Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 12.9
Bible en Swahili de l’est


Jugement du roi et dispersion d’Israël

1 Neno la Bwana likanijia tena, kusema,
2 Mwanadamu, wewe unakaa kati ya nyumba iliyoasi, watu ambao wana macho ya kuona, ila hawaoni, wana masikio ya kusikia, ila hawasikii; kwa maana ni nyumba iliyoasi.
Esaïe 6.9-6.10 Jean 9.39-9.41 Luc 8.10 Ezéchiel 2.3 Ezéchiel 2.5-2.8
3 Basi, mwanadamu, funga tayari vyombo kwa uhamisho, ukahame wakati wa mchana mbele ya macho yao; nawe utahama toka mahali pako hapa mpaka mahali pengine mbele ya macho yao; labda watafahamu, wajapokuwa ni nyumba iliyoasi.
Jérémie 36.3 2 Timothée 2.25 Jérémie 26.3 Luc 20.13 Jérémie 36.7
4 Nawe utatoa vyombo vyako, wakati wa mchana, mbele ya macho yao, kana kwamba ni vyombo vya kuhamishwa; nawe mwenyewe utatoka, wakati wa jioni, mbele ya macho yao, kama watu watokavyo katika kuhamishwa.
Jérémie 39.4 Ezéchiel 12.12 2 Rois 25.4 Jérémie 52.7
5 Toboa mahali ukutani mbele ya macho yao, ukachukue vitu kwa kuvipitisha pale.
Jérémie 39.2-39.4 2 Rois 25.4
6 Mbele ya macho yao utajitwika begani pako, na kuvichukua nje gizani; utafunika uso wako, hata usiione nchi; kwa maana nimekuweka uwe ishara kwa nyumba ya Israeli.
Ezéchiel 4.3 Ezéchiel 24.24 Esaïe 8.18 1 Samuel 28.8 Ezéchiel 12.11-12.12
7 Nikafanya vile vile kama nilivyoamriwa; nalitoa vyombo vyangu wakati wa mchana kana kwamba ni vyombo vya kuhamishwa, na wakati wa jioni nikautoboa ukuta kwa mkono wangu; nikavitoa gizani, nikavichukua begani, mbele ya macho yao.
Ezéchiel 24.18 Ezéchiel 37.7 Ezéchiel 37.10 Actes 26.19 Jérémie 32.8-32.12
8 Asubuhi neno la Bwana likanijia, kusema,
9 Mwanadamu, nyumba ya Israeli, je! Nyumba ile iliyoasi, hawakukuambia, Unafanya nini wewe?
Ezéchiel 17.12 Ezéchiel 24.19 Ezéchiel 20.49 Ezéchiel 2.5-2.8 Ezéchiel 12.1-12.3
10 Waambie, Bwana MUNGU asema hivi; Ufunuo huu wamhusu mkuu wa Yerusalemu, na nyumba yote ya Israeli walio kati yao.
Esaïe 13.1 2 Rois 9.25 Jérémie 21.7 Malachie 1.1 Jérémie 38.18
11 Sema, Mimi ni ishara kwenu; kama mimi nilivyotenda, wao nao watatendwa vile vile; watahamishwa, watakwenda kufungwa.
Jérémie 15.2 Jérémie 52.15 Jérémie 52.28-52.30 Ezéchiel 12.6
12 Naye mkuu aliye kati yao atachukua begani katika giza; naye atatoka kwenda zake; watatoboa mahali ukutani, wapate kuvichukua vyombo vyao nje; atafunika uso wake, kwa sababu hataiona nchi kwa macho yake.
2 Rois 25.4 Ezéchiel 12.6 Jérémie 39.4 Jérémie 52.7 Jérémie 42.7
13 Tena wavu wangu nitautandika juu yake, naye atanaswa kwa mtego wangu; nami nitampeleka Babeli, mpaka nchi ya Wakaldayo; lakini hataiona, angawa atakufa huko.
Ezéchiel 17.20 Osée 7.12 Esaïe 24.17-24.18 Jérémie 39.7 Ezéchiel 17.16
14 Nami nitawatawanya kwa pepo zote wote wamzungukao ili wamsaidie, na vikosi vyake vyote; nami nitaufuta upanga nyuma yao.
Ezéchiel 5.2 Ezéchiel 17.21 2 Rois 25.4-25.5 Ezéchiel 14.17 Jérémie 42.16
15 Nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana; nitakapowatawanya kati ya mataifa, na kuwatupa-tupa katika nchi zote.
Ezéchiel 6.7 Ezéchiel 12.16 Ezéchiel 6.14 Ezéchiel 12.20 Ezéchiel 7.4
16 Lakini nitawasaza watu wachache miongoni mwao na kuwaokoa na upanga, na njaa, na tauni ili watangaze habari ya machukizo yao yote, kati ya mataifa huko waendako; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Jérémie 22.8-22.9 Ezéchiel 14.22-14.23 Ezéchiel 6.8-6.10 Esaïe 24.13 Matthieu 7.14
17 Tena neno la Bwana likanijia, kusema,
18 Mwanadamu, ule chakula chako kwa matetemo, ukanywe maji yako kwa kutetemeka na kwa kuyatunza sana;
Lévitique 26.26 Psaumes 102.4-102.9 Job 3.24 Ezéchiel 4.16-4.17 Lévitique 26.36
19 ukawaambie watu wa nchi, Bwana MUNGU asema hivi, katika habari zao wakaao Yerusalemu, na katika nchi ya Israeli; Watakula chakula chao kwa kukitunza sana, na maji yao watayanywa kwa ushangao, nchi yao iwe ukiwa, kwa kukosa vitu vyote viijazavyo, kwa sababu ya udhalimu wao wote wakaao ndani yake.
Zacharie 7.14 Michée 7.13 Ezéchiel 6.14 Ezéchiel 6.6-6.7 Jérémie 10.22
20 Na miji yote yenye watu itakuwa maganjo, nayo nchi itakuwa ukiwa; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Esaïe 7.23-7.24 Jérémie 4.7 Esaïe 3.26 Jérémie 25.9 Jérémie 19.11
21 Neno la Bwana likanijia, kusema,
22 Mwanadamu, ni mithali gani hii mliyo nayo katika nchi ya Israeli, mkisema, Siku hizo zinakawia na maono yote hayatimizwi.
Ezéchiel 11.3 Ezéchiel 12.27 Ezéchiel 18.2-18.3 Amos 6.3 Jérémie 23.33-23.40
23 Basi uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Nitaikomesha mithali hii, wasiitumie tena kama mithali katika Israeli; lakini uwaambie, Siku hizo ni karibu, na utimilizo wa maono yote.
Sophonie 1.14 Joël 2.1 Esaïe 28.22 Ezéchiel 12.25 Ezéchiel 18.3
24 Kwa maana hayatakuwapo tena maono yo yote ya ubatili, wala ubashiri wa kujipendekeza, katika nyumba ya Israeli.
Ezéchiel 13.23 Zacharie 13.2-13.4 Jérémie 14.13-14.16 1 Thessaloniciens 2.5 Jérémie 23.14-23.29
25 Maana mimi ni Bwana; mimi nitanena, na neno lile nitakalolinena litatimizwa; wala halitakawilishwa tena; maana katika siku zenu, Ewe nyumba iliyoasi, nitalinena neno hilo na kulitimiza, asema Bwana MUNGU.
Ezéchiel 12.28 Esaïe 55.11 Habakuk 1.5 Esaïe 14.24 Jérémie 16.9
26 Neno la Bwana likanijia tena, kusema,
27 Mwanadamu, tazama, hao wa nyumba ya Israeli husema, Maono hayo ayaonayo ni ya siku nyingi zijazo, naye anatabiri habari ya nyakati zilizo mbali sana.
Daniel 10.14 Ezéchiel 12.22 2 Pierre 3.4 Esaïe 28.14-28.15
28 Basi uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Maneno yangu hayatakawilishwa tena hata moja, bali neno nitakalolinena litatimizwa, asema Bwana MUNGU.
Matthieu 24.48-24.51 Ezéchiel 12.23-12.25 Luc 21.34-21.36 Jérémie 44.28 Apocalypse 3.3

Cette Bible est dans le domaine public.