1 Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote;
2 Timothée 2.24  Tite 3.2  Jacques 5.16  1 Timothée 2.4  1 Corinthiens 15.3  
 2 kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, tuishi maisha ya utulivu na amani, katika utauwa wote na ustahivu.
Esdras 6.10  Jérémie 29.7  Romains 13.1-13.7  Proverbes 24.21  1 Thessaloniciens 4.11  
 3 Hili ni zuri, nalo lakubalika mbele za Mungu Mwokozi wetu;1 Timothée 1.1  Luc 1.47  1 Timothée 5.4  1 Pierre 2.5  Romains 12.1-12.2  
 4 ambaye hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli.
Ezéchiel 18.32  Ezéchiel 18.23  2 Pierre 3.9  Tite 2.11  2 Timothée 2.25  
 5 Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu;
Galates 3.20  1 Corinthiens 8.6  Esaïe 44.6  Hébreux 7.25  Deutéronome 6.4  
 6 ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake.
Matthieu 20.28  1 Timothée 6.15  1 Corinthiens 1.6  Tite 1.3  Galates 4.4  
 7 Nami kwa ajili ya huo naliwekwa niwe mhubiri na mtume, (nasema kweli, sisemi uongo), mwalimu wa Mataifa katika imani na kweli.
2 Timothée 1.11  Actes 9.15  Ephésiens 3.7-3.8  Romains 9.1  Ecclésiaste 1.12  
 8 Basi, nataka wanaume wasalishe kila mahali, huku wakiinua mikono iliyotakata pasipo hasira wala majadiliano.
Psaumes 134.2  Psaumes 63.4  Jean 4.21  1 Timothée 5.14  Tite 3.8  
 9 Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
Proverbes 31.22  1 Pierre 3.3-3.5  Esaïe 3.16  Jérémie 2.32  Esther 5.1  
 10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.
Actes 9.36  2 Pierre 3.11  1 Pierre 2.12  Tite 2.14  Tite 3.8  
 11 Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.
1 Corinthiens 14.34-14.35  Genèse 3.16  Esther 1.20  Colossiens 3.18  1 Pierre 3.1  
 12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu.
1 Corinthiens 14.34  
 13 Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye.
Genèse 2.18  1 Corinthiens 11.8-11.9  Genèse 2.22  Genèse 2.7  Genèse 1.27  
 14 Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa.
Genèse 3.6  2 Corinthiens 11.3  Genèse 3.12-3.13  
 15 Walakini ataokolewa kwa uzazi wake, kama wakidumu katika imani na upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi.
1 Timothée 1.5  Tite 2.12  1 Pierre 4.7  1 Timothée 2.9  Genèse 3.15-3.16