Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 2.4
Bible en Swahili de l’est


Guérison d’un paralysé

1 Akaingia Kapernaumu tena, baada ya siku kadha wa kadha, ikasikiwa ya kwamba yumo nyumbani.
Matthieu 9.1 Luc 18.35-18.38 Jean 4.47 Marc 7.24 Luc 5.18
2 Wakakusanyika watu wengi, isibaki nafasi hata mlangoni; akawa akisema nao neno lake.
Marc 2.13 Marc 1.45 Marc 4.1-4.2 Matthieu 5.2 Actes 16.6
3 Wakaja watu wakimletea mtu mwenye kupooza, anachukuliwa na watu wanne.
Luc 5.18-5.26 Matthieu 4.24 Matthieu 9.1-9.8
4 Na walipokuwa hawawezi kumkaribia kwa sababu ya makutano, waliitoboa dari pale alipokuwapo; na wakiisha kuivunja wakalitelemsha godoro alilolilalia yule mwenye kupooza.
Luc 5.19 Deutéronome 22.8
5 Naye Yesu, alipoiona imani yao, akamwambia yule mwenye kupooza, Mwanangu, umesamehewa dhambi zako.
Matthieu 9.2 Jacques 5.15 Matthieu 9.22 Jean 5.14 Luc 5.20
6 Na baadhi ya waandishi walikuwako huko, wameketi, wakifikiri mioyoni mwao,
Luc 5.21-5.22 Marc 8.17 Matthieu 16.7-16.8 2 Corinthiens 10.5
7 Mbona huyu anasema hivi? Anakufuru. Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye Mungu?
Esaïe 43.25 Luc 7.49 Jean 20.20-20.23 Marc 14.64 Psaumes 130.4
8 Mara Yesu akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao, akawaambia, Mbona mnafikiri hivi mioyoni mwenu?
Actes 8.22 Jean 6.64 Marc 7.21 Hébreux 4.13 Ezéchiel 38.10
9 Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende?
Matthieu 9.5 Luc 5.22-5.25
10 Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (hapo amwambia yule mwenye kupooza),
Daniel 7.13-7.14 Actes 5.31 Matthieu 9.6-9.8 Jean 5.20-5.27 1 Timothée 1.13-1.16
11 Nakuambia, Ondoka, ujitwike godoro lako uende nyumbani kwako.
Jean 6.63 Jean 5.8-5.10 Marc 1.41
12 Mara akaondoka, akajitwika godoro lake, akatoka mbele yao wote; hata wakastaajabu wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, Namna hii hatujapata kuiona kamwe.
Matthieu 9.33 Matthieu 9.8 Luc 7.16 Marc 1.27 Luc 5.26

Réactions face à Jésus

13 Akatoka tena, akaenda kando ya bahari, mkutano wote ukamwendea, akawafundisha.
Marc 1.45 Marc 3.7-3.8 Proverbes 1.20-1.22 Matthieu 13.1 Marc 3.20-3.21
14 Hata alipokuwa akipita, akamwona Lawi wa Alfayo, ameketi forodhani, akamwambia, Nifuate. Akaondoka akamfuata.
Marc 3.18 Luc 5.27-5.32 Luc 6.15 Matthieu 4.19-4.22 Matthieu 9.9-9.13
15 Hata alipokuwa ameketi chakulani nyumbani mwake, watoza ushuru wengi na wenye dhambi waliketi pamoja na Yesu na wanafunzi wake; kwa maana walikuwa wengi wakimfuata.
Luc 15.1 Matthieu 9.10-9.11 Matthieu 21.31-21.32 Luc 5.29-5.30 Luc 6.17
16 Na waandishi na Mafarisayo walipomwona anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi, waliwaambia wanafunzi wake, Mbona anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?
Luc 19.7 Esaïe 65.5 Actes 23.9 Luc 18.11 1 Corinthiens 2.15
17 Yesu aliposikia aliwaambia, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio hawawezi; sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.
Luc 5.31-5.32 Matthieu 9.12-9.13 Luc 19.10 1 Timothée 1.15-1.16 Luc 15.7
18 Nao wanafunzi wake Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga; basi walikuja, wakamwambia, Kwani wanafunzi wa Yohana na wanafunzi wa Mafarisayo hufunga, bali wanafunzi wako hawafungi?
Luc 18.12 Matthieu 6.16 Matthieu 6.18 Matthieu 9.14-9.17 Matthieu 23.5
19 Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kufunga maadamu bwana-arusi yupo pamoja nao? Muda wote walipo na bwana-arusi pamoja nao hawawezi kufunga.
Matthieu 25.1-25.10 Juges 14.10-14.11 Genèse 29.22 Cantique 6.8 Psaumes 45.14
20 Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana-arusi, ndipo watakapofunga siku ile.
Esaïe 54.5 Luc 17.22 Apocalypse 19.7 1 Corinthiens 7.5 2 Corinthiens 6.5
21 Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu; ikiwa ashona, kile kipya kilichotiwa huliharibu lile vazi kuukuu, na pale palipotatuka huzidi.
Matthieu 9.16 Psaumes 103.13-103.15 1 Corinthiens 10.13 Esaïe 57.16
22 Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu; ikiwa atia, ile divai mpya itavipasua viriba vile, divai ikamwagika, vile viriba vikaharibika. Bali hutia divai mpya katika viriba vipya.
Matthieu 9.17 Luc 5.37-5.38 Josué 9.13 Psaumes 119.83 Job 32.19

Jésus et le sabbat

23 Ikawa alipokuwa akipita mashambani siku ya sabato, wanafunzi wake walianza kuendelea njiani wakivunja masuke.
Luc 6.1-6.5 Matthieu 12.1-12.8 Deutéronome 23.24-23.25
24 Mafarisayo wakamwambia, Tazama, mbona wanafanya lisilokuwa halali siku ya sabato?
Exode 20.10 Matthieu 15.2-15.3 Exode 31.15 Matthieu 7.3-7.5 Matthieu 23.23-23.24
25 Akawaambia, Hamkusoma popote alivyofanya Daudi, alipokuwa ana haja, na kuona njaa, yeye na wenziwe?
1 Samuel 21.3-21.6 Matthieu 21.16 Luc 10.26 Matthieu 19.4 Matthieu 21.42
26 Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu, zamani za kuhani mkuu Abiathari, akaila mikate ile ya Wonyesho, ambayo si halali kuliwa ila na makuhani, akawapa na wenziwe?
2 Samuel 8.17 Lévitique 24.5-24.9 1 Chroniques 24.6 1 Samuel 21.1 1 Samuel 22.20-22.22
27 Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato.
Colossiens 2.16 Deutéronome 5.14 Exode 23.12 Luc 6.9 Ezéchiel 20.12
28 Basi Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato pia.
Apocalypse 1.10 Jean 9.14 Luc 6.5 Jean 5.9-5.11 Jean 9.5-9.11

Cette Bible est dans le domaine public.