Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 44
Bible en Swahili de l’est


L’Éternel et les idoles

1 Lakini sikia sasa, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na Israeli, niliyekuchagua;
Esaïe 41.8 Jérémie 30.10 Jérémie 46.27-46.28 Luc 13.34 Deutéronome 7.6-7.8
2 Bwana, aliyekufanya, na kukuumba toka tumboni, yeye atakayekusaidia, asema hivi; Usiogope, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na wewe, Yeshuruni, niliyekuchagua.
Jérémie 1.5 Esaïe 43.1 Esaïe 44.24 Esaïe 49.1 Esaïe 43.7
3 Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa;
Joël 2.28 Actes 2.17 Esaïe 59.21 Jean 7.37-7.39 Apocalypse 21.6
4 nao watatokea katika manyasi, kama mierebi karibu na mifereji ya maji.
Psaumes 1.3 Esaïe 58.11 Lévitique 23.40 Psaumes 92.13-92.15 Esaïe 61.11
5 Mmoja atasema, Mimi ni wa Bwana; na mwingine atajiita kwa jina la Yakobo; na mwingine ataandika juu ya mkono wake, Kwa Bwana, na kujiita kwa jina la Israeli.
Néhémie 9.38-10.29 Jérémie 50.5 Galates 6.16 1 Pierre 2.9 Psaumes 116.16
6 Bwana, Mfalme wa Israeli, Mkombozi wako, Bwana wa majeshi, asema hivi; Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho; zaidi yangu mimi hapana Mungu.
Esaïe 41.4 Apocalypse 1.8 Esaïe 43.10-43.11 Esaïe 48.12 Apocalypse 22.13
7 Naye ni nani kama mimi atakayeita, na kuyahubiri haya, na kunitengenezea, tangu nilipowaweka watu wa kale? Na mambo yanayokuja na yatakayotokea, wayatangaze.
Esaïe 41.26 Esaïe 41.22 Esaïe 43.12 Esaïe 43.9 Esaïe 45.21
8 Msiogope wala msifanye hofu; je! Sikukuhubiri haya zamani na kuyaonyesha? Na ninyi ni mashahidi wangu. Je! Yuko Mungu zaidi yangu mimi? Hakika hapana Mwamba; mimi sijui mwingine.
Esaïe 43.10 1 Samuel 2.2 Deutéronome 4.35 Deutéronome 4.39 Jean 10.30
9 Wachongao sanamu, wote ni ubatili; wala mambo yao yawapendezayo hayatafaa kitu; wala mashahidi wao wenyewe hawaoni, wala hawajui; ili watahayarike.
Esaïe 41.24 Esaïe 41.29 Psaumes 97.7 Psaumes 135.18 1 Corinthiens 8.4
10 Ni nani aliyejichongea mungu mmoja, au aliyesubu sanamu isiyofaa kitu?
Jérémie 10.5 Actes 19.26 Habakuk 2.18 Daniel 3.1 Esaïe 41.29
11 Tazama, wenziwe wote watatahayari; na mafundi, hao ni wanadamu; na wakusanyike pamoja, wakasimame; wataogopa na kutahayari pamoja.
Esaïe 42.17 Esaïe 45.16 Psaumes 97.7 Esaïe 1.29 Jérémie 51.17
12 Mfua chuma hufanza shoka, hufanya kazi kwa makaa, huitengeneza sanamu kwa nyundo, huifanyiza kwa nguvu za mkono wake; naam, huona njaa, nguvu zake zikampungukia; asipokunywa maji huzimia.
Esaïe 41.6-41.7 Esaïe 40.19 Esaïe 46.6-46.7 Exode 32.4 Habakuk 2.13
13 Seremala hunyosha uzi; huiandika kwa kalamu ya mate; huitengeneza kwa randa, huiandika kwa bikari, huifanza kwa mfano wa mwanadamu, sawasawa na uzuri wa mwanadamu, ili ikae nyumbani.
Juges 17.4-17.5 Psaumes 115.5-115.7 Deutéronome 27.15 Esaïe 41.7 Juges 18.24
14 Yeye hujikatia mierezi, hutwaa mtiriza, na mwaloni, hujichagulia mti mmoja katika miti ya msituni; hupanda mvinje, mvua ikausitawisha.
Esaïe 40.20 Jérémie 10.3-10.8 Habakuk 2.19 Osée 4.12
15 Kisha utamfaa mwanadamu kwa kuni; hutwaa kipande, akaota moto; naam, huuwasha moto, akaoka mkate; naam, huufanya mungu, akauabudu; huifanya sanamu ya kuchonga, akaisujudia.
2 Chroniques 25.14 Juges 2.19 Apocalypse 9.20 Esaïe 44.10 Esaïe 45.20
16 Sehemu moja huiteketeza; kwa sehemu nyingine hula nyama; huoka chakula kiokwacho, akashiba; naam, huota moto, akasema, Aha, nimeota moto, nimeona moto;
17 na kwa sehemu iliyobakia hufanya mungu, yaani, sanamu yake ya kuchonga; husujudu mbele yake akaiabudu, akaiomba, akasema, Uniokoe; maana wewe u mungu wangu.
Esaïe 45.20 Esaïe 37.38 Daniel 6.20-6.22 Daniel 3.29 Daniel 3.17
18 Hawajui wala hawafikiri; maana amewafumba macho, wasione, na mioyo yao, wasiweze kufahamu.
2 Corinthiens 4.3-4.4 Psaumes 81.12 Esaïe 6.9-6.10 Jean 12.39-12.40 Jérémie 10.14
19 Wala hapana atiaye moyoni, wala hapana maarifa, wala fahamu kusema, Nimeteketeza sehemu motoni, naam, pia nimeoka mkate juu ya makaa yake; nimeoka nyama nikaila; nami, je! Kilichobaki nikifanye kuwa chukizo? Je! Nisujudie shina la mti?
Deutéronome 27.15 1 Rois 11.7 2 Rois 23.13 1 Rois 11.5 Deutéronome 32.46
20 Hula majivu; moyo uliodanganyika umempotosha, asiweze kuiokoa nafsi yake, wala kusema, Je! Sio uongo mkononi mwangu?
Psaumes 102.9 Job 15.31 Romains 1.28 Osée 4.12 Romains 1.25

Retour d’Israël chez lui

21 Kumbuka haya, Ee Yakobo; nawe Israeli, maana wewe u mtumishi wangu; nimekuumba; u mtumishi wangu; Ee Israeli, hutasahauliwa na mimi.
Esaïe 44.1-44.2 Esaïe 43.15 Deutéronome 4.23 Esaïe 43.1 Romains 11.28-11.29
22 Nimeyafuta makosa yako kama wingu zito, na dhambi zako kama wingu; unirudie; maana nimekukomboa.
Esaïe 43.25 1 Corinthiens 6.20 Esaïe 48.20 Psaumes 51.1 1 Pierre 1.18-1.19
23 Imbeni, enyi mbingu, maana Bwana ametenda hayo; Pigeni kelele, enyi mabonde ya nchi; Pazeni nyimbo, enyi milima; Nawe, msitu, na kila mti ndani yake. Maana Bwana amemkomboa Yakobo, Naye atajitukuza katika Israeli.
Psaumes 69.34 Esaïe 49.13 Psaumes 96.11-96.12 Jérémie 51.48 Psaumes 98.7-98.8
24 Bwana, mkombozi wako, yeye aliyekuumba tumboni, asema hivi; Mimi ni Bwana, nifanyaye vitu vyote; nizitandaye mbingu peke yangu; niienezaye nchi; ni nani aliye pamoja nami?
Esaïe 42.5 Esaïe 43.14 Esaïe 45.12 Esaïe 40.22 Esaïe 44.2
25 Nizitanguaye ishara za waongo, na kuwatia waganga wazimu; niwarudishaye nyuma wenye hekima, na kuyageuza maarifa yao kuwa ujinga;
2 Samuel 15.31 Psaumes 33.10 Job 5.12-5.14 Jérémie 50.36 Jérémie 51.57
26 nilithibitishaye neno la mtumishi wangu, na kuyafikiliza mashauri ya wajumbe wangu; niuambiaye Yerusalemu, Utakaliwa na watu, nayo miji ya Yuda, Itajengwa, nami nitapainua mahali pake palipobomoka;
Zacharie 1.6 Esaïe 58.12 Amos 9.14 Actes 2.25-2.28 Esaïe 42.9
27 niviambiaye vilindi, Kauka, nami nitaikausha mito yako;
Jérémie 50.38 Jérémie 51.36 Esaïe 42.15 Esaïe 43.16 Esaïe 51.15
28 nimwambiaye Koreshi, Mchungaji wangu, naye atayatenda mapenzi yangu; hata ataunena Yerusalemu, Utajengwa; na hilo hekalu, Msingi wako utawekwa.
2 Chroniques 36.22-1.3 Esaïe 45.1 Esaïe 45.13 Esdras 6.3-6.18 Esaïe 45.3

Cette Bible est dans le domaine public.