Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Josué 11.3
Bible en Swahili de l’est


Conquêtes dans le nord

1 Kisha ikawa, hapo huyo Yabini, mfalme wa Hazori, aliposikia habari ya mambo hayo, akatuma mjumbe aende kwa Yobabu, mfalme wa Madoni, na kwa mfalme wa Shimroni, na mfalme wa Akshafu,
Josué 11.10 Juges 4.2 Psaumes 83.1-83.3 Josué 10.3-10.4 Esaïe 26.11
2 na hao wafalme waliokuwa upande wa kaskazini, katika nchi ya vilima, na katika Araba upande wa kusini wa Kinerethi, na katika Shefela, na katika nchi zilizoinuka za Dori upande wa magharibi,
Juges 1.27 Josué 12.3 Nombres 34.11 Josué 17.11 Josué 12.23
3 na kwa Mkanaani upande wa mashariki, na upande wa magharibi, na kwa Mwamori, na Mhiti, na Mperizi na Myebusi katika nchi ya vilima, na kwa Mhivi pale chini ya Hermoni katika nchi ya Mispa.
Juges 3.3 Josué 18.26 Genèse 31.49 Josué 13.11 Josué 15.63
4 Nao wakatoka nje, wao na jeshi zao zote pamoja nao, watu wengi mno, kama mchanga ulio ufuoni mwa bahari kwa wingi, pamoja na farasi na magari mengi sana.
Juges 7.12 1 Samuel 13.5 Genèse 32.12 Genèse 22.17 2 Samuel 17.11
5 Wafalme hao wote wakakutana pamoja; wakaenda na kupanga mahema yao pamoja hapo penye maji ya Meromu, ili kupigana na Israeli.
Esaïe 8.9 Psaumes 118.10-118.12 Psaumes 3.1 Apocalypse 16.14
6 Bwana akamwambia Yoshua, Usiche wewe kwa ajili ya hao; kwani kesho wakati kama huu nitawatoa hali wameuawa wote mbele ya Israeli; utawatema farasi zao, na magari yao utayapiga moto.
Josué 10.8 2 Samuel 8.4 Josué 11.9 Psaumes 20.7-20.8 Proverbes 20.7
7 Basi Yoshua akaenda, na watu wote wa vita pamoja naye, ili kupigana nao hapo penye maji ya Meromu ghafula; wakawaangukia.
Josué 10.9 1 Thessaloniciens 5.2-5.3
8 Bwana akawatia mkononi mwa Israeli, nao wakawapiga, na kuwafukuza hata kufikilia Sidoni ulio mkuu, na hata kufikilia Misrefoth-maimu, tena hata kufikilia bonde la Mispa upande wa mashariki; wakawapiga hata wasiwasaze hata mtu mmoja aliyesalia.
Josué 13.6 Josué 19.28 Josué 21.44 Josué 11.3 Zacharie 9.2
9 Yoshua akawafanyia vile vile kama Bwana alivyomwamuru; akawatema farasi zao, na magari yao akayapiga moto.
Josué 11.6 Ezéchiel 39.9-39.10
10 Yoshua akarudi wakati huo na kuutwaa Hazori, akampiga mfalme wa Hazori kwa upanga; kwa kuwa Hazori hapo kwanza ulikuwa ni kichwa cha falme hizo zote.
Juges 4.2 Josué 11.1
11 Nao wakawapiga wote pia waliokuwamo ndani ya Hazori kwa makali ya upanga, wakawaangamiza kabisa; hakusazwa hata mmoja aliyevuta pumzi; kisha akauteketeza Hazori kwa moto.
Josué 10.40 Deutéronome 20.16
12 Tena miji yote ya wafalme hao, na wafalme wake wote, Yoshua akawatwaa, akawapiga kwa makali ya upanga, na kuwaangamiza kabisa; vile vile kama huyo Musa mtumishi wa Bwana alivyomwamuru.
Deutéronome 7.2 Deutéronome 20.16-20.17 Josué 10.32 Josué 10.30 Josué 10.35
13 Lakini katika habari ya miji hiyo iliyosimama katika vilima vyao, Israeli hawakuipiga moto miji hiyo, isipokuwa ni mji wa Hazori tu; mji huo Yoshua aliupiga moto.
Jérémie 30.18
14 Tena nyara zote za miji hiyo, na wanyama wa miji, wana wa Israeli walitwaa kuwa nyara zao wenyewe; lakini kila mtu wakampiga kwa makali ya upanga, hata walipokuwa wamewaangamiza wote, wala hawakumsaza mmoja mwenye kuvuta pumzi.
Josué 11.11 Nombres 31.9 Deutéronome 20.14 Josué 8.27 Josué 10.40
15 Vile vile kama Bwana alivyomwamuru Musa mtumishi wake, ndivyo Musa alivyomwamuru Yoshua; naye Yoshua akafanya vivyo; hakukosa kufanya neno lo lote katika hayo yote Bwana aliyomwamuru Musa.
Josué 1.7 Deutéronome 7.2 Exode 34.11-34.13 1 Samuel 15.11 1 Samuel 15.8-15.9
16 Hivyo Yoshua akatwaa nchi hiyo yote, hiyo nchi ya vilima, na nchi yote ya Negebu, na nchi yote ya Gosheni, na hiyo Shefela, na hiyo Araba na nchi ya vilima vilima ya Israeli, na hiyo nchi tambarare;
Josué 10.41 Josué 12.8 Josué 11.21 Ezéchiel 36.8 Deutéronome 34.2-34.3
17 tangu kilima cha Halaki, kiendeleacho upande wa Seiri, mpaka Baal-gadi katika bonde la Lebanoni chini ya kilima cha Hermoni; naye akawatwaa wafalme wao wote, akawapiga, na kuwaua.
Deutéronome 7.24 Josué 13.5 Josué 11.3 Deutéronome 33.2 Josué 12.7-12.24
18 Yoshua akapiga vita siku nyingi na wafalme hao wote.
Josué 14.7-14.10 Josué 11.23
19 Haukuwapo mji hata mmoja uliofanya amani na wana wa Israeli, isipokuwa ni wale Wahivi wenye kukaa Gibeoni; wakaitwaa yote vitani.
Josué 9.3-9.27
20 Kwa kuwa lilikuwa ni la Bwana kuifanya mioyo yao kuwa migumu, hata wakatoka kupigana na Israeli, ili apate kuwaangamiza kabisa, wasihurumiwe lakini apate kuwaangamiza, kama vile Bwana alivyomwamuru Musa.
Romains 9.18 Exode 4.21 Deutéronome 20.16-20.17 Deutéronome 7.16 Deutéronome 2.30
21 Wakati huo Yoshua akaenda na kuwakatilia mbali hao Waanaki watoke nchi ya vilima, kutoka Hebroni, na kutoka Debiri, na kutoka Anabu, na kutoka katika nchi yote ya vilima vilima ya Yuda, na kutoka katika nchi yote ya vilima vilima ya Israeli; Yoshua akawaangamiza kabisa na miji yao.
Deutéronome 9.2 Nombres 13.22-13.23 Deutéronome 1.28 Josué 15.13-15.14 Juges 1.10-1.11
22 Hawakusalia Waanaki hata mmoja katika nchi ya wana wa Israeli; isipokuwa katika Gaza, na katika Gathi, na katika Ashdodi walisalia.
1 Samuel 17.4 Josué 15.46 1 Chroniques 18.1 1 Rois 2.39 Néhémie 13.23-13.24
23 Basi Yoshua akaitwaa hiyo nchi yote, sawasawa na hayo yote Bwana aliyokuwa amemwambia Musa; Yoshua naye akawapa Israeli kuwa ni urithi wao, sawasawa na walivyogawanyikana kwa kabila zao. Kisha nchi ikatulia isiwe na vita tena.
Nombres 26.52-26.55 Josué 14.1-14.15 Josué 21.44-21.45 Josué 22.4 Psaumes 46.9

Cette Bible est dans le domaine public.