Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 16.17
Bible en Swahili de l’est


Résurrection de Jésus

1 Hata sabato ilipokwisha kupita, Mariamu Magdalene na Mariamu mamaye Yakobo, na Salome walinunua manukato wapate kwenda kumpaka.
Marc 15.40 Jean 19.25 Marc 15.47 Jean 19.31 Marc 14.3
2 Hata alfajiri mapema, siku ya kwanza ya juma, wakaenda kaburini, jua lilipoanza kuchomoza;
Jean 20.1 Luc 24.1 Matthieu 28.1
3 wakasemezana wao kwa wao, Ni nani atakayetuvingirishia lile jiwe mlangoni pa kaburi?
Matthieu 27.60-27.66 Marc 15.46-15.47
4 Hata walipotazama, waliona ya kuwa lile jiwe limekwisha kuvingirishwa; nalo lilikuwa kubwa mno.
Jean 20.1 Luc 24.2 Matthieu 28.2-28.4
5 Wakaingia kaburini wakaona kijana ameketi upande wa kuume, amevaa vazi jeupe; wakastaajabu.
Jean 20.11-20.12 Matthieu 28.3 Luc 1.12 Daniel 10.5-10.9 Luc 24.3-24.5
6 Naye akawaambia, Msistaajabu; mnamtafuta Yesu Mnazareti, aliyesulibiwa; amefufuka; hayupo hapa; patazameni mahali walipomweka.
Matthieu 28.4-28.7 Proverbes 8.17 Actes 10.38-10.40 Apocalypse 1.17-1.18 Matthieu 14.26-14.27
7 Lakini enendeni zenu, mkawaambie wanafunzi wake, na Petro, ya kwamba awatangulia kwenda Galilaya; huko mtamwona, kama alivyowaambia.
Marc 14.28 Matthieu 26.32 Matthieu 28.7 Matthieu 28.10 Matthieu 28.16-28.17
8 Wakatoka nje, wakakimbia kutoka kaburini; kwa maana wameingia tetemeko na ushangao; wala hawakumwambia mtu neno, maana waliogopa. [
2 Rois 4.29 Luc 24.22-24.24 Luc 10.4 Matthieu 28.8 Marc 16.5-16.6

Apparitions de Jésus ressuscité

9 Naye alipofufuka alfajiri siku ya kwanza ya juma, alimtokea kwanza Mariamu Magdalene, ambaye kwamba alimtoa pepo saba.
Jean 20.14-20.19 Actes 20.7 Marc 15.40 1 Corinthiens 16.2 Luc 8.2
10 Huyo akashika njia akawapasha habari wale waliokuwa pamoja naye, nao wakali wanaomboleza na kulia.
Marc 14.72 Matthieu 24.30 Matthieu 9.15 Luc 24.17 Jean 20.18
11 Walakini hao waliposikia kama yu hai, naye amemwona, hawakusadiki.
Luc 24.11 Marc 16.13-16.14 Luc 24.23-24.35 Marc 9.19 Exode 6.9
12 Baada ya hayo akawatokea watu wawili miongoni mwao, ana sura nyingine; nao walikuwa wakishika njia kwenda shamba.
Luc 24.13-24.32 Jean 21.14 Marc 16.14 Jean 21.1
13 Na hao wakaenda zao wakawapa habari wale wengine; wala hao hawakuwasadiki.
Jean 20.25 Luc 24.33-24.35 Jean 20.8 Luc 16.31
14 Baadaye akaonekana na wale kumi na mmoja walipokuwa wakila, akawakemea kwa kutokuamini kwao na ugumu wa mioyo yao, kwa kuwa hawakuwasadiki wale waliomwona alipofufuka katika wafu.
1 Corinthiens 15.5 Luc 24.36-24.43 Matthieu 11.20 Psaumes 95.8-95.11 Hébreux 3.7-3.8
15 Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.
Matthieu 28.19 Marc 13.10 Actes 1.8 Luc 24.47-24.48 Romains 16.26
16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.
Jean 3.36 Romains 10.9-10.14 Jean 3.18-3.19 Actes 2.38 Jean 8.24
17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;
1 Corinthiens 12.30 1 Corinthiens 12.28 1 Corinthiens 12.10 Actes 5.16 Actes 10.46
18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.
Luc 10.19 Jacques 5.14-5.15 Marc 5.23 Actes 4.30 Actes 19.12
19 Basi Bwana Yesu, baada ya kusema nao, akachukuliwa juu mbinguni, akaketi mkono wa kuume wa Mungu.
1 Pierre 3.22 Hébreux 1.3 Hébreux 12.2 Hébreux 8.1 Psaumes 110.1
20 Nao wale wakatoka, wakahubiri kotekote, Bwana akitenda kazi pamoja nao, na kulithibitisha lile neno kwa ishara zilizofuatana nalo.]
Actes 14.3 Hébreux 2.4 Actes 5.12 1 Corinthiens 2.4-2.5 Romains 15.19

Cette Bible est dans le domaine public.