniques 13.6 Josué 18.15 Juges 18.12 2 Samuel 6.2 Josué 9.17
10 kisha mpaka ukazunguka kutoka Baala kwendelea upande wa magharibi hata kilima Seiri, kisha ukaendelea hata upande wa mlima wa Yearimu upande wa kaskazini (huo ndio Kesaloni), kisha ukatelemkia Beth-shemeshi, na kwendelea karibu na Timna;
Juges 14.1 1 Samuel 6.12-6.21 Josué 15.57 Juges 14.5 Genèse 38.12-38.13
11 kisha mpaka ukatokea hata kufikilia upande wa Ekroni upande wa kaskazini; tena mpaka ulipigwa hata Shikroni, na kwendelea hata kilima cha Baala, kisha ukatokea hapo Yabneeli; na matokeo ya mpaka yalikuwa baharini.
Josué 19.43-19.44 1 Samuel 7.14 2 Rois 1.2-1.3 Josué 15.45 2 Rois 1.6
12 Na mpaka wa upande wa magharibi ulifikilia hata bahari kubwa, na mpaka wake. Huo ndio mpaka wa wana wa Yuda kwa kuzunguka kote kote sawasawa na jamaa zao.
Nombres 34.6-34.7 Ezéchiel 47.20 Josué 15.47 Deutéronome 11.24
13 Kisha alimpa huyo Kalebu mwana wa Yefune sehemu kati ya wana wa Yuda, kama Bwana alivyomwamuru Yoshua, maana ni Kiriath-arba, ni huyo Arba aliyekuwa babaye Anaki (huo ndio Hebroni).
Nombres 14.23-14.24 Nombres 13.30 Josué 14.6-14.15 Deutéronome 1.34-1.36
14 Huyo Kalebu aliwafukuza watoke hapo hao wana watatu wa Anaki, nao ni Sheshai, na Ahimani, na Talmai, wana wa Anaki.
Juges 1.10 Juges 1.20 Josué 11.21 Nombres 13.33 Nombres 13.22-13.23
15 Kisha akakwea kutoka huko ili kuwaendea wenyeji wa Debiri; jina la Debiri hapo kwanza lilikuwa Kiriath-seferi.
Josué 10.38 Josué 10.3 Juges 1.11-1.13
16 Kalebu akasema, Yeye atakayeupiga Kiriath-seferi na kuutwaa, mimi nitampa Aksa binti yangu awe mkewe.
Juges 1.6 Juges 1.12-1.13
17 Naye Othnieli mwana wa Kenazi, nduguye Kalebu, aliutwaa; basi akampa Aksa binti yake awe mkewe.
Juges 3.9 Juges 1.13 Josué 14.6 Juges 3.11 1 Chroniques 2.49
18 Kisha ikawa, hapo huyo mwanamke alipokwenda kwa mumewe, akamtaka aombe shamba kwa baba yake; akashuka katika punda wake; Kalebu akamwuliza, Wataka nini?
Genèse 24.64 1 Samuel 25.23
19 Huyo mwanamke akasema, Nipe baraka; kwa kuwa umeniweka katika nchi ya kusini, unipe na chemchemi za maji pia. Ndipo akampa chemchemi za maji ya juu, na chemchemi za maji ya chini.
Genèse 33.11 Juges 1.14-1.15 Deutéronome 33.7 2 Corinthiens 9.5 1 Samuel 25.27
20 Huu ndio urithi wa kabila ya wana wa Yuda sawasawa na jamaa zao.
Genèse 49.8-49.12 Deutéronome 33.7
21 Miji ya mwisho ya kabila ya wana wa Yuda upande wa kuelekea mpaka wa Edomu katika nchi ya Negebu ilikuwa ni Kabseeli, na Ederi, na Yaguri;
Genèse 35.21 Néhémie 11.25
22 na Kina, na Dimona, na Adada;
23 na Kedeshi, na Hazori, na Ithnani;
Josué 12.22 Deutéronome 1.19 Nombres 33.37
24 na Zifu, na Telemu, na Bealothi;
1 Samuel 23.14 1 Samuel 23.19 1 Samuel 23.24 1 Samuel 15.4 Psaumes 54.1
25 na Hazor-hadata, na Kerioth-hezroni (ndio Hazori);
26 na Amamu, na Shema, na Molada;
1 Chroniques 4.28
27 na Hasar-gada, na Heshmoni, na Bethpeleti;
Néhémie 11.26
28 na Hasarshuali, na Beer-sheba, na Biziothia;
Genèse 26.33 Genèse 21.14 1 Chroniques 4.28 Genèse 21.31-21.33 Josué 19.2-19.3
29 na Baala, na Iyimu, na Esemu;
Josué 19.3 1 Chroniques 4.29 Josué 15.9-15.11
30 na Eltoladi, na Kesili, na Horma;
Josué 19.4 Deutéronome 1.44 Juges 1.17 Nombres 14.45
31 na Siklagi, na Madmana, na Sansana;
1 Samuel 27.6 1 Samuel 30.1 1 Chroniques 12.1 Josué 19.5
32 na Lebaothi, na Shilhimu, na Aini, na Rimoni; miji hiyo yote ni miji ishirini na kenda, pamoja na vijiji vyake.
Nombres 34.11 Néhémie 11.29
33 Katika nchi ya Shefela, Eshtaoli, na Sora, na Ashna,
Juges 13.25 Juges 16.31 Nombres 13.23 Josué 19.41
34 na Zanoa, na Enganimu, na Tapua, na Enamu;
Josué 15.53 Josué 12.17
35 na Yarmuthi, na Adulamu, na Soko, na Azeka;
1 Samuel 17.1 1 Samuel 22.1 Josué 10.3 Néhémie 11.29 Josué 15.48
36 na Shaarimu, na Adithaimu, na Gedera, na Gederothaimu miji kumi na minne, pamoja na vijiji vyake.
1 Samuel 17.52
37 Senani, na Hadasha, na Migdal-gadi;
38 na Dilani, na Mispe, na Yoktheeli;
2 Rois 14.7 Juges 20.1 1 Samuel 7.16 Juges 21.5 Genèse 31.48-31.49
39 na Lakishi, na Boskathi, na Egloni;
Josué 10.3 2 Rois 22.1 Josué 10.31-10.32 2 Rois 18.14 2 Rois 14.19
40 na Kaboni, na Lamasi, na Kithilishi;
41 na Gederothi, na Beth-dagoni, na Naama, na Makeda; miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
Josué 10.21 Josué 10.28 Josué 10.10 Josué 12.16
42 Libna, na Etheri, na Ashani;
Josué 10.29 2 Rois 8.22 Josué 19.7 Josué 12.15
43 na Yifta, na Ashna, na Nesibu;
44 na Keila, na Akizibu, na Maresha; miji kenda, pamoja na vijiji vyake.
Michée 1.14-1.15 1 Samuel 23.1-23.14 Genèse 38.5
45 Ekroni, pamoja na miji yake na vijiji vyake;
Josué 13.3 Sophonie 2.4 Amos 1.8 1 Samuel 6.17 Zacharie 9.5-9.7
46 kutoka huko Ekroni mpaka baharini, yote iliyokuwa upande wa Ashdodi, pamoja na vijiji vyake.
2 Chroniques 26.6 1 Samuel 5.1 1 Samuel 5.6 Amos 1.8 Esaïe 20.1
47 Ashdodi, na miji yake na vijiji vyake; na Gaza, na miji yake na vijiji vyake; mpaka kijito cha Misri, na bahari kubwa, na mpaka wake.
Josué 15.4 Juges 16.1-16.21 Jérémie 47.1 Josué 13.3 Sophonie 2.4
48 Na katika nchi ya vilima, Shamiri, na Yatiri, na Soko;
Josué 21.14
49 na Dana, na Kiriath-sana (ambao ni Debiri);
Josué 15.15 Juges 1.11
50 na Anabu, na Eshtemoa, na Animu;
51 na Gosheni, na Holoni, na Gilo; miji kumi na mmoja, pamoja na vijiji vyake.
Josué 10.41 Josué 11.16 2 Samuel 15.12
52 Arabu, na Duma, na Eshani;
Esaïe 21.11
53 na Yanumu, na Beth-tapua, na Afeka;
54 na Humta, na Kiriath-arba (ndio Hebroni), na Siori; miji kenda, pamoja na vijiji vyake.
Josué 15.13 Genèse 23.2 Josué 14.15
55 Maoni, na Karmeli, na Zifu, na Yuta;
1 Samuel 25.2 Josué 15.24 1 Samuel 23.25 1 Samuel 25.7 2 Chroniques 26.10
56 na Yezreeli, na Yokdeamu, na Zanoa;
57 na Kaini, na Gibea, na Timna; miji kumi, pamoja na vijiji vyake.
Josué 15.10 Jérémie 14.1 Genèse 38.12
58 Halhuli, na Bethsuri, na Gedori;
1 Chroniques 4.39
59 na Maarathi, na Bethanothi, Eltekoni; miji sita, pamoja na vijiji vyake.
60 Kiriath-baali (ndio Kiriath-yearimu), na Raba; miji miwili, pamoja vijiji vyake.
Josué 18.14 1 Samuel 7.1
61 Huko nyikani, Betharaba, na Midini, na Sekaka;
Josué 15.6 Josué 18.18
62 na Nibshani, na huo Mji wa Chumvi, na Engedi; miji sita, pamoja na vijiji vyake.
1 Samuel 23.29 2 Chroniques 20.2
63 Tena katika habari ya Wayebusi, hao wenye kukaa Yerusalemu, wana wa Yuda hawakuweza kuwatoa; lakini hao Wayebusi walikaa pamoja na wana wa Yuda huko Yerusalemu hata hivi leo.
Juges 1.21 Juges 1.8 1 Chroniques 11.4-11.8 2 Samuel 5.6-5.9 Romains 7.14-7.21

Cette Bible est dans le domaine public.