Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 18.14
Bible en Swahili de l’est


Mort et résurrection de Jésus

Arrestation de Jésus

1 Alipokwisha kusema hayo, Yesu alitoka pamoja na wanafunzi wake kwenda ng’ambo ya kijito Kedroni, palipokuwapo bustani; akaingia yeye na wanafunzi wake.
Matthieu 26.36 Marc 14.32 2 Samuel 15.23 Luc 22.39-22.40 Jean 18.26
2 Naye Yuda, yule aliyetaka kumsaliti, alipajua mahali pale; kwa sababu Yesu alikuwa akienda huko mara nyingi pamoja na wanafunzi wake.
Luc 22.39 Luc 21.37 Marc 11.11-11.12
3 Basi Yuda, akiisha kupokea kikosi cha askari na watumishi waliotoka kwa wakuu wa makuhani na Mafarisayo, akaenda huko na taa na mienge na silaha.
Jean 18.12 Luc 22.47-22.53 Actes 1.16 Marc 14.43-14.50 Psaumes 22.12
4 Basi Yesu, hali akijua yote yatakayompata, akatokea, akawaambia, Ni nani mnayemtafuta?
Jean 13.1 Jean 18.7 Actes 2.28 Jean 19.28 1 Rois 18.14-18.18
5 Wao wakamjibu, Ni Yesu Mnazareti. Yesu akawaambia, Ni mimi. Yuda naye aliyemsaliti alikuwa amesimama pamoja nao.
Jérémie 8.12 Esaïe 3.9 Matthieu 2.23 Jean 1.46 Jean 19.19
6 Basi alipowaambia, Ni mimi, walirudi nyuma, wakaanguka chini.
Psaumes 70.2-70.3 Actes 4.29-4.30 Psaumes 40.14 Psaumes 27.2 Psaumes 129.5
7 Basi akawauliza tena, Mnamtafuta nani? Wakasema, Yesu Mnazareti.
Jean 18.4
8 Yesu akajibu, Nimekwisha kuwaambieni ya kwamba ni mimi; basi ikiwa mnanitafuta mimi, waacheni hawa waende zao.
Matthieu 26.56 Ephésiens 5.25 Jean 13.1 2 Corinthiens 12.9 Esaïe 53.6
9 Ili litimizwe lile neno alilolisema, Wale ulionipa sikumpoteza hata mmoja wao.
Jean 17.12
10 Basi Simoni Petro alikuwa na upanga, akaufuta, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio la kuume. Na yule mtumwa jina lake ni Malko.
Marc 14.47 Luc 22.33 Jean 18.26 Marc 14.30 Matthieu 26.51-26.54
11 Basi Yesu akamwambia Petro, Rudisha upanga alani mwake; je! Kikombe alichonipa Baba, mimi nisikinywee?
Matthieu 20.22 Matthieu 26.39 Matthieu 26.42 Luc 22.42 Psaumes 75.8

Jésus devant les autorités juives

12 Basi wale askari na yule jemadari na wale watumishi wa Wayahudi walimkamata Yesu, wakamfunga.
Jean 18.3 Matthieu 26.57 Marc 15.1 Matthieu 27.2 Luc 22.54
13 Wakamchukua kwa Anasi kwanza; maana alikuwa mkwewe Kayafa, yule aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule.
Jean 18.24 Luc 3.2 Matthieu 26.3 Actes 4.6 Matthieu 26.57
14 Naye Kayafa ndiye yule aliyewapa Wayahudi lile shauri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu.
Jean 11.49-11.52
15 Wakamfuata Yesu, Petro na mwanafunzi mwingine. Na mwanafunzi huyo alikuwa amejulikana na Kuhani Mkuu, akaingia pamoja na Yesu katika behewa ya Kuhani Mkuu.
Luc 22.54 Marc 14.54 Matthieu 26.58-26.68 Matthieu 26.3
16 Lakini Petro akasimama nje mlangoni. Basi yule mwanafunzi mwingine aliyejulikana na Kuhani Mkuu akatoka, akasema na mngoja mlango, akamleta Petro ndani.
Matthieu 26.69 Marc 14.66-14.68 Luc 22.55-22.57
17 Basi yule kijakazi, aliyekuwa mngoja mlango, akamwambia Petro, Wewe nawe, je! Hu mwanafunzi mmojawapo wa mtu huyu? Naye akasema, Si mimi.
Jean 18.25 Luc 22.56-22.57 Luc 22.54 Marc 14.66-14.68 Matthieu 26.33
18 Na wale watumwa na watumishi walikuwa wakisimama, wamefanya moto wa makaa; maana ilikuwa baridi; wakawa wakikota moto. Petro naye alikuwapo pamoja nao, anakota moto.
Marc 14.54 Jean 18.25 Luc 22.44 Ephésiens 5.11-5.12 Marc 14.67
19 Basi Kuhani Mkuu akamwuliza Yesu habari za wanafunzi wake, na habari za mafundisho yake.
Marc 14.55-14.65 Luc 22.63-22.71 Luc 20.20 Matthieu 26.59-26.68 Luc 11.53-11.54
20 Yesu akamjibu, Mimi nimesema na ulimwengu waziwazi; sikuzote nalifundisha katika sinagogi na katika hekalu, wakusanyikapo Wayahudi wote; wala kwa siri mimi sikusema neno lo lote.
Jean 7.26 Esaïe 48.16 Matthieu 4.23 Esaïe 45.19 Jean 7.4
21 Ya nini kuniuliza mimi? Waulize wale waliosikia ni nini niliyowaambia; wao wanajua niliyoyanena.
Matthieu 26.59-26.60 Actes 24.18-24.20 Actes 24.12-24.13 Marc 14.55-14.59 Luc 22.67
22 Basi aliposema hayo, mtumishi mmojawapo aliyesimama karibu alimpiga Yesu kofi akisema, Wamjibu hivi Kuhani Mkuu?
Luc 22.63-22.64 Jean 18.3 Job 16.10 Actes 23.2-23.5 Michée 5.1
23 Yesu akamjibu, Kama nimesema vibaya, ushuhudie ule ubaya; bali kama nimesema vema, wanipigia nini?
Actes 23.2-23.5 2 Corinthiens 10.1 Matthieu 5.39 1 Pierre 2.20-2.23
24 Basi Anasi akampeleka hali amefungwa kwa Kayafa, Kuhani Mkuu.
Jean 18.13 Matthieu 26.57
25 Na Simoni Petro alikuwa akisimama huko, anakota moto. Basi wakamwambia, Wewe nawe, je! Hu mwanafunzi wake mmojawapo? Naye akakana, akasema, Si mimi.
Matthieu 26.69 Luc 22.56 Genèse 18.15 Proverbes 29.25 Marc 14.67-14.72
26 Mtumwa mmojawapo wa Kuhani Mkuu, naye ni jamaa yake yule aliyekatwa sikio na Petro, akasema, Je! Mimi sikukuona wewe bustanini pamoja naye?
Jean 18.1 Jean 18.10 Proverbes 12.19 Marc 14.70-14.71 Matthieu 26.73
27 Basi Petro akakana tena, na mara akawika jimbi.
Jean 13.38 Marc 14.71-14.72 Luc 22.60-22.62 Matthieu 26.34 Marc 14.68

Jésus devant les autorités romaines

28 Kisha wakamchukua Yesu kutoka kwa Kayafa mpaka Praitorio, nayo ikawa alfajiri;lakini wao wenyewe hawakuingia ndani ya ile praitorio,wasije wakanajisika,bali wapate kuila Pasaka.
Jean 18.33 Jean 19.9 Matthieu 27.27 Actes 11.3 Marc 15.1-15.5
29 Basi Pilato akawatokea nje, akasema, Ni mashitaka gani mnayoleta juu ya mtu huyu?
Actes 23.28-23.30 Marc 15.2-15.5 Matthieu 27.11-27.14 Actes 25.16 Matthieu 27.23
30 Wakajibu, wakamwambia, Kama huyu asingekuwa mtenda mabaya, tusingemleta kwako.
Luc 24.7 Jean 19.12 Marc 10.33 Marc 15.3 Actes 3.13
31 Basi Pilato akawaambia, Haya! Mtwaeni ninyi, mkamhukumu kwa ile torati yenu! Wayahudi wakamwambia, Sisi hatuna ruhusa ya kuua mtu.
Ezéchiel 21.26-21.27 Actes 25.18-25.20 Jean 19.15 Genèse 49.10 Jean 19.6-19.7
32 Ili litimie lile neno lake Yesu alilolisema, akionyesha ni mauti gani atakayokufa.
Matthieu 26.2 Matthieu 20.19 Jean 3.14 Jean 12.32-12.33 Luc 18.32-18.33
33 Basi Pilato akaingia tena ndani ya Praitorio, akamwita Yesu, akamwambia, Je! Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?
Jean 19.9 Marc 15.2 1 Timothée 6.13 Zacharie 9.9 Psaumes 2.6-2.12
34 Yesu akamjibu, Wewe wasema hivi kwa nafsi yako, au watu wengine walikuambia habari zangu?
35 Pilato akajibu, Ama! Ni Myahudi mimi! Taifa lako na wakuu wa makuhani ndio waliokuleta kwangu. Umefanya nini?
Actes 18.14-18.16 Actes 25.19-25.20 Jean 18.28 Actes 21.38 Jean 19.11
36 Yesu akajibu, Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wangenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi. Lakini ufalme wangu sio wa hapa.
Jean 6.15 Luc 17.20-17.21 Colossiens 1.12-1.14 Romains 14.17 Daniel 2.44
37 Basi Pilato akamwambia, Wewe u mfalme basi? Yesu akajibu, Wewe wasema, kwa kuwa mimi ni mfalme. Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya mimi nalikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Kila aliye wa hiyo kweli hunisikia sauti yangu.
1 Jean 4.6 Jean 8.14 Jean 8.47 1 Jean 3.19 Esaïe 55.4
38 Pilato akamwambia, Kweli ni nini? Naye akiisha kusema neno hilo akawatokea Wayahudi tena, akawaambia, Mimi sioni hatia yo yote kwake.
Jean 19.4 Luc 23.4 Jean 19.6 Luc 23.14-23.16 Actes 17.19-17.20
39 Lakini kwenu kuna desturi ya mimi kuwafungulia mtu mmoja wakati wa Pasaka; basi, mwapenda niwafungulie Mfalme wa Wayahudi?
Matthieu 27.15-27.18 Matthieu 27.20-27.23 Marc 15.6-15.14 Luc 23.16-23.23
40 Basi wakapiga kelele tena kusema, Si huyu, bali Baraba. Naye yule Baraba alikuwa mnyang’anyi.
Marc 15.7 Matthieu 27.16 Marc 15.15 Matthieu 27.26 Luc 23.18-23.19

Cette Bible est dans le domaine public.