Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 44.21
Bible en Swahili de l’est


L’Éternel et les idoles

1 Lakini sikia sasa, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na Israeli, niliyekuchagua;
Jérémie 30.10 Esaïe 41.8 Jérémie 46.27-46.28 Esaïe 55.3 Romains 11.5-11.6
2 Bwana, aliyekufanya, na kukuumba toka tumboni, yeye atakayekusaidia, asema hivi; Usiogope, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na wewe, Yeshuruni, niliyekuchagua.
Jérémie 1.5 Esaïe 43.1 Esaïe 44.24 Esaïe 49.1 Esaïe 43.7
3 Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa;
Joël 2.28 Actes 2.17 Esaïe 59.21 Jean 7.37-7.39 Apocalypse 21.6
4 nao watatokea katika manyasi, kama mierebi karibu na mifereji ya maji.
Esaïe 58.11 Psaumes 1.3 Actes 2.41-2.47 Psaumes 137.1-137.2 Job 40.22
5 Mmoja atasema, Mimi ni wa Bwana; na mwingine atajiita kwa jina la Yakobo; na mwingine ataandika juu ya mkono wake, Kwa Bwana, na kujiita kwa jina la Israeli.
Deutéronome 26.17-26.19 Zacharie 13.9 2 Corinthiens 8.5 Zacharie 8.20-8.23 Exode 13.9
6 Bwana, Mfalme wa Israeli, Mkombozi wako, Bwana wa majeshi, asema hivi; Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho; zaidi yangu mimi hapana Mungu.
Esaïe 41.4 Apocalypse 1.8 Esaïe 48.12 Apocalypse 22.13 Esaïe 43.10-43.11
7 Naye ni nani kama mimi atakayeita, na kuyahubiri haya, na kunitengenezea, tangu nilipowaweka watu wa kale? Na mambo yanayokuja na yatakayotokea, wayatangaze.
Esaïe 41.26 Esaïe 41.22 Genèse 17.7-17.8 Actes 17.26 Esaïe 46.9-46.10
8 Msiogope wala msifanye hofu; je! Sikukuhubiri haya zamani na kuyaonyesha? Na ninyi ni mashahidi wangu. Je! Yuko Mungu zaidi yangu mimi? Hakika hapana Mwamba; mimi sijui mwingine.
Esaïe 43.10 Deutéronome 4.35 1 Samuel 2.2 Deutéronome 4.39 Jean 1.1
9 Wachongao sanamu, wote ni ubatili; wala mambo yao yawapendezayo hayatafaa kitu; wala mashahidi wao wenyewe hawaoni, wala hawajui; ili watahayarike.
Esaïe 41.24 Esaïe 41.29 Psaumes 97.7 Daniel 5.23 Jérémie 10.3-10.8
10 Ni nani aliyejichongea mungu mmoja, au aliyesubu sanamu isiyofaa kitu?
Jérémie 10.5 Habakuk 2.18 Actes 19.26 1 Corinthiens 8.4 1 Rois 12.28
11 Tazama, wenziwe wote watatahayari; na mafundi, hao ni wanadamu; na wakusanyike pamoja, wakasimame; wataogopa na kutahayari pamoja.
Esaïe 42.17 Esaïe 45.16 Psaumes 97.7 Esaïe 1.29 1 Samuel 5.3-5.7
12 Mfua chuma hufanza shoka, hufanya kazi kwa makaa, huitengeneza sanamu kwa nyundo, huifanyiza kwa nguvu za mkono wake; naam, huona njaa, nguvu zake zikampungukia; asipokunywa maji huzimia.
Esaïe 40.19 Esaïe 41.6-41.7 Esaïe 46.6-46.7 Habakuk 2.13 Exode 32.8
13 Seremala hunyosha uzi; huiandika kwa kalamu ya mate; huitengeneza kwa randa, huiandika kwa bikari, huifanza kwa mfano wa mwanadamu, sawasawa na uzuri wa mwanadamu, ili ikae nyumbani.
Juges 17.4-17.5 Psaumes 115.5-115.7 Actes 17.29 Genèse 35.2 Genèse 31.19
14 Yeye hujikatia mierezi, hutwaa mtiriza, na mwaloni, hujichagulia mti mmoja katika miti ya msituni; hupanda mvinje, mvua ikausitawisha.
Esaïe 40.20 Jérémie 10.3-10.8 Habakuk 2.19 Osée 4.12
15 Kisha utamfaa mwanadamu kwa kuni; hutwaa kipande, akaota moto; naam, huuwasha moto, akaoka mkate; naam, huufanya mungu, akauabudu; huifanya sanamu ya kuchonga, akaisujudia.
2 Chroniques 25.14 Apocalypse 9.20 Esaïe 44.10 Esaïe 45.20 Juges 2.19
16 Sehemu moja huiteketeza; kwa sehemu nyingine hula nyama; huoka chakula kiokwacho, akashiba; naam, huota moto, akasema, Aha, nimeota moto, nimeona moto;
17 na kwa sehemu iliyobakia hufanya mungu, yaani, sanamu yake ya kuchonga; husujudu mbele yake akaiabudu, akaiomba, akasema, Uniokoe; maana wewe u mungu wangu.
Esaïe 45.20 Esaïe 36.19-36.20 1 Rois 18.26 Daniel 6.16 Daniel 6.27
18 Hawajui wala hawafikiri; maana amewafumba macho, wasione, na mioyo yao, wasiweze kufahamu.
2 Corinthiens 4.3-4.4 Psaumes 81.12 Esaïe 6.9-6.10 Esaïe 29.10 Jérémie 5.21
19 Wala hapana atiaye moyoni, wala hapana maarifa, wala fahamu kusema, Nimeteketeza sehemu motoni, naam, pia nimeoka mkate juu ya makaa yake; nimeoka nyama nikaila; nami, je! Kilichobaki nikifanye kuwa chukizo? Je! Nisujudie shina la mti?
Deutéronome 27.15 1 Rois 11.7 2 Rois 23.13 1 Rois 11.5 Esaïe 5.13
20 Hula majivu; moyo uliodanganyika umempotosha, asiweze kuiokoa nafsi yake, wala kusema, Je! Sio uongo mkononi mwangu?
Job 15.31 Psaumes 102.9 Osée 4.12 Romains 1.25 Osée 12.1

Retour d’Israël chez lui

21 Kumbuka haya, Ee Yakobo; nawe Israeli, maana wewe u mtumishi wangu; nimekuumba; u mtumishi wangu; Ee Israeli, hutasahauliwa na mimi.
Esaïe 44.1-44.2 Esaïe 43.15 Deutéronome 4.9 Esaïe 43.7 Deutéronome 32.18
22 Nimeyafuta makosa yako kama wingu zito, na dhambi zako kama wingu; unirudie; maana nimekukomboa.
Esaïe 43.25 1 Corinthiens 6.20 Esaïe 43.1 Esaïe 48.20 Psaumes 51.1
23 Imbeni, enyi mbingu, maana Bwana ametenda hayo; Pigeni kelele, enyi mabonde ya nchi; Pazeni nyimbo, enyi milima; Nawe, msitu, na kila mti ndani yake. Maana Bwana amemkomboa Yakobo, Naye atajitukuza katika Israeli.
Esaïe 49.13 Psaumes 69.34 Jérémie 51.48 Psaumes 98.7-98.8 Esaïe 49.3
24 Bwana, mkombozi wako, yeye aliyekuumba tumboni, asema hivi; Mimi ni Bwana, nifanyaye vitu vyote; nizitandaye mbingu peke yangu; niienezaye nchi; ni nani aliye pamoja nami?
Esaïe 42.5 Esaïe 43.14 Esaïe 45.12 Esaïe 51.13 Job 9.8
25 Nizitanguaye ishara za waongo, na kuwatia waganga wazimu; niwarudishaye nyuma wenye hekima, na kuyageuza maarifa yao kuwa ujinga;
Psaumes 33.10 Job 5.12-5.14 2 Samuel 15.31 Jérémie 50.36 Jérémie 51.57
26 nilithibitishaye neno la mtumishi wangu, na kuyafikiliza mashauri ya wajumbe wangu; niuambiaye Yerusalemu, Utakaliwa na watu, nayo miji ya Yuda, Itajengwa, nami nitapainua mahali pake palipobomoka;
Zacharie 1.6 1 Rois 13.3-13.5 Jérémie 32.15 Daniel 9.25 1 Rois 18.36-18.38
27 niviambiaye vilindi, Kauka, nami nitaikausha mito yako;
Esaïe 42.15 Jérémie 50.38 Jérémie 51.36 Esaïe 11.15-11.16 Jérémie 51.32
28 nimwambiaye Koreshi, Mchungaji wangu, naye atayatenda mapenzi yangu; hata ataunena Yerusalemu, Utajengwa; na hilo hekalu, Msingi wako utawekwa.
Esaïe 45.1 Esaïe 45.13 2 Chroniques 36.22-1.3 Esaïe 48.14-48.15 Esaïe 46.11

Cette Bible est dans le domaine public.