Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 6.9
Bible en Swahili de l’est


Désignation de sept assistants

1 Hata siku zile wanafunzi walipokuwa wakiongezeka hesabu yao, palikuwa na manung’uniko ya Wayahudi wa Kiyunani juu ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahauliwa katika huduma ya kila siku.
Actes 4.35 Actes 9.29 Actes 2.41 Actes 9.41 Actes 2.47
2 Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, Haipendezi sisi kuliacha neno la Mungu na kuhudumu mezani.
Deutéronome 1.9-1.14 Exode 18.17-18.26 2 Timothée 2.4 Nombres 11.11-11.13 Néhémie 6.3
3 Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili;
Deutéronome 1.13 Jacques 3.17-3.18 Job 32.7-32.8 Actes 13.2-13.3 Genèse 41.38-41.39
4 na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno.
Actes 1.14 Philippiens 1.9-1.11 Ephésiens 3.14-3.21 Colossiens 1.9-1.13 1 Corinthiens 9.16
5 Neno hili likapendeza machoni pa mkutano wote; wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, na Prokoro, na Nikanori, na Timoni, na Parmena, na Nikolao mwongofu wa Antiokia;
Actes 11.24 Actes 6.8 Actes 21.8 Actes 6.3 Actes 13.1
6 ambao wakawaweka mbele ya mitume, na walipokwisha kuomba wakaweka mikono yao juu yao.
Actes 1.24 2 Timothée 1.6 Actes 8.17 1 Timothée 4.14 Actes 9.17
7 Neno la Mungu likaenea; na hesabu ya wanafunzi ikazidi sana katika Yerusalemu; jamii kubwa ya makuhani wakaitii ile Imani.
Actes 19.20 Actes 12.24 Colossiens 1.6 Romains 1.5 2 Chroniques 30.24

Arrestation et exécution d’Étienne

8 Na Stefano, akijaa neema na uwezo, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa katika watu.
1 Timothée 3.13 Actes 6.5 Actes 8.6 Actes 6.10 Actes 4.29-4.30
9 Lakini baadhi ya watu wa sinagogi lililoitwa sinagogi la Mahuru, na la Wakirene, na la Waiskanderia, na la wale wa Kilikia na Asia, wakaondoka na kujadiliana na Stefano;
Actes 23.34 Actes 15.23 Actes 15.41 Actes 22.3 Actes 19.10
10 lakini hawakuweza kushindana na hiyo hekima na huyo Roho aliyesema naye.
Luc 21.15 Esaïe 54.17 Job 32.18 Job 32.8 Jérémie 15.20
11 Hata wakashawishi watu waliosema, Tumemsikia mtu huyu akinena maneno ya kumtukana Musa na Mungu.
Matthieu 26.59-26.60 Jean 10.33-10.36 Actes 25.7 1 Timothée 1.13 Jean 9.29
12 Wakawataharakisha watu na wazee na waandishi, wakamwendea, wakamkamata, wakampeleka mbele ya baraza.
Proverbes 15.18 Actes 14.2 Actes 13.50 Actes 5.18 Actes 21.27
13 Wakasimamisha mashahidi wa uongo waliosema, Mtu huyu haachi kusema maneno ya kufuru juu ya mahali hapa patakatifu na juu ya torati;
Actes 21.28 Actes 6.11 Psaumes 56.5 Actes 7.58 Actes 25.8
14 maana tumemsikia akisema kwamba Yesu huyo Mnazareti atapaharibu mahali hapa, na kuzibadili desturi tulizopewa na Musa.
Actes 21.21 Daniel 9.26 Actes 15.1 Galates 3.23 Jérémie 7.4-7.14
15 Watu wote walioketi katika ile baraza wakamkazia macho yao, wakamwona uso wake kuwa kama uso wa malaika.
Ecclésiaste 8.1 2 Corinthiens 3.7-3.8 Matthieu 17.2 Exode 34.29-34.35 Matthieu 5.22

Cette Bible est dans le domaine public.