Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 8.10
Bible en Swahili de l’est


Ministère de Jésus en Galilée

Guérison d’un lépreux

1 Naye aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata.
Matthieu 8.18 Matthieu 4.25-5.1 Matthieu 19.2 Marc 3.7 Matthieu 20.29
2 Na tazama, akaja mtu mwenye ukoma akamsujudia, akisema, Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa.
Matthieu 18.26 Matthieu 15.25 Deutéronome 24.8-24.9 Luc 5.12-5.14 Apocalypse 22.8-22.9
3 Yesu akanyosha mkono, akamgusa, akisema Nataka; takasika. Na mara ukoma wake ukatakasika.
Luc 5.13 Psaumes 33.9 Genèse 1.3 2 Rois 5.14 Marc 7.34
4 Yesu akamwambia, Angalia, usimwambie mtu; ila enenda zako, ukajionyeshe kwa kuhani, ukaitoe sadaka kama alivyoamuru Musa, iwe ushuhuda kwao.
Lévitique 14.2-14.32 Matthieu 9.30 Luc 5.14 Marc 7.36 Luc 17.14

Guérisons à Capernaüm

5 Hata alipoingia Kapernaumu, akida mmoja alimjia,
Luc 7.1-7.10 Matthieu 9.1 Actes 23.17 Matthieu 4.13 Actes 27.31
6 akamsihi, akisema, Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani, mgonjwa wa kupooza, anaumwa sana.
Matthieu 4.24 Job 31.13-31.14 Colossiens 3.11 Actes 10.7 Marc 2.3-2.12
7 Yesu akamwambia, Nitakuja, nimponye.
Matthieu 9.18-9.19 Marc 5.23-5.24 Luc 7.6
8 Yule akida akamjibu, akasema, Bwana, mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu; lakini sema neno tu, na mtumishi wangu atapona.
Psaumes 107.20 Luc 7.6-7.7 Luc 15.21 Jean 1.27 Jean 13.6-13.8
9 Kwa maana mimi nami ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, mwenye askari chini yangu; nikimwambia huyu, Nenda, huenda; na huyu, Njoo, huja; na mtumwa wangu, Fanya hivi, hufanya.
Luc 4.39 Psaumes 119.91 Luc 4.35-4.36 Ephésiens 6.5-6.6 Colossiens 3.22
10 Yesu aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia wale waliomfuata, Amin, nawaambieni, Sijaona imani kubwa namna hii, kwa ye yote katika Israeli.
Matthieu 15.28 Luc 5.20 Marc 6.6 Luc 7.9 Luc 7.50
11 Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;
Luc 13.28-13.29 Malachie 1.11 Michée 4.1-4.2 Ephésiens 2.11-2.14 Esaïe 2.2-2.3
12 bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Matthieu 13.42 Matthieu 25.30 Luc 13.28 Matthieu 13.50 Matthieu 24.51
13 Naye Yesu akamwambia yule akida, Nenda zako; na iwe kwako kama ulivyoamini. Mtumishi wake akapona saa ile ile.
Matthieu 9.22 Ecclésiaste 9.7 Marc 7.29 Marc 9.23 Jean 4.50
14 Hata Yesu alipofika nyumbani kwa Petro, akamwona mkwe wa Petro, mamaye mkewe, amelala kitandani hawezi homa.
Luc 4.38-4.41 Marc 1.29-1.34 1 Corinthiens 9.5 Hébreux 13.4 Matthieu 8.20
15 Akamgusa mkono, homa ikamwacha; naye akaondoka, akawatumikia.
2 Rois 13.21 Actes 19.11-19.13 Matthieu 9.29 Matthieu 9.20 Marc 1.41
16 Hata kulipokuwa jioni, wakamletea wengi wenye pepo; akawatoa pepo kwa neno lake, akawaponya wote waliokuwa hawawezi,
Actes 19.13-19.16 Luc 4.40 Marc 1.32-1.34 Marc 5.8 Matthieu 14.14
17 ili litimie lile neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu.
Esaïe 53.4 1 Pierre 2.24 Matthieu 1.22

Jésus, plus fort que la nature et les démons

18 Naye Yesu alipoona makutano mengi wakimzunguka, aliamuru kuvuka kwenda ng’ambo.
Marc 4.35 Luc 8.22 Matthieu 14.22 Jean 6.15 Marc 8.13
19 Mwandishi mmoja akamwendea, akamwambia, Mwalimu, nitakufuata ko kote uendako.
Luc 22.33-22.34 1 Corinthiens 1.20 Luc 9.57-9.60 Marc 12.32-12.34 Luc 14.25-14.27
20 Yesu akamwambia, Mbweha wana pango, na ndege wa angani wana viota; lakini Mwana wa Adamu hana pa kulaza kichwa chake.
Psaumes 84.3 Matthieu 12.40 Luc 2.16 Luc 2.7 Matthieu 16.13
21 Mwingine katika wanafunzi wake akamwambia, Bwana, nipe ruhusa kwanza, niende nikamzike baba yangu.
Luc 9.59-9.62 Lévitique 21.11-21.12 Nombres 6.6-6.7 Aggée 1.2 2 Corinthiens 5.16
22 Lakini Yesu akamwambia, Nifuate; waache wafu wazike wafu wao.
Jean 1.43 Ephésiens 5.14 Colossiens 2.13 Luc 15.32 Matthieu 9.9
23 Akapanda chomboni, wanafunzi wake wakamfuata.
Luc 8.22-8.25 Marc 4.36-4.41 Matthieu 9.1 Luc 7.22
24 Kukawa msukosuko mkuu baharini, hata chombo kikafunikizwa na mawimbi; naye alikuwa amelala usingizi.
Luc 8.23 Jean 6.17-6.18 Jonas 1.4-1.5 Marc 4.37-4.38 Actes 27.14-27.38
25 Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwamsha, wakisema, Bwana, tuokoe, tunaangamia.
Marc 4.38-4.39 2 Chroniques 20.12 Esaïe 51.9-51.10 Psaumes 10.1 2 Chroniques 14.11
26 Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga, enyi wa imani haba? Mara akaondoka, akazikemea pepo na bahari; kukawa shwari kuu.
Esaïe 41.10-41.14 Matthieu 6.30 Psaumes 65.7 Psaumes 107.28-107.30 Luc 8.24-8.25
27 Wale watu wakamaka wakisema, Huyu ni mtu wa namna gani hata pepo na bahari zamtii?
Marc 1.27 Matthieu 14.33 Matthieu 15.31 Marc 6.51 Marc 7.37
28 Naye alipofika ng’ambo, katika nchi ya Wagerasi, watu wawili wenye pepo walikutana naye, wanatoka makaburini, wakali mno, hata mtu asiweze kuipitia njia ile.
Marc 5.1-5.20 Actes 10.38 Luc 8.26-8.39 Matthieu 4.24 Juges 5.6
29 Na tazama, wakapiga kelele, wakisema, Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?
Marc 1.24 Luc 4.34 2 Samuel 16.10 Marc 5.7 Jean 2.4
30 Basi, kulikuwako mbali nao kundi la nguruwe wengi wakilisha.
Esaïe 66.3 Lévitique 11.7 Deutéronome 14.8 Marc 5.11 Esaïe 65.3-65.4
31 Wale pepo wakamsihi, wakisema, Ukitutoa, tuache twende, tukaingie katika lile kundi la nguruwe.
Apocalypse 20.1-20.2 Apocalypse 12.12 Luc 8.30-8.33 Marc 5.7 Marc 5.12
32 Akawaambia, Nendeni. Wakatoka, wakaingia katika nguruwe; na kumbe! Kundi lote wakatelemka kwa kasi gengeni hata baharini, wakafa majini.
Job 2.3-2.8 Job 1.10-1.19 Luc 8.33 Actes 4.28 1 Rois 22.22
33 Lakini wachungaji walikimbia, wakaenda zao mjini, wakazieneza habari zote na habari za wale wenye pepo pia.
Luc 8.34-8.36 Marc 5.14-5.16 Actes 19.15-19.17
34 Na tazama, mji wote ukatoka kwenda kumlaki Yesu; nao walipomwona, walimsihi aondoke mipakani mwao.
Actes 16.39 Luc 5.8 1 Rois 17.18 Luc 8.37-8.39 1 Rois 18.17

Cette Bible est dans le domaine public.