Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lamentations 5.16
Bible en Swahili de l’est


Après la prise de Jérusalem

1 Ee Bwana, kumbuka yaliyotupata; Utazame na kuiona aibu yetu.
Psaumes 44.13-44.16 Lamentations 3.61 Lamentations 1.20 Psaumes 123.3-123.4 Néhémie 1.3
2 Urithi wetu umegeuka kuwa mali ya wageni; Na nyumba zetu kuwa mali ya makafiri.
Sophonie 1.13 Esaïe 1.7 Psaumes 79.1-79.2 Esaïe 5.17 Esaïe 63.18
3 Tumekuwa yatima waliofiwa na baba; Mama zetu wamekuwa kama wajane.
Jérémie 18.21 Exode 22.24 Osée 14.3 Jérémie 15.8
4 Tumekunywa maji yetu kwa fedha; Kuni zetu twauziwa.
Esaïe 3.1 Ezéchiel 4.9-4.17 Deutéronome 28.48
5 Watufuatiao wa juu ya shingo zetu; Tumechoka tusipate raha yo yote.
Néhémie 9.36-9.37 Lamentations 1.14 Jérémie 27.11-27.12 Jérémie 27.2 Actes 15.10
6 Tumewapa hao Wamisri mkono; Na Waashuri nao, ili tushibe chakula.
Osée 9.3 Osée 12.1 Osée 7.11 Ezéchiel 17.18 Esaïe 57.9
7 Baba zetu walitenda dhambi hata hawako; Na sisi tumeyachukua maovu yao.
Jérémie 16.12 Ezéchiel 18.2 Jérémie 31.29 Exode 20.5 Zacharie 1.5
8 Watumwa wanatutawala; Hakuna mtu wa kutuokoa na mikono yao.
Zacharie 11.6 Néhémie 5.15 Proverbes 30.22 Psaumes 7.2 Job 10.7
9 Twapata chakula kwa kujihatarisha nafsi zetu; Kwa sababu ya upanga wa nyikani.
Jérémie 40.9-40.12 Ezéchiel 12.18-12.19 2 Samuel 23.17 Jérémie 41.18 Jérémie 42.14
10 Ngozi yetu ni nyeusi kama tanuu; Kwa sababu ya hari ya njaa ituteketezayo.
Lamentations 4.8 Job 30.30 Lamentations 3.4 Psaumes 119.83
11 Huwatia jeuri wanawake katika Sayuni; Na mabikira katika miji ya Yuda.
Zacharie 14.2 Esaïe 13.16 Deutéronome 28.30
12 Wakuu hutungikwa kwa mikono yao; Nyuso za wazee hazipewi heshima.
Lamentations 4.16 Esaïe 47.6 Jérémie 39.6-39.7 Jérémie 52.10-52.11 Jérémie 52.25-52.27
13 Vijana huyachukua mawe ya kusagia; Na watoto hujikwaa chini ya kuni.
Juges 16.21 Esaïe 58.6 Néhémie 5.1-5.5 Esaïe 47.2 Exode 2.11
14 Wazee wameacha kwenda langoni; Na vijana kwenda ngomani.
Jérémie 7.34 Jérémie 16.9 Apocalypse 18.22 Job 30.1 Lamentations 1.19
15 Furaha ya mioyo yetu imekoma; Machezo yetu yamegeuka maombolezo.
Amos 8.10 Psaumes 30.11 Jacques 4.9-4.10 Jérémie 25.10 Amos 6.4-6.7
16 Taji ya kichwa chetu imeanguka; Ole wetu! Kwa kuwa tumetenda dhambi.
Psaumes 89.39 Jérémie 13.18 Esaïe 3.9-3.11 Lamentations 1.1 Job 19.9
17 Kwa sababu hiyo mioyo yetu imezimia; Kwa ajili ya hayo macho yetu hayaoni vema.
Esaïe 1.5 Lamentations 2.11 Psaumes 6.7 Job 17.7 Psaumes 31.9
18 Kwa ajili ya mlima Sayuni ulio ukiwa, Mbweha hutembea juu yake.
Michée 3.12 1 Rois 9.7-9.8 Jérémie 9.11 Jérémie 52.13 Psaumes 74.2-74.3
19 Wewe, Bwana, unadumu milele; Kiti chako cha enzi ni tangu kizazi hata kizazi.
Psaumes 102.12 Psaumes 45.6 Psaumes 102.25-102.27 Psaumes 9.7 Psaumes 145.13
20 Mbona watusahau sikuzote; Na kutuacha muda huu mwingi?
Psaumes 13.1 Psaumes 44.24 Psaumes 74.1 Psaumes 89.46 Psaumes 77.7-77.10
21 Ee Bwana, utugeuze kwako, nasi tutageuka; Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale.
Psaumes 80.3 Jérémie 31.18 Psaumes 80.19 Psaumes 80.7 Malachie 3.4
22 Isipokuwa wewe umetukataa kabisa; Nawe una hasira nyingi sana juu yetu.
Psaumes 60.1-60.2 Osée 1.6 Psaumes 44.9 Jérémie 15.1-15.5 Esaïe 64.9

Cette Bible est dans le domaine public.