Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 9.5
Bible en Swahili de l’est


Israël et les non-Juifs dans le plan de Dieu

Israël et la promesse de Dieu

1 Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu,
Galates 1.20 1 Timothée 2.7 Romains 1.9 2 Corinthiens 11.10 Romains 8.16
2 ya kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu.
Psaumes 119.136 Ezéchiel 9.4 Philippiens 3.18 Jérémie 13.17 Luc 19.41-19.44
3 Kwa maana ningeweza kuomba mimi mwenyewe niharimishwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili;
Exode 32.32 Galates 1.8 1 Corinthiens 16.22 Romains 11.14 1 Corinthiens 12.3
4 ambao ni Waisraeli, wenye kule kufanywa wana, na ule utukufu, na maagano, na kupewa torati, na ibada ya Mungu, na ahadi zake;
Ephésiens 2.12 Psaumes 147.19 Genèse 17.2 Exode 4.22 1 Rois 8.11
5 ambao mababu ni wao, na katika hao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili. Ndiye aliye juu ya mambo yote, Mungu, mwenye kuhimidiwa milele. Amina.
Romains 1.25 Jean 1.1-1.3 Colossiens 1.16-1.19 Romains 10.12 1 Jean 5.20
6 Si kana kwamba neno la Mungu limetanguka. Maana hawawi wote Waisraeli walio wa uzao wa Israeli.
Galates 6.16 Romains 2.28-2.29 Nombres 23.19 Jean 1.47 Romains 3.3
7 Wala hawawi wote wana kwa kuwa wazao wa Ibrahimu, bali, Katika Isaka wazao wako wataitwa;
Genèse 21.12 Hébreux 11.18 Galates 4.23 Luc 16.30 Jean 8.33
8 yaani, si watoto wa mwili walio watoto wa Mungu, bali watoto wa ile ahadi wanahesabiwa kuwa wazao.
Jean 1.13 Romains 4.11-4.16 Galates 3.26-3.29 Romains 8.14 Psaumes 87.6
9 Kwa maana neno la ahadi ni hili, Panapo wakati huu nitakuja, na Sara atakuwa na mwana.
Genèse 18.10 Genèse 18.14 Genèse 17.21 Hébreux 11.11-11.12 Genèse 21.2
10 Wala si hivyo tu, lakini Rebeka naye, akiisha kuchukua mimba kwa mume mmoja, naye ni Isaka, baba yetu,
Romains 5.3 Genèse 25.21-25.23 Romains 5.11 Luc 16.26
11 (kwa maana kabla hawajazaliwa wale watoto, wala hawajatenda neno jema wala baya, ili lisimame kusudi la Mungu la kuchagua, si kwa sababu ya matendo, bali kwa sababu ya nia yake aitaye),
Romains 4.17 Apocalypse 17.14 1 Pierre 5.10 2 Pierre 1.10 2 Thessaloniciens 2.13-2.14
12 aliambiwa hivi, Mkubwa atamtumikia mdogo.
Genèse 25.22-25.23 2 Samuel 8.14 1 Rois 22.47
13 Kama ilivyoandikwa, Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia.
Malachie 1.2-1.3 Deutéronome 21.15 Genèse 29.33 Genèse 29.31 Jean 12.25
14 Tuseme nini basi? Kuna udhalimu kwa Mungu? Hasha!
2 Chroniques 19.7 Deutéronome 32.4 Psaumes 145.17 Job 8.3 Psaumes 92.15
15 Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye.
Exode 33.19 Romains 9.16 Exode 34.6-34.7 Michée 7.18 Romains 9.18-9.19
16 Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu.
1 Pierre 2.9-2.10 Jean 3.8 Tite 3.3-3.5 Romains 9.11 Ephésiens 2.8
17 Kwa maana maandiko yasema juu ya Farao, ya kwamba, Nilikusimamisha kwa kusudi hili, ili nionyeshe nguvu zangu kwako, jina langu likatangazwe katika nchi yote.
Exode 9.16 Jean 17.26 Proverbes 16.4 Psaumes 83.17-83.18 Galates 4.30
18 Basi, kama ni hivyo, atakaye kumrehemu humrehemu, na atakaye kumfanya mgumu humfanya mgumu.
Romains 9.15-9.16 Josué 11.20 Exode 4.21 2 Thessaloniciens 2.10-2.12 Deutéronome 2.30
19 Basi, utaniambia, Mbona angali akilaumu? Kwa maana ni nani ashindanaye na kusudi lake?
Daniel 4.35 2 Chroniques 20.6 1 Corinthiens 15.35 Psaumes 76.10 Esaïe 46.10-46.11
20 La! Sivyo, Ee binadamu; wewe u nani umjibuye Mungu? Je! Kitu kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, Kwani kuniumba hivi?
Esaïe 29.16 Esaïe 45.9-45.11 Esaïe 64.8 Job 33.13 Job 40.2
21 Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?
Esaïe 64.8 Actes 9.15 2 Timothée 2.20-2.21 Romains 9.22-9.23 Romains 9.18
22 Ni nini basi, ikiwa Mungu kwa kutaka kuonyesha ghadhabu yake, na kuudhihirisha uweza wake, kwa uvumilivu mwingi, alichukuliana na vile vyombo vya ghadhabu vilivyofanywa tayari kwa uharibifu;
Proverbes 16.4 Jude 1.4 1 Pierre 2.8 Romains 9.21 2 Timothée 2.20
23 tena, ili audhihirishe wingi wa utukufu wake katika vile vyombo vya rehema, alivyovitengeneza tangu zamani vipate utukufu;
Romains 2.4 Ephésiens 3.16 1 Pierre 1.2-1.5 Colossiens 1.12 Romains 5.20-5.21
24 ndio sisi aliotuita, si watu wa Wayahudi tu, ila na watu wa Mataifa pia?
Romains 8.28-8.30 Romains 10.12 Romains 15.8-15.16 Actes 15.14 1 Pierre 5.10
25 Ni kama vile alivyosema katika Hosea, Nitawaita watu wangu wale wasiokuwa watu wangu, Na mpenzi wangu yeye asiyekuwa mpenzi wangu.
Osée 2.23 1 Pierre 2.10 Romains 1.7 Ezéchiel 16.8 Jean 16.27
26 Tena itakuwa mahali pale walipoambiwa, Ninyi si watu wangu, Hapo wataitwa wana wa Mungu aliye hai.
Esaïe 43.6 Romains 8.16 Osée 1.9-1.10 Galates 3.26 Matthieu 16.16
27 Isaya naye atoa sauti yake juu ya Israeli, kusema, Hesabu ya wana wa Israeli,ijapokuwa ni kama mchanga wa bahari,ni mabaki yao tu watakaookolewa.
Romains 11.4-11.6 Esaïe 10.20-10.23 Osée 1.10 Jérémie 5.10 Esaïe 1.1
28 Kwa maana Bwana atalitekeleza neno lake juu ya nchi, akilimaliza na kulikata.
Esaïe 5.16 Esaïe 30.12-30.14 Psaumes 65.5 Actes 17.31 Esaïe 10.23
29 Tena kama Isaya alivyotangulia kunena, Kama Bwana wa majeshi asingalituachia uzao, Tungalikuwa kama Sodoma, tungalifananishwa na Gomora.
Esaïe 1.9 Esaïe 13.19 Jérémie 50.40 Jacques 5.4 Jérémie 49.18

L’erreur d’Israël

30 Tuseme nini, basi? Ya kwamba watu wa Mataifa, wasioifuata haki, walipata haki; lakini ni ile haki iliyo ya imani;
Philippiens 3.9 Hébreux 11.7 Romains 4.11 Galates 2.16 Romains 10.6
31 bali Israeli wakiifuata sheria ya haki hawakuifikilia ile sheria.
Romains 11.7 Romains 3.20 Galates 3.21 Romains 9.30-9.32 Esaïe 51.1
32 Kwa sababu gani? Kwa sababu hawakuifuata kwa njia ya imani, bali kana kwamba kwa njia ya matendo. Wakajikwaa juu ya jiwe lile likwazalo,
1 Pierre 2.8 Actes 16.30-16.34 1 Corinthiens 1.23 1 Jean 5.9-5.12 Romains 10.3
33 kama ilivyoandikwa, Tazama, naweka katika Sayuni jiwe likwazalo, na mwamba uangushao; Na kila amwaminiye hatatahayarika.
Esaïe 28.16 Romains 10.11 Joël 2.26-2.27 Psaumes 25.2-25.3 Romains 5.5

Cette Bible est dans le domaine public.