Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Romains 9.3
Bible en Swahili de l’est


Israël et les non-Juifs dans le plan de Dieu

Israël et la promesse de Dieu

1 Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu,
1 Timothée 2.7 Galates 1.20 Romains 1.9 2 Corinthiens 12.19 2 Corinthiens 11.10
2 ya kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu.
Luc 19.41-19.44 Lamentations 3.51 Psaumes 119.136 Ezéchiel 9.4 Philippiens 3.18
3 Kwa maana ningeweza kuomba mimi mwenyewe niharimishwe na kutengwa na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili;
Exode 32.32 Galates 1.8 1 Corinthiens 16.22 Romains 11.14 1 Corinthiens 12.3
4 ambao ni Waisraeli, wenye kule kufanywa wana, na ule utukufu, na maagano, na kupewa torati, na ibada ya Mungu, na ahadi zake;
Ephésiens 2.12 Psaumes 147.19 Exode 4.22 Genèse 17.2 1 Rois 8.11
5 ambao mababu ni wao, na katika hao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili. Ndiye aliye juu ya mambo yote, Mungu, mwenye kuhimidiwa milele. Amina.
Romains 1.25 Colossiens 1.16-1.19 Jean 1.1-1.3 Esaïe 7.14 Esaïe 11.1
6 Si kana kwamba neno la Mungu limetanguka. Maana hawawi wote Waisraeli walio wa uzao wa Israeli.
Galates 6.16 Romains 2.28-2.29 Jean 1.47 Nombres 23.19 Romains 3.3
7 Wala hawawi wote wana kwa kuwa wazao wa Ibrahimu, bali, Katika Isaka wazao wako wataitwa;
Genèse 21.12 Hébreux 11.18 Philippiens 3.3 Jean 8.37-8.39 Galates 4.23
8 yaani, si watoto wa mwili walio watoto wa Mungu, bali watoto wa ile ahadi wanahesabiwa kuwa wazao.
Romains 8.14 Jean 1.13 Romains 4.11-4.16 Galates 3.26-3.29 Galates 4.22-4.31
9 Kwa maana neno la ahadi ni hili, Panapo wakati huu nitakuja, na Sara atakuwa na mwana.
Genèse 18.10 Genèse 18.14 Genèse 17.21 Hébreux 11.17 Hébreux 11.11-11.12
10 Wala si hivyo tu, lakini Rebeka naye, akiisha kuchukua mimba kwa mume mmoja, naye ni Isaka, baba yetu,
Romains 5.3 Luc 16.26 Genèse 25.21-25.23 Romains 5.11
11 (kwa maana kabla hawajazaliwa wale watoto, wala hawajatenda neno jema wala baya, ili lisimame kusudi la Mungu la kuchagua, si kwa sababu ya matendo, bali kwa sababu ya nia yake aitaye),
Romains 4.17 Ephésiens 1.9-1.11 Ephésiens 1.4-1.5 Apocalypse 17.14 1 Pierre 5.10
12 aliambiwa hivi, Mkubwa atamtumikia mdogo.
Genèse 25.22-25.23 1 Rois 22.47 2 Samuel 8.14
13 Kama ilivyoandikwa, Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia.
Malachie 1.2-1.3 Genèse 29.31 Deutéronome 21.15 Genèse 29.33 Proverbes 13.24
14 Tuseme nini basi? Kuna udhalimu kwa Mungu? Hasha!
2 Chroniques 19.7 Deutéronome 32.4 Job 8.3 Psaumes 92.15 Psaumes 145.17
15 Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye.
Exode 33.19 Romains 9.16 Romains 9.18-9.19 Exode 34.6-34.7 Michée 7.18
16 Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu.
Esaïe 65.1 1 Pierre 2.9-2.10 Jean 3.8 Tite 3.3-3.5 Romains 9.11
17 Kwa maana maandiko yasema juu ya Farao, ya kwamba, Nilikusimamisha kwa kusudi hili, ili nionyeshe nguvu zangu kwako, jina langu likatangazwe katika nchi yote.
Exode 9.16 Proverbes 16.4 Jean 17.26 Romains 11.4 Exode 10.1-10.2
18 Basi, kama ni hivyo, atakaye kumrehemu humrehemu, na atakaye kumfanya mgumu humfanya mgumu.
Romains 9.15-9.16 Josué 11.20 Exode 4.21 2 Thessaloniciens 2.10-2.12 Deutéronome 2.30
19 Basi, utaniambia, Mbona angali akilaumu? Kwa maana ni nani ashindanaye na kusudi lake?
Daniel 4.35 2 Chroniques 20.6 1 Corinthiens 15.35 Actes 4.27-4.28 Marc 14.21
20 La! Sivyo, Ee binadamu; wewe u nani umjibuye Mungu? Je! Kitu kilichoumbwa kimwambie yeye aliyekiumba, Kwani kuniumba hivi?
Esaïe 29.16 Esaïe 45.9-45.11 Job 33.13 Esaïe 64.8 1 Timothée 6.5
21 Au mfinyanzi je! Hana amri juu ya udongo, kwa fungu moja la udongo kuumba chombo kimoja kiwe cha heshima, na kimoja kiwe hakina heshima?
Esaïe 64.8 Actes 9.15 2 Timothée 2.20-2.21 Romains 9.22-9.23 Romains 9.18
22 Ni nini basi, ikiwa Mungu kwa kutaka kuonyesha ghadhabu yake, na kuudhihirisha uweza wake, kwa uvumilivu mwingi, alichukuliana na vile vyombo vya ghadhabu vilivyofanywa tayari kwa uharibifu;
Proverbes 16.4 Jude 1.4 1 Pierre 2.8 Romains 9.21 2 Timothée 2.20
23 tena, ili audhihirishe wingi wa utukufu wake katika vile vyombo vya rehema, alivyovitengeneza tangu zamani vipate utukufu;
Romains 2.4 Ephésiens 3.16 1 Pierre 1.2-1.5 Ephésiens 1.6-1.8 Romains 8.29
24 ndio sisi aliotuita, si watu wa Wayahudi tu, ila na watu wa Mataifa pia?
Apocalypse 19.9 Genèse 49.10 Romains 3.29-3.30 1 Corinthiens 1.9 Romains 8.28-8.30
25 Ni kama vile alivyosema katika Hosea, Nitawaita watu wangu wale wasiokuwa watu wangu, Na mpenzi wangu yeye asiyekuwa mpenzi wangu.
Osée 2.23 1 Pierre 2.10 Osée 1.1-1.2 Romains 1.7 Ezéchiel 16.8
26 Tena itakuwa mahali pale walipoambiwa, Ninyi si watu wangu, Hapo wataitwa wana wa Mungu aliye hai.
1 Jean 3.1-3.3 2 Corinthiens 6.18 Jean 11.52 Esaïe 43.6 Romains 8.16
27 Isaya naye atoa sauti yake juu ya Israeli, kusema, Hesabu ya wana wa Israeli,ijapokuwa ni kama mchanga wa bahari,ni mabaki yao tu watakaookolewa.
Esaïe 10.20-10.23 Romains 11.4-11.6 Osée 1.10 Jérémie 5.10 Esaïe 24.13
28 Kwa maana Bwana atalitekeleza neno lake juu ya nchi, akilimaliza na kulikata.
Psaumes 9.8 Esaïe 28.22 Apocalypse 19.11 Esaïe 5.16 Esaïe 30.12-30.14
29 Tena kama Isaya alivyotangulia kunena, Kama Bwana wa majeshi asingalituachia uzao, Tungalikuwa kama Sodoma, tungalifananishwa na Gomora.
Esaïe 1.9 Esaïe 13.19 Jérémie 50.40 Jacques 5.4 Amos 4.11

L’erreur d’Israël

30 Tuseme nini, basi? Ya kwamba watu wa Mataifa, wasioifuata haki, walipata haki; lakini ni ile haki iliyo ya imani;
Philippiens 3.9 Hébreux 11.7 Romains 4.11 Galates 2.16 Romains 10.6
31 bali Israeli wakiifuata sheria ya haki hawakuifikilia ile sheria.
Romains 11.7 Jacques 2.10-2.11 Galates 3.10-3.11 Romains 3.20 Galates 3.21
32 Kwa sababu gani? Kwa sababu hawakuifuata kwa njia ya imani, bali kana kwamba kwa njia ya matendo. Wakajikwaa juu ya jiwe lile likwazalo,
1 Corinthiens 1.23 1 Pierre 2.8 Actes 16.30-16.34 Luc 2.34 Romains 4.16
33 kama ilivyoandikwa, Tazama, naweka katika Sayuni jiwe likwazalo, na mwamba uangushao; Na kila amwaminiye hatatahayarika.
Romains 10.11 Esaïe 28.16 Joël 2.26-2.27 Psaumes 25.2-25.3 Romains 5.5

Cette Bible est dans le domaine public.