Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 16.13
Bible en Swahili de l’est


La sainteté

Le jour des expiations

1 Bwana akasema na Musa, baada ya kufa kwa hao wana wawili wa Haruni, walipokaribia mbele za Bwana, wakafa;
Lévitique 10.1-10.2
2 Bwana akamwambia Musa, Sema na Haruni ndugu yako, kwamba asiingie wakati wo wote katika mahali patakatifu ndani ya pazia, mbele ya kiti cha rehema, kilicho juu ya sanduku, asije akafa; maana, mimi nitaonekana katika lile wingu juu ya kiti cha rehema.
Exode 30.10 1 Rois 8.10-8.12 Hébreux 9.25 Exode 40.34-40.35 Hébreux 10.19-10.20
3 Haruni ataingia katika patakatifu na vitu hivi; ng’ombe mume mchanga kwa sadaka ya dhambi, na kondoo mume kwa sadaka ya kuteketezwa.
Lévitique 4.3 Hébreux 9.7 Hébreux 9.24-9.25 Lévitique 8.18 Lévitique 1.10
4 Ataivaa ile kanzu takatifu ya kitani, atakuwa na zile suruali za kitani mwilini mwake, atafungwa ule mshipi wa kitani, naye atavaa ile kofia ya kitani; hayo ndiyo mavazi matakatifu, naye ataoga mwili wake majini, na kuyavaa.
Exode 28.39-28.43 Exode 30.20 Ezéchiel 44.17-44.18 Exode 39.27-39.29 Lévitique 8.6-8.7
5 Kisha atatwaa mikononi mwa mkutano wa Waisraeli mbuzi waume wawili, kwa sadaka ya dhambi; na kondoo mume kwa sadaka ya kuteketezwa.
2 Chroniques 29.21 Esdras 6.17 Nombres 29.11 Hébreux 7.27-7.28 Romains 8.3
6 Na Haruni atamtoa yule ng’ombe wa sadaka ya dhambi, aliye kwa ajili ya nafsi yake, na kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, na kwa ajili ya nyumba yake.
Lévitique 9.7 Hébreux 9.7 Hébreux 7.27 Hébreux 5.2-5.3 Job 1.5
7 Kisha atawatwaa wale mbuzi wawili na kuwaweka mbele za Bwana mlangoni pa hema ya kukutania.
Lévitique 1.3 Matthieu 16.21 Romains 12.1 Lévitique 4.4 Lévitique 12.6-12.7
8 Na Haruni atapiga kura juu ya wale mbuzi wawili; kura moja kwa ajili ya Bwana; na kura ya pili kwa ajili ya Azazeli.
Actes 1.23-1.26 Nombres 33.54 Proverbes 16.33 Ezéchiel 48.29 Josué 18.10-18.11
9 Na Haruni atamleta yule mbuzi aliyeangukiwa na kura kwa ajili ya Bwana, na kumtoa awe sadaka ya dhambi.
Actes 2.23 Actes 4.27-4.28
10 Bali yule mbuzi aliyeangukiwa na kura kwa ajili ya Azazeli atawekwa hai mbele za Bwana ili kumfanyia upatanisho, ili kumpeleka jangwani kwa ajili ya Azazeli.
1 Jean 2.2 Romains 3.25 Hébreux 7.26-7.27 Esaïe 53.4-53.11 Romains 4.25
11 Na Haruni atamsongeza ng’ombe wa sadaka ya dhambi, aliye kwa ajili ya nafsi yake, na kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, na kwa ajili ya nyumba yake; naye atamchinja yule ng’ombe wa sadaka ya dhambi, aliye kwa ajili ya nafsi yake.
Lévitique 16.6 Hébreux 7.27 Hébreux 9.7 Lévitique 16.3
12 Kisha atatwaa chetezo kilichojaa makaa ya moto yatokayo katika madhabahu iliyo mbele za Bwana, na konzi mbili za uvumba mzuri uliopondwa sana, mikononi mwake, naye atauleta ndani ya pazia.
Lévitique 10.1 Exode 30.34-30.38 Nombres 16.18 Nombres 16.46 Apocalypse 8.3-8.4
13 Kisha atatia ule uvumba juu ya moto mbele za Bwana, ili moshi wa ule uvumba ukisitiri kiti cha rehema kilicho juu ya ushuhuda, asije akafa.
Exode 25.21 Exode 30.1 Exode 30.7-30.8 Apocalypse 8.3-8.4 Lévitique 22.9
14 Kisha atatwaa baadhi ya damu ya yule ng’ombe, na kuinyunyiza kwa kidole chake juu ya kiti cha rehema upande wa mashariki; na mbele ya kiti cha rehema atainyunyiza ile damu kwa kidole chake mara saba.
Hébreux 9.25 Hébreux 9.13 Lévitique 4.5-4.6 Hébreux 10.4 Hébreux 9.7
15 Kisha atamchinja yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, aliye kwa ajili ya watu, na kuileta damu yake ndani ya pazia, na kwa damu hiyo atafanya vile vile kama alivyofanya kwa damu ya ng’ombe, na kuinyunyiza juu ya kiti cha rehema, na mbele ya kiti cha rehema,
Hébreux 9.7 Hébreux 9.12 Hébreux 9.3 Hébreux 2.17 Hébreux 6.19
16 naye atafanya upatanisho kwa ajili ya mahali patakatifu, kwa sababu ya mambo machafu ya wana wa Israeli, na kwa sababu ya makosa yao, naam, kwa ajili ya dhambi zao zote; naye atafanya vile vile kwa ajili ya hema ya kukutania, ikaayo pamoja nao katikati ya machafu yao.
Exode 29.36-29.37 Lévitique 16.18 Hébreux 9.22-9.23 Lévitique 8.15 Ezéchiel 45.18-45.19
17 Wala hapatakuwa na mtu katika hema ya kukutania, wakati aingiapo ili kufanya upatanisho katika patakatifu, hata atakapotoka nje, baada ya kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, na kwa ajili ya nyumba yake, na kwa ajili ya mkutano wote wa Israeli.
Luc 1.10 1 Pierre 3.18 Daniel 9.24 Hébreux 9.7 1 Pierre 2.24
18 Kisha atatoka na kuiendea madhabahu iliyo mbele za Bwana na kufanya upatanisho kwa ajili yake; atatwaa baadhi ya damu ya yule ng’ombe, na ya damu ya yule mbuzi, na kuitia juu ya pembe za madhabahu pande zote.
Lévitique 4.7 Exode 30.10 Lévitique 4.18 Lévitique 16.16 Hébreux 9.22-9.23
19 Tena atanyunyiza baadhi ya damu juu ya madhabahu kwa kidole chake mara saba, na kuitakasa, ili machafu yote ya wana wa Israeli yaitoke.
Zacharie 13.1 Ezéchiel 43.18-43.22
20 Naye akiisha kufanya upatanisho kwa ajili ya mahali patakatifu, na hema ya kukutania, na madhabahu, atamleta yule mbuzi aliye hai.
Lévitique 16.16 Ezéchiel 45.20 Colossiens 1.20 Hébreux 7.25 2 Corinthiens 5.19
21 Na Haruni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha yule mbuzi aliye hai, na kuungama juu yake uovu wote wa wana wa Israeli, na makosa yao, naam, dhambi zao zote; naye ataziweka juu ya kichwa chake yule mbuzi, kisha atampeleka aende jangwani kwa mkono wa mtu aliye tayari.
2 Corinthiens 5.21 Esaïe 53.6 Psaumes 51.3 Néhémie 1.6-1.7 Lévitique 26.40
22 Na yule mbuzi atachukua juu yake uovu wao wote, mpaka nchi isiyo watu; naye atamwacha mbuzi jangwani.
Jean 1.29 Hébreux 9.28 Esaïe 53.11-53.12 1 Pierre 2.24 Michée 7.19
23 Na Haruni ataingia katika hema ya kukutania, naye atavua mavazi yake ya kitani, aliyoyavaa alipoingia katika patakatifu, atayaacha humo;
Ezéchiel 42.14 Ezéchiel 44.19 Lévitique 16.4 Hébreux 9.28 Philippiens 2.6-2.11
24 naye ataosha mwili wake kwa maji mahali patakatifu, na kuvaa nguo zake, na kutoka, na kusongeza sadaka ya kuteketezwa yake mwenyewe, na sadaka ya kuteketezwa ya watu, naye atafanya upatanisho kwa ajili ya nafsi yake, na kwa ajili ya watu.
Lévitique 16.3-16.5 Hébreux 10.19-10.22 Lévitique 14.9 Lévitique 22.6 Exode 29.4-29.5
25 Na mafuta ya sadaka ya dhambi atayateketeza juu ya madhabahu.
Exode 29.13 Lévitique 4.8-4.10 Lévitique 4.19 Lévitique 16.6
26 Na mtu yule amwachaye mbuzi wa Azazeli aende zake, ataosha nguo zake, na kuosha mwili wake kwa maji, na baadaye ataingia katika marago.
Lévitique 16.10 Lévitique 15.5-15.11 Lévitique 14.8 Lévitique 15.27 Lévitique 16.28
27 Na yule ng’ombe wa sadaka ya dhambi, na yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, ambao damu yao ililetwa ndani ifanye ukumbusho katika patakatifu, watachukuliwa nje ya marago; nao watachoma moto ngozi zao, na nyama yao, na mavi yao.
Lévitique 4.21 Lévitique 6.30 Lévitique 4.11-4.12 Matthieu 27.31-27.33 Hébreux 13.11-13.14
28 Na yeye awachomaye moto atafua nguo zake, na kuosha mwili wake kwa maji, na baadaye ataingia maragoni.
29 Amri hii itakuwa amri ya milele kwenu; katika mwezi wa saba, siku ya kumi ya mwezi, mtajitaabisha roho zenu, msifanye kazi ya namna yo yote, mzalia na mgeni akaaye kati yenu.
Nombres 29.7 Esaïe 58.3 Psaumes 35.13 Lévitique 23.7-23.8 Daniel 10.12
30 Kwa maana siku hiyo upatanisho utafanywa kwa ajili yenu, ili kuwatakasa; nanyi mtatakaswa na dhambi zenu zote mbele za Bwana.
Jérémie 33.8 Ephésiens 5.26 Psaumes 51.2 Hébreux 10.1-10.2 Psaumes 51.10
31 Ni Sabato ya raha ya makini kwenu nanyi mtajitaabisha roho zenu; ni amri ya milele.
Lévitique 23.32 Esaïe 58.5 Lévitique 25.4 Esaïe 58.3 Exode 35.2
32 Na kuhani atakayetiwa mafuta na kuwekwa wakfu badala ya baba yake, ataufanya huo upatanisho, naye atayavaa mavazi ya kitani, yaani, yale mavazi matakatifu.
Lévitique 16.4 Exode 29.29-29.30 Lévitique 4.5 Nombres 20.26-20.28 Lévitique 4.16
33 Naye atafanya upatanisho kwa ajili ya patakatifu, naye atafanya upatanisho kwa ajili ya hema ya kukutania, na kwa ajili ya madhabahu; naye atafanya upatanisho kwa ajili ya makuhani, na kwa ajili ya watu wote wa kusanyiko.
Lévitique 16.16 Lévitique 16.24 Lévitique 16.6 Lévitique 16.18-16.19 Lévitique 16.11
34 Na amri hii itakuwa amri ya milele kwenu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya wana wa Israeli kwa sababu ya dhambi zao zote, mara moja kila mwaka. Naye akafanya vile vile kama Bwana alivyomwamuru Musa.
Hébreux 9.7 Hébreux 9.25 Exode 30.10 Hébreux 10.14 Lévitique 23.31

Cette Bible est dans le domaine public.