Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 8.28
Bible en Swahili de l’est


Ministère de Jésus en Galilée

Guérison d’un lépreux

1 Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata.
Matthieu 8.18 Matthieu 4.25-5.1 Luc 5.15 Matthieu 15.30 Matthieu 12.15
2 Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.
Matthieu 18.26 Matthieu 15.25 Marc 9.22-9.24 Lévitique 13.44-13.46 Deutéronome 24.8-24.9
3 Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika.
Psaumes 33.9 Luc 5.13 Genèse 1.3 2 Rois 5.14 Marc 7.34
4 Yesu akamwambia, Angalia, usimwambie mtu; ila enenda zako, ukajionyeshe kwa kuhani, ukaitoe sadaka kama alivyoamuru Musa, iwe ushuhuda kwao.
Lévitique 14.2-14.32 Luc 5.14 Marc 7.36 Matthieu 9.30 Marc 5.43

Guérisons à Capernaüm

5 Hata alipoingia Kapernaumu, akida mmoja alimjia,
Luc 7.1-7.10 Matthieu 9.1 Actes 27.13 Matthieu 27.54 Marc 15.39
6 akamsihi, akisema, Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza, anaumwa sana.
Matthieu 4.24 Colossiens 4.1 Philémon 1.16 Actes 9.33 Matthieu 9.2
7 Yesu akamwambia, Nitakuja, nimponye.
Matthieu 9.18-9.19 Marc 5.23-5.24 Luc 7.6
8 Yule akida akamjibu, akasema, Bwana, mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu; lakini sema neno tu, na mtumishi wangu atapona.
Psaumes 107.20 Luc 7.6-7.7 Psaumes 33.9 Matthieu 15.26-15.27 Nombres 20.8
9 Kwa maana mimi nami ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, mwenye askari chini yangu; nikimwambia huyu, Nenda, huenda; na huyu, Njoo, huja; na mtumwa wangu, Fanya hivi, hufanya.
Jérémie 47.6-47.7 Luc 7.8 Tite 2.9 Ezéchiel 14.17-14.21 Luc 4.39
10 Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia wale waliomfuata, Amin, nawaambieni, Sijaona imani kubwa namna hii, kwa ye yote katika Israeli.
Matthieu 15.28 Luc 5.20 Marc 6.6 Luc 7.9 Luc 7.50
11 Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;
Luc 13.28-13.29 Malachie 1.11 Ephésiens 3.6 Michée 4.1-4.2 Ephésiens 2.11-2.14
12 bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Matthieu 13.42 Matthieu 25.30 Luc 13.28 Matthieu 13.50 Matthieu 24.51
13 Naye Yesu akamwambia yule akida, Nenda zako; na iwe kwako kama ulivyoamini. Mtumishi wake akapona saa ile ile.
Matthieu 9.22 Matthieu 8.4 Matthieu 17.20 Jean 4.52-4.53 Matthieu 9.29-9.30
14 Hata Yesu alipofika nyumbani kwa Petro, akamwona mkwe wa Petro, mamaye mkewe, amelala kitandani hawezi homa.
Luc 4.38-4.41 Marc 1.29-1.34 1 Corinthiens 9.5 Matthieu 8.20 Matthieu 17.25
15 Akamgusa mkono, homa ikamwacha; naye akaondoka, akawatumikia.
2 Rois 13.21 Actes 19.11-19.13 Matthieu 14.36 Matthieu 20.34 Matthieu 8.3
16 Hata kulipokuwa jioni, wakamletea wengi wenye pepo; akawatoa pepo kwa neno lake, akawaponya wote waliokuwa hawawezi,
Actes 19.13-19.16 Luc 4.40 Matthieu 12.22 Matthieu 8.33 Marc 9.25
17 ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu.
Esaïe 53.4 1 Pierre 2.24 Matthieu 1.22

Jésus, plus fort que la nature et les démons

18 Naye Yesu alipoona makutano mengi wakimzunguka, aliamuru kuvuka kwenda ng’ambo.
Marc 4.35 Luc 8.22 Jean 6.15 Matthieu 14.22 Marc 1.35-1.38
19 Mwandishi mmoja akamwendea, akamwambia, Mwalimu, nitakufuata ko kote uendako.
Luc 14.25-14.27 Esdras 7.6 Jean 13.36-13.38 Luc 22.33-22.34 1 Corinthiens 1.20
20 Yesu akamwambia, Mbweha wana pango, na ndege wa angani wana viota; lakini Mwana wa Adamu hana pa kulaza kichwa chake.
Psaumes 84.3 Luc 2.16 Luc 2.7 Matthieu 12.40 Matthieu 12.32
21 Mwingine katika wanafunzi wake akamwambia, Bwana, nipe ruhusa kwanza, niende nikamzike baba yangu.
Luc 9.59-9.62 Lévitique 21.11-21.12 Nombres 6.6-6.7 Aggée 1.2 1 Rois 19.20-19.21
22 Lakini Yesu akamwambia, Nifuate; waache wafu wazike wafu wao.
Jean 1.43 Ephésiens 5.14 Ephésiens 2.1 Ephésiens 2.5 Colossiens 2.13
23 Akapanda chomboni, wanafunzi wake wakamfuata.
Luc 8.22-8.25 Marc 4.36-4.41 Matthieu 9.1 Luc 7.22
24 Kukawa msukosuko mkuu baharini, hata chombo kikafunikizwa na mawimbi; naye alikuwa amelala usingizi.
Luc 8.23 Actes 27.14-27.38 Jean 6.17-6.18 Jonas 1.4-1.5 Marc 4.37-4.38
25 Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwamsha, wakisema, Bwana, tuokoe, tunaangamia.
2 Chroniques 14.11 Luc 8.24 Psaumes 44.22-44.23 Jonas 1.6 Marc 4.38-4.39
26 Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga, enyi wa imani haba? Mara akaondoka, akazikemea pepo na bahari; kukawa shwari kuu.
Esaïe 41.10-41.14 Matthieu 6.30 Psaumes 65.7 Matthieu 16.8 Psaumes 89.9
27 Wale watu wakamaka wakisema, Huyu ni mtu wa namna gani hata pepo na bahari zamtii?
Marc 1.27 Matthieu 15.31 Marc 6.51 Marc 7.37 Matthieu 14.33
28 Naye alipofika ng’ambo, katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile.
Actes 10.38 Luc 8.26-8.39 Marc 5.1-5.20 Matthieu 4.24 Juges 5.6
29 Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?
Marc 1.24 Luc 4.34 Jean 2.4 2 Samuel 16.10 Marc 5.7
30 Basi, kulikuwako mbali nao kundi la nguruwe wengi wakilisha.
Marc 5.11 Esaïe 65.3-65.4 Luc 8.32 Esaïe 66.3 Lévitique 11.7
31 Wale pepo wakamsihi, wakisema, Ukitutoa, tuache twende, tukaingie katika lile kundi la nguruwe.
Apocalypse 12.12 Luc 8.30-8.33 Marc 5.7 Marc 5.12 Apocalypse 20.1-20.2
32 Akawaambia, Nendeni. Wakatoka, wakaingia katika nguruwe; na kumbe! Kundi lote wakatelemka kwa kasi gengeni hata baharini, wakafa majini.
1 Rois 22.22 Actes 2.23 Marc 5.13 Apocalypse 20.7 Job 2.3-2.8
33 Lakini wachungaji walikimbia, wakaenda zao mjini, wakazieneza habari zote na habari za wale wenye pepo pia.
Luc 8.34-8.36 Marc 5.14-5.16 Actes 19.15-19.17
34 Na tazama, mji wote ukatoka kwenda kumlaki Yesu; nao walipomwona, walimsihi aondoke mipakani mwao.
Actes 16.39 Luc 5.8 1 Rois 17.18 Job 22.17 Job 21.14

Cette Bible est dans le domaine public.