Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 16.30
Bible en Swahili de l’est


1 Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana.
Proverbes 19.21 Proverbes 16.9 Matthieu 10.19-10.20 Proverbes 20.24 Philippiens 2.13
2 Njia zote za mtu ni safi machoni pake mwenyewe; Bali Bwana huzipima roho za watu.
Proverbes 21.2 1 Samuel 16.7 Proverbes 30.12 Luc 16.15 Jérémie 17.10
3 Mkabidhi Bwana kazi zako, Na mawazo yako yatathibitika.
Proverbes 3.6 Psaumes 37.4-37.5 Psaumes 55.22 Philippiens 4.6 1 Pierre 5.7
4 Bwana amefanya kila kitu kwa kusudi lake; Naam, hata wabaya kwa siku ya ubaya.
Romains 9.22 Esaïe 43.21 1 Pierre 2.8 Esaïe 43.7 Romains 11.36
5 Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa Bwana; Hakika, hatakosa adhabu.
Proverbes 6.16-6.17 Proverbes 11.21 Proverbes 8.13 Jacques 4.6 Romains 2.8-2.9
6 Kwa rehema na kweli uovu husafishwa; Kwa kumcha Bwana watu hujiepusha na maovu.
Proverbes 14.16 Daniel 4.27 Job 28.28 Luc 11.41 Proverbes 8.13
7 Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye.
Genèse 33.4 2 Chroniques 17.10 1 Jean 3.22 Jérémie 15.11 Hébreux 13.21
8 Afadhali mali kidogo pamoja na haki, Kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.
Psaumes 37.16 Proverbes 15.16 Michée 6.10 Jérémie 17.11 1 Timothée 6.6-6.9
9 Moyo wa mtu huifikiri njia yake; Bali Bwana huziongoza hatua zake.
Proverbes 19.21 Proverbes 16.1 Psaumes 37.23 Proverbes 20.24 Jérémie 10.23
10 Kukata maneno huwa katika midomo ya mfalme; Kinywa chake hakitakosa katika hukumu.
Esaïe 32.1-32.2 Proverbes 16.12-16.13 Amos 6.12 Deutéronome 17.18-17.20 Osée 10.4
11 Mizani ya haki na vitanga vyake ni vya Bwana; Mawe yote ya mfukoni ni kazi yake.
Proverbes 11.1 Amos 8.5 Deutéronome 25.13-25.15 Proverbes 20.23 Michée 6.11
12 Wafalme wakitenda yasiyo haki ni chukizo; Maana kiti cha enzi huthibitika kwa haki.
Proverbes 25.5 Proverbes 29.14 Proverbes 20.18 Luc 12.48 Apocalypse 19.11
13 Midomo ya haki ni furaha ya wafalme; Nao humpenda yeye asemaye yaliyo sawa.
Proverbes 14.35 Proverbes 22.11 Psaumes 101.5-101.7
14 Hasira ya mfalme ni kama wajumbe wa mauti; Lakini mtu mwenye hekima ataituliza.
Proverbes 19.12 Proverbes 20.2 Marc 6.27 Proverbes 17.11 Luc 12.4-12.5
15 Kuna uhai katika nuru ya uso wa mfalme, Na fadhili zake ni kama wingu la masika.
Job 29.23-29.24 Psaumes 72.6 Proverbes 19.12 Psaumes 21.6 Actes 2.28
16 Si afadhali kupata hekima kuliko dhahabu? Naam, yafaa kuchagua ufahamu kuliko fedha.
Proverbes 8.19 Proverbes 8.10-8.11 Job 28.13-28.28 Proverbes 4.7 Matthieu 16.26
17 Njia kuu ya mwenye haki ni kujitenga na uovu; Yeye ashikaye njia yake huihifadhi nafsi yake.
Apocalypse 3.10 Esaïe 35.8 Actes 24.16 Proverbes 4.24-4.27 Jude 1.21
18 Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.
Proverbes 11.2 Proverbes 18.12 Esaïe 2.11-2.12 Abdias 1.3-1.4 Proverbes 29.23
19 Afadhali kuwa na roho ya unyenyekevu pamoja na maskini, Kuliko kugawanya nyara pamoja na wenye kiburi.
Esaïe 57.15 Exode 15.9 Esaïe 10.13-10.15 Psaumes 138.6 Esaïe 9.3
20 Atakayelitafakari neno atapata mema; Na kila amwaminiye Bwana ana heri.
Psaumes 2.12 Proverbes 19.8 Psaumes 34.8 Proverbes 13.15 Esaïe 30.18
21 Aliye na hekima moyoni ataitwa mwenye busara; Utamu wa maneno huongeza elimu.
Proverbes 16.23-16.24 Esaïe 50.4 1 Rois 3.12 Psaumes 45.2 Jean 7.46
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake aliye nao; Bali kufundishwa kwa wapumbavu ni upuzi wao.
Jean 5.24 Luc 6.39-6.40 Proverbes 13.14 Proverbes 10.11 Proverbes 15.2
23 Moyo wake mwenye hekima hufundisha kinywa chake; Huzidisha elimu ya midomo yake.
Proverbes 15.28 Matthieu 12.34-12.35 Psaumes 45.1 Psaumes 37.30-37.31 Proverbes 22.17-22.18
24 Maneno yapendezayo ni kama sega la asali; Ni tamu nafsini, na afya mifupani.
Proverbes 24.13-24.14 Proverbes 4.22 Psaumes 19.10 Proverbes 25.11-25.12 Psaumes 119.103
25 Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu; Lakini mwisho wake ni njia za mauti.
Proverbes 14.12 Actes 26.9 Proverbes 12.15 2 Corinthiens 13.5 Proverbes 12.26
26 Nafsi yake mfanya kazi hujifanyia kazi; Maana kinywa chake humtia bidii.
Ecclésiaste 6.7 Proverbes 14.23 1 Thessaloniciens 4.11-4.12 Proverbes 9.12 2 Thessaloniciens 3.8-3.12
27 Mtu asiyefaa kitu huchimba shimo la madhara; Katika midomo yake mna moto uteketezao.
Jacques 3.6 Psaumes 57.4 Proverbes 6.12 1 Samuel 25.17 Esaïe 5.18
28 Mtu mshupavu huondokesha fitina; Na mchongezi huwafarakanisha rafiki.
Proverbes 17.9 Proverbes 15.18 Proverbes 18.8 1 Samuel 24.9 2 Corinthiens 12.20
29 Mtu mkali humshawishi mwenzake; Humwongoza katika njia isiyo njema.
Proverbes 3.31 1 Samuel 23.19-23.21 2 Pierre 3.17 Proverbes 12.26 Proverbes 2.12-2.15
30 Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka; Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya.
Jean 3.20 Matthieu 14.7-14.8 Esaïe 6.10 Proverbes 6.12-6.14 Matthieu 13.15
31 Kichwa chenye mvi ni taji ya utukufu, Kama kikionekana katika njia ya haki.
Proverbes 20.29 1 Samuel 12.2-12.5 Proverbes 3.1-3.2 Lévitique 19.32 Genèse 47.7-47.10
32 Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa; Na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu atekaye mji.
Proverbes 14.29 Proverbes 19.11 Proverbes 15.18 Jacques 1.19 Proverbes 25.28
33 Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za Bwana.
Jonas 1.7 Néhémie 11.1 1 Samuel 14.41-14.42 Josué 18.10 Actes 1.26

Cette Bible est dans le domaine public.